Mke wangu alifariki kama mwaka na nusu hivi umepita, alifariki kifo kibaya sana maana aliniachia mtoto mchanga wa wiki tatu. Baada ya kuhuzunika sana sikuwa na jinsi, nikamuomba Sister wangu ahamie kwangu ili maisha ya pale home yasisimame maana nina mtoto mwingine mkubwa kidogo. Yule mdogo alichukuliwa na Bibi yake.
Sasa sister kanigeuka yaani, amekuwa ni mtu wa kujiachia mno na maisha, bahati mbaya kazi zangu ni za kusafiri safiri sana sasa kila ninaporudi nyumbani ni kukarabati vitu tu maana hakuna usimamizi kabisa, mwanangu huyo mkubwa ni kama anajilea mwenyewe akifanya homework ni sawa asipofanya ni sawa pia! Muda mwingi sister anakuwa kazini na kwenye mishe mishe. Kila nikianzisha kaujenzi fulani pale home au chochote pesa inaishia kwenye castle lite tu sasa hata pesa nayotoa ya kula inaishia kwenye castle lite na viwanja, mtoto anakula 'kinachopatikana'.
Nikapata mwenzangu nikaanza kumshirikisha na maisha yangu, kama kununua chakula na kuwapelekea pale home au kama kuna ka project namtumia pesa awalipe mafundi sasa kumewaka moto! Sister anani mind ile mbaya na anazambaza maneno hasa kwa ndugu na jamaa, wamemchafua mno binti wa watu kuanzia kuambiwa mshirikina na mengineyo ila mimi, baba yangu na baadhi ya ndugu hatuuoni huo ubaya wake, nifanye nini waungwana wa JF? lengo langu ni kumuoa huyu binti na kujaribu kujenga upya familia yangu, hadi sasa sijaona kosa lake na anaonekana kumjali mtoto wangu(?).
Kwanza nakupa pole ya kuondokewa mkeo. Innalillahi wainailayhi rajuun. Mwenyezi Mungu atakufanyia wepesi inshaallah.
Suluhisho la hiyo shida yako ni kupata mwenzio mnayependana, kama hakuna mapenzi ni bora hata uajiri housegerl akutunzie mwanao. Huyo unayesema umepata ni ana mapenzi au anatafutia kwako cheti cha ndoa, kutumbua mali zako na haki ya kurithi? Angalia vizuri.