UBINAFSI NA UFISADI WA MENGI NA CHUKINA FITINA KATIKA MAENDELEO.
[FONT=Times New Roman, serif]Hivikaribuni kumekuwepo na malalamiko kutoka kwa baadhi ya watanzaniadhidi ya Waziri wa Wizara ya Nishati na Madini Mhe. Prof SospeterMuhongo yakiongozwa na Mwenyekiti wa Taasisi ya Sekta BinafsiTanzania (TPSF) ambae pia ni Mwenyekiti wa Makampuni ya IPP, BwanaReginald Mengi. Malalamiko hayo ambayo yameendelea kunukuliwa nabaadhi ya vyombo vya habari na kupelekea hata baadhi ya wahusikakutoka wizarani, Idara na Mashirika yake kulazimika kujibu na kutoleaufafanuzi malalamiko na tuhuma hizo nzito dhidi yao. Moja ya vyombohivyo ni gazeti la NIPASHE linalomilikiwa na IPP media la tarehe6septemba, 2013 katika ukurasa wake wa tatu kuna habari inasema"SERIKALI YAZIDI KUPUUZA USHAURI WA TPSF" Inaeleza habari hiyokuwa " ..Wakatitaasisi ya sekta binafsi (TPSF) ikiishaurikuharakisha sera ya gesibadala ya ugawaji vitalu, serikaliimeendelea kupuuza ushauri huo nasasa kupitia Shirika la maendeleoya petroli Tanzania (TPDC)imetangaza rasmi kuharakisha suala hilokwa madai ya kuwahi ushindaniwa masoko ulimwenguni.."
LakiniTPDF nao katika gazeti la UHURU la jana Ijumaa katika ukurasa wakewatatu imeandikwa habari yenye anuani "MWENYEKITI TPDC: UBINAFSIUNAWAPONZA WATANZANIA. ->wengi wanalalamika uwezohawana,
->Zabuniza vitalu mwezi ujao." katika habari hiyo Mwandishi ameandikakuwa "Mwenyekitiwa Bodi ya wakurugenzi ya Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania(TPDC) , Michael Mwanda, amesema ubinafsi miongoni mwa watanzaniandio unaowafanya washindwe kunufaika na fursa za kiuchumi zilizoponchini, zikiwemo mafuta na gesi. Mwanda alisema hayo jana jijini Dares salaam, alipokuwa akijibu moja ya maswali ya waandishi wa habarijuu ya malalamiko ya baadhi ya watanzania kuwa hawapewi nafasikushiriki katika utafutaji na uchimbaji wa mafuta nagesi."
Malumbanohayo kupitia vyombo vya habari baina ya pande mbili yaani Mengi naIPPyake na Muhongo na Mashirika yake ambayo yamedumu kwa muda, sasayanachukua sura mpya baada ya kuwepo kwa taarifa za chini chini kuwaMwenyekiti huyo wa TPSF na IPP ameandaa mpango wa kuwatumia vijanawaChama Cha Siasa cha Upinzani (CHADEMA) kufanya kongamano lenyemaudhui "rasilimali za nchi na manufaa kwa wazalendo" ambapokongamano hilo limepangwa kupewa airtime katika kituo maarufu chatelevision hapa nchini cha ITV ambacho kinamilikiwa na IPP medialakini pia posho, chakula na incentives mbalimbali zimepangwakutolewa katika Kongamano hilo.
Kamailivyo katika mkakati huo, lengo lililopo nyuma ya pazia la kongamanohilo ni kutaka kuionyesha jamii kuwa Waziri na Wizara kwa ujumlahaijali maslahi ya wazawa na kwamba viongozi wakuu wa Wizara husikahawana Utaifa wala Uzalendo (kwa maana ya upendo kwa Taifa) hivyowanataka kuzitumia nafasi zao ndani ya wizara katika kujitajirishabinafsi na kufanya upendeleo kwa wawekezaji wageni ambao hawanamanufaa ya moja kwa moja katika maendeleo ya wananchi.
Madhumuniya andiko langu hili na kuvuta utafakari makini na wa wengi katikasuala hili ambalo kama hatua muhimu na za haraka hazitachukuliwakatika kulikabili linaweza kuleta tafsiri hasi kwa jamii na hivyokuwagawa na kuwavuruga watanzania na hasa kuwafanya wapoteze imani namatumaini yao kwa Serikali, Waziri, Wizara, Idara na Mashirikayaliyopewa dhamana ya usimamizi wa rasilimali za nchi hii.
Naombaikumbukwe kuwa si mara ya kwanza kwa seke seke la aina hii kuzuka amakuzushwa chini ya uratibu na usimamizi wa Mzee Mengi. Na mara zoteamekuwa akitumia nguvu ya ushawishi wa vyombo vya habarianavyovimiliki katika kutafuta kuungwa mkono na hata kuonyesha ubayawa wabaya wake. Ubaya, malumbano na mizengwe mingi ambayo huzalishwana kusimamiwa na Mzee Mengi asili yake ni Ubinafsi na kuguswa kwamaslahi ya kiuchumi aliyonayo katika Sekta mbalimbali hapanchini.
