Mungu wangu! Siamini kama ile ni kondoa

mataka

JF-Expert Member
Feb 4, 2011
286
61
Jamani wana jf tembea uone, uangalie jinsi Tanzania ilivyo, nilibahatika kwenda kondoa miezi iliyopita hali ya uko hususan miundombinu ya barabara inatisha, mimi nilipanda basi la kondoa via kiteto, yani ile tunaiacha barabara ya kwenda makao makuu ya nchi na chama, barabara yote kuanzia hapo ni vumbi tupu na makorongo mbaya zaidi usafiri wa uko ni shida,watu wanabanana afadhali hata ya posta asubuhi, kwa kifupi wilaya nzima haina lami?

Lami uchwara inaonekana kwenye daraja lilojengwa enzi za mkoloni, naona kwa wakazi wa hapo ambao hawajawahi kutoka nje ya wilaya yao lami wanaionea hapo, huwezi kudhani kama hapo ndo makao makuu ya wilaya nyumba za polisi utadhani mabanda ya ng'ombe, benki wana moja tu NMB.

Kondoa jinsi ilivyo utadhani si mji wa kihistoria, manake una michoro ya mapangoni na mali kare kibao. Kwa kifupi kondoa ovyo.
 
Sikonge hata LAMI UCHWARA haipo na watu wanapangwa humo ndani kama meli ya kubeba Konteina.

Halafu basi lenyewe la Shakira unakuta hadi sakafu yake imetoboka chini na limepigwa welding kila kona.

Sisi sasa tusemeje? Ila wenyewe tulichagua November mwaka jana viongozi waliokuwepo waendelee.

Sasa leo tunamlilia nani? Utavuna ulichopanda. (Chini, SHAKIRA BUS upande wa kushoto).

attachment.php
 
Hiyo ndiyo faida ya Miaka 50 ya Uhuru ngoja wakazi wa Kondoa wafaidi matunda ya Uhuru. Kisha napenda kujua jimbo hilo safari hii linaongozwa na Mbunge wa Chama gani?. Kama bado ni wa CCM no comment hiyo ni halali yao.
 
Hiyo ya Kondoa ni picha tu nenda Kbondo ukaone ya dunia kuna basi la Mwarabu linatoka Kigoma hadi Kahama lenyewe tu ni vumbi linalotembea ukiwa ndani unaweza kuona hata matairi yanavyozunguka lakini bado linapakia binadamu,kwa maeneo ya Kondoa Babati au kanda ya kaskazini haliwezi kupakia hata ng`ombe sembuse binadamu, lakini linafanya kazi na polisi wanaliangalia tu.
 
Wee MATAKA inaonekana ni mgenii hapa nchini, au umekuwa mtoto wa mjini maana unashangaa. Unashangaa nini? WENZIO TUSHAZOEA, ,MIMI KAZINI KWANGU KILA MWAKA HUWA NINAPATA BAHATI YA KWENDA MIKOANI NA HUCHAGUA MKOA NIUTAKAO, KWA SASA NIMESHAONA MENGI NA NIMECHOKA. MAENEO MENGINE UKIBAHATIKA KUKUTANA NA MAJI YA MTO YANATIRIRIKA UNASEMA ALHAMDULIAHI, UNAPIGA MAGOTI UNAKUNYWA KAMA NG'OMBE, MAANA HUJUI UTAKUTANA NAYO WAPI, USAFIRI SAHAU, HATA KAMA UNA HELA ZAKO HAKUNA CHA KUKODI HATA BAISKELI HAKUNA, UNACHAPA KWA MGUU KILOMETA 30, NA KUENDELEA. SEMBUSE WEWE HUKO KUNA BASI JAPO NI UCHWARA.

KAZI NI KWAKO
 
Watu wa kondoa hawajui chama kingine zaidi ya CUF au CCM.Mimi nimesoma shule ya Miningani kama unaenda kondoa girls, darasani tulikua wakristu wawili tu.Shule nzima ilikuwa na wakristu wasiozidi 20.
itakuwa ni sababu maana hawa jamaa huwa hawana maono ni
 
AKondoa-Mjini+(26).jpg


Mheshimiwa Kikwete akimnadi mgombea ubunge Jimbo la Kondoa, Mheshimiwa Zubein Mhita baada ya kuhutubia mkutano mkubwa wa kampeni Kondo Mjini leo hii.

Maelfu ya wanachama wa CCM wamempa mapokezi makubwa Mwenyekiti wa CCM taifa na mgombea wa Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete Kondoa mjini alipowasili kufanya mkutano wa kampeni.



Mheshimiwa Kikwete alichukua muda mwingi wa hotuba yake kufafanua jitihada zitakazochukuliwa na CCM kama ikirudi kuongoza serikali kuhakikisha kuwa huduma bora ya afya inapatikana kwa kila Mtanzania. Alielezea ujenzi wa zahanati kila kata, utoaji wa vyandarua viwili kwa kila kaya, na jitihada za kuchanja wanawake bure kuzuia kansa ya shingo ya uzazi.



