Ndugu umemaliza biashara huyo KIRANGA ni kishetani kazini jamani ukishindana na shetani ili ushinde inabidi nawe uwe shetani .
Shetani naye ni hadithi nyingine tu kama mungu. The duality of "Good vs Evil" predates Christ by over a thousand years.
Kwa hiyo ili mungu wa maboksi awe na maana, ilibidi kumtengeneza shetani wa maboksi.
Hata waswahili wanajua, wamesema "Ibilisi wa mtu ni mtu". Hakuna shetani wala mungu.
Kuna watu, wanafanya vitendo vizuri na vibaya.
Na kuuliza maswali kama ninavyouliza mimi hakuwezi kuwa kitu kibaya.
If anything hata kama mungu akiwepo (for arguments sake) na akawa ndiye muumba, wale wanaoamini baada ya kuuliza maswali na kujiridhisha kwa kiasi watakuwa wamemtukuza huyu mungu, kwamba ana uwezo wa kuwaumba na akili za kujiuliza, na wanazitumia.
Wasiotaka maswali, hata kama mungu yupo na ni muumba wa vyote (for arguments sake) watakuwa hawamtukuzi huyu mungu, watakuwa wanamtukana kwamba ulimwengu wake unashindwa kujibu maswali ya kibinadamu.
Kwa hiyo kama kuna shetani (for arguments sake) atataka usiwe na akili ya kuuliza maswali.
Kuuliza maswali hakuwezi kuwa ushetani.Mungu gani anayeogopa challenge ya maswali ya kibinadamu?
Kutokuuliza na ujinga ndiyo kunaweza kuwa matakwa ya shetani (for arguments sake, if he exists) kwa sababu atajua wanadamu wakijiuliza watamuona mungu.
So far hatujamuona, which begs the question.
Kama mungu kashindwa kujidhihirisha kwa watu wanaomtafuta kwa akili zao zote, hata kama yupo (for arguments sake) mungu huyo atawalaumu wanadamu hao kama hawatamjua?
Kesho nikifa na kukutana naye mbinguni halafu akaniuliza "Wewe Kiranga mbona ulikuwa unanipinga sana JF na kusema mimi sipo, niambie kwa nini nisikuchome moto sasa?"
Nikimwambia "Nilisema hupo kwa sababu hukunipa akili za kukutambua" atanijibu vipi?
Akili zote tunapata kutoka kwake!
Wengine wanasema tunamjua kwa neema zake tu.
Sasa kama mimi hajanijalia neema na akili za kumtambua makosa ya nani?
That is if he exists at all, which of course, from the questions raised here, there is no iota of evidence that he does.