Muongo Vs. Mengi. Kimenuka !

Muongo Vs. Mengi. Kimenuka !

ivi huyu mengi mbona anakimbelembele sana ana mabwana wanaomuagiza kuropoka
Tatizo bw. Mengi hukimbilia media na wananchi anaposhindwa kushawishi juu ya mambo yake ya kibiashara.

I support Muhongo kwamba watanzania hatuna uwezo.....suluhisho sio kuwapa wageni bali ni kama alivyotuasa baba wa Taifa!
Mengi na kundi lake waache ulaghai.
 
Awww Hapa wote wamekosea kusema kweli tuache utani mh mengi kujifanya kwamba sisi watanzania tuna 100m usd na zaidi kufanyia utafiti tu wa mafuta huu ni utafiti mnaweza fika chini hamna kitu ni kudanganyana sio watanzania wengi wenye huu uwezo lakini pia huyu prof kutoa majibu Kama haya sio vizuri mengi ana tabla ya Kwenda kwenye vyombo vya habari yaaani ni la vile mwalimu mkuu basi akitangaza shule nzima isikilize suluhisho ni hawa watu kukaa pamoja naamini bongo kuna watu wana bilioni 2/3 pengine hadi bil 10 wakikusanywa hawa wakaundiwa kampuni au serikali ikawaalika wananchi kununua hisa ili kupata mtaji am pretty sure hizo hela zitapatikana lakini sio kubishana ili kila mmoja ajione ye zaidi yaaani hawa watu hawana washauri ? Pumbaf Kabisa

Well said. But I am pretty skeptical on the highlighted part. I have not forgotten on what happened to the National Investments Company (NICO). Will things become different this time? Why?

Kinachohitajika ni serikali kujigawia vitalu vyake yenyewe amabvyo inaweza kuchimba hapo mbeleni. Tunaweza kuwapa wananchi wetu lakini watafute pesa na siyo wapewe vya mkopo na wakishapewa wanyang'anywe kama wawekezaji wengine.

Ninachokiona mimi hapa ni wajanja wachache wanataka wapewe hivyo vitalu halafu waviuze kwa wawekezaji. Hao ndiyo Watanzania ninaowajua mimi hasa wanaowekeza kwenye madini. Mengi si ana vitalu vingi vya madini, amefanya navyo nini?
 
kama Mengi anazo 25b$ na kendelea basi apewe tu, maana industry ya OIL & GAS sio masihara , na si kila mtu anafanya
 
Bahati mbaya mjadala huu umekuja na masuala binafsi ya Bw. Mengi. Inawezekana mengi asiwe mjumbe mzuri wa suala hili lakini ukweli unabaki pale pale kwamba Waziri Muhongo hana busara wala mkakati makini wa kuendeleza sekta anazosimamia katika nchi yetu. Hana kauli za kistaarabu na hana mantiki inayokubalika katika anayoyasema. Nakumbuka amekuwa hadi sasa aking'ang'ania kujenga hoja ya uongo kwamba watu wa Mtwara wanataka "gesi ibakie kwao na wanufaike wao tu" wakati suala hilo limeshajadiliwa na kufafanuliwa inavyostahili.

Kinachoshangaza kingine ni wale walioshikilia kwamba Watanzania hawana pesa ya kuwekeza kwenye miradi mikubwa kama ya gesi. Sijui ni wawekezaji gani hao wenye pesa iliyolala tu ikisubiri fursa katika dunia hii. Watu wanatafuta fursa kwanza ndipo pesa huibuliwa. Ndio maana tunazungumzia "financial resource mobilisation" (uibuaji wa rasilimali pesa) katika dhana za uchumi. Ukishakuwa na fursa maridhawa na ukaijengea muswada muruwa, ziko taasisi na na wenye rasilimali kadhaa watakaokuwa tayari kukuchangia pesa ya kuwekeza. Ndivyo mambo yanavyokwenda.

Nchi zilizo makini na maendeleo yao duniani huhakikisha fursa hizo zinamilikiwa kwa kiasi kikubwa na watu wake. Wageni wanakaribishwa kuchangia mitaji na teknolojia tu pale inapobidi. Malaysia, Mauritius, Singapore ndivyo walivyofanya, China ndivyo wanavyofanya n.k. Ukija Afrika, nchi kama Ethiopia ndivyo wanavyofanya tena kwa kuhusisha Diaspora yao ambayo ni kubwa sana. Hata kama hawaendi kwa kasi kubwa ya "kukua kwa uchumi" kama tunavyosifiwa na WB/IMF, lakini wanajenga msingi imara wa maendeleo yao na matokeo yake yanawafikia wananchi wake kwa kiasi kikubwa.

Hata kama Mengi hafai, ni budi Serikali iwekeze kwenye kuwawezesha wawekezaji wa ndani (walio makini) kwa mustakabali wa muda mrefu wa nchi. Nimesikia mtu kama Subash Patel amepewa uwekezaji kwenye mradi wa Liganga na Mchuchuma. Sijui yeye anazo "pesa" zinazovuka kiwango cha juizi na matunda? Tuache mzaha; sifa za kuongoza kwa kuwa na "mazingira mazuri ya uwekezaji" na "uchumi unaokua kwa kasi" barani Afrika ilhali matokeo yake yanaelekea nchi za nje walikotoka wawekezaji wake hazina maana kabisa kwetu. Ni kejeli ya siri wanayotutolea hao wana-taasisi za "Bretton Woods".
 
Samahani ila siwez kumlaumu Mengi mana hali ya kiuchumi iliopo sasa hivi hadi Migodi inaamua kupunguza wafanyakazi kwa sabab bei ya Madini imeshuka especially dhahabu na hata Madini yakikaa ardhini hayaozi na anachofanya Mengi ni kuinvest na katika Investment unaweza weka sasa hivi then baadae ukaanza kuvuna,Ina maana Nduu Nyerere alivokua anawaambia watu waache madini yetu mpaka Vijana wakijua how to extract it aikua nae ni hajui kama vile vitu vina umuhimu?
Nahisi ndugu Muhongo nae anataka umaarufu baada ya kuona kua hana airtime za kutosha na kama anataka afanye ya maana ajaribu kuangalia kodi tunayopewa na wawekezaji kutoka migodini ndo ntamuona wa maana na sio kupambana na Mzawa mwenzetu.
 
Sekta ya mafuta na gesi ni moja ya sekta zinazohitaji mitaji mikubwa na tekinolojia ya hali ya juu,kwa mfano kuchimba kisima kimoja cha baharini kina kirefu(offshore deep water) kinahitaji si chini ya $100 na pia sio kwamba 100% utafanikiwa kupata gesi ya kibiashara kwa hiyo risk ni kubwa,,Mengi anapodai heti serikali isitoe leseni kwa wageni na kusubiri wazalendo waje wawekeze hilo swala si sahihi kabisa,kwani hapa Tanzania hakuna mtu binafsi mwenye msuli wa kuwekeza ktk gesi sembuse kina kirefu cha maji,na pia akumbuke si kweli kua Tanzania haina sera ya mafuta na gesi,sera ya mafuta na gesi ipo na ndio iliyotumika kutoa leseni zilizopita,,pia akumbuke tuna ushindani wa kuvutia uwekezaji ktk sekta hii,kwani kwa sasa Afrika mashariki nzima nchi zipo ktk tafiti za mafuta na gesi,,tukichelewa itakula kwetu.,kwani ushindani ni mkubwa,Msumbiji washagundua zaidi ya 150 trillion cubic feet,,wakati sisi tumegundua 43 trillion cubic feet tu..TUKUMBUKE GESI NA MAFUTA UPATIKANA TU KULE YANAPOTAFUTWA.
 
Kuna ubaya gani wawekezajiwakiingia ubia na wazalendo au shirika letu la Petroli basi.Hivi toka wawekezaji wamewekeza kwenye dhahabu watanzania tumepata nini?
 
Uzitegemee maendelea yataletwa na wageni. Kuna haja ya kuangalia uwekezaji wa ndani kuliko wageni. Wageni faida wanachota na kupeleka kwao pia unakuta kuna fasi fulani za ajira wanazikalia hata ambazo watanzania wanaziweza. lkn mzawa faida ataendelea kuiwekeza hapa nyumbani nakujenga uchumi zaidi nakuongeza fursa za ajira.
 
Blackgold nadhani suala si uwezo wa kufanya tafiti au kuchimba kwani ni ukweli usiopingika kuwa gharama za uwekezaji kwenye gas ni kubwa mno. Nadhani kinachokera ni pale government minister anapojibu kwa dharau swali la msingi kama hili linahusu gesi. Bwana Mengi hana hatia kwa kutoa ushauri kwa serikali kuhusu vibali, kwa maoni yake kama m-Tanzania. Wewe pia una haki ya msingi kabisa kutoa maoni yako. Naomba nikwambie tu ya kuwa ni nchi chache sana duniani ambazo uwekezaji wa ndani ulisubiri mpaka wananchi wawe na uwezo wa kifedha. Tutasubiri mpaka kufa. Profesa Muhongo alitakiwa kujibu na kuwaelewesha wa-Tanzania juu ya gharama na mikakati ya serikali kuwawezesha wa-Tanzania ili waweze kushiriki katika utafutaji na uchimbaji wa gesi. Wewe ukiwa ni mhandisi katika oil and gas unajua wazi kuwa uchimbaji wa gesi unahusisha vitu/shughuli nyingi ambazo hufanya kazi in concert ili kufanikisha zoezi zima. Uchimbaji gesi sio kama kuchimba choo kwamba vibarua wale wale wanaochimba msingi ndio watajenga jengo la choo, nla hasha.

Mimi ninaamini kuna wa-Tanzania wanaweza anzisha kampuni zitakazofanya support functions kama providing drill bits, equipment, cementing, lab testing, and other specialized activities that can be done by locals. Mbona Nigeria wameweza? Tusiendekeze utamaduni wa kuabudu wazungu hawa na kuona wao ndio wenye hela na ujuzi pekee yao. Wengi wao wanaokuja huku kwanza wanajifunzia kazi hapa na mara nyingi wanafundishwa na locals. Profesa angeweza kabisa kutumia lugha iliyonyooka bila kutoa kejeli kwa wa-Tanzania wanaomlipa mshahara. Ukiwa profesa haina maana una haki ya kuona wasio ma-profesa kama mazuzu. Tumia elimu yako kwa busara ili unaowaongoza waiheshimu elimu yako. Lakini kama unaendelea kupayuka kama mlevi wa pombe chafu nadhani elimu yako haikusaidii. Of what use is your PhD if you have no wisdom?
 
Kwenye hiyo wizara kila anaeingia ni mpigaji tu!!!
 
Namie nina ufahamu mdogo. Naomba unieleze hao wawekezaji wanapata wapi mitaji ambapo watanzania, viongozi wao wala serikali yao hawapajuii?
 
Sekta ya mafuta na gesi ni moja ya sekta zinazohitaji mitaji mikubwa na tekinolojia ya hali ya juu,kwa mfano kuchimba kisima kimoja cha baharini kina kirefu(offshore deep water) kinahitaji si chini ya $100 na pia sio kwamba 100% utafanikiwa kupata gesi ya kibiashara kwa hiyo risk ni kubwa,,Mengi anapodai heti serikali isitoe leseni kwa wageni na kusubiri wazalendo waje wawekeze hilo swala si sahihi kabisa,kwani hapa Tanzania hakuna mtu binafsi mwenye msuli wa kuwekeza ktk gesi sembuse kina kirefu cha maji,na pia akumbuke si kweli kua Tanzania haina sera ya mafuta na gesi,sera ya mafuta na gesi ipo na ndio iliyotumika kutoa leseni zilizopita,,pia akumbuke tuna ushindani wa kuvutia uwekezaji ktk sekta hii,kwani kwa sasa Afrika mashariki nzima nchi zipo ktk tafiti za mafuta na gesi,,tukichelewa itakula kwetu.,kwani ushindani ni mkubwa,Msumbiji washagundua zaidi ya 150 trillion cubic feet,,wakati sisi tumegundua 43 trillion cubic feet tu..TUKUMBUKE GESI NA MAFUTA UPATIKANA TU KULE YANAPOTAFUTWA.

hapo ulipoandika si chini ya $ 100 ndivyo ilivyo au umekosea?
 
Sekta ya mafuta na gesi ni moja ya sekta zinazohitaji mitaji mikubwa na tekinolojia ya hali ya juu,kwa mfano kuchimba kisima kimoja cha baharini kina kirefu(offshore deep water) kinahitaji si chini ya $100 na pia sio kwamba 100% utafanikiwa kupata gesi ya kibiashara kwa hiyo risk ni kubwa,,Mengi anapodai heti serikali isitoe leseni kwa wageni na kusubiri wazalendo waje wawekeze hilo swala si sahihi kabisa,kwani hapa Tanzania hakuna mtu binafsi mwenye msuli wa kuwekeza ktk gesi sembuse kina kirefu cha maji,na pia akumbuke si kweli kua Tanzania haina sera ya mafuta na gesi,sera ya mafuta na gesi ipo na ndio iliyotumika kutoa leseni zilizopita,,pia akumbuke tuna ushindani wa kuvutia uwekezaji ktk sekta hii,kwani kwa sasa Afrika mashariki nzima nchi zipo ktk tafiti za mafuta na gesi,,tukichelewa itakula kwetu.,kwani ushindani ni mkubwa,Msumbiji washagundua zaidi ya 150 trillion cubic feet,,wakati sisi tumegundua 43 trillion cubic feet tu..TUKUMBUKE GESI NA MAFUTA UPATIKANA TU KULE YANAPOTAFUTWA.
You can't be serious. USD 100 tu, Mengi hawezi kukosa hicho kiasi. Hata kama ni zaidi, kwani kazi ya Wizara ya uwezeshaji ni nini? Iwawezeshe wazawa basi waweze kutafuta na kuvuna gesi.
 
With due respect to mzee mengi jee yeye anaufahamu mzuri kuhusu gesi?
Yeye ni mfanyabiashara mzalendo tu naye anamapungufu mengi tuu. mnakumbuka sakata la uuzwaji wa kilimanjaro hotel alipokosa tenda alinukisha kiasi kwamba wengi walifikiri kulikuwa na mnuso wa rushwa lakini baadaye somo lilieleweka kwani ilikuwa hadithi ya sungura kukosa zabibu.
 
Ninachokiona mimi hapa ni wajanja wachache wanataka wapewe hivyo vitalu halafu waviuze kwa wawekezaji. Hao ndiyo Watanzania ninaowajua mimi hasa wanaowekeza kwenye madini. Mengi si ana vitalu vingi vya madini, amefanya navyo nini?

Nadhani hiko ndio anachotaka disaini ya 'Bonite Bottles' kucheza na pesa ya wengine kwenye soko landani si vibaya. Hila sasa naona tamaa ya huyu babu imezidi hiyo hela ya kwenda kufanya exploration na kuchukua risk sidhani kama anayo hivi vitu vinafanywa na watu ambao wapo tayari kupoteza ma mia ya mamilioni bila ya kujutia.

Kwa bwana mengi labda apewe sehemu ambazo zimeshathibitishwa na zina estimated volumes kadhaa na ambazo zina faida ya kibiashara na hata huko pia yeye mwenyewe hawezi bila ya mkopo wa nje au aingie ubia na wawekezaji something that the government is doing kwa kukosa hela. Sasa yeye anachotaka ni kuingia kwa design ya mtanzania badala ya serikali inachofanya kwa ajili ya watanzania na afaidike yeye na K-Lyn.


Embu tuwe wakweli serikali ikimaliza matumizi ya ndani ya inampango wa kuuza nchi jirani mengi hataweza kushindana na serikali katika soko hili, wazungu wanaokuja ni makampuni makubwa na tayari wanamasoko yao, huyo mengi anaenda kuuza wapi ama soko lake liko wapi asipo ingia ubia na wazungu si ni kitu kile kile serikali inachofanya only this time na yeye hawemo kwenye ulaji.


Vitu ambavyo vinatuumiza kila siku tunaacha kuvijadili kwa kina na vyenye huwezekano wakutatuliwa na uongozi bora; with a little bit of creativity. Hila yakija maswala ambayo yako complicated ndio kila mtu anageuka expert ama kweli waafrika tunapenda makubwa na yaliyoiva si ajabu amna washabiki wa 'Wigan Athletic' kwenye bara la afrika wanini wale watu wanataka established clubs.
 
"An empty stomach, is not a good political adviser"
Albert einstein.
 
Back
Top Bottom