Muslim University of Moro Graduates huishia wapi?

MUM mkijipanga mtazoa wanafunzi mpaka muwakatae ila mkidhani mnaeneza dini badala ya elimu MTAKWAMA na hv yule mliemkimbia NEKTA kaibukia kwa mbele /kawalia denge. Hatakagi figisu figisu zenu
 
Mkuu secrete sina uhakika sana mara ya mwisho nilisikia MUM hawako TCU.Kwa maneno rahisi ikiwa hawako huko maana yake wanachukua wanafunzi ambao hawajakidhi sifa za kujiunga University.

Niko tayari kusahihishwa.
Ni kweli kabisa, mum hawakujiunga tcu na wanascreen wanafunzi kwa kupitia viongozi wa dini lengwa.
 
Mum ni miongoni mwa vyuo best Tanzania, hufundishi pale kama huna GPA ya atleast 3.8 undergraduate na 4.0 masters, tofauti na st John au Tumaini! Thus y mwalim akikosekana watachukua mwl kutoka udsm au SUA
 
Hebu rudia tena Tuseme viongozi wa dini ndo wanadahili wanafunzi pale?
 
Mkimaliza mabishano yenu ktk wigo wa kidini, mrudi tu katika hoja kuu kuwa Elimu ya Tanzania ktk level zote, kwa sekta binafsi na serikali ni magumashi. Hamna kitu na ndio maana watanzania ni miongoni mwa Raia duniani walio na uelewa mdogo na ufahamu mdogo kuliko. Sasa nyie endeleeni na huo ubaguzi wa kujiona walio sehemu fulani kupitia denomination fulani wapo juu ili hali hata hapo Kenya hamuwezi kuajiriwa.

**By the way hivi Udini humu JF ni namna fulani ya watu kuondoa stress zao za ugumu wa maisha au ?????
 
Mkuu secrete sina uhakika sana mara ya mwisho nilisikia MUM hawako TCU.Kwa maneno rahisi ikiwa hawako huko maana yake wanachukua wanafunzi ambao hawajakidhi sifa za kujiunga University.

Niko tayari kusahihishwa.
MUM wapo TCU mkuu pitia kitabu cha TCU 2015/2016 mum kipo
 
Vyuo vikuu hivi vinavyomilikiwa na taasisi za dini ni kazi sana asee unakuta sijui shehe/ulamaa sijui padiri elimu yenyewe ya kuunga unga nae ana cheo huko chuoni sijui Faculty Dean, sijui Deputy Vice Chancellor yaani ukimcheki tu kwa jicho la haraka haraka bora mbunge wetu wa pale stendi ya kwenda nje ya dar.
Hahahaha Hahahahahaha mkuu unajua hii topic ni very serious usinichekeshe mpaka nashindwa kuchangia,
 
Mum ni miongoni mwa vyuo best Tanzania, hufundishi pale kama huna GPA ya atleast 3.8 undergraduate na 4.0 masters, tofauti na st John au Tumaini! Thus y mwalim akikosekana watachukua mwl kutoka udsm au SUA
GPA ya 3.8 Kutoka Chuo gani??
Ukiona kuwa Prof Ndalichacho alishatengua mfumo wa GPA ambao watahiniwa wa sekondary walikua wanapewa ili kuepuka aibu ya kufeli unafikili Vyuo vikuu vina walimu wa namna gani??
 
MUM mkijipanga mtazoa wanafunzi mpaka muwakatae ila mkidhani mnaeneza dini badala ya elimu MTAKWAMA na hv yule mliemkimbia NEKTA kaibukia kwa mbele /kawalia denge. Hatakagi figisu figisu zenu
Yafuatayo ni makosa aliyo ainisha Prof Ndalichako:
(1)Tatizo la elimu ya Wanafunzi
(2)Tatizo la Elimu na uelewa wa walimu waliofundisha wanafunzi hao.
Mwalimu anaweza kuwa Prof au Dkt lakini hana uwezo wa kufundisha Nondo
Angalia vyio feki ambavyo baadhi ya wanasiasa wamepata PhD vipo Marekani!!
Sasa huko wapo watu wana PhD lakini mambo yao yanafahamika
(3)Kwa hali ya sasa tatizo linaweza kuwa kwa wanafunzi pia angalia ule mwaka zimeanza GPA kwa sekondary wanafunzi walifeli kwa asilimia zaidi ya 60 ndipo wakachakachua matokeo.
Sasa hivi wanafunzi wengi wanavalia suruali kwenye .............hawasomi
 
Vyuo vikuu Binafsi viwekwe chini ya UANGALIZI wa vyuo vikuu vya umma kwa miaka 10 kabla ya kupewa MAMLAKA KAMILI. Maana wengi wao ni wababaishaji
Mkuu hata vya umma for the last 7yrs vyuo vikuu nchini vyote kwa ujumla vimekua vikifanya admission ya wanafunzi failure . Lakini pia serikali ndiyo ya kulaumu kwa kufanya mabadiliko ya taratibu za admission na hivyo kuruhusu failures kujiunga. Ungesikilia bunge leo ungeelewa na prof. Kitila mkumbo alipokua anaongea kupitia jahazi ya clouds in response to ndalichako kuwatumbua TCU.

Serikali ya Tanzania in-focus kwenye quantity enrolment katika level zote na sio quality education. Anglia na sera yao ya kusomesha mtoto wa kike ni kusomesha taifa hata failures wamejiunga vyuo vikuu in the name of priority for woman . TAALUMA SIO SWALA LA GENDER NI ONE'S CAPACITY THAT
'S ALL
 
Mkimaliza mabishano yenu ktk wigo wa kidini, mrudi tu katika hoja kuu kuwa Elimu ya Tanzania ktk level zote, kwa sekta binafsi na serikali ni magumashi. Hamna kitu na ndio maana watanzania ni miongoni mwa Raia duniani walio na uelewa mdogo na ufahamu mdogo kuliko. Sasa nyie endeleeni na huo ubaguzi wa kujiona walio sehemu fulani kupitia denomination fulani wapo juu ili hali hata hapo Kenya hamuwezi kuajiriwa.

**By the way hivi Udini humu JF ni namna fulani ya watu kuondoa stress zao za ugumu wa maisha au ?????
Ukienda Kenya mtafute Mwanafunzi ambaye anaweza kujiunga na Course ya Engineering UDSM
Ukimpata huyo nijulishe!!!
Ni rahisi sana kupata kutoka Uganda lakini sik Kenya
 
Huyo alotoa ranks za vyuo..ni kuwa vingi tunajua nick name ya degree sitolewazo....kuna rushwa za kila aina mpaka za kujiuza...tunajua na zimeandikwa...kuna madada wale wakipiga mapicha ya uchi huko huko uni zenu mnazo zipa ranks....hakuna cha kujivunia..
 
Back
Top Bottom