Mwakyembe ageukwa

Hao wanaolalamika fukuza isije ikiwa kama jairo,safisa wapo watenda kazi kibao mtaani wanazagaa

Hapa hatuongelei siasa au unafiki, simfahamu wala sijawahi kumuona huyu Chizi lakini sifa zake ziko clear kabisa kwa mtu unayejishugulisha kujua mambo. Tatizo wabongo kila kitu unataka utafuniwe na magazeti hujishugulishi kujua undani wake. Biashara ya ndege ni ngumu sana huwezi kumchukua mtu yoyote mtaani ukamwambia aongoze hata awe na elimu kiasi gani, uzoefu ndio unamata na Chizi ni mzoefu. Mwakyembe na Kilango ni wababaishaji tu na watu wa kukurupuka kutaka sifa. Sijaona bajeti ya wizara ya Mwakyembe lakini kama anataka kusaidia shirika atenge fedha za kulipa mafao wafanyakzi ili shirika liwapunguze wabakie wachache wenye uwezo. Ila kwa stahili hii hata kama hiyo hela imetengwa watapunguzwa majembe na kubakia mishipa ambayo ni ndugu zao
 
HIVI MNAONGELEA MFANYAKAZI AU WAFANYA KAZI?
KUMBE ATC KUNA WAFANYAKAZI NA NDEGE MOJA YA KUKODI?WANALIPWAJE?
NGOJA NIACHE KAZI NINUNUE DALADALA KUMBE NAWEZA KUAJIRI WAFANYAKAZI HATA KUMI NIJIZOLEE MAUJIKO YA KUITWA BOSI.
mmenikumbusha usemi wa jino moja mswaki wa nini?kweli kumfukuza chizi ni uchizi.
 
Ingekuwa vizuri kama ungetueleza hii habari umeitoa wapi na kama ndivyo, Siyo jambo la ajabu kupigwa zenge kwa sababu wengi wao wanahisi kama kibarua kitawatoka. Wengi wao wanafanya kazi kimazoea kwa hiyo watakuwa wako mbele kupinga mabadiliko yoyote.
 
ukiacha sababu aliyotoa Mwakyembe hivi bwana Chizi ana kosa gani? Kapewa atcl ipo taabani ...mi naamini ni zengwe! Time ll tell

Huyo mzee ni mpiga kazi sana mm namfahamu, alishawahi pia kuwa mkurugenzi kwenye Community airline. Lakini mambo ya kisiasa yalilifanya shilika kufa! Ukiwauliza watu waliofanyanaye kaza watakueleza utendaji kazi wa huyo Ndg, Poul Chizi. Nawasiwasi kumuondoa kwake kwaweza kuwa ni zengwe, muda ukifika yote yatakuwa kweupe.
 
hao wanaomtetea huyo chizi ni wezi wenzie
ujue ni kama wale walosukuma gari la yule kibaka mwingine jah hiro
make wanakula wote ofisi nzima loh fukuza wote warudi shamba wakalime viazi ulaya nyambaf kabisa
 
mi nimeskia kwenye magazeti asubuhi
Ingekuwa vizuri kama ungetueleza hii habari umeitoa wapi na kama ndivyo, Siyo jambo la ajabu kupigwa zenge kwa sababu wengi wao wanahisi kama kibarua kitawatoka. Wengi wao wanafanya kazi kimazoea kwa hiyo watakuwa wako mbele kupinga mabadiliko yoyote.
 
Naona Waandishi wengi na watangazaji wanajitahidi kumtetea Mr Chizi sijui wamekula cha juu au jamaa alikuwa mtendaji kweli. Katika hali iliyopo Mwakyembe anahitaji kutoa ufafanuzi wa uhakika kuhusu hii issue. Maana naona ushabiki umeingia hapa. watu hawaongelei na wengine waliosimamishwa naye ila wanamshabikia Mr Chizi alikuwa mchapa kazi. Sioni kazi yoyote aliyochapa.
Tena ikiwezekana fukuza wafanyakazi wote wa ATC na uajiri upya coz walishazoea kukaa bila kazi kwa muda mrefu. Kwa hiyo sitegemei kwamba wataliletea maendeleo shirika zaidi ya majungu tu.
 
We jamaa (Precise pangolin) kuwa na adabu, ukurutu maana yake nini! kumbuka hujafa hujaumbika.
 
Hapa hatuongelei siasa au unafiki, simfahamu wala sijawahi kumuona huyu Chizi lakini sifa zake ziko clear kabisa kwa mtu unayejishugulisha kujua mambo. Tatizo wabongo kila kitu unataka utafuniwe na magazeti hujishugulishi kujua undani wake. Biashara ya ndege ni ngumu sana huwezi kumchukua mtu yoyote mtaani ukamwambia aongoze hata awe na elimu kiasi gani, uzoefu ndio unamata na Chizi ni mzoefu. Mwakyembe na Kilango ni wababaishaji tu na watu wa kukurupuka kutaka sifa. Sijaona bajeti ya wizara ya Mwakyembe lakini kama anataka kusaidia shirika atenge fedha za kulipa mafao wafanyakzi ili shirika liwapunguze wabakie wachache wenye uwezo. Ila kwa stahili hii hata kama hiyo hela imetengwa watapunguzwa majembe na kubakia mishipa ambayo ni ndugu zao

Mkuu, umeongea vzr. Hata ukitafuta kwenye Google utaona elimu yake + uzoefu ktk mambo ya Ndege na kazi anazofanya kama mshauri ktk mambo ya biasha na huduma kwa wateja. Kumbuka pia alishawahi kuwa Meneja masoko wa Air Tanzania nchini South Africa, aliacha kazi yeye mwenyewe na akajikita ktk kazi zake mwenye.
 
Hao wanaolalamika ndio hao wanaoliua shirika la ndege na uchukuzi na usafirishaji kwa ujumla
 
Huu ni mizengwe full screen , chizi mwemyewe Anajua makosa yalivo mengi na ya kutosha hata kuto deserve kwenda hewani ku challenge uamzi wa mwakyembe. Sasa a few relatives na wakabila ndiyo Hii reaction Yao ! Best wishes!!
 
hahahahaaa,,,,,pole sana mdau,,,so u mean PRECISION huwa inafaulisha abiria kama coaster za dar-moro???au isuzu journey zinazotoka ifakara kuja moro,,,,,,


Waingereza wana msemo "jabbering with words" na huyo aliyekwepa tatizo la ATCL ambamo kodi zetu zinakwenda akaanza attack a private company started from the scratch by a vibrant, entrepreneur, local, humble Tanzanian na kuifanya ikapata sifa ya kuandikishwa kwenye soko la hisa la Dar es Salaam ni wa kusamehe. ATCL and Precision Air are two characters diametrically opposed though both belong in the same industr. yKwanza mtu anayelinganisha kuchukua abiria Dar ukawapeleka JNB, Jommo Kenyatta Intl Airport, Entebbe au kwingineko na wakapanda ndege nyingine naye akalinganisha na daladala nafikiri au kafanya kwa makusudi na hali yeye ana exposure au hajui Operations Management. Hiki ni kitu cha kawaida maana mashirika mengi duniani yana utaratatibu wa aina hiyo either kwa makubaliano au kama una abiria pungufu na unaona kwenda sehemu iliyokusudiwa ni hasara unawaweka kwenye ndege nyingine. Hiki si kioja labda anayetaka kukifanya kionja ndiye amechemka.

Sasa turudi kwenye mada ya ATCL. Hivi wafanyakazi wa hili shirika si wana mikataba. Watuonyeshe ni wapi kwenye mikataba wameambiwa ili wafanye kazi kwa ufanisi labda awepo Chizi. Kama kipengele hicho kipo basi MWAKYMEBAMECHEMKA. Kama hakipo Mr.Twambombo is right lazima sheria zifuatwe
 
Sioni tatizo hata kama Mwakyembe angemteua mtoto wake wa kuzaa. Sina shida kabisa na hilo. Cha muhimu mtu ana sifa, uwezo, na ataleja mafanikio. And if it takes mtu wa kabila fulani to sort the mess at ATC let it be. Tukikazana na mambo ya ukabila tutajikuta tunaacha watu wenye uwezo kwa sababu hutaki kuonekana kuwa umeteuwa kabila lako. Watu wapewe kazi kutokana na uwezo wao na sio kuangalia amezaliwa upande gani. Tulishauziwa mbuzi kwenye gunia kuhusu u-spika kwamba alitakiwa mwanamke look what happened! total chaos.

Mambo ambayo kwangu ningetaka kuona yanafanyiwa kazi haraka ni haya:
1. Serikali ijiondoe kwenye huu mtindo wa kizamani wa kuteuwa watendaji kwenye mashirika. Nafasi zitangazwe, watu wafanyiwe interview kama ilivyo kwenye private sector, na wapewe kazi kwa mikataba, wakiboronga wanaondokak

2. Ni mara chache sana kwa technocrat kuwa na management skillls. Huyu bwana Lusajo anaweza akawa rubani mahiri, lakini anaweza kuwa rubbish kwenye utawala.
 
hao wanaomtetea huyo chizi ni wezi wenzie
ujue ni kama wale walosukuma gari la yule kibaka mwingine jah hiro
make wanakula wote ofisi nzima loh fukuza wote warudi shamba wakalime viazi ulaya nyambaf kabisa
Tatizo la hii nchi kudhania kila kitu ni siasa. Hakuna utetezi kwenye suala la siasa ili wengi waseme anafaa. Inawekwa rekodi ya utendaji ya Chizi na iko clear kuwa ni mmoja wa na CEO bora afrka mashariki na ana proven records. Sasa suala la wewe unampenda Mwakyembe unatetea kila kitu alichofanya hata kama kibaya kuna siku utakuja kumpenda hata David Cameron halafu ujute kuzaliwa. Kumtoa mtu mzoefu katika uongozi wa mashirika ya ndege na kumuweka rubani kwa kuwa ana uzoefu wa kuendesha ndege ni ubazazi. Ndo maana tunachekwa na dunia nzima kwa ubwege wetu kwa kuwa kila kitu tunaweka siasa. Hebu we kilaza niambie shirika gani hapa A.Mashariki lina Boeing 737-500? Sio kukurupukia kila hoja maadam uko JF
 
Back
Top Bottom