Muswada kurudishwa bungeni

Muswada kurudishwa bungeni

Wapinzani inabidi wasikilizwe, suala la katiba sio la kuamuliwa na chama kimoja.

Katiba ni kwa ajili ya watanzania wote

I can't believe if you were the one who wrote this post. Nahisi kama vile uliingia JF kisha ukatoka kidogo ukaacha Computer yako bila ku-log out kisha kuna mtu akaandika na kupost huo ujumbe, ikiwa ni wewe mwenyewe ulieandika, naweza kuamini kuwa ikitokea maiti akivalishwa viatu vya matairi anaweza kutembea.
 
wapinzani inabidi wasikilizwe, suala la katiba sio la kuamuliwa na chama kimoja.

Katiba ni kwa ajili ya watanzania wote

sasa umekua chris kama ungekuwa cku zote hivi naamini elimu ya uraia uloisoma from std 3 ya enzi za mwl na hii ya sasa ungekuwa far sanaaa....kweli umeanza kutoka porini na kusogea barabarani.leo umeamka bye big up lukosi kwa kuanza kuwakubali oposition.
 
Wadau, changieni mtakavyochangia, lakini mjue kuwa CHUMBA CHA SIRI ni CHRIS LUKOS. M sipoteze muda wenu kwa mambo ya Lukos, yupo jamvini anacheka sana hadi mbavu na taya vinauma!!! Chris acha ujinga huu, tuna mambo mengi ya kutafakari- Westgate, madawa ya kulevya na kipindi hiki tunaanza kutayarisha mashamba. Wanajf tusihadaike, hayatokei namna hiyo!!
 
katiba ni maridhiano ya pande tofauti tofaut mh.jk naomba utumie busara zako katika huru ikulu ni taasisi hebu fanya uchunguzi wako na kama madai yana mashiko plz rudisha mswada bungeni#non-partisan
 
kuna watu wamekariri majibu.kila mada ikiwekwa wanataka 'SOURCE',hatuwezi kuishi kwa utumwa wa akili.kuna habari zingine mtu hawezi kuweka source kwaajili ya usalama,mfano:Labda Rais JK kamdokeza mtu mmoja tu wa karibu na anaemuamini juu ya kutosaini mswaada,huyo mtu hawezi kuweka source hapa jamvini.HATA KWA SAIKOLOJIA YA KAWAIDA TU NI KWAMBA JK HAWEZI KUKUBALI NCHI IINGIE KWENYE VURUGU KISA KATIBA,HALAFU YEYE AKASIMAMISHWE THE HEGUE PEKE YAKE wakati akina chikawe,werema,ndugai wamcheke.
 
kwanini wasianze kuujadili jumatati badala yake waujadili jumanne?. mia
 
Maamuzi juu ya katiba mpya inayogusa maisha ya watanzania tulio wengi siyo kitu cha kukichezea chezea kwa kupiga makofi ya kinafiki!!"we need changes for the betterment of the recent and coming generation"MUNGU IBARIKI TANZANIA
 
Wapinzani inabidi wasikilizwe, suala la katiba sio la kuamuliwa na chama kimoja.

Katiba ni kwa ajili ya watanzania wote
Umewakandia walivyoitisha kikao jangwani leo unawashabikia? Leo imekuwaje umetoa wazo nzuri?
 
Tafsiri rahisi ya hili kama ni kweli ni kuwa, Raisi alileta hoja ya kupitisha Rasimu ya katiba (na serikali zake tatu), wabunge wakiongozwa na chama chake wakaipinga, kwa hiyo lazima atafute kuungwa mkono ili kukamilisha kile anachoamini yeye kuwa ni chema.
 
[Kwani wewe nani hadi useme tunajipa moyo. Kwani hii nchi ni yako? Hebu jiangalie hapo ulipo, katiba ni yako au ya watanzania?Kama si yako basi ujue kila mtu ana haki ya kusema chochote akitakacho kwenye katiba. Usiite wagonjwa kwa sababu hii nchi si yako wewe, na huna mamlaka juu yake kuliko sisi wananchi.QUOTE=sailor1;7409363]Endeleeni kujipa matumaini nyie wagonjwa ili Daktari akija awape dawa ya kusogeza siku.
Hivi hata akili hamna mnaanza kujadili na kujipa ushindi kwa habari za udaku?
Rais hayupo..
Waziri Mkuu yuko Kanda ya Kaskazini kwa ziara.....
Wassira yuko jimboni kwake kwa ziara ....
Katibu wa Chama dume yuko ziara akiwa na Nape Mkoa wa Mara....
Makamu wa Rais yuko Ofisini kwa shughuli za Kiserikali......
Chikawe na AG wana majukumu ya Kitaifa wako busy na mambo mengine kabisa..
Hayo mumeyatoa wapi?
Kweli nyie ni Mbulalists.[/QUOTE]
 
Kama ni kweli litakuwa jambo jema, hongera kwa wana muungano.
 
Wadau, changieni mtakavyochangia, lakini mjue kuwa CHUMBA CHA SIRI ni CHRIS LUKOS. M sipoteze muda wenu kwa mambo ya Lukos, yupo jamvini anacheka sana hadi mbavu na taya vinauma!!! Chris acha ujinga huu, tuna mambo mengi ya kutafakari- Westgate, madawa ya kulevya na kipindi hiki tunaanza kutayarisha mashamba. Wanajf tusihadaike, hayatokei namna hiyo!!


Ooh ok? Lakini nadhani kama ni yeye basi amepata tetesi fulani na ameunganisha dots kupitia hotuba ya JK ktk ziara yake ya sasa USA,aliposema hayuko sure kama ktk Katiba mpya dual citizenship itaruhusiwa!

Ndugu zetu wengi walioko ughaibuni,dual citizenship imekua kichocheo cha wao kuiunga mkono CCM kwa matumaini kwamba CCM inawaunga mkono kubadili hiyo sheria!

Tetesi zilizopo ni kwamba ktk maoni ya TISS na SMZ wamekataa Dual Citizenship! Na hawa ni wadau muhimu ktk maoni ya Katiba mpya!
 
Wapinzani inabidi wasikilizwe, suala la katiba sio la kuamuliwa na chama kimoja.

Katiba ni kwa ajili ya watanzania wote

Leo imekuwaje??
Si majuzi tu hapa ulikuwa ukiwabeza WAPINZANI?? Leo ulikula dawa ya Dr Paurine mapema kabla ya kuandika hapa??
Anyway, ulichosema ni kweli katiba ni kwa ajili ya Watz wote, na wale wabunge waliopitisha ule mswaada kishabiki ni kutowaruhusu warudi tena Bungeni 2015.
 
Mkuu una watoto?

Kama una watoto basi wafikirie wao kwanza then ndio utajua umuhimu wa katiba kuamuliwa na watanzania, sio watu wa upande mmoja.

Mimi mwenyewe huu mchakato wa katiba unanigusa kwa aslimia 100%

Naitwa CHRISTOPHER LUKOSI, Nimezaliwa Mbeya nimekulia Iringa, Kabila langu mhehe wa Kalenga Iringa.

HEBU NIAMBIE UNA JEURI GANI YA KUNIITA FOREIGNER,

NENE MWALUKOSI WA KUKALENGA NDINA FITINDI FYA ULASI FYOLOFU HIILO!

Leo hii ninapofika airport ninakuwa treated kama foreigner wakati ukumbuke mimi ni ex police wa Tanzania na wazazi wangu wote ni watanzania na wako Tanzania.

Huo ni mfano tu wa yanayotuhusu kwenye katiba bila kusahau suala la mgombea binafsi nk.

Ili kupunguza rushwa kwenye chaguzi zetu na kusaidia kuchagua viongozi watakaotufaa inabidi mgombea binafsi aruhusiwe. Hii itasaidia sana kama mtu akipigwa zengwe kwenye chama chake basi anakwenda gombea kama mgombea binafsi inabaki kuwa kazi ya wananchi kuamua

Yako mengi lakini siwezi andika yote

nilikuwa napatwa na upofu kila nilipokuwa nasoma maneno yako au sentensi zako humu jf.Ila leo macho yangu yameona ulichoandika kwa mara ya kwanza.
 
Back
Top Bottom