X-PASTER
JF-Expert Member
- Feb 12, 2007
- 11,610
- 1,810
- Thread starter
- #41
Atomu zisizo na fahamu zatoa DNA!
Swali la kujiuliza ni kama Atomu zisizo na fahamu iwapo zinaweza kujilipukia tu na kufanya molekuli za DNA ambazo ni msingi wa maisha na protini.
DNA (Deoxyribonucleic Acid) ni jina la kitaalamu kwa tindikali hii, ambayo katika nucleasi ya celli, inakusanya njia kuu zote za mwili wa binaadamu.
Siri ya njia hizi za fahamu ni mtandao mgumu na wa ajabu sana kiasi ambacho wanasayansi wengi imekuwa vigumu kuutafsiri angalau kwa uchache mpaka kwenye miaka ya 1940 hivi. DNA ambayo huwa na taarifa zote muhimu zinazohusu maisha, vile vile huwa na uwezo unaotokana na mkusanyiko wa atomu zinazohifadhi na jinsi zinavyozaliana kwa kujirudufisha bado ni maswali yasiyo na majibu.
Protini ni matofali yajengayo maisha ya viumbe na huwa na kazi muhimu katika shughuli muhimu za viumbe. Kwa mfano, haemoglobin ambayo ni sehemu muhimu kwenye damu husafirisha Oksijen mahali pote katika mwili, wakati antibodies hukinga maradhi katika miili yetu, na enzymes husaidia kuyeyusha vyakula tulavyo na kugeuza ili tupate nguvu. Fomula inayopatikana katika DNA yetu utengenezaji wa aina 50,000 tafauti za protini. Kama ilivyo wazi, protini ni muhimu sana kwa maisha ya viumbe hai na kutokuwepo kwake kutafanya maisha kutokuwezekana. Haiwezekani kisayansi kuwa DNA na protini kila mojawapo ikiwa ni molekuli kubwa, muhimu kuwa ni kitu tu cha kujitokezea kwa kubahatisha hivi hivi. Mwenyezi Mungu SW anatuambia katika Quran tukufu:
Kinamtukuza Mwenyezi Mungu kila kilichomo mbinguni na ardhini, na yeye ndiye mwenye nguvu, mwenye hikima. Ufalme wa mbingu na ardhi ni wake, Anahuisha na kufisha. Na yeye ni Mwenye uweza juu ya kila kitu...
surat alhadid:1-2
DNA ni mfululizo wa mpangilio madhubuti wa kile wanasayansi wanachokiita nucleotides. Protini ni mfululizo vile vile wa tindikali ya Amino iliyo katika mpangilio madhubuti sana. Kwanza kabisa, kimahesabu haiwezekani kuwa ama molekuli ya DNA au ya protini ambazo huja katika maelfu ya aina kuamua kuchgua aina maalum ambayo ni umuhimu kwa maisha kwa kubatisha. Katika mahesabu ya kubahatisha ya probability inaonesha kuwa uwezo kuwa molekuli ya protini kuweza kufikia usahihi wa kuweza kubahatisha kwa ajili ya maisha ni sifuri. Tunachoweza kusema ni kuwa yote haya yameumbwa na Mwenyezi Mungu (s.w) ambaye ni mkamilifu wa kila kitu.
Kwa nyongeza ya hili ya kutokuwezekana kwa kimahesabu, kuna matatizo ya kimsingi ya kikemikali kwamba molekuli hizi zimetokea kwa kubahatisha. Ikiwa uhusiano kati ya DNA na protini ni matokeo ya muda, kubahatisha, pilika pilika za asili, basi kungekuwa na tabia ile ya kikemikali kwa molekuli hizi za DNA na protini kuingiliana, kuchanganyikana, kuathiriana kwa sababu tindikali na kinyume chake huathiriana. Kwa mantiki hii, kama kubahatisha ingekuwa na nafasi hivyo basi, tindikali za sukari, aminephosphoric na kemikali zote za asili zingeathiriana na mtandao mzima wa DNA na protini, hivyo maisha yote tuonayo leo hii yasingekuwepo.
Je tabia hii ya asili ya vipande vya DNA na protini kuathiriana kikemikali, hupendekeza kuwa muda, kubahatisha na kanuni za kikemikali, mwisho wake utasababisha maisha kutokana na mchanganyiko huu wa molekuli? Jibu ni hapana na tuseme ni kinyume chake. Tatizo ni kuwa athari yote ya hizi kemikali za asili ni ile yenye madhara kama maisha hasa inavyohusika. Kuachia muda, ubahatishaji na tabia ya kikemikali ya DNA na protini, athari yake ni maangamizi ya maisha na maendeleo ya kuishi. Mwenyezi Mungu(s.w) anatueleza katika Quran kwamba:
Na vinamsujudia Mwenyezi Mungu vyote vinavyokwenda mbinguni na katika ardhi; katika wanayama na malaika pia nao hawatakabari. Wanamuogopa Mola wao aliye juu yao, na wanatenda wanayoamrishwa.
Surat an Nahal: 49-50
Kama tunavyoona, ni kuwa haitowezekana kwa DNA na protini ambayo kwa namna yoyote ile haiwezi kufanyika hovyo hovyo bila ya kuwa na mdhibiti ili kuifanya kuwa maisha. Bwana mmoja aitwaye Jean Gruiton, mwanafalsafa akielezea kutokuwezekana huku katika kitabu chake kiitwachoDieu et la Science(Mwenyezi Mungu na sayansi), anasema kuwa maisha yasingewezekana kutokea kwa kubahatisha:
Kutokea na kubahatisha kupi ambako atomu zinasogeleana kufanya molekuli za amino acid? Vile vile, kwa vipi kubahatisha kutokee DNA, anauliza maswali haya rahisi kama mwanasayansi wa kibailojia kama alivyofanya Francois Jacob:
Nani aliyepanga kuwepo molekuli ya DNA ya awali, kutoa taarifa ya kuzaliwa kwa Cell ya mwanzo iliyo hai?
Kama kuna yeyote anayeridhika na dhana hii ya kubahatisha, maswali haya na mengine mengi bado hayana majibu; Hii ndio sababu wanabaiolojia wengi miaka hii ya karibuni wameanza kubadili mitazamo yao. Bado watafiti wakubwa hawaridhishwi na kanuni za Darwin, bila ya kufikiri zaidi upungufu wa nadharia hizi. Nadharia hizi zimeegemea wazo la uongozi kuliko mabadiliko ya maada.
Bwana Jean Guitton anasema sayansi imefikia mahali ambapo, kwa mwanga uliopatikana baada ya tafiti za uvumbuzi mbali mbali kwenye karne ya 20, kuwa Nadharia za Darwin za evolution hazinapakushika kwa vyovyote vile. Mwanasayansi, mwanabiolojia aitwaye Michael Behe anazungumzia jambo hili kwenye kitabu chake kiitwacho Darwins Black Box (Boksi jeusi la Darwin):
Sayansi imepiga maendeleo makubwa katika kufahamu jinsi kemia ya maisha inavyofanya kazi, lakini ugumu na uthabiti uliopo katika maumbile ya molekuli zifanyazo maumbile ya kibaiolojia, zimefanya sayansi kupata taabu kuyatolea maelezo. Imeshindikana kutoa ufafanuzi wa chanzo hasa cha vitu maalum kama biomolecular, angalau tu kwa maendeleo yake.
Kama jinsi ulimwengu mzima ulivyoumbwa pasipo na chochote, hivyo hivyo viumbe viishivyo vimeumbwa pasipo na chochote. Kama tuseme hakukuwa na chochote inavyotokea ikiwepo bila ya kuwepo chochote kwa kubahatisha, vitu visivyo na uhai hawezekani kujiunganishi kwa kubahatisha kufanya vilivyohai. Ni Allah(s.w), Mmiliki wa uwezo usio na kifani, mwenye busara na ufahamu usio na kifani ndiye Mwenye Nguvu ya kufanya vyote hivi: Quran:
Hakika Mola wenu ni Mwenyezi Mungu aliyeziumba mbingu na ardhi kwa nyakati sita. Kisha akatawala juu ya arshi yake. Huufunika usiku kwa mchana, uufuatiao (upesi upesi). Na (ameliumba) jua na mwezi na nyota Na vyote vimetiishwa kwa amri yake (Mwenyezi Mungu) viwe vya manufaa makubwa. Fahamuni kuumba (Ni kwake tu Mwenyezi Mungu) na amri zote ni zake (Mwenyezi Mungu). Ametutaka kabisa Mwenyezi Mungu, Mola wa limwengu zote...
