Muziki wa Injili umeingiliwa

Muziki wa Injili umeingiliwa

ki uhalisia waimbaji jitathimin upya. heri muimbe bongo freva kuliko kujifanya mnaimba injili wakat physically you are not supporting

[emoji375][emoji375]
 
Mungu aliwaambia wana wa Israel wayafue mavazi yao siku Tatu kabla hajakutana nao mlimani, kule jangwani. Hivyo hilo halina ubishi, mavazi ni sehemu ya Ibada. Pale Midian Mungu alimwambia Musa avue viatu kwa kuwa mahali aliposimama ni patakatifu. Mwisho, wakati Mungu anatoa maelekezo juu ya utumishi wa Hema takatifu, alimwambia haruni namna ya kuvaa anapokuwa kwenye zamu ya utumishi katika Hema takatifu. Mavazi na Ibada vinaenda Sawa, najua wengine watasema Mungu anamaanisha mavazi ya Rohoni, lakini jua kila ukionacho mwilini kimeanzia Rohoni. Barikiwa sana
Nani alikudanganya... Mavazi pia ni ibada ndugu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mimi nina mapungufu kama wenzangu, lakini siungi mkono suala la kulikosea adabu kanisa/hekalu la Mungu kwa visingizio vyo vyote viwavyo. Ukija kwenye kusanyiko la Mungu umevaa Bikini au kimini maana yake uko hivyo rohoni/moyoni mwako. Pili, aina ya viongozi wetu wa dini tunaowapata nyakati hizi ni changamoto nyingine.
 
Huu upumbavu yani sijui mavazi ni rohoni umekua ni dili sana. Yani muumini wa kitanzania we mpe aya hata za kupinda pinda ili kumuhalalishia kile anachokipenda , basi hapo utamla sadaka tu.

Nakutana na mtu eti anajiita mlokole:, amevaa kiji skin jeans (tutako tumevimbaa) , kavaa kitopu na ziwa kaliboost, mirangi ya mdogo kama kala nyama mbichi, mikucha na mikope ya kubadinda. Ukimuiliza nakujibu Mungu anangalia rohoni.

Upuuzi mtupu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Shalom wana wa Mungu

Jumapili ya leo nimeamua niitumie kuyatoa ya moyoni juu ya muziki wa injili hapa Tanzania.

Ki ukweli hawa waimbaji wa siku hizi wa injili wamakera sana na nachelea kusema ninapata mashaka na Mungu wanayemwabudu.

Dressing code yao ni hovyo sana, yani wanavaa kisharobaro, yaani ni mavazi ambayo hayaleti utukufu kwa Mungu, sijui kama kuna watu wanawashauri katika hili. Nawazungumzia hawahawa wakina Gooddluck Gozbert, Akina Paul Clement na hao wengine mnaowakubali wa type hiyo. Yani ukifungua TV alaf uka mute sauti unaweza ukamaliza wimbo bila kujua kama ni Bongo fleva au ni injili.

Ee Mungu tusamehe turudishie waimbaji wetu wenye adabu na staha kwenye ramani. Akina Ambwene Mwasongwe, Mchungaji Abihudi, Christina Shusho na wengine wa type hyo...

Hawa wa sasa wanaondoa kabisa utukufu wako

Acha kukariri mambo yanabadilika.

Unaenda kanisani au msikitini unakuta muongoza ibada anakwambia fuata maneno yangu usifuate matendo kazi ni kwako kuangalia mavazi Au kusikiliza ujumbe unaopatikana katika huo wimbo.
 
Acha kukariri mambo yanabadilika.

Unaenda kanisani au msikitini unakuta muongoza ibada anakwambia fuata maneno yangu usifuate matendo kazi ni kwako kuangalia mavazi Au kusikiliza ujumbe unaopatikana katika huo wimbo.
Shetani kazini! We lini ulienda misikitini na kuona mtu kavaa mlegezo ndani au ki skin tight?
 
Acha kukariri mambo yanabadilika.

Unaenda kanisani au msikitini unakuta muongoza ibada anakwambia fuata maneno yangu usifuate matendo kazi ni kwako kuangalia mavazi Au kusikiliza ujumbe unaopatikana katika huo wimbo.
Mkuu hapa ndipo tunapokosea yaani mtu huwezi Kutushwishi kusikiliza ujumbe ulionao wakati kuonekano wako unaleta ujumbe tofauti...

Mkuu ukipata nafasi nenda YouTube angalia nyimbo ya Bella Kombo inaitwa Alfa na Omega yani yule Dada ameacha mgongo wote wazi. Hivi kuna injili kweli hapo?
 


Angalia nyimbo hii, mtu ameacha mgongo wote wazi, alafu useme kuna injili hapa
 


Angalia huyu dogo naye kimodo alichovaa, hivi inawashinda nini kuvaa nguo za heshma? Shame on you
 
Mkuu hapa ndipo tunapokosea yaani mtu huwezi Kutushwishi kusikiliza ujumbe ulionao wakati kuonekano wako unaleta ujumbe tofauti...

Mkuu ukipata nafasi nenda YouTube angalia nyimbo ya Bella Kombo inaitwa Alfa na Omega yani yule Dada ameacha mgongo wote wazi. Hivi kuna injili kweli hapo?

Basi Kwakuwa umeshaona tatizo ni mavazi katika video haina haja Ya Wewe kutafuta video Tafuta audio sikiliza na msifu Bwana bila kungalia video ukitaka kuangalia video tafuta mahubiri Ya wachungaji uangalie Ili kumkwepa shetani ni kazi rahisi sana.
 
Pia kinachoharibu zaidi watu wakikosolewa wanakimbilia kusema "Usihukumu kabla hujahukumiwa" hii sentensi pia inatupoteza sana !
Tukubali kukosolewa !
 
Shetani kazini! We lini ulienda misikitini na kuona mtu kavaa mlegezo ndani au ki skin tight?

Wapi kwenye Biblia walisema wanaume wasivae milegezo Au skirt?

Sema tuanaishi kwa kukaririshwa tokea tumezaliwa na tumezoea makaririsho na siyo imani hapo zaman kabla Ya ukoloni wazee wetu walikuwa wanavaa nusu utupu na kwenda kuabudu na kufanya matambiko

Baada Ya wakoloni kuja na dini zao wakaweka na sheria zao Pia na tumeamua kuzifuata cha ajabu hao wazungu wenyewe wanawake wanaenda kanisani wamevaa suruali za jeans na skirt fupi na wanafanya ibada Kama kawaida.
Ila kwa Sisi ambao hatujuwi ata machimbuko Ya hzo dini ndio tumekaa kushupalia mambo yasiyo na msingi.
 
Wale wanaobisha kuhusu umuhimu wa mavazi wanajiongopea wao na nafsi zao.
Tukumbuke Mungu ni tajiri kwa wanaomuabudu.Hana shida na Ibada yako.Ibada ni kwa ajili yako binafsi.Hivyo usipoifikia kwa vigezo vyake ni sawa na kupika mboga bila chumvi.
Ibada italipwa kwa kadri ya viwango vyake.Hatusemi hautalipwa bali shida ni malipo kiasi gani?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
never uovu hata uupambe vip hauwezi kuwa ukwel

[emoji375][emoji375]
na Hakuna dhambi ndogo mbele za bwana, usihukumu maana nawe utahukumiwa asema bwana wa majeshi. Luka 6:36-38
 
Back
Top Bottom