Kwa nini unafikiri jibu ni lazima liwe ama vitu vimeumbwa na Mungu, au vimetokea vyenyewe?
Umejiridhisha vipi kwamba majibu yapo humo tu?
Unaujua vipi mchakato wa cause and effect kwa anthropic bias inayokupa vantage point ambayo haikuoneshi vitu vya msingi?
Unajua kwamba dhana nzima ya "hiki kinaleta kile" ina makosa sana?
Vitu vyote ni vipi?
Unaelewa kwamba, kama "vitu vyote" vimetokea vyenyewe, au kama havijatokea vyenyewe, majibu yote yaanaonesha Mungu hahitajiki?
Soma hapa
Researchers demonstrate superpositions using a device comprising a single atom. Andrew Masterson reports.
cosmosmagazine.com
Kujibu swali lako.
Kama vimetokea vyenyewe, Mungu muumba vyote hahitajiki.
Kama havijatokea vyenyewe, na kila kilichopo kinahitaji muumba, hata Mungu mwenyewe naye atahitaji muumba na hivyo Mungu muumba vyote atakuwa hayupo.
Unaelewa kwamba jibu lolote nitakalokupa kwenye swali hilo halitatuonesha kwamba Mungu yupo au hata anahitajika kuwepo?
Unaelewa majibu yote hayo yanaonesha Mungu huyo hayupo?