Kwa upande wa utoaji huduma ya maji, Mheshimiwa Kikwete alieleza kuwa vijiji 27 vya Kondoa Mjini vitapata maji ya uhakika kwa kupitia mpango mkubwa wa kusambaza maji kwa kushirikiana na Benki ya dunia. Mheshimiwa Kikwete alisema wilaya nyingi nchini mpango huu unashirikisha vijiji 10 hadi 15, lakini kwa kutambua ukubwa wa tatizo la maji Wilayani Kondoa ndipo maamuzi ya vijiji 27 yalifikiwa.



Mheshimiwa Kikwete pia alifafanua mafanikio yaliyopatikana kwenye upande wa elimu ya msingi na sekondari, sekta ya kilimo na mifugo, uwezeshwaji wa wananchi kiuchumi na ujenzi wa barabara.



Mwishoni Mheshimiwa Kikwete aliwanadi wagombea udiwani na ubunge na kuomba wananchi wachague CCM na wagombea wote kwa staili ya mafiga matatu.


 
AKondoa-Mjini+(26).jpg


Mwishoni Mheshimiwa Kikwete aliwanadi wagombea udiwani na ubunge na kuomba wananchi wachague CCM na wagombea wote kwa staili ya mafiga matatu.


Wananchi nao bila ya kuchanganya na ….zao, wakachagua kweli CCM!
 
kama ni sehemu ya historia wanarekebisha ya nini? maajabu ya kuandika ungeyapata wapi, hawa watu wanaogopa kenya isijesema na kwenyewe ni sehemu ya mali yao ya historia kwa kuwa binadamu wa kale alipatika pale, wakiboresha njia itakula kwetu, waache wabaki hivyo hivyo kama hifadhi ya taifa, isije haribiwa kama makumbusho sehemu ya hifadhi inakuwa ya burudani na uaribifu alafu unaita makumbusho!!! tunakmbuka nini pale kwenye starehe?
 
Sasa huyu mbunge wao mbona hata bungeni hasikiki akisema au kumbana magufuli atengeneze barabara ya dodoma-kondoa anapokea posho tu na kupiga uzingizi kweli wajinga ndio waliwao,hapo ndio unajiuliza kila mahali watu wamelogwa tu.
 
Jamani msipindishe kauli,hiyo barabara ni kipande cha international road ya RSA TO MISRI.na kipande kuanzia mtera hadi mazengo shule ya msingi{mean iringa road} na kipande cha kuanzia mwisho wa lami maili mbili hadi babati kupitia kondoa ndo hakina lami.

Na hela imeshatengwa na upembuzi yakinifu ulifanywa.katika bajet ya mwaka jana kama sio juzi,pesa yake ilitoka kwa pinde sana.
 
Jamani wana jf tembea uone, uangalie jinsi Tanzania ilivyo, nilibahatika kwenda kondoa miezi iliyopita hali ya uko hususan miundombinu ya barabara inatisha, mimi nilipanda basi la kondoa via kiteto, yani ile tunaiacha barabara ya kwenda makao makuu ya nchi na chama, barabara yote kuanzia hapo ni vumbi tupu na makorongo mbaya zaidi usafiri wa uko ni shida,watu wanabanana afadhali hata ya posta asubuhi, kwa kifupi wilaya nzima haina lami? Lami uchwara inaonekana kwenye daraja lilojengwa enzi za mkoloni, naona kwa wakazi wa hapo ambao hawajawahi kutoka nje ya wilaya yao lami wanaionea hapo, huwezi kudhani kama hapo ndo makao makuu ya wilaya nyumba za polisi utadhani mabanda ya ng'ombe, benki wana moja tu NMB.kondoa jinsi ilivyo utadhani si mji wa kihistoria, manake una michoro ya mapangoni na mali kare kibao. Kwa kifupi kondoa ovyo.

Sikonge hata LAMI UCHWARA haipo na watu wanapangwa humo ndani kama meli ya kubeba Konteina.

Halafu basi lenyewe la Shakira unakuta hadi sakafu yake imetoboka chini na limepigwa welding kila kona.

Sisi sasa tusemeje? Ila wenyewe tulichagua November mwaka jana viongozi waliokuwepo waendelee.

Sasa leo tunamlilia nani? Utavuna ulichopanda.

Hiyo ya Kondoa ni picha tu nenda Kbondo ukaone ya dunia kuna basi la Mwarabu linatoka Kigoma hadi Kahama lenyewe tu ni vumbi linalotembea ukiwa ndani unaweza kuona hata matairi yanavyozunguka lakini bado linapakia binadamu,kwa maeneo ya Kondoa Babati au kanda ya kaskazini haliwezi kupakia hata ng`ombe sembuse binadamu, lakini linafanya kazi na polisi wanaliangalia tu.

Wee MATAKA inaonekana ni mgenii hapa nchini, au umekuwa mtoto wa mjini maana unashangaa. Unashangaa nini? WENZIO TUSHAZOEA, ,MIMI KAZINI KWANGU KILA MWAKA HUWA NINAPATA BAHATI YA KWENDA MIKOANI NA HUCHAGUA MKOA NIUTAKAO, KWA SASA NIMESHAONA MENGI NA NIMECHOKA. MAENEO MENGINE UKIBAHATIKA KUKUTANA NA MAJI YA MTO YANATIRIRIKA UNASEMA ALHAMDULIAHI, UNAPIGA MAGOTI UNAKUNYWA KAMA NG'OMBE, MAANA HUJUI UTAKUTANA NAYO WAPI, USAFIRI SAHAU, HATA KAMA UNA HELA ZAKO HAKUNA CHA KUKODI HATA BAISKELI HAKUNA, UNACHAPA KWA MGUU KILOMETA 30, NA KUENDELEA. SEMBUSE WEWE HUKO KUNA BASI JAPO NI UCHWARA.

KAZI NI KWAKO

itakuwa ni sababu maana hawa jamaa huwa hawana maono ni

Wakuu simulizini zenu zimeniacha mbavu sina!!! Naona itabidi tuanzishe thread wachangiaji wawe wanatoa shuhuda za aina hii kutoka vijiji mbalimbali...
 
Katika nchi yetu hali za vijiji ni mbaya sana,unaongelea barabara peke yake nenda kwenye maswala ya maji huko utatoa machozi kwani mabomba yanatoa kutu na tope.mungu ibariki tanzania.
 
Katika nchi yetu hali za vijiji ni mbaya sana,unaongelea barabara peke yake nenda kwenye maswala ya maji huko utatoa machozi kwani mabomba yanatoa kutu na tope.mungu ibariki tanzania.
We hapo umependekeza kweli, mi nipo Kahama huku sasa shughuli zangu ziko vijijini hayo mnayosema ni ya kawaida.

Acha barabara hazina lami, Bomba watu hawalijui, huduma za afya hadi Kahama mjini. Kama wana mgonjwa mikokoteni ya ng'ombe inakesha na huko Kahama wanapiga kambi hospitali wanapika hapohapo. Vijiji kama Kawe, Ishiki, Budutu, Ufala, yaani huenda wanajua Nyerere bado rais.

Hali mbaya sana hata kama kuna njaa hakuna takwimu. Kuna kazi kubwa sana kuwaelimisha na serikali ina take advantage kutowafumbua macho ili iongoze kwa urahisi. Ila wkt Wa vita vya Uganda kila mji ulichangishwa ng'ombe mmoja eti mboga ya wanajeshi!

Sijui kama ilikuwa sera ya serikali au ufisadi ulifanyika. It's very sad talking about this.
 
Jamani wana jf tembea uone, uangalie jinsi Tanzania ilivyo, nilibahatika kwenda kondoa miezi iliyopita hali ya uko hususan miundombinu ya barabara inatisha, mimi nilipanda basi la kondoa via kiteto, yani ile tunaiacha barabara ya kwenda makao makuu ya nchi na chama, barabara yote kuanzia hapo ni vumbi tupu na makorongo mbaya zaidi usafiri wa uko ni shida,watu wanabanana afadhali hata ya posta asubuhi, kwa kifupi wilaya nzima haina lami? Lami uchwara inaonekana kwenye daraja lilojengwa enzi za mkoloni, naona kwa wakazi wa hapo ambao hawajawahi kutoka nje ya wilaya yao lami wanaionea hapo, huwezi kudhani kama hapo ndo makao makuu ya wilaya nyumba za polisi utadhani mabanda ya ng'ombe, benki wana moja tu NMB.kondoa jinsi ilivyo utadhani si mji wa kihistoria, manake una michoro ya mapangoni na mali kare kibao. Kwa kifupi kondoa ovyo.
kinachorudisha nyuma watu wa kondoa ni unafiki, udini, elimu duni na kumsikiliza mbunge mpumbavu na aliyelaaniwa kama zabein mhita

Ban me mods
 
Watu wa kondoa hawajui chama kingine zaidi ya CUF au CCM.

Mimi nimesoma shule ya Miningani kama unaenda kondoa girls, darasani tulikua wakristu wawili tu.
Shule nzima ilikuwa na wakristu wasiozidi 20.
kinachowaua warangi ni ile division ya udini inayopandwa na wachache.... imefikia hatua hata kama unapita tu kwennda babati au hata kiteto unaweza kuulizwa dini, ole wako useme mkristu

watakuacha hapohapo hata kama umepata matatizo
 
Sasa huyu mbunge wao mbona hata bungeni hasikiki akisema au kumbana magufuli atengeneze barabara ya dodoma-kondoa anapokea posho tu na kupiga uzingizi kweli wajinga ndio waliwao,hapo ndio unajiuliza kila mahali watu wamelogwa tu.
hivi unamjua vizuri huyu mama?
 
Pole sana kwa kuishi "Posta" miaka yote hiyo. Yanii ndo'umeanza leo kiijua nchi yako? Ukitoka huko pita na Makete, kibondo, chamwino, kantaramba, na kwingineko alafu ndo'uchukue hatua..
 
Back
Top Bottom