Mag3
Platinum Member
- May 31, 2008
- 13,580
- 23,915
Mdogo wangu Chris Lukosi, nakiri kuna wakati sikuelewi kabisaaa...hebu fikiria wakati ndugu zako Watanzania unapowaita misukule kwa sababu tu mnatofautiana kimawazo kiitikadi! Niliwahi kukupa ushauri kufikiria mara mbili kabla hujakurupuka humu jamvini kwani wengi unaojibizana nao huwajui ingawa wao wanakujua! Hukutaka kusikia. Kwa mfano nanukuu;Wapinzani inabidi wasikilizwe, suala la katiba sio la kuamuliwa na chama kimoja.
Katiba ni kwa ajili ya watanzania wote
Nilikuwa na hakika kabisa kwamba baada ya matokeo kutangazwa siku ya pili, ungechukua time out kidogo ukatafakari msimamo wako na kauli zako...tofauti yako na wana jamvi wengi ni kuwa unao ndugu wa karibu, marafiki na washikaji wanaokusoma na kwa kweli unawasononesha. Hebu fikiria na hii, nanukuu;Tarehe 15/6/2013 - Ndugu zanguni, Kama mjuavyo, kesho ndio uchaguzi wa madiwani sehemu mbali mbali nchini, sote tunajua CCM watafunika viti vyote Mbeya na sehemu nyinginezo. Lakini kuna sehemu moja tu ambayo nina uhakika matokeo yakitoka makamanda wanaweza kuzimia.
Nimefuatilia kampeni na mikutano ya Mheshimiwa Mwigulu Nchemba na Nape na nimewaonea huruma sana makamanda kwani wameonyeshwa tofauti kati ya Chuma na plastiki.
Nawaomba watu wa msalaba mwekundu wawe standby kesho kuhakikisha wanawasaidia makamanda watakaozidiwa baada ya vipimo kutoka kwa daktari ambaye ni sanduku la kupigia kura. CCM ushindi ni uhakika kesho 16/03/2013
Unaona sasa? Halafu leo unaona matunda ya harakati za wapigania haki, wewe huyo eti huyoo unatoa pongezi! Chris Lukosi, ukiona vyaelea vimeundwa! Unakula kivulini kwa sababu tu kuna watu wamehangaika juani ingawaje kwako ni misukule. Grow up kid and congratulations for coming down back to earth and now let's all join hands and together we confront the problems that haunt us day and night...ni ushauri tu!Tarehe 20/9/2013 - Ndugu zanguni, Nasikia kuna watu bado wanataka kufanya mkutano wa hadjhara kesho wakati serikali imepiga marufuku.
Mimi ningependa kuwashauri tu ndugu zangu makamanda kuwa hata kama wakiwapa viroba vya kumwaga, chonde chonde msiende kwenye huo mkutano kesho kwani maumivu ya virungu hayaponi haraka na pia msisahau kuwa mkitupwa jela kwa kuvunja amani basi watakaopata tabu ni familia zenu wakati hao wanaowatuma watakuwa wanakula bata wakiwacheki kwenye TV.
JHebu fikiria kesho jioni wanao wanakusubiri nyumbani halafu mpaka jua limetua hujarudi. Hamuoni ni kuwatia huzuni watoto? Au mnapenda kuja kutembelewa mkiwa sero?