Mume wangu amempa mimba mdogo wangu

Mume wangu amempa mimba mdogo wangu

Kosa unalo dada, Kwanza ulisahau Mdogo wako ni mwanamke Kama wewe, hukufunga milango Kwa kidingizio cha undugu, hapo umekosa.
Pili baada ya kosa kutokea umelipeleka kwa Watu wengi ungetulia wewe na Mume wako Kwanza muongee na wakati huo mdogo wako akiwa ameondoka kwenu. Hata hivyo nikushauri, Huyo bado ni Mume wako na wewe ni mke wake, panda teremka Mwisho mrudishe kaaeni wawili myamalize, msamehe Mumeo,huyo Mdogo wako ni nyoka achana Naye kabisaaa hakuhusu, Chora msitari

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ilaaa huyu c ndo yule mdada aliyeanzisha uzi wa kuwapoteza familia yake ikiwemo Baba Mama na mdogo wake alivyokuwa wanaenda kweny harusi ya mdgo wake?

Sent using Jamii Forums mobile app

Sijui ndo kamroga amuue mdogo wake???

Kumbe kwenye gari wako na wazazi wake familia nzima. Nawaza tu kwa sauti
 
Katika baadhi ya makabila hapa Tanzania na Afrika kuna utamaduni ambapo ndugu wa mwanaume anaweza kupewa jukumu la kuzaa na mke wa ndugu yake ili kuokoa jahazi hasa wanapokuwa wamekaa muda mrefu bila kupata mtoto. Mfano huu nimeuweka ili ujaribu kuchuja kama upo katika mazingira hayo ingekuwaje?

Je huwezi kuichukulia in a positive way? Japo it hurts a lot!
 
Dada fanya maisha yako, mdogo wako sio tatizo. Tatizo ni hilo janaume lisilo na busara, fukuza huyo janaume bwege. Kaa na mdogo wako mtunze mdogo wako na muonyeshe upendo wote ka ujumla msamehe huyo ni damu yako hata ufanyeje huyo atabaki kuwa nduguyo. Ila ukiolewa tena mdogo wako mtafutie maisha yake usikae nae tena. Yangu ni hayo tu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nimejaribu kusoma kisa chao ila nimebaini kuwa...uamuzi umeshaufanya (utaki kuishi na uyo mwanaume tena na wala utaki kumuona) kwa mtazamo wangu ilo ni wazo zuri sana uwezi kuwa na kidonda alafu ukamruhusu inzi akifyize atasababisha upate kansa ( mm nakuunga mkono tu)

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Thread yako mpya umesema umepoteza ndugu zako walipata ajari ya Noah.. means na huyo mdogo wako aliyekuchukulia mume nae ni R.I.P pole sana
 
Thread yako mpya umesema umepoteza ndugu zako walipata ajari ya Noah.. means na huyo mdogo wako aliyekuchukulia mume nae ni R.I.P pole sana

Ameshaulizwa kwenye uzi huu na kujibu swali lako.

Tunasubiri updatenya kujua mtoto alizaliwa na mchumba wa mdogo wake alikuwa nani.. kwa sababu kaandika leo aliachana na mumewe.
 
Habari za asubuhi wanajamvi,

Nimekuwa kwenye wakati mgumu kwa muda sasa.

Nimeolewa na Nina miaka miwili kwenye ndoa lakn sikuwa tayari kuzaa kwakuwa tulikubaliana mpaka nimalizie masomo yangu ya masters ambayo natarajia kumaliza mwaka huu.

Tumekuwa tunaishi vizuri tu na mume wangu nikimtii na kuwajibika kwa majukumu yangu yote kama mke kwa mumewe pamoja kuwa Ninafanya kazi na kusoma pia.

Mimi ni muajiriwa lkn mume wangu wangu ni mfanyabiashara kariakoo.

Nina mdogo wangu ambaye aligraduate mwaka jana akaomba akae kwangu wakati anatafuta kazi, sikuona shida nikamkubalia.

Tangu aje tumekuwa tukiishi vizuri tena kwa amani.

Kama Dada nilijitahidi kumtengea mdogo wangu bajeti yake toka kwenye mshahara wangu kwa kila mwenzi iliaweze kumudu kufuatilia mambo yake kirahisi.

Baada yakuwa nae kwa miaezi mitano nikaanza kuona mabadiriko kadhaa.
Akawa karibu na mume wangu sana, sikujali nikajua ni ushemeji tu.

Siku moja nilirudi nyumbani mapema sikukuta mtu.

Nikaendelea na maandalizi ya chakula cha jioni, nikiwa jikoni nikasikia sauti ya mume wangu na mdogo wangu wanabishana.

Niliposogea dirishani nisikilize vizuri huku nikichungulia nje nikaona dogo analia na mume wangu anambembeleza huku akimfuta machozi.

Nikatulia nione nini kinaendelea, nikasikia mume wangu anamwambia itabidi tuitoe maana Dada yako akijua wote tutakuwa nawakati mgumu..

Nikachukua simu yangu nikawa nawarekodi, baada ya muda wakaingia ndani nami nikajifanya sijui chchte.

Sikuwauliza chchte nikijipa muda wa kufanya utafiti zaidi.

Baada ya wiki, mdogo wangu akaniambia kuwa ana shida na Mimi.

Nikamsikiliza akaniambia kuwa ana mimba..

Sikuhamaki wala kuonyesha kama najua chchte, nilimuulize nani muhusika akajibu hajui.

Nikamwambia kama hujui sina namna ya kukusaidia siku ukijua utