Upendo Furaha Peneza
Member
- Aug 7, 2014
- 8
- 95
Wengi mtakuwa mlisikia juu ya ajali mbaya niliyopata mimi na makamanda wengine watatu tukielekea kwenye mkutano wa hadhara, Geita. Ni moja ya ajali mbaya kiasi kwamba kila mtu akiona gari lilivyoharibika hakuna anayeamini kuna aliyebaki salama.
Namshukuru Mungu sana aliyesikia maombi yetu tulipomlilia tangu gari lilipoacha njia. NI HAKIKA MUNGU ALIKUWEPO NDANI YA GARI LILE NA MUNGU AMETENDA MUUJIZA.
Nawashukuru sana kwa dua na maombi yenu tuko hai na tunaendelea vizuri sana.
Lengo langu kwa leo sio kuiongelea ajari ile, ninachokusudia kusema ni kwamba kama ajari ile ingeniua, kuna mambo mengi ya msingi ambayo yangehairishwa kufanywa. La msingi kuliko vyote nisijamtumikia Mungu vya Kutosha na utoaji wa elimu ya uraia, sijafanya kwa kiwango cha kukata kiu yangu.
Ninacholenga kuongelea hapa ni juu ya kukomboa wakati na kufanya kazi kana kwamba hatutapata muda mwingine tena,kutokuhairisha mambo kwa visingizio visivyo vya msingi maana kesho yaweza kuwa sio yako. Kama tungeunganisha muda wote tunaopoteza kwa visingizio dhaifu tungegundau nusu ya maisha yetu tumepoteza bila kazi za msingi.
Namshukuru Mungu kwa ulinzi wake na kunipa nafasi nyingine,namwahidi kumtumikia kwa nguvu zaidi,Namwomba Mungu kunijalia hekima na maarifa kutumikia watu wake wa dunia hii kwa uadilifu.
Namwahidi Mungu kuendeleza kukemea maovu yanayotendeka na kuwaelimisha watanzania wenzangu juu ya haki na wajibu wao na mimi kujielimisha mwenyewe kwa bidii.
Natoa wito kwenu rafiki zangu tusiwe wavivu,tusiweke matumaini yetu kwa kesho, linalowezekana leo lisingoje kesho.
Nawashukuru sana kwa maombi yenu na salamu za pole nilizopata kwa njia ya simu, Jamii forums, Facebook na njia zinginezo.
Ndugu zangu mmenionesha upendo mkubwa sana, mbarikiwe wote kwa kujali sana. Mmeigusa roho yangu kwa namna ya pekee; Nimejiona napendwa.
Mungu awabariki sana na awape furaha katika maisha yenu.
Mbarikiwe sana,
Upendo Furaha Peneza
Namshukuru Mungu sana aliyesikia maombi yetu tulipomlilia tangu gari lilipoacha njia. NI HAKIKA MUNGU ALIKUWEPO NDANI YA GARI LILE NA MUNGU AMETENDA MUUJIZA.
Nawashukuru sana kwa dua na maombi yenu tuko hai na tunaendelea vizuri sana.
Lengo langu kwa leo sio kuiongelea ajari ile, ninachokusudia kusema ni kwamba kama ajari ile ingeniua, kuna mambo mengi ya msingi ambayo yangehairishwa kufanywa. La msingi kuliko vyote nisijamtumikia Mungu vya Kutosha na utoaji wa elimu ya uraia, sijafanya kwa kiwango cha kukata kiu yangu.
Ninacholenga kuongelea hapa ni juu ya kukomboa wakati na kufanya kazi kana kwamba hatutapata muda mwingine tena,kutokuhairisha mambo kwa visingizio visivyo vya msingi maana kesho yaweza kuwa sio yako. Kama tungeunganisha muda wote tunaopoteza kwa visingizio dhaifu tungegundau nusu ya maisha yetu tumepoteza bila kazi za msingi.
Namshukuru Mungu kwa ulinzi wake na kunipa nafasi nyingine,namwahidi kumtumikia kwa nguvu zaidi,Namwomba Mungu kunijalia hekima na maarifa kutumikia watu wake wa dunia hii kwa uadilifu.
Namwahidi Mungu kuendeleza kukemea maovu yanayotendeka na kuwaelimisha watanzania wenzangu juu ya haki na wajibu wao na mimi kujielimisha mwenyewe kwa bidii.
Natoa wito kwenu rafiki zangu tusiwe wavivu,tusiweke matumaini yetu kwa kesho, linalowezekana leo lisingoje kesho.
Nawashukuru sana kwa maombi yenu na salamu za pole nilizopata kwa njia ya simu, Jamii forums, Facebook na njia zinginezo.
Ndugu zangu mmenionesha upendo mkubwa sana, mbarikiwe wote kwa kujali sana. Mmeigusa roho yangu kwa namna ya pekee; Nimejiona napendwa.
Mungu awabariki sana na awape furaha katika maisha yenu.
Mbarikiwe sana,
Upendo Furaha Peneza