Mungu anaangalia roho sio mavazi, Makanisa muwaachie dada zetu kuwa huru kuvaa wanavyotaka, hata vipensi ni mavazi, tunachoangalia ni roho

sky soldier

JF-Expert Member
Mar 30, 2020
5,408
19,033
1696423607932.png


Hapo zamani nilishuhudia kwa macho yangu makanisa yalikuwa na tabia za ajabu kuwavisha kanga wanawake waliokuja wamevaa sketi zilizobana kwa mbali, waliovaa suruali hata ziwe pana walifukuzwa kabisa kurudi nyumbani.

Tunashukuru kadri muda umeenda makanisa yamejitambua, Leo hii wanawake wanaruhusiwa hata kuvaa suruali, gauni zinazowachoresha ili wapendeze, gauni zenye uwazi wa kupitisha hewa vifuani na mgongoni, n.k.

Kero kubwa ipo kwa makanisa kujitungia sheria za kukataza vimini na vipensi, huu ni ubaguzi !! Wadada wavae wanavyotaka, makanisa yasiingilie.

Sheria za agano la kale zilishapitwa na wakati,
-sheria za aina ya mavazi na makatazo ya kuchonga nywele zilishapitwa na wakati leo hii karibu kila mkristo anachonga nywele
  • sheria za vyakula zilishapitwa na wakati kuna uhuru wa kula kitimoto.
  • Sheria za kukataza kusuka nywele zilishapitwa na wakati leo hii makanisani ruksa kuvaa mawigi, kusuka rasta, weaving, n.k.
 
Warumi 12:1-2. Soma hilo Andiko na omba Mungu akufunulie. Uondoshe hii Roho ya shetani iliyoleta Mada hii.
Agano la kale lilipitwa na wakati, tupo agano jipya, tunakula hata kitimoto kilizokatazwa kwenye sheria za agano la kale.

Wadada wavae wanavyotaka, makanisa yasiingilie
 
Hapo zamani makanisa yalikuwa na tabia za ajabu kuwafukuza ama kuwavisha kanga wanawake waliothubutu hata kuvaa suruali za pana kufanyia mazoezi...
Unasali ndugu yangu?

1 Wakorintho 6:19.

*Au hamjui ya kuwa mwili wenu ni hekalu la Roho Mtakatifu aliye ndani yenu, Mliepewa na Mungu? Wala Si Mali yenu wenyewe.
 
Wavae vizuri.

Mavazi ni indicator au (yaliyomo) moyoni. Wengine wanavaa bila kujua aliyempa wazo la kuvaa ni pepo ili apoze watu kiroho.

Naunga mkono wanaowavalisha khanga. Ila walitakiwa wote wakusanywe wapelekwe kwenye chumba maalum cha maombi na kufunguliwa.

Wachukuliwe kama magonjwa mahututi wanaohitaji msaada wa haraka.
 
Mwanamke aliyevaa kikahaba anaweza zini na wanaume 500 kwa siku moja na kuwatia dhambini wote.
Kila mwanaume aliyemtamani tayari amekwisha zini nae.
 
Ni wapi wameandika mavazi ?
Ulisema kinacho angaliwa ni Roho. Nami nimekupa hilo fungu.

Kuhusu Mavazi.

1 Timotheo 2:9-10.

9 Vivyo hivyo wanawake na wajipambe kwa mavazi ya kujisitiri, pamoja na adabu nzuri, na moyo wa kiasi; si kwa kusuka nywele, wala kwa dhahabu na lulu, wala kwa nguo za thamani;
10 bali kwa matendo mema, kama iwapasavyo wanawake wanaoukiri uchaji wa Mungu.
 
Back
Top Bottom