Mungu haijui kesho yako

Mungu haijui kesho yako

Hapana. Ishu ni kwamba anaziona njia zako, matendo yako, maamuzi yako, mfumo wa moyo wako na matamanio yake hivyo yeye kujua kuwa utabadilika au kuacha unachokifanya ni rahisi, huwezi kumfanyia suprice., mwisho wako anaujua.

Ni kama vile wewe unaangalia movie ambayo ulishaiona, unajua kabisa kitakachotokea sio kwa sababu umekifanya kitokee au umepanga ila ni kwa sababu unajua kitatokea sababu una uzoefu wa hiyo filamu.

Sasa MUNGU anaona matamanio ya moyo wako na anajua matokeo ya hayo matamanio siku zote ni nini kitafuata maana matendo ya binadamu ni yale yale tu hakuna jipya ambalo litakuwa suprice.
Kwa hiyo jinsi moyo wangu unavyokuwa na matamanio yake mimi ndio naamua huo moyo uwe hivyo ama mungu ndio huamua moyo wako uwe hivi ama vile?
 
Hoja yangu ni kwamba kama mungu anajua ya kesho yako au maisha yako yatakavyokuwa hapa duniani basi hakuna haja ya kwepo kwa dhambi maana alishajua kwamba wewe utakuwa mizi

Na pia kama mungu anajua kesho yako basi

Bado hujanielewa vizuri ni hivi inamaana tunawaambia wattoto wetu wawe na bidii masomoni ili iweje, kama ni mungu alipanga mwanangu atakua mwalimu basi akae tu nyumbani
Pia tunawalea watoto wetu kwa maadili mazuri ili iweje maana mungu alishapanga kwamba atakuwa mwema, mtoto umleavyo ndio akuavyo mungu hapo anahusikaje
Kwahiyo wale panya roads hawakulelewa vizuri na wazazi wao?

Usilolijua ni usiku wa giza.
 
Kwa hiyo jinsi moyo wangu unavyokuwa na matamanio yake mimi ndio naamua huo moyo uwe hivyo ama mungu ndio huamua moyo wako uwe hivi ama vile?
Ni training yako mwenyewe. Kama vile unavyotaka mwili wako uwe na misuli wenye afya au ujae sumu za sigara, shisha bangi. Ts all about you. Ni mwili wako, moyo wako, roho yako.
 
Na kama uwezo wa kutuzuia anao ila anaamua kutuacha maana yake anafanya uovu, kitaalam tunaita ‘Sadism’, yaani ni Sadist, ana-enjoy kuona mateso ya wengine, otherwise why uruhusu na unao uwezo wa kuzuia?
Acheni upumbavu, mbona hukanyagi moto ukuunguze mguu ilihali uwezo wa kuukanyaga unao?

Au mbona hujipeleki huko vitani Ukraine ukafe nakati uwezo wa kwenda unao?

Au kwanini hujilazi kwenye reli ili treni ikija ipite nawe ufe nakati una uwezo huo?
 
Ni training yako mwenyewe. Kama vile unavyotaka mwili wako uwe na misuli wenye afya au ujae sumu za sigara, shisha bangi. Ts all about you. Ni mwili wako, moyo wako, roho yako.
Ok kwa hiyo mimi ndio nikaamua moyo wangu uwe vipi kutokana na training yangu, so sio mungu anayeamua moyo wangu uwe na tamaa fulani, na sio mungu anayeamua wala kujua future yangu iwe vipi, sio?
 
Ni ukweli ulio wazi ila ni ngumu kukubalika hasa kwa watu waliokaririshwa imani,

Iko hivi Mungu angekuwa anaijua kesho yako kusingekuwepo na kitu kinachoitwa dhambi, kwa sababu, mfano mtu amechinjwa hapo hakuna dhambi maana tayari mungu alishapanga utachinjwa au huo uovu unaoufanya sasa ungekuwa sio dhambi maana mungu alishapanga.

Njia unayoipitia ndiyo hatima ya maisha yako.

Kuna watu wanamtumikia Mungu mpaka wanazeeka na pia wapo wanamtumikia shetani mpaka wanazeeka.

Pia wapo walikuwa wanamtumikia Mungu ila hawajauona hata ujana

Maisha ni kama simu tu utachagua uitumieje vile unaitumia ndiyo inakupa majibu unayoyataka wewe
Mimi kuna issue flani nimezinote watu wenye roho mbaya, makatili na washenzi ndio naona wanafanikiwa huku duniani kuliko watu wema sijui hizi hesabu zimekaaje
mwenye uelewa afafanue. Mimi ni mtu wa dini pia naamini Mungu yupo
 
Changamoto za maisha zinawafanya watu wakufuru
 
Ok kwa hiyo mimi ndio nikaamua moyo wangu uwe vipi kutokana na training yangu, so sio mungu anayeamua moyo wangu uwe na tamaa fulani, na sio mungu anayeamua wala kujua future yangu iwe vipi, sio?
Sasa unachanganya. Kuna tofauti ya kujua future yako na kuamua future yako. Anayeamua future yako ni wewe ila iyo future MUNGU anaijua kutokana na maamuzi yako na mambo yanayoumba matamanio yako ndani yako.

Kama wewe binadamu ukimuona binti anatamani kutembea na kila mwanaume unajua kabisa huyu ataishia kupata mimba na ukimwi yeye MUNGU ambaye anawatazama binadamu vizazi na vizazi atashindwaje kujua matokeo ya maamuzi yako? Kuna jambo gani jipya utakalofanya asijue litakapokupeleka? Kama anauwezo wa kuona ndani mawazo ya matamanio yako anashindwa vipi kujua huyu kutokana na hii tamaa atafanya nn?
 
Sasa unachanganya. Kuna tofauti ya kujua future yako na kuamua future yako. Anayeamua future yako ni wewe ila iyo future MUNGU anaijua kutokana na maamuzi yako na mambo yanayoumba matamanio yako ndani yako.

Kama wewe binadamu ukimuona binti anatamani kutembea na kila mwanaume unajua kabisa huyu ataishia kupata mimba na ukimwi yeye MUNGU ambaye anawatazama binadamu vizazi na vizazi atashindwaje kujua matokeo ya maamuzi yako? Kuna jambo gani jipya utakalofanya asijue litakapokupeleka? Kama anauwezo wa kuona ndani mawazo ya matamanio yako anashindwa vipi kujua huyu kutokana na hii tamaa atafanya nn?
Kwa hiyo kama hiyo future yangu naamua mimi, so Mungu anajua nitakachoamua kabla hata sijaamua?
 
Yani hata usipoenda jua ndivyo ilivyopangwaaa 😀 😀 usidhani kwamba ukienda sijui kuna mpango utaubadilisha hapana ndo maana unaweza toka kanisani na still ukagongwa na gari ukafa... haubadilishi kitu ila hivyo ndivyo ilivyoandikwa juu ya maisha yako zaidi ukienda Kanisani unatengeneza maisha yako baada ya kifo.
maisha baada ya kifo unayatengenezaje wakati nayo pia yashapangwa
 
Mbona mnatumia nguvu nyingi kutuaminisha Mungu hayupo? Kama shetani yupo basi MUNGU YUPO! kama umeamua Mungu hayupo sio lazima utushirikishe.


Kumb 30:19 ''Nazishuhudiza mbingu na nchi juu yenu hivi leo, kuwa nimekuwekea mbele yako uzima na mauti, baraka na laana; basi chagua uzima, ili uwe hai, wewe na uzao wako;''
 
Mimi kuna issue flani nimezinote watu wenye roho mbaya, makatili na washenzi ndio naona wanafanikiwa huku duniani kuliko watu wema sijui hizi hesabu zimekaaje
mwenye uelewa afafanue. Mimi ni mtu wa dini pia naamini Mungu yupo
Kwa mimi mafanikio ni kuwa na amani ya roho, tena sihitaji mijumba ya kifahari, mali wala mipesa mingi maana naona karibu asimilia kubwa ya vyanzo vya uovu ni ukwasi, kama ilivyokuwa kwa Mfalme Suleiman alipoomba hekima akazidishiwa na utajiri.

Matokeo yake uliyaona hadi mwishowe Mfalme Suleiman alikuwa na Michepuko tele, alimwasi Mungu na alikiri kuwa "yote ni ubatili mtupu bila ya kumcha Mungu"
 
Kwa hiyo kama hiyo future yangu naamua mimi, so Mungu anajua nitakachoamua kabla hata sijaamua?
Ni kama wewe unavyojua hili gari litakula mafuta kiasi fulani hata kabla hujaliendesha kwa sababu unafahamu mfumo wa cc zake na matokeo ya kuendesha gari lenye hizo cc.

MUNGU nae anaangalia matamanio yako anajua utakapoelekea. Hakunaga suprice katika maamuzi, lolote utakalolifanya palikuwa na maandalizi, yale maandalizi ndiyo MUNGU huyaona, ukijiandaa kughairi au kubadilika anaona unavyojiandaa kabla hata hujabadilika.
 
Ni kama wewe unavyojua hili gari litakula mafuta kiasi fulani hata kabla hujaliendesha kwa sababu unafahamu mfumo wa cc zake na matokeo ya kuendesha gari lenye hizo cc.

MUNGU nae anaangalia matamanio yako anajua utakapoelekea. Hakunaga suprice katika maamuzi, lolote utakalolifanya palikuwa na maandalizi, yale maandalizi ndiyo MUNGU huyaona, ukijiandaa kughairi au kubadilika anaona unavyojiandaa kabla hata hujabadilika.
Lakini hilo gari linakua limeundwa hivyo ili kula hizo CC kwa umbali kadhaa, kwa hiyo unasema hata moyo wa mtu kuwa na matamanio fulani ni mungu anakua ameumba hivyo tangia mwanzo?
 
Lakini hilo gari linakua limeundwa hivyo ili kula hizo CC kwa umbali kadhaa, kwa hiyo unasema hata moyo wa mtu kuwa na matamanio fulani ni mungu anakua ameumba hivyo tangia mwanzo?
Hilo gari limeundwa ni mashine halina utambuzi, nimelitumia tu kama mfano uone katika kipengele cha kufahamu jambo kutokana na sifa za hilo jambo. Sifa za cc kubwa ni kula mafuta sijaongelea uhusika wa uumbaji wake.

Binadamu ana uhuru wa kuchagua ila chaguzi zina maandalizi. MUNGU anayaona maandalizi ndipo anajua utakachokifanya.
 
Unachosema ni kwamba binadamu hana uchaguzi, hayupo huru zaidi ya kufuata kilichopangwa jambo ambalo si kweli.

Mm nachoona hatufanyi mambo kwa sababu MUNGU amepanga ila MUNGU anajua tutakalofanya kutokana na tabia zetu za maamuzi na tamaa anayoiona ndani yetu.

Kama tu wewe unavyomtambua mwanao wa kiume kiasi kwamba unajua pamoja na kumuonya sana ila nikisafiri nikamuacha atavuta bangi. Wewe kujua kuwa atavuta bangi haimaanishi kuwa ulipanga avute bangi.
Uwezo wa mungu usiulinganishe na WA Binadamu.
 
  • Thanks
Reactions: Tsh

Similar Discussions

Back
Top Bottom