Mungu haijui kesho yako

Mungu haijui kesho yako

Mwanadamu umepewa uwezo wa kuishinda dhambi,kiburi chako tu.
Dunia imewekwa kwenye kanuni Ili uishi vyema, maana kuishi ni ibada na kufa ni faida.
Amejuaje kama nitakuwa nina kiburi, je nikiamua kuacha kuwa na kiburi, bado tu nitatenda dhambi kisa ameshajua kwamba nitatenda dhambi?
 
Sababu wanaishi kwa kufuata Sheria na kanuni za MUNGU.
Ukifata kanuni za MUNGU yaani kuishi Maisha matakatifu ya utauwa huwezi kuwa na dhambi, dhambi zitakukimbia.
Kwanini wao wanafuata kanuni za Mungu ila sisi Duniani ndio hatufuati kanuni hizo, kwanini?
 
Amejuaje kama nitakuwa nina kiburi, je nikiamua kuacha kuwa na kiburi, bado tu nitatenda dhambi kisa ameshajua kwamba nitatenda dhambi?
Kiburi ni dhambi,dhambi ufanywa na mtu ambae ni mjinga.
 
Uko sahihi , Mungu anayeijua kesho Yako Hawezi kukupa mitihani

Ana kupaje mitihani wakati tayari anaijua kesho yako anajua kuwa utashindwa mitihani hiyo au utashinda ,

Kitendo Cha kukupa mitihani kina onyesha kwamba Hajui kuhusu kesho Yako Hana uhakika na hatima Yako

Itoshe kusema kwamba mungu ni Human made character tulipigwa
 
hoja dhaifu sana. Kesho ya Kila mtu huwa imepangwa na Mungu mwenyew tena Mungu humwazia mema kila mtu ila dhambi ndio hublock baraka bora za kesho ya mtu na kwakua ibilisi yuko against na mema Mungu anayowatakia watu wake. hutumia mlango wa dhambi kama kichocheo cha kublock baraka hizo kwakushawishi wanadamu kujiingiza huko. hakuna baya au zuri linalo mpata mtu kwa mpango wa mungu lile lisilo bora kwa huyo mtu. elewa sio kila jambo baya linalomtokea mtu Mungu anataka limpate
Kwahiyo mungu ana zidiwa maarifa /nguvu na shetani!?
 
Hapa wachague moja kati ya haya mawili

1.) Mungu kama anaijua kesho yetu maana yake ameshapanga kesho yetu, hivyo dhambi zote mtuhumiwa namba 1 ni yeye.

2.) Kama dhambi ni zetu, maana yake yeye hakupanga sisi tufanye dhambi bali ni uamuzi wetu sisi wenyewe, hivyo haijui kesho yetu.

Chagueni moja hapo
Huwa hawana hoja zenye logic wanaishia porojo tu

Mungu Yuko overrated, kwanza hayupo kabisa Kwa sababu maandiko yanayo elezea uwepo wa mungu na yanayo taja wasifu wake Yana contradiction nyingi , na Ukiya challenge Kwa maswali hayana majibu sahihi , so Hilo Lina dhihirisha kuwa mungu ni nadharia
 
Kwa hiyo mungu alikuwa anajua kesho ya Wana Ukraine kuwa watavamiwa na Russia

Na mungu muweza wa yote mwenye upendo wa yote akaamua Awaache tu wauwawe !?

Hahahaha huyu mungu wenu mnae muhubiri ni waajabu sana
 
Haimake Sense hata kidogoo! Maisha ya mwanadamu kila kinachotokea kina sababu na Mungu anajua sio kesho yako tu hata maisha yako yote hapa duniani mwanzo mpaka mwisho.
Kwhyo mtu akifa kwenye dhambi ni sir God alipanga kabisa amchome moto?
 
Ukimchunguza sana utamchukia.

Ukweli ni kwamba, ni lazima uupokee ufalme wa Mungu kama mtoto mdogo anavyopokea vitu, la si hivyo hautauingia.” Luka 18:17, Marko 10:15, maana alijua ukiupokea kama mtu mzima lazma utaanza kuhoji hizo contradictions

Mm naamin Mungu hajui kesho yangu ila anaweza kuhamua iweje.
 
Kama anajua kesho yako jiulize:
Kwann alimuumba shetani ilihali anajua atamsariti?
Kama alijua kesho ilikuwa akaweka mti wa mema na mabaya pale edeni ilihali anajua kuwa kesho Adam ataula?
Kama alijua kesho ya viumbe vyake Kwann aliruhusu nyoka awe ni mwelevu kuliko wanyama wengine ilihali alijua mwisho wake utakuwa mbaya Kwa kuwashawishi viumbe vyake kwenda kinyume na maagizo yake?
Kama alijua kesho Kwann alimuangusha shetan duniani ilihali alijua ata chafua viumbe vyake?
Kama anajua kesho yako bas hakuna haja au wokovu hauna maana tena. Maana ulipozaliwa tu yeye alijua ww ni WA motoni au peponi

Ama ni kweli anajua ila hana uwakika kama anajua kwaiyo anaamua aechi ili ajithibitishie ?
 