Suratil Al Aaraf: 54
Swali la kujiuliza ni kama Atomu zisizo na fahamu iwapo zinaweza kujilipukia tu na kufanya molekuli za DNA ambazo ni msingi wa maisha na protini.
DNA (Deoxyribonucleic Acid) ni jina la kitaalamu kwa tindikali hii, ambayo katika nucleasi ya celli, inakusanya njia kuu zote za mwili wa binaadamu.
Siri ya njia hizi za fahamu ni mtandao mgumu na wa ajabu sana kiasi ambacho wanasayansi wengi imekuwa vigumu kuutafsiri angalau kwa uchache mpaka kwenye miaka ya 1940 hivi. DNA ambayo huwa na taarifa zote muhimu zinazohusu maisha, vile vile huwa na uwezo unaotokana na mkusanyiko wa atomu zinazohifadhi na jinsi zinavyozaliana kwa kujirudufisha bado ni maswali yasiyo na majibu.
Protini ni matofali yajengayo maisha ya viumbe na huwa na kazi muhimu katika shughuli muhimu za viumbe. Kwa mfano, haemoglobin ambayo ni sehemu muhimu kwenye damu husafirisha Oksijen mahali pote katika mwili, wakati antibodies hukinga maradhi katika miili yetu, na enzymes husaidia kuyeyusha vyakula tulavyo na kugeuza ili tupate nguvu. Fomula inayopatikana katika DNA yetu utengenezaji wa aina 50,000 tafauti za protini. Kama ilivyo wazi, protini ni muhimu sana kwa maisha ya viumbe hai na kutokuwepo kwake kutafanya maisha kutokuwezekana. Haiwezekani kisayansi kuwa DNA na protini kila mojawapo ikiwa ni molekuli kubwa, muhimu kuwa ni kitu tu cha kujitokezea kwa kubahatisha hivi hivi. Mwenyezi Mungu SW anatuambia katika Quran tukufu:
Kinamtukuza Mwenyezi Mungu kila kilichomo mbinguni na ardhini, na yeye ndiye mwenye nguvu, mwenye hikima. Ufalme wa mbingu na ardhi ni wake, Anahuisha na kufisha. Na yeye ni Mwenye uweza juu ya kila kitu...
surat alhadid:1-2
DNA ni mfululizo wa mpangilio madhubuti wa kile wanasayansi wanachokiita nucleotides. Protini ni mfululizo vile vile wa tindikali ya Amino iliyo katika mpangilio madhubuti sana. Kwanza kabisa, kimahesabu haiwezekani kuwa ama molekuli ya DNA au ya protini ambazo huja katika maelfu ya aina kuamua kuchgua aina maalum ambayo ni umuhimu kwa maisha kwa kubatisha. Katika mahesabu ya kubahatisha ya probability inaonesha kuwa uwezo kuwa molekuli ya protini kuweza kufikia usahihi wa kuweza kubahatisha kwa ajili ya maisha ni sifuri. Tunachoweza kusema ni kuwa yote haya yameumbwa na Mwenyezi Mungu (s.w) ambaye ni mkamilifu wa kila kitu.
Kwa nyongeza ya hili ya kutokuwezekana kwa kimahesabu, kuna matatizo ya kimsingi ya kikemikali kwamba molekuli hizi zimetokea kwa kubahatisha. Ikiwa uhusiano kati ya DNA na protini ni matokeo ya muda, kubahatisha, pilika pilika za asili, basi kungekuwa na tabia ile ya kikemikali kwa molekuli hizi za DNA na protini kuingiliana, kuchanganyikana, kuathiriana kwa sababu tindikali na kinyume chake huathiriana. Kwa mantiki hii, kama kubahatisha ingekuwa na nafasi hivyo basi, tindikali za sukari, aminephosphoric na kemikali zote za asili zingeathiriana na mtandao mzima wa DNA na protini, hivyo maisha yote tuonayo leo hii yasingekuwepo.
Je tabia hii ya asili ya vipande vya DNA na protini kuathiriana kikemikali, hupendekeza kuwa muda, kubahatisha na kanuni za kikemikali, mwisho wake utasababisha maisha kutokana na mchanganyiko huu wa molekuli? Jibu ni hapana na tuseme ni kinyume chake. Tatizo ni kuwa athari yote ya hizi kemikali za asili ni ile yenye madhara kama maisha hasa inavyohusika. Kuachia muda, ubahatishaji na tabia ya kikemikali ya DNA na protini, athari yake ni maangamizi ya maisha na maendeleo ya kuishi. Mwenyezi Mungu(s.w) anatueleza katika Quran kwamba:
Na vinamsujudia Mwenyezi Mungu vyote vinavyokwenda mbinguni na katika ardhi; katika wanayama na malaika pia nao hawatakabari. Wanamuogopa Mola wao aliye juu yao, na wanatenda wanayoamrishwa.
Surat an Nahal: 49-50
Kama tunavyoona, ni kuwa haitowezekana kwa DNA na protini ambayo kwa namna yoyote ile haiwezi kufanyika hovyo hovyo bila ya kuwa na mdhibiti ili kuifanya kuwa maisha. Bwana mmoja aitwaye Jean Gruiton, mwanafalsafa akielezea kutokuwezekana huku katika kitabu chake kiitwachoDieu et la Science(Mwenyezi Mungu na sayansi), anasema kuwa maisha yasingewezekana kutokea kwa kubahatisha:
Kutokea na kubahatisha kupi ambako atomu zinasogeleana kufanya molekuli za amino acid? Vile vile, kwa vipi kubahatisha kutokee DNA, anauliza maswali haya rahisi kama mwanasayansi wa kibailojia kama alivyofanya Francois Jacob:
Nani aliyepanga kuwepo molekuli ya DNA ya awali, kutoa taarifa ya kuzaliwa kwa Cell ya mwanzo iliyo hai?
Kama kuna yeyote anayeridhika na dhana hii ya kubahatisha, maswali haya na mengine mengi bado hayana majibu; Hii ndio sababu wanabaiolojia wengi miaka hii ya karibuni wameanza kubadili mitazamo yao. Bado watafiti wakubwa hawaridhishwi na kanuni za Darwin, bila ya kufikiri zaidi upungufu wa nadharia hizi. Nadharia hizi zimeegemea wazo la uongozi kuliko mabadiliko ya maada.
Bwana Jean Guitton anasema sayansi imefikia mahali ambapo, kwa mwanga uliopatikana baada ya tafiti za uvumbuzi mbali mbali kwenye karne ya 20, kuwa Nadharia za Darwin za evolution hazinapakushika kwa vyovyote vile. Mwanasayansi, mwanabiolojia aitwaye Michael Behe anazungumzia jambo hili kwenye kitabu chake kiitwacho Darwins Black Box (Boksi jeusi la Darwin):
Sayansi imepiga maendeleo makubwa katika kufahamu jinsi kemia ya maisha inavyofanya kazi, lakini ugumu na uthabiti uliopo katika maumbile ya molekuli zifanyazo maumbile ya kibaiolojia, zimefanya sayansi kupata taabu kuyatolea maelezo. Imeshindikana kutoa ufafanuzi wa chanzo hasa cha vitu maalum kama biomolecular, angalau tu kwa maendeleo yake.
Kama jinsi ulimwengu mzima ulivyoumbwa pasipo na chochote, hivyo hivyo viumbe viishivyo vimeumbwa pasipo na chochote. Kama tuseme hakukuwa na chochote inavyotokea ikiwepo bila ya kuwepo chochote kwa kubahatisha, vitu visivyo na uhai hawezekani kujiunganishi kwa kubahatisha kufanya vilivyohai. Ni Allah(s.w), Mmiliki wa uwezo usio na kifani, mwenye busara na ufahamu usio na kifani ndiye Mwenye Nguvu ya kufanya vyote hivi: Quran:
Hakika Mola wenu ni Mwenyezi Mungu aliyeziumba mbingu na ardhi kwa nyakati sita. Kisha akatawala juu ya arshi yake. Huufunika usiku kwa mchana, uufuatiao (upesi upesi). Na (ameliumba) jua na mwezi na nyota Na vyote vimetiishwa kwa amri yake (Mwenyezi Mungu) viwe vya manufaa makubwa. Fahamuni kuumba (Ni kwake tu Mwenyezi Mungu) na amri zote ni zake (Mwenyezi Mungu). Ametutaka kabisa Mwenyezi Mungu, Mola wa limwengu zote...
Suratil Al Aaraf: 54