Mwakyembe amfukuza mfanyakazi aliyestaafu 2013

Maana yake alikuwa bado analipwa mshahara hewa.
Huwezi kumlaumu Mwakyembe moja moja hapo. Yale majina anapelekewa na watu wa chini kwa utekelezaji tu.
Imagine jina lipite ngazi zote mpaka kwa waziri!!!!!!
 
Serikali hawana Mfumo mmoja km Titus anaumoja na Mwakyembe angemtafuta kwanza..,alafu inamaana kuna mishahara hewa ming nchi hii 2ache muvi iendelee...
 
Sasa hapo waziri Kamani anataka kutueleza nini?

Ni kama vile, anapingana na uamuzi wa waziri mwenzie.

Inaelekea Kamani anataka uendelezwe mfumo ule ule, wa wafanyakazi wa serikali kuendelea kuboronga na kuendelea kulindwa, ukiona mfanyakazi wa serikali kawajibishwa sana, basi atahamishwa kituo cha kazi, ili akaendeleze hayo madudu katika kituo chake kipya.

Kama kweli mmoja wa wafanyakazi waliotimuliwa kazi na Mwakyembe, alishastaafu kazi, basi inawezekana wakubwa wa wizara ya kilimo, hawakutaka kumwondoa kwenye payroll, ili waendelee 'kufaidi' mishahara ya mstaafu huyo!!

huo ndo ukwel
 
Sasa hapo waziri Kamani anataka kutueleza nini?

Ni kama vile, anapingana na uamuzi wa waziri mwenzie.

Inaelekea Kamani anataka uendelezwe mfumo ule ule, wa wafanyakazi wa serikali kuendelea kuboronga na kuendelea kulindwa, ukiona mfanyakazi wa serikali kawajibishwa sana, basi atahamishwa kituo cha kazi, ili akaendeleze hayo madudu katika kituo chake kipya.

Kama kweli mmoja wa wafanyakazi waliotimuliwa kazi na Mwakyembe, alishastaafu kazi, basi inawezekana wakubwa wa wizara ya kilimo, hawakutaka kumwondoa kwenye payroll, ili waendelee 'kufaidi' mishahara ya mstaafu huyo!!

Hongera Mwakyembe,itabidi Kamani ajiuzulu.Fukuza fukua imefichua mfanyakazi hewa!Kamani alikuwa wapi wakati kuna mtu wa Idara yake anaripoti kazini bila yeye kujua
 
Hata Kama Kweli Mwakyembe kakosea ..KULIKUWA na haja gani ya waziri Kamani kuongea HADHARANI bila kuongea wenyewe kwa Siri ....hata Kama kakosea bado Waziri Mwakyembe anabaki na haki ya kuchukua hatua kwa kuwa wafanyakazi husika ...wamekuwa posted uwanja wa ndege na kuna AGIZO la Rais la kusafisha vitendo Vya RUSHWA ,aibu ,Madawa ya kulevya pale uwanjani ..Sasa Kama waziri anataka kuendelea kuwatumia wafanyakazi wake wa wizara ya Kilimo walioko pale ...Njia rahisi angewapangia tu sehemu nyingine mbali na uwanja wa ndege au Bandarini
 
Hii ndiyo tanzania!yaani hakuna serikali kabisa

Mi naamini Mwakyembe anaweza kuwa sahihi kwamba jamaa alishastaafu lakini aliendelea kula shavu airport, hawezi kuwa amekurupuka tu.

Lazima Mwakyembe atakuwa ana orodha ya wafanyakazi wa airport ambapo alimuona huyu jamaa.

Kwa upande wa Kamani inabidi na yeye aulizwe kama mtu alistaafu tokea 2013 yet anaendelea kufanya kazi yeye kama Waziri alikuwa wapi kuligundua hili, hastahili hicho kiti kabisa.
 
Duh! huku sasa kuumbuana.kwa nini waziri kamani asimtafute kwanzan Dr. Mwakyembe ili waweke sawa records zao kabla ya kuruka hewani?

na hapa ndipo panapotia mashaka kwa hawa watawala wetu, huku ni kukurupuka kama si kujidhalilisha,kulikuwa kuna ulazima gani sasa wa huyo kamani kukimbilia kwenye media huku akidai kusubiri taarifa ya mwakiembe, wame expose udhaifu wao sasa!
 
Kwa hiyo hao jamaa kwenye CCTV wanaoonekana wanachukua mpango angewaacha tu, au sivyo!

Mwakyembe ameweka mambo adharani kuhusu watuhumiwa.Sasa ni kazi ya wizara husika kujiuliza hao wanaodaiwa ni wafanyakazi wa wizara hizo walikuwa kazini Airport kama wafanyakazi wa wizara ipi?Ni majanga.
 
Waziri Titus kamani amesema mmoja wa watu waliotangazwa na Mwakyembe juwa wamefukuzwa aiport jana alishastaafu tangu 2013 na sio mfanyakazi wa serikali tangu wakati huo.

Waziri Kamani amesema ameshangazwa kuona mstaafu anatangazwa kuwa alikuwa mfanyakazi wa wizara yake kama alivyotangaza Mwakyembe jana.

Hata hivyo waziri kamani amesema anasubiri taarifa zaidi toka kwa Dr Mwakyembe kuhusu hatua alizotangaza jana kufukuza wafanyakazi wa wizara yake waliokuwa wakifanya kazi JKNIA.

Source:Radio one Habari

Kama anasubiri taarifa zaidi kwa nn atangaze? Si angesubiri hyo taarifa zaidi apate kitu cha uhakika? Kama watu wa wizara yake ndo wameendelea kuweka hilo jina la hyo staff wake kamani atakuja kusema tena nn?
 
Sasa hapo waziri Kamani anataka kutueleza nini?

Ni kama vile, anapingana na uamuzi wa waziri mwenzie.

Inaelekea Kamani anataka uendelezwe mfumo ule ule, wa wafanyakazi wa serikali kuendelea kuboronga na kuendelea kulindwa, ukiona mfanyakazi wa serikali kawajibishwa sana, basi atahamishwa kituo cha kazi, ili akaendeleze hayo madudu katika kituo chake kipya.

Kama kweli mmoja wa wafanyakazi waliotimuliwa kazi na Mwakyembe, alishastaafu kazi, basi inawezekana wakubwa wa wizara ya kilimo, hawakutaka kumwondoa kwenye payroll, ili waendelee 'kufaidi' mishahara ya mstaafu huyo!!

Mbona jina la huyo mfanyakazi halitajwi? Na je hilo ni kosa la Mwakyembe? Ni obvious Mwakyembe hajui majina ya hao wafanyakazi against picha za CCTV. Mwakyembe alitajiwa majina tu na huyo aliyechomeka jina la mstaafu inabidi ale kibano.

Tiba
 
na hapa ndipo panapotia mashaka kwa hawa watawala wetu, huku ni kukurupuka kama si kujidhalilisha,kulikuwa kuna ulazima gani sasa wa huyo kamani kukimbilia kwenye media huku akidai kusubiri taarifa ya mwakiembe, wame expose udhaifu wao sasa!

Huko ndiko kunaitwa kukurupuka. Lakini pia sina uhakika taratibu za kazi serikalini zinasemaje kama Waziri anaweza kumfukuza kazi mfanyakazi yeyote wa serkali hata kama hayuko kwenye wizara yake!!!!! Nafikiri kwa kuweka mambo sawa Mwakyembe angetangaza kuwafukuza hao wafanyakazi kutoka kwenye nafasi zao ndani ya airport ili warudi kwenye wizara zao na huko angemshauri waziri mwenzake kuwafukuza kazi. Lakini sio yeye kuwafukuza kazi.

Tiba
 
Na kwanini Waziri Mwakyembe asimtafute mwenzie Kamani ili wajadiliane kabla ya kuwafukuza wafanyakazi wa wizara ya mwenzie kazi?

Hii mijadala ndo inachelwesha utendaji. Hata hivyo wabongo ni wanafiki sana, tunataka afanyeje? aunde tume kwanza ama? Akifukuza watu waovu tunasema kakurupuka, akiwaachia uchunguzi uendelee tunasema wanabebwa, sasa mnataka iweje? bongo bila kuwa kauzu huwezi. Dawa ndo hiyo na kama mawaziri na watendaji wote wangekuwa wakali mambo yangeenda. Hata hivyo hajawafukuza kazi ila kawatoa uwanja wa ndege. Hilo swala hata mimi liliwahi kunikuta pale nilitozwa sh 50,000 eti kwa ajili ya cheti cha ugonjwa wa manjano wakati kinauzwa sh 5000 tu
 
Huko ndiko kunaitwa kukurupuka. Lakini pia sina uhakika taratibu za kazi serikalini zinasemaje kama Waziri anaweza kumfukuza kazi mfanyakazi yeyote wa serkali hata kama hayuko kwenye wizara yake!!!!! Nafikiri kwa kuweka mambo sawa Mwakyembe angetangaza kuwafukuza hao wafanyakazi kutoka kwenye nafasi zao ndani ya airport ili warudi kwenye wizara zao na huko angemshauri waziri mwenzake kuwafukuza kazi. Lakini sio yeye kuwafukuza kazi.

Tiba
Kama nimesikia vizuri Mwakyembe hajawafukuza kazi, ila amewarudisha kwa muajiri wao yeye hataki kuwaona pale airport
 
Kama nimesikia vizuri Mwakyembe hajawafukuza kazi, ila amewarudisha kwa muajiri wao yeye hataki kuwaona pale airport

Mkuu mbali ya kuipata hii habari hapa JF, nimesoma pia gazeti la mwananchi. Gazeti linasema Mwakyembe amewafukuza kazi na kutaka wizara zao kuwachukulia hatua za kisheria. Kwa kuelewa kwangu amewafukuza kazi na anataka wizara zao ziwashitaki.

Inawezekana nimeelewa kinyume.

Tiba
 
Huyu Mwakyembe angeshungulikia pale bandarini mizigo yetu inaliwa hela pale
 
wachangiaji wengi humu mmenisikitisha sana km ndo mawazo yetu watz haya itatuchukua karne nzima kupata maendeleo. Mm nilidhani tungemuunga mkono mwakyembe kwa kuwafukuza wezi hao wala rushwa wakubwa wanaotuchafua mpaka mataifa mengine. Pia Dr Mwakyembe anao ushahidi wa video uliopatikana CCTV kwa maana kwamba hata huyo wanaesema ni mstaafu ameonekana kwenye video akifanya vitendo vya wizi na rushwa. Na kwann watu wanashangaa mstaafu kufukuzwa kazi? kwan mliambiwa mtu akistaafu ndo mwisho wake wa kufanya kazi? watu so wanaajiriwa kwa mkataba? na km alikuwa huyo mstaafu hana mkataba pale uwanja wa ndege alikuwa anafanya nn? Nan aliyekuwa kamuweka pale? maanake ushahidi wa video upo. Mi nadhani waziri kamani ndo mkurupukaji na anaonekana hajafurahishwa na maamuzi ya Dr Mwakyembe na sijui ni kwa interest zipi. Tunahitaji viongozi wanaochukua hatua kwa wahalifu km mwakyembe na sio kuwalea. waziri kamani ameonyesha udhaifu mkubwa na wala mpenda maendeleo hawezi kumuunga mkono isipokuwa wala rushwa na waficha wezi. Halafu mwakyembe amewafukuza kazi airport na kuwarudisha kwenye wizara zao sio kwamba amewafuta kazi serikalini. so its up to them kuwachukulia hatua au kuendelea kuwalea ila airport hawatakiwi kutia pua zao.
 
Hii mijadala ndo inachelwesha utendaji. Hata hivyo wabongo ni wanafiki sana, tunataka afanyeje? aunde tume kwanza ama? Akifukuza watu waovu tunasema kakurupuka, akiwaachia uchunguzi uendelee tunasema wanabebwa, sasa mnataka iweje? bongo bila kuwa kauzu huwezi. Dawa ndo hiyo na kama mawaziri na watendaji wote wangekuwa wakali mambo yangeenda. Hata hivyo hajawafukuza kazi ila kawatoa uwanja wa ndege. Hilo swala hata mimi liliwahi kunikuta pale nilitozwa sh 50,000 eti kwa ajili ya cheti cha ugonjwa wa manjano wakati kinauzwa sh 5000 tu

ukweli tulipofikia sasa watanzania tunahitaji kiongozi dikteta yaan ubabe ubabe sio viongoz sio raia wote wamekubwa na ujinga
 
Kampeni za urais zimeanza.......! Wanaanza kupigana vijembe punde si punde utasikia mmojawapo katangaza nia. Tayari ameshaonyesha dalili. Hii ngoma ya urais si mchezo watu wataweza toana ngeu. Mitandao inajidhihirisha wazi wazi sasa hivi hakuna usiri wala uficho kama zamani.
 
Mkuu mbali ya kuipata hii habari hapa JF, nimesoma pia gazeti la mwananchi. Gazeti linasema Mwakyembe amewafukuza kazi na kutaka wizara zao kuwachukulia hatua za kisheria. Kwa kuelewa kwangu amewafukuza kazi na anataka wizara zao ziwashitaki.

Inawezekana nimeelewa kinyume.

Tiba
kwa mujibu wa hiyo link hapo chini nanukuu baadhi Waziri wa Uchukuzi, Dk. Harrison Mwakyembe, amewatimua vigogo 13 kutoka Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika, Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi na Afya na Ustawi wa Jamik atika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) na kuwarejesha kwenye wizara husika kwa hatua zaidi za kinidhamu na kisheria
wavuti: Majina ya vigogo 12 waliotimuliwa JNIA baada ya Dk Mwakyembe kupokea ripoti ya wala rushwa na wabughudhi abiria
 
Serikali hawana Mfumo mmoja km Titus anaumoja na Mwakyembe angemtafuta kwanza..,alafu inamaana kuna mishahara hewa ming nchi hii 2ache muvi iendelee...

Me nimeshalipwa salary 2 kwa mwaka 1.5 hiv nchi hii ni shida sanaaaa.
 
Back
Top Bottom