Haimake Sense hata kidogoo! Maisha ya mwanadamu kila kinachotokea kina sababu na Mungu anajua sio kesho yako tu hata maisha yako yote hapa duniani mwanzo mpaka mwisho.
Hiki ulichoandika hapa kinaaminiwa na wengi ila kina mkanganyiko sana.

Kama anajua kesho yangu kwa maana hiyo anajua kabisa kua kesho nitatenda kuua?
Na kama ni hivo ni ipi sababu ya mtu kuuawa ikiwa kuua ni dhambi? Kama alimpangia mtu atakufa kifo cha kuuawa si ni lazima auawe na mtu ambae alipangiwa kua ataua, sasa hapo dhambi ya kuua inakujaje??

Nadhani kuna sintofahamu hapa, kuna namna maandiko yametafsiliwa vibaya.
 
Unachosema ni kwamba binadamu hana uchaguzi, hayupo huru zaidi ya kufuata kilichopangwa jambo ambalo si kweli.

Mm nachoona hatufanyi mambo kwa sababu MUNGU amepanga ila MUNGU anajua tutakalofanya kutokana na tabia zetu za maamuzi na tamaa anayoiona ndani yetu.

Kama tu wewe unavyomtambua mwanao wa kiume kiasi kwamba unajua pamoja na kumuonya sana ila nikisafiri nikamuacha atavuta bangi. Wewe kujua kuwa atavuta bangi haimaanishi kuwa ulipanga avute bangi.
Nimekupata sana
 
  • Thanks
Reactions: Tsh
Ni ukweli ulio wazi ila ni ngumu kukubalika hasa kwa watu waliokaririshwa imani.

Iko hivi Mungu angekuwa anaijua kesho yako kusingekuwepo na kitu kinachoitwa dhambi, kwa sababu, mfano mtu amechinjwa hapo hakuna dhambi maana tayari mungu alishapanga utachinjwa au huo uovu unaoufanya sasa ungekuwa sio dhambi maana mungu alishapanga.

Njia unayoipitia ndiyo hatima ya maisha yako.

Kuna watu wanamtumikia Mungu mpaka wanazeeka na pia wapo wanamtumikia shetani mpaka wanazeeka.

Pia wapo walikuwa wanamtumikia Mungu ila hawajauona hata ujana.

Maisha ni kama simu tu utachagua uitumieje vile unaitumia ndiyo inakupa majibu unayoyataka wewe.
MPUMBAVU amesema moyoni mwake kuwa hakuna MUNGU.
 
Ni ukweli ulio wazi ila ni ngumu kukubalika hasa kwa watu waliokaririshwa imani.

Iko hivi Mungu angekuwa anaijua kesho yako kusingekuwepo na kitu kinachoitwa dhambi, kwa sababu, mfano mtu amechinjwa hapo hakuna dhambi maana tayari mungu alishapanga utachinjwa au huo uovu unaoufanya sasa ungekuwa sio dhambi maana mungu alishapanga.

Njia unayoipitia ndiyo hatima ya maisha yako.

Kuna watu wanamtumikia Mungu mpaka wanazeeka na pia wapo wanamtumikia shetani mpaka wanazeeka.

Pia wapo walikuwa wanamtumikia Mungu ila hawajauona hata ujana.

Maisha ni kama simu tu utachagua uitumieje vile unaitumia ndiyo inakupa majibu unayoyataka wewe.
Akili za new members hizi 🤣
 
Unachosema ni kwamba binadamu hana uchaguzi, hayupo huru zaidi ya kufuata kilichopangwa jambo ambalo si kweli.

Mm nachoona hatufanyi mambo kwa sababu MUNGU amepanga ila MUNGU anajua tutakalofanya kutokana na tabia zetu za maamuzi na tamaa anayoiona ndani yetu.

Kama tu wewe unavyomtambua mwanao wa kiume kiasi kwamba unajua pamoja na kumuonya sana ila nikisafiri nikamuacha atavuta bangi. Wewe kujua kuwa atavuta bangi haimaanishi kuwa ulipanga avute bangi.
Kwaiyo Mungu wenu Yuko Kama mwanadam? Ukiunda robot zumuni lako si lifanye kazi uliyo likusudia. lisipo fanya Kama ulivyo li program kosa sio la robot Ni lako wewe mtengenezaji
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom