Mungu haijui kesho yako

Mungu haijui kesho yako

Inamaanisha kuwa kitu dhaifu hakiwezi chambua kitu kisicho dhaifu na kuvumbua madhaifu ya kisicho dhaifu.

Mfano: unadhani wale mende chumbani kwako wanaweza kukaa na kujadili uwezo wako?
Kwa hiyo unamaanisha hujui?
 
Hapa wachague moja kati ya haya mawili

1.) Mungu kama anaijua kesho yetu maana yake ameshapanga kesho yetu, hivyo dhambi zote mtuhumiwa namba 1 ni yeye.

2.) Kama dhambi ni zetu, maana yake yeye hakupanga sisi tufanye dhambi bali ni uamuzi wetu sisi wenyewe, hivyo haijui kesho yetu.

Chagueni moja hapo
Mungu amempa binadamu uamuzi wa kufanya lolote alitakalo...
kuna tofauti sana kwa anayeleta hoja flani kwa kutaka kuelewa na mwngine kwa kuleta ubishani hawa ni watu tofauti ukweli unauelewa ila unaamua kuleta kubisha



chief ukweli ww unaujua ila unaleta hoja ili kuleta ubishani. kuna tofauti kubwa ya mtu kuleta hoja kwa kutaka kuelewa na kutaka kuleta ubishani

mithali 26:4 " usimjibu mpumbavu sawa sawa na upumbavu wake usije ukafanana nae, umjibu mpumbavu sawa sawa na upumbavu wake asije akawa mwenye hekima machoni pake"

hapa inategemea mpumbavu unae deal nae kuna ya kujibu pale anapohitaji kuelewa mtu kuna wa kukaa kimya pale anapohitaji tufanane kwa upumbavu
Aloo we mchungaji..taaaratibu punguza munkari jibu maswali🤣🤣🤣🤣
 
Ni ukweli ulio wazi ila ni ngumu kukubalika hasa kwa watu waliokaririshwa imani.

Iko hivi Mungu angekuwa anaijua kesho yako kusingekuwepo na kitu kinachoitwa dhambi, kwa sababu, mfano mtu amechinjwa hapo hakuna dhambi maana tayari mungu alishapanga utachinjwa au huo uovu unaoufanya sasa ungekuwa sio dhambi maana mungu alishapanga.

Njia unayoipitia ndiyo hatima ya maisha yako.

Kuna watu wanamtumikia Mungu mpaka wanazeeka na pia wapo wanamtumikia shetani mpaka wanazeeka.

Pia wapo walikuwa wanamtumikia Mungu ila hawajauona hata ujana.

Maisha ni kama simu tu utachagua uitumieje vile unaitumia ndiyo inakupa majibu unayoyataka wewe.
Hoja yako inaonyesha unataka ku-escape responsibilities zako na kumshutumu muumba wako. Alikupa akili na utashi vya kazi gani kama jukumu la kukuziwia wewe usifanye dhambi ni lake? Aliumba mwanadamu timamu mwenye kujua mema na mabaya na sio roboti wa kuongozwa kwa vibatani na vitufe. Mipango ya maisha yako ni wajibu wako, Mungu anahusika kwenye kuifanikisha mipango yako pale tu atakapoamua kumtafuta kwa moyo wako wote, akili zako zote na nguvu zako zote, ndivyo alivyoagiza tumtafute kwa namna hiyo. Mungu anafanya kazi pamoja na wampendao coz hao ndo watendao mapenz yake.

Mithali 16:9
"Moyo wa mtu huifikiri njia yake; Bali BWANA huziongoza hatua zake."

Proverbs 16:9
"A man's mind plans his way, but the Lord directs his steps and makes them sure."

Hivyo, mwenendo mbaya wa maisha yako ni matokeo ya matumizi ya mabaya ya akili ulzopewa, umeamua kuishi bora liende na madhara yanakupata sababu ya maamuzi na matendo yako, afu unataka Mungu awajibishwe, kweliiiiiii?

Mungu anaijua kesho yako coz anajua matokeo ya njia yoyote utakayoamua kuipita, Mungu ni wa utaratibu na kanuni na kila taratibu na kanuni zina matokeo yake.

Kumbukumbu la torati 11:26-28
26 Angalieni, nawawekea mbele yenu hivi leo baraka na laana;
27 baraka ni hapo mtakapoyasikiza maagizo ya BWANA, Mungu wenu, niwaagizayo leo;
28 na laana ni hapo msiposikiza maagizo ya BWANA, Mungu wenu, mkikengeuka katika njia niwaagizayo leo, kwa kuandama miungu mingine msiyoijua.

Ata ivo Mungu alipomuumba mwanadamu alimuweka duniani ili aitawale, hivyo tangu hapo Mungu hajiamuli mambo hovyo hovyo pasipo kushirikiana na mwanadamu.
Kasome stori ya Sodoma na Gomora, Mungu alimshirikisha Ibrahimu na wakabageini kimtindo ili Mungu asiangamize miji ile. Kipindi cha gharika, Nuhu alimshirikisha Nuhu.

Note: Kujua tabia ya Mungu na kwa nini anaruhusu maovu kuendelea kutokea, inabidi ukae karibu sana na NENO lake ujifunze kwa makini, yena ukiwa open minded.

Kwa kuhitimisha.
Mungu aliweka utaratibu wa maisha ambao mwanadamu anapaswa kuishi kwa kuufuata na alikua na matarajio ya sisi kuishi kwa utaratibu huo, LAKINI sisi ndio tumeasi na kumtenda dhambi Mungu, na tumeamua kuzifuata njia zetu wenyewe ambazo ni za mauti na majuto na maumivu.

Mithali 14:12
"Iko njia ionekanayo kuwa sawa machoni pa mtu, Lakini mwisho wake ni njia za mauti."

Kwa hiyo kutenda kwako dhambi ni UTASHI wako na kiburi chako na ujeuri wako wa kutotii maagizo ya Mungu. Iko wazi kabisa mshahara wa dhambi ni mauti.

Haya mabaya na maovu yanayoendelea na matokeo ya utashi wetu na matumizi ya akili zetu, na ubinafsi uliotujaa. Tumeamua kumtii shetani na haya ndo malipo yetu, bali kama tungeamua kumtii Mungu stori ingekua nyngne kabsa, coz nia ya Mungu kwa wanadamu inajulikana na nia ya shetani vivyo hivyo! Naomba kuwasilisha.
 
Sasa mbona ulikuwa unajadili tangu mwanzo
Najadili kile kilicho ndani ya capacity yetu. Ubongo wako na wangu hauna hadhi ya kujua kama MUNGU anaweza kujua jambo ambalo hujalifikiri kulifanya na kujiandaa kulifanya. Tutapiga porojo tu. Ila tunaweza kujadili kuhusu unalojiandaa kulitenda kuwa analijua hama halijui.
 
Title yako tu inaonesha usivyomjua Mungu. Ni bora ungekiri kuwa Mungu hayupo kuliko kukirinuwspo wake kisha ukamshusha uwezo wake!! Mungu anajua yaliyopita, yaliyopo na yajayo (Omniscient). Utambuzi wa Mungu hauna mipaka!
Jibu kwa kutetea hoja ili na wengine wajifunze
Unabadilisha Nini wakati kasha panga ukitoka kanisani unaenda kwa mchepuko? Je tunaweza kumshangaza Mungu kwa kutenda Jambo ambalo yeye hakulipanga? Kama jibu Ni ndio Basi hajui Kila kitu na Kama jibu Ni hapana Basi huna utakacho badilisha iwe kwa kwenda kanisani au msikitini
Unabadilisha Nini wakati kasha panga ukitoka kanisani unaenda kwa mchepuko? Je tunaweza kumshangaza Mungu kwa kutenda Jambo ambalo yeye hakulipanga? Kama jibu Ni ndio Basi hajui Kila kitu na Kama jibu Ni hapana Basi huna utakacho badilisha iwe kwa kwenda kanisani au msikitini
Umemjibu vizuri sana asante kwa kuniasidia kujibu
 
Ni ukweli ulio wazi ila ni ngumu kukubalika hasa kwa watu waliokaririshwa imani.

Iko hivi Mungu angekuwa anaijua kesho yako kusingekuwepo na kitu kinachoitwa dhambi, kwa sababu, mfano mtu amechinjwa hapo hakuna dhambi maana tayari mungu alishapanga utachinjwa au huo uovu unaoufanya sasa ungekuwa sio dhambi maana mungu alishapanga.

Njia unayoipitia ndiyo hatima ya maisha yako.

Kuna watu wanamtumikia Mungu mpaka wanazeeka na pia wapo wanamtumikia shetani mpaka wanazeeka.

Pia wapo walikuwa wanamtumikia Mungu ila hawajauona hata ujana.

Maisha ni kama simu tu utachagua uitumieje vile unaitumia ndiyo inakupa majibu unayoyataka wewe.
Uko sahihi kabisa!! sibishi hapo ukijua wazi kuwa huyo ni mungu wako pekee!! na hao mnao muabudu km weye!! na ni wazi kuwa (miungu ni wengi sana Humu Duniani) leo mpaka kesho inategemea wewe umeamuaje!!

Mfano kuna miungu Baal, Olympio gods, OSLIS nk!...kwa uchache ni makosa ya akili/kutokujua ku generalise mungu wako na Mungu wa wengine! ambaye kamwe kwa hali hii hutamjua!

Lkn Mungu wangu bana! mie amenipa full autonomy nina uwezo wa kuumba km yeye! na nimeumbwa kwa mfano wake!! amenipa uchaguzi wa kuua au nisiue.........kutegemea na nature ya kosa ilivyo;

Kwa mfano Mungu wa Musa kwa kutoa na kumpa maelekezo Musa! aliua wanajeshi kibao wa Misri...paleee Bahari ya sham mpaka leo panaitwa RED SEA KM Hujui sababu kuuubwa ya bahari hii kuitwa ivo ndo hii!!......

kwa mfano mwingine wakoma walipokuwa na uwezo wa Mungu waliwashinda/ua ....Washami........Lkn kumbuka hata Cain kwa uwezo wa shetani alifanikiwa kumuua mdogowe Abel ......

lkn cain muovu aliishi na kuzaa mitoto kibao.....na kizazi hiko kipo wapi kwa siku hizi unadhani?? nakupa home work!

Je unajua kizazi cha cain leo hii ni kipi???.........
 
Uko sahihi kabisa!! sibishi hapo ukijua wazi kuwa huyo ni mungu wako pekee!! na hao mnao muabudu km weye!! na ni wazi kuwa (miungu ni wengi sana Humu Duniani) leo mpaka kesho inategemea wewe umeamuaje!!

Mfano kuna miungu Baal, Olympio gods, OSLIS nk!...kwa uchache ni makosa ya akili/kutokujua ku generalise mungu wako na Mungu wa wengine! ambaye kamwe kwa hali hii hutamjua!

Lkn Mungu wangu bana! mie amenipa full autonomy nina uwezo wa kuumba km yeye! na nimeumbwa kwa mfano wake!! amenipa uchaguzi wa kuua au nisiue.........kutegemea na nature ya kosa ilivyo;

Kwa mfano Mungu wa Musa kwa kutoa na kumpa maelekezo Musa! aliua wanajeshi kibao wa Misri...paleee Bahari ya sham mpaka leo panaitwa RED SEA KM Hujui sababu kuuubwa ya bahari hii kuitwa ivo ndo hii!!......

kwa mfano mwingine wakoma walipokuwa na uwezo wa Mungu waliwashinda/ua ....Washami........Lkn kumbuka hata Cain kwa uwezo wa shetani alifanikiwa kumuua mdogowe Abel ......

lkn cain muovu aliishi na kuzaa mitoto kibao.....na kizazi hiko kipo wapi kwa siku hizi unadhani?? nakupa home work!

