Mwakyembe awaliza watu wa Kyela

leo katika mikutano miwili iliyofanyika jimboni kwake Mhe Mwakyembe amewaliza watu baada ya kuamua kuvua kofia yake na gloves na miwani waone jinsi alivyoathiliwa na sumu kali. Katika hotuba yake ametumia muda kuwasihi wananchi kuacha majungu badala yake wamuunge mkono ili amalizie kipindi chake cha uongozi. Hata hivyo hakutaja watu waliomdhuru lakini aliwashukuru wananchi kwa maombi yao na madaktari kwa juhudi zao katika kuokoa uhai wake.

Teacher1,
Mbona Mwakyembe hakuongelea kabisa mambo ya kuathiriwa na sumu? Kasema ni ugonjwa tu na anakunywa vidonge 25 kwa siku.

Pia kasema hata Sitta alikuwa na haki kusema aliyosema kwani ilikuwa ni hisia zake kwa jinsi alivyomwona Mwakyembe akiumwa. Anasema itakuwa makosa serikali kumshitaki Sitta maana alisema alichokuwa anahisi.

Anasema 2015 atakuja kuwaambia kama anagombea au hagombei. Ila wananchi wamchague anayeweza mapambano kama yeye maana huko kuna mapambano makubwa kama wanavyo mwona yeye alivyosasa, hayo ni matokeo ya mapambano.

Pia aliwaambia wananchi wampokee tu Lowassa akija kuchangisha pesa kwenye kanisa. kwamba ni kiongozi mwenzake na yeye Mwakyembe atakuwepo pia kwenye hiyo harambee ya Lowassa.

Mengine aliongelea barabara ya Kikusya mpaka Matema kwamba mchakato umekamilika na itajengwa kwa kiwango cha lami mpaka matema.

Pia aliwashukuru wananchi kwa maombi yao ambayo yamesaidia kumponya.

Hakukubali maswali maana wananchi walitaka kumuuliza hasa hilo la sumu au sio sumu.

Baada ya mkutano wananchi kwenye makundi gumzo lilikuwa imekuwaje ghafla kageuka mpiga debe wa Lowassa wakati kwa miaka kama minne sasa kila akiwa Kyela ilikuwa ni kumtukana Lowassa?

kwa kifupi ni hayo, wengine waongezee waliyoyasikia.
 
amesema asijadiliwe, then anavua kofia na gloves ili watu wamuhurumie, huyu jamaa ni MNAFIKI

Angel Msofe;huyu Dr Mwakyembe kaishiwa kisiasa na hajatimiza hata ahadi moja kati ya 13 alizotuhaidi so anakimbilia kwenye ugonjwa wa ngozi ili tumuonee huruma!

Naichukua Kyela mwaka 2015 kiurahisi mno na put my words on your bank account ili isije mkasema kama sikuwaambia hivyo!
 
Teacher1,
Anasema 2015 atakuja kuwaambia kama anagombea au hagombei. Ila wananchi wamchague anayeweza mapambano kama yeye maana huko kuna mapambano makubwa kama wanavyo mwona yeye alivyosasa, hayo ni matokeo ya mapambano.

Pia aliwaambia wananchi wampokee tu Lowassa akija kuchangisha pesa kwenye kanisa. kwamba ni kiongozi mwenzake na yeye Mwakyembe atakuwepo pia kwenye hiyo harambee ya Lowassa.

Mengine aliongelea barabara ya Kikusya mpaka Matema kwamba mchakato umekamilika na itajengwa kwa kiwango cha lami mpaka matema.

Baada ya mkutano wananchi kwenye makundi gumzo lilikuwa imekuwaje ghafla kageuka mpiga debe wa Lowassa wakati kwa miaka kama minne sasa kila akiwa Kyela ilikuwa ni kumtukana Lowassa?
.

Kwanza mwaka jana akiwa Kasumulu Dr Mwakyembe alituambia HAGOMBEI MWAKA 2015 lkn sasa kabadili kauli yake;huyu jamaa ni mroho wa madaraka sana!

Pili;Ingawaje wataalam waliomtibu walitaja hata aina ya ugonjwa anaoumwa lkn yeye kakazania tu kusema ni sumu na kauli yake hapo inathibitisha hivyo

Tatu;ahadi ya barabara ya Nkuyu-ipinda-Matema sasa ni mwaka 8 tunaambiwa hivyo hivyo kama imetengewa hela bila utekelezaji wowote ule!

Mwisho kama tu Nape,Sendeka na yeye kaamua kujiunga kwenye kambi ya Lowassa maana kajua wazi kuwa mwaka 2015 hawana uwezo wa kumzuia Lowassa asipite kwenye kugombea U-Rais kwa tiketi ya CCM!

Mwaka 2015 akigombea Dr Mwakyembe atavuna aibu kubwa mno;utakuwa ni uchaguzi rahisi kupata kutokea kwenye historia ya wabunge wa TZ!Mwakyembe ni janga la kiwilaya-Kyela;ana maneno matamu sana na mengi lkn utekelezaji wa ahadi zake ni ziro!
 
Mwakyembe hajaathirika na sumu. Hebu acheni majungu. Nashangaa sana mheshimiwa waziri anatembelea Kyela kisiasa wakati ana kazi ofisini, kwani yupo leave?
ameadhiliwa ma nini sasa mbona unatumiwa vibaya,gamba nini!!!!!!!!!!!!!!!!huna cha kuchangia au umetumwa na waliomwekea sumu.
 
nenda kaoge mtoni kwanza kwani ni mchafu sisi watu wa kyela hatuna nia ya kuwa na kiongozi wenye mawazo machafu kama yako! mwakyembe palepale!
 
Utashangaa sana!
Ukitaka kushangaa zaidi na kuacha mdomo wazi hadi inzi wajae mdomoni, nenda Arumeru, utakuta Mawaziri kibao wako huko kwa mwezi mzima na walishaweka makufuli maofisini kwao!

Na posho ya ofisi na ya chama yote wana sign na gari la kodi zetu na mafuta na dereva

 
Praff ngoja nikusaidie

1. huyu bana alijipambanua kuwa yeye ni mpinga ufisadi...lakini in the same government ya kifisadi akapewa uwaziri na akakubali

2. huyu bana hakumuhoji Lowassa kuhusu richmond na akamhukumu kwa ushahidi wa vi-note na mazingira

3. akasema waziwazi kuwa hakusema yote kuhusu richmond ila kuna mengine aliyabakiza ambayo yangemshtua kila mtu!!

4. waligombania eneo moja na rostam aziz kwa ajili ya kufulia umeme, na by this time kila mtu akajua kumbe naye ni mjasiriamali aliyeko serikalini na ana mradi wa kufua umeme wa upepo, hili halikujulikana kabla ya tume ile ya bunge

5. kabla ya hapo kumbuka aliongoza mapambano ya kuvunja mkataba ambaoleo hii tunadaiw bilion 94!!!

6. akasema ataeleza kila kitu kuhusu wabaya wake waliompa sumu

7. amerudi anasema tusimjadili juu ya afya yake, yet anawafunulia watu upara wake

swali ni nani anayetaka kumuua

1. Kikwete ambaye hakutajwa kwenye richmond scandal na yeye ndiye chief architect wa richmond

2. au EL analipiza kisasi

3. au mtu yeyote yule anayetumia mwanya huu kumdhuru , walikuwa na uadui wa siku nyingi

?????????????????

Waberoya, sidhani kama kuna mtu anamlipizia kisasi, bali ni dua za waTZ kukaa gizani na kudanganywa ndiyo zimemgeuka na zimekuwa laana kwake. Mwakyembe hakutuambia ukweli, na huo ndiyo unaomtafuna!!!!!
 
Kule ndio jimboni kwake hajaenda tangu alipoanza ugua, sasa ulitaka aende Arumeru?

Mwakyembe hajaathirika na sumu. Hebu acheni majungu. Nashangaa sana mheshimiwa waziri anatembelea Kyela kisiasa wakati ana kazi ofisini, kwani yupo leave?
 
Yeye hajaenda kupiga kambi Arumeru? ameamua kwenda jimboni kuomba huruma ya wapiga kura.
 
Kama sumu imeshindwa kummaliza sasa ajiandae kukabiliana na athari za uroho wa madaraka.
Kwa kiwango ambacho mwili wake umepita kwenye misukosuko mikubwa tunategemea kuona busara zake kama kweli anajipenda yeye mwenyewe, apumzike ili afya yake itengemae vizuri.

Amekuwa anapiga kelele akisaidiwa ni mnafiki mwenzake SITTA katika namna inayoonyesha kwamba matatizo yote aliyopitia yanatokana na ushiriki wake kwenye mambo ya kisiasa, Mwenyezi Mungu amemnusuru na mauti, kwa nini asiachane na siasa au ndio anajipanga kulipiza kisasi kiaina.

Muambieni asiwe mtumwa wa siasa, ajiulize maswali ya msingi, was he a politician when he was born and eating from his mother's breasts? those times when he was in primary school and doing very well in his studies was he a politican? had he joined CCM those days when he was strong,ambitious,scoring As in English and History in O Level studies, when he was lecturing at University of Dar es Salaam was he under the supervision of NAPE,KIKWETE,MKAMA and PINDA.

Kwa nini Binaadamu tuko wepesi sana kusahau chanzo cha nguvu na uwezo wetu, why have we grown so stupid that we fear men who dies tomorrow and turn to soil just like a dog?

A professor, Profesa mzima kweli kabisa, tena wa sheria, Tanzania hii, anakosa ujasiri wakufanya maamuzi ya kulinda uhai wake mwenyewe? wadogo na watoto wetu wajifunze nini?
 
Wazazi mtuliage kwenye taaluma zenu angekaa darasani mawsala ya kofia na gloves yangempata wapi ...................siasa za majitaka .....ndo hizo na habari ndo hiyo atavua mpaka mkwega
 
Angewavulia mpaka kufuli lake ili wananchi wajionee kama kweli nywele za magogoni zimenyonyoka ili tuamini kama kweli ni sumu. La sivyo hatutamuamini hata chembe.

True implies False = False
Mnafiki mzandiki a.k.a mchumia tumbo
 
Kutoka gazeti la Nipashe
Mwakyembe: Vita vya ubunge vikiwa vikubwa sana nitaamua kuachia ngazi
Na Thobias Mwanakatwe
31st March 2012
Ila sitamuachia jimbo mtu anayechekacheka
Kimsingi nilikuwa nimekufa, Mungu akaniokoa
Awaelezea kwa kina Wanakyela ugonjwa wake

Mbunge wa Kyela na Naibu Waziri wa Ujenzi, Dk. Harrison Mwakyembe, amewasili jimboni kwake jana na kutoa kauli nzito kuhusu ubunge wake.

Dk. Mwakyembe ambaye amekuwa nje ya jimbo lake kwa zaidi ya miezi saba kutokana na kuugua ugonjwa unaodaiwa kuwa umetokana na sumu na kwenda kutibiwa nchini India, alisema kama ataona vita vya ubunge ni vikubwa sana atachukua hatua ya kuachia ngazi nafasi hiyo.

Akiwa katika kijiji cha Sanu mpakani mwa Wilaya ya Rungwe na Kyela, Dk Mwakyembe alipokelewa na mamia ya wananchi, magari zaidi ya 30, pikipiki zaidi 60, huku wakiwa na mabango yaliyoandikwa “Mwakyembe endeleza mapambano dhidi ya ufisadi tupo nyuma yako”, “Mwakyembe na Mwandosya poleni sana Mungu atawajali mtapona”.

Akifafanua juu ya kauli yake hiyo, alisema hali anayoiona hivi sasa katika jimbo hilo ni watu kupigiana majungu na fitina na kwamba kama vita hivyo vikizidi ataachia ngazi.

Hata hivyo, alisema hatakubali kuachia ngazi mpaka atakapohakikisha kuwa amepatikana mtu makini wa kuliongoza jimbo hilo na sio mtu wa kuchekacheka.

Akizungumza na mamia ya wananchi wa kata ya Ipinda, alisema katika kipindi cha miaka minne kilichobaki wananchi wa Kyela waachane na siasa za fitina na kutokubali kutumiwa na watu ambao sio wazaliwa wa Kyela kwa ajili ya maslahi yao binafsi.

‘Kipindi tulichobaki nacho ni cha miaka minne tushikamane, tuweke pembeni siasa za fitina, tusikubali kutumiwa na watu ambao sio wana Kyela hawana uchungu na Kyela, kama ni ubunge mimi naomba niwaapie na wazazi wangu wapo hapa wazee, mimi nikiona vita vya ubunge ni vikubwa sana nitawaachia,” alisema Mwakyembe.

Akielezea kuugua kwake, alisema kimsingi alikuwa amekufa lakini Mungu amemrejesha ili aendeleze mapambano ya kupigania maslahi ya taifa bila woga wala kigugumizi kwa manufaa ya Watanzani wote.

“Naamini Mungu amenirudisha, ndugu zangu nilikuwa nimekufa, nikisema hivi watu mnasikitika, naamini kwamba Mungu hajanirudisha ili niwe mume bora kwa huyu mama (Mke wake), hata….wala hajanirudisha ili watoto wangu waendelee kuwa na baba,..hapana, nadhani Mungu anajua changamoto tulizonazo kama taifa, wilaya na anataka hizi changamoto sisi tuliopewa hizi nafasi, tuzivalie njuga bila kuogopa bila kigugumizi, “ alisema Dk. Mwakyembe.

Alisema wilaya ya Kyela mara kwa mara ni kitovu cha mabadiliko ya kisiasa na mwalimu siasa nchi hii na ndiyo maana hata katika mapokezi yake wamehudhuria pia viongozi wa vyama vya siasa vya upinzani.

Alisema kitendo kilichofanywa na viongozi wa vyama vya siasa ni uzalendo na tabia ambayo inapaswa kuigwa na kila mtu kwani lazima wanasiasa watambue kuwa siasa haziwezi kutugawa wananchi na Watanzania kwa ujumla.



Alisema hakubaliani na watu wanaosema chama kwanza kwani anavyofahamu utaifa kwanza chama baadaye.

“Mimi sikubalini na mtu yeyoye anayesema kitu cha kwanza ni chama chako,…hapana, mimi kitu cha kwanza kwangu siyo CCM, cha kwanza mimi ni Mtanzania, cha pili ndiyo tunaingia kwenye vyama,….mtu anayekimbilia chama kuwa cha kwanza hivi hicho chama kingetokea wapi kama siyo taifa,” alisema Dk.Mwakyembe.

Aliongeza kuwa ugonjwa unaomsumbua hajawahi kumweleza mtu yeyote lakini ni ugonjwa adimu ambao sio wa kawaida sana ambao umekuwa ukimtesa tokea mwezi wa Mei mwaka jana hadi Agosti, mwaka jana hali ipozidi kuwa mbaya.

Alisema alipokwenda Hospitali ya Taifa ya Muhimbili alielezwa na madaktari kwamba alikuwa anasumbuliwa na kisukari ambapo wakati huo hali iliendelea kuwa mbaya huku nywele zikinyofoka, kope na mifupa ikawa inapinda.

Aliongeza kuwa wakati akiendelea kuugua daktari mmoja (hakumtaja jina), alimweleza kuwa ugonjwa unaomsumbua siyo wa kisukari bali alikuwa ameathirika na sumu katika chakula (food poison) jambo ambalo lilizidi kumchanganya na kushindwa kuelewa anaumwa ugonjwa gani.

Alisema ilikuwa kila sehemu anapokaa ngozi inanyofoka na alipokwenda India, serikali ya nchi hiyo iliposikia kuna waziri anaumwa alipelekewa daktari bingwa wa magonjwa ya ngozi ambaye alimhakikishia kuwa atapona baada ya wiki mbili na kuruhusiwa kurejea Tanzania.’

“Wiki mbili zilipopita daktari aliyekuwa akinitibu alipokuja kunipa dawa alikuta nimevimba mwili mzima, mwili unapasuka, nimepukutika mwili mzima, daktari akaniangalia akasema anafuta maelezo yake ya awali kwamba atapona haraka huu ugonjwa ni mgumu., baadaye walianza kunipima damu kupeleka kila hospitali pamoja na kunitoa nyama mgongoni na mfupa kwa ajili kufanya uchunguzi wa kitaalam zaidi,” alisema.

Aliongeza kuwa ugonjwa huo unaomsumbua umemuathiri sana kwani siku ya tatu daktari aliyekuwa anamtibu alipokwenda hospitalini alienda akiwa na uzi mwekundu mkono wa kushoto ambapo kijana mmoja wa Kihindu “akaniambia huyu daktari ameanza kuomba Mungu upone” maana hata heshima yake imeanza kushuka kwani fani yake inaweza kupotea kwa kushindwa kunitibu.

Aliongea kuwa kutokana na hali mbaya aliyokuwa nayo ndiyo maana hata Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta, alikuwa akiongea kwa hasira akishinikiza jeshi la polisi kufanya uchunguzi wa ugonjwa unaomsumbua kwani alifahamu kuwa kulikuwa na dalili zote za kwamba amelishwa sumu.

“Madaktari walivyoendelea kupima wakasema huu ni ugonjwa mpya ambao bado wanasayansi hawajajua unatokana na nini, Sitta akasema basi huu ni ugonjwa wa kutengeneza, na ndiyo maana hakueleweka na vyombo vya habari vya mafisadi alipoidai polisi kufanya uchunguzi wa kina kwa sababu anasema dalili zote za sumu zinaonekana sasa chunguzeni siyo kwamba anasema kuna sumu hapana,” alisema Dk. Mwakyembe.

Katika mkutano huo, Mwenyekiti wa Chadema kata ya Ipinda, Sadati Mwambungu, alisema Chadema itaendelea kumpigania Dk. Mwakyembe kwa sababu mambo anayoyapigania ya mafisadi ndiyo ambayo pia yanapigiwa kelele na chama hicho.
 
Back
Top Bottom