Mwaka mmoja umetueleza mengi

Mwaka mmoja umetueleza mengi

Naona vijana wameanza kumuelewa.
Naona Sizonje yupo jikon, anaota moto huku anawaza namna gani anaweza kuvuna mamilion ya pesa kutoka kwa jf members.
Kwahiyo tujiandae
 
Huu mwaka mmoja tokea awe madarakani umetuonyesha mengi na sasa tunaweza walau hata kuanza kuhitimisha kuwa kumbe wala hayuko tofauti kivile na wengine na huenda akawa ni bomu kabisa kuliko wote waliomtangulia.
...

Juzi sherehe za uhuru zikafanyika. Maajabu! Manake mwaka jana hakukuwa na sababu ya kusherehekea kwa sherehe kubwa kwa ajili ya gharama kuwa juu lakini mwaka sijui hakukuwa na hizo gharama...

Sasa leo yamekuja haya ya kufanyia mikutano ya CCM ikulu.
...
Mikwara yote ile kumbe hamna lolote...bora hata gesi ya CocaCola...[/B]
Nyani Ngabu: kichwani mwako kimeingia mdudu gani anafukunyua akili zako.

Nahisi kama umekata tamaa vile. Kwa vyovyote vile unajua ulitendalo na siwezi kukusemea moyoni. Umediriki hata kuandika kwamba "you are smart".

1) Naanza kuamini kwamba nawe hauko kivile ukilinganisha bandiko zako za awali na za sasa. Unaweza kuwa bomu la JF likalipuka na kuangamiza jukwaa letu la kupumulia mahasira yetu.

2) Niamini kuwa una takwimu za matumizi ya sherehe za Uhuru za mwaka huu, kiasi cha kupiga dongo hilo kwa utawala. Mtu makini, mwenye busara na akili pevu angerejea na kuchambua hotuba yake kuhusu sababu alizozitoa za kufanya sherehe mwaka huu na siyo mwaka jana.

3) Kama nilivyodokeza kwenye 2) hapo juu ungerejea na kuchambua hotuba yake kuhusu sababu ya kufanyia kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM Ikulu.

Rais Magufuli kwangu namwona kama mwanasiasa wa vitendo, na kwa jinsi hiyo, wanasiasa uchwara na wale wanaoendesha siasa za mikutano ya hadhara na maandamano, hakika mwisho wa siku watajikuta wako pekee majukwaani au barabarani bila wafuasi. Wafuasi wako mitandaoni wakijificha nyuma ya ID kama 'Nyani Ngabu' na wenzake.

Mikwara yote hiyo "Nyani Ngabu" kumbe hamna lolote...bora hata vijana wa kijiweni!
 
Nyani Ngabu ,

..sisi wengine tulishaonya kwamba huyu mtu haamini ktk demokrasia na uhuru wa kutoa mawazo.

..pia tulionya kwamba hata anapotekeleza sheria anatumia ubabe na anakomoa.

..lingine ni kwamba hashauriki. Alipuuza ushauri wa wanasheria kesi ikaenda mahakamani na serikali ikahukumiwa kulipa bilioni 15.

..tulionya kuhusu jinsi alivyoshiriki kuuza nyumba za serikali kwa bei ya kutupa. Na kuhusu kivuko mkweche.

..wapinzani na media wangemfuatilia kwa umakini wangeyaona haya niliyoyaeleza hapo juu.

..uchaguzi uliopita nili support ukawa/cdm. Lengo langu lilikuwa kuona demokrasia na rule of law vinaimarika zaidi. Vilevile nilipendelea kusiwe na chama chenye absolute majority bungeni.

Nb:

..uchaguzi ulipambanisha two very flawed candidates. Mmoja alihusika na richmond, mwingine alihusika kuuza nyumba za serikali kwa bei ya kutupa.

Cc MTAZAMO
 
....you will go down as the worst president in the history of our existance...past...present and future..
Hapa umenena, hili jambo limenichukiza na kufuta kila jema alilowahi kujaribu au hata kulifanya.
Nimeshindwa kuelewa kama ana ufahamu sahihi na hili eneo aliko.
Ikulu ni mahali pa watanzania wote na sio chama au mali ya mtu, haipaswi kugeuzwa ukumbi wa mikutano ya kikundi chochote hasa hiki kiovu cha chama kileeee
 
Huu mwaka mmoja tokea awe madarakani umetuonyesha mengi na sasa tunaweza walau hata kuanza kuhitimisha kuwa kumbe wala hayuko tofauti kivile na wengine na huenda akawa ni bomu kabisa kuliko wote waliomtangulia.

Wahshi kabisa....you will go down as the worst president in the history of our existence...past...present...and future!

Mikwara yote ile kumbe hamna lolote...bora hata gesi ya CocaCola.

NB: Pia iliwahi kuripotiwa kuwa angetuonyesha pay stubs za mshahara wake. Kumbe ilikuwa ni uongo tu. Mpaka leo hamna kitu na hakuna anayejali [ukiacha mimi labda].
SPIDI YA MKOJO.....
 
Unapotosha umma..una uhakika pogba hajawahi funga goli tangu asajiliwe na Man U??

JE unajua kuwa goli alilofunga pogba dhidi ya Swansea ndio goli bora mwezi Old trafford... kama hauna fact bora ukae kimya..Idiot
Kama umeelewa alichokiongea jamaa then nawewe ukaongea ukiwa unamaanisha alichokiongea you are still great thinker otherwise this is beyond your etc
 
Nimesoma ii thread vizuri na comments zenu zote ma comreds but acha nikae kimya for now sitachangia for good reason dont ask.
 
NB: Pia iliwahi kuripotiwa kuwa angetuonyesha pay stubs za mshahara wake. Kumbe ilikuwa ni uongo tu. Mpaka leo hamna kitu na hakuna anayejali [ukiacha mimi labda].


Hahaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa! Mbavu zangu!
Hiyo risechi umefanya wapi kuwa wanaosoma aliyeweza kusoma namba ni wewe tu?.

Pole Max na wengineo ndani ya JF. Nchi ya Mabubu tu inakuja.
 
huu uzi ni nzuri sana mtoa post ww n mtu makini sana uzi bora kabisa
big up
 
Nyani Ngabu: kichwani mwako kimeingia mdudu gani anafukunyua akili zako.

Nahisi kama umekata tamaa vile. Kwa vyovyote vile unajua ulitendalo na siwezi kukusemea moyoni. Umediriki hata kuandika kwamba "you are smart".

1) Naanza kuamini kwamba nawe hauko kivile ukilinganisha bandiko zako za awali na za sasa. Unaweza kuwa bomu la JF likalipuka na kuangamiza jukwaa letu la kupumulia mahasira yetu.

2) Niamini kuwa una takwimu za matumizi ya sherehe za Uhuru za mwaka huu, kiasi cha kupiga dongo hilo kwa utawala. Mtu makini, mwenye busara na akili pevu angerejea na kuchambua hotuba yake kuhusu sababu alizozitoa za kufanya sherehe mwaka huu na siyo mwaka jana.

3) Kama nilivyodokeza kwenye 2) hapo juu ungerejea na kuchambua hotuba yake kuhusu sababu ya kufanyia kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM Ikulu.

Rais Magufuli kwangu namwona kama mwanasiasa wa vitendo, na kwa jinsi hiyo, wanasiasa uchwara na wale wanaoendesha siasa za mikutano ya hadhara na maandamano, hakika mwisho wa siku watajikuta wako pekee majukwaani au barabarani bila wafuasi. Wafuasi wako mitandaoni wakijificha nyuma ya ID kama 'Nyani Ngabu' na wenzake.

Mikwara yote hiyo "Nyani Ngabu" kumbe hamna lolote...bora hata vijana wa kijiweni!
unafikiri jf ni.mali ya lumumba
ukweli on the fleck
 
Back
Top Bottom