Je unajua kizazi cha cain leo hii ni kipi???.........
Kwanza Kuna ushahidi wowote unao dhibitisha pasi na kuacha Shaka yoyote kwamba Cain aliwahi kuwepo duniani.
 
Kwanza Kuna ushahidi wowote unao dhibitisha pasi na kuacha Shaka yoyote kwamba Cain aliwahi kuwepo duniani.
Looool! km hujui jambo dogo nmana huyu?? hivi/....... kamwe hutanielewa Maisha yako yoooote !! naongea na kilaza wa imani bin kizazi cha nyoka!...wapi na wapi!....... nyie bana neno haliwahusu!! hata tuwapige nyundo za utosini!

Jambo dooogo hivi ??? uliza mambo makubwa makubwa!
 
Neno linasema,"Nalikujua wewe tangu tumboni mwa mama yako"

Kabla hujazaliwa, ashajua huyu ni wa motoni
Over.
 
Hii mada ngumu sana. Nadhani tuongelee tu katiba mpya ya Chama Cha Mbowe maana hapa hatutapata majibu.
 
God is not limited to TIME..kumtaja na kumuhusisha Mungu na time (KESHO)..tayari ni mchanganyiko
 
Dhambi ni uasi dhidi ya Mungu na atendae dhambi ni wa ibilisi.
Bila shetani hakuna Mungu, ili Mungu awe valid lazima shetani awepo na ndiyo maana wafia dini wote Kila siku ni shetani tu!
 
Mungu niurumie Sana na unifanye kuwa na hofu juu yako Wala nisije kukukosea
Amina
 
Ni ukweli ulio wazi ila ni ngumu kukubalika hasa kwa watu waliokaririshwa imani.

Iko hivi Mungu angekuwa anaijua kesho yako kusingekuwepo na kitu kinachoitwa dhambi, kwa sababu, mfano mtu amechinjwa hapo hakuna dhambi maana tayari mungu alishapanga utachinjwa au huo uovu unaoufanya sasa ungekuwa sio dhambi maana mungu alishapanga.

Njia unayoipitia ndiyo hatima ya maisha yako.

Kuna watu wanamtumikia Mungu mpaka wanazeeka na pia wapo wanamtumikia shetani mpaka wanazeeka.

Pia wapo walikuwa wanamtumikia Mungu ila hawajauona hata ujana.

Maisha ni kama simu tu utachagua uitumieje vile unaitumia ndiyo inakupa majibu unayoyataka wewe.
Mungu ameumbwa na binadamu, ndo maana ha-make sense.

Mungu ni mjumuisho tu wa falsafa mbalimbali za binadamu wa kale ambao walikuwa nyuma kisayansi kulinganisha na leo.
 
Looool! km hujui jambo dogo nmana huyu?? hivi/....... kamwe hutanielewa Maisha yako yoooote !! naongea na kilaza wa imani bin kizazi cha nyoka!...wapi na wapi!....... nyie bana neno haliwahusu!! hata tuwapige nyundo za utosini!

Jambo dooogo hivi ??? uliza mambo makubwa makubwa!
Badala ya kujibu ulichoulzwa unatoa maelezo meengi yasiyo na maana
 
Badala ya kujibu ulichoulzwa unatoa maelezo meengi yasiyo na maana
Akili kubwa kamwe haiwezi kamatwa na akili kisoda!! daima hamuelewagi! tunalijua hilo kitambo sana!! hapo hkn maelezo mengi!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom