Eiyer
JF-Expert Member
- Apr 17, 2011
- 28,259
- 20,914
Huna point, that is to say this is pointless! Sasa wewe uliyesema mimi ni mwanamke na ukashindwa kuthibitisha kuwa mimi ni mwanamke kwanini unayemwambia hayo maneno asikudai huo ushahidi?
Hebu fikiria
Mmekaa mnazungumza na kusema kuwa mlima kilimanjaro uko SINGIDA na mnaendelea story zenu vizuri tu,halafu anatokea mtu huko anakuja na kuwaambia kuwa huo mlima hauko SINGIDA bali uko RUKWA inabidi mkae kimya ili mumsikilize,baada ya kukaa kimya na yeye kumaliza kuongea mnamuuliza sasa wewe ushahidi wako wa kuunga mkono madai yako uko wapi?Anawajibu hana kisha anawaambia kuwa nyie ndio mthibitishe kwanza!!!!!!!!
Sasa hyu mtu ametoa wapi ujasiri wa kubisha au kukataa?
Binafsi mimi najua kuwa mwendawazimu ndie anaebisha au kufanya jambo bila kuwa na sababu yoyote!
Iweje mtu anaedai kuwa ana akili timamu na msomi afanye mambo kama ya mwendawazimu?
Sisi tumeamua kuamini Mungu yupo na hatujawahi kumlazimisha mtu yoyote aamini kama sisi,sasa nyie mnaokuja kuanza kutukatalia uwepo wa Mungu ndio inabidi mtuambie kwanini mnakataa na kwa ushahidi gani
Msitudai ushahidi kwakuwa hatujawakatalia namna mnavyoamini nyie mnaokuja hapa na kuleta vurugu kwenye thread yoyote inayomzungumzia Mungu ndio mtuambie ni kwanini mnafanya hivyo!!!!!