Hivikaribuni kulizuka sekeseke mfano wa hili la sasa ambalo lilihusuVING'AMUZI na kabla ya hapo TBC, UBINAFSISHAJI WA KILIMANJAROHOTEL,SUALA LA YUSUPH MANJI, SHEIKH AL BASALEHE na katika migogoroyote hiyo Mzee Mengi amekuwa akitumia vyombo vya habari katikakuwakandamiza, kuwazushia, kuwatuhumu na hata kuwadhalilishawapinzani wake. Nitaomba wanajamvi wakumbuke kuwa Mwaka 2008kulipokuwepo mgogoro baina ya Mzee Mengi na Al Basalehe, Katikamgogoro huo Mzee mengi alimrubuni Ustadhi Mmoja wa madrasa (jinalinahifadhiwa kwa sababu za kimaadili) na kuwatumia wanafunzi wamadrasa hiyo kutunga nyimbo za kaswida za kumdhalilisha SheikhAlBasalahe na kisha nyimbo hiyo kupewa airtime katika kituo cha ITV,na kwa mfano kama huo akaitumia ITV kuwataja washindani wake kiuchumikuwa ni MAFISADI PAPA.
Sinakumbukumbu kuwa alitumia vigezo gani kuwataja wapinzani wake haokibiashara kama mafisadi papa, ila kumbukumbu yangu inaniambiaaliwataja hadharani na kupelekea baadhi kumpeleka mahakamani nakumfungilia kesi ambazo hata hivyo hazikupata airtime za kutoshakwenye vyombo vya habari na hata mwisho wake haukuwa umefahamika kwawengi.
Tukirudikatika hoja yetu ya vitalu vya gesi ambavyo Mwenyekiti huyo wa IPPnaTPSF amekuwa akividai kwa hamu kubwa na kuwatuhumu Viongozi waWizara, Wakuu wa Idara na Mashirika yanayohusu Rasilimali gesi namafuta kuwa hawana hata chembe ya Uzalendo na wabinafsi, na hofunitaeleweka vibaya kwa baadhi ya watu nikisema kuwa kauli hii hainauhalisia na si ya kweli, na kwamba inalenga kuchochea hisia za chukina imetolewa kwa misingi ya Chuki, it's simply a hate speech thathate are produced.
Kwamujibu wa TPDC, kuchimba kisima kimoja kwa ajili ya kutafuta gesi namafuta katika nchi kavu ni dola za Marekani milioni 40 (Tshs.Bilioni64) na kwa kina kirefu cha bahari ni dola 120 (Tshs Bilioni190) na pia ili kupata mafuta au gesi baada ya kupata uhakika,mwekezaji anapaswa kuchimba visima vinne hadi vitano, hivyo inahitajimwekezaji kuwa na mtaji usiopungua dola za kimarekani milioni 600 ~800 kiasi ambacho watanzania wengi hawana (MENGI akiwemo) na kwaKauli ya Mwanda, Mwenyekiti wa TPDC alisema kuwa Watanzania iliwaweze kunufaika na rasilimali hiyo, hawana budi kuungana na wabiawenye uwezo wa kimtaji na teknolojia (Suala ambalo Mengianalipinga)
Tatizola kimsingi hapa ni Ubinafsi wa baadhi ya watu ambao wanatakaupendeleo kwa maslahi binafsi ya kibiashara kwa nembo ya uzalendo nauzawa. Kumekuwepo na rekodi zenye kusikitisha ambazo zinaonyeshatatizo la msingi linalowakabili hawa tycoon wetu katika mikopowaliyochukua katika mabenki makubwa mbalimbali hapa nchini na hatanje ambapo bado hawajarejesha mikopo hiyo na hivyo kutokopesheka tenakwa miradi mikubwa kama hii ya vitalu vya gesi lakini pia zipo rekodinyingine zinazoonyesha wametumia mikopo kwa shughuli ambazohawakuombea mikopo hiyo ikiwemo mikopo kutoka benki ya kilimo(Takwimuzipo)
Kamahayo ya mikopo hayatoshi, tayari Kampuni za Mzee Mengi zinashikiliavitalu takribani 59 vya madini vyenye Ukubwa wa mita za mraba3,752.37 (sq km) na baadhi ya vitalu hivyo alivyovishikiliaameshindwa kuviendeleza na matokeo yake Serikali inakosa mapatokutokana na kutoendelezwa kwa vitalu hivyo lakini pia watanzaniawanakosa ajira na manufaa mengine, najiuliza kama hii ndio tafsiri yaUZAWA ambayo Mzee Mengi anaizungumza ama ni AINA nyingine ya UFISADIambayo watanzania walio wengi bado hawajaung'amua kwa kuwa vyombo vyahabari haviandiki wala kusema kuhusu habari hizi. Katika attachmentni orodha ya vitalu mbalimbali vya madini vinavyomilikiwa na Kampuniza Mzee Mengi hapa nchini.
Tunawezakutofautiana katika mengine lakini katika yale yanayohusumustakabaliwa nchi naomba watanzania tuungane na tuseme hapana.Matumizi ya Vyama vya Siasa, wanasiasa na hata pressure group katikakutetea maslahi ya baadhi ya tycoon wa hapa nchini na hata nje nikatika makosa makubwa ambayo yanaweza kutuletea madhara makubwa sanahasa kutokana na rasilimali zilizopo hivi sasa hapa nchini ambazozinatolewa macho na mamilionea wakubwa wa ndani na nje na hata nchitajiri duniani.
Nitoeombi kwa Vijana hawa wa Chadema wanaoandaa Kongamano hilo, watambuenafasi yao kama vijana na Safari waliyonayo ya kuijenga kesho yao nakusahau posho hizo za siku moja na vyakula. Ni wakati wa kusimamiahaki na kuitetea kweli, hata ikiwa kweli hiyo inakinzana na maslahibinafsi. Si wakati wa kutanguliza maslahi ya tumbo, ama maslahi yachama bali ni wakati wa kutanguliza UTAIFA na UPENDO wa kweli kwanchi yetu.
MunguIbariki TANZANIA. [/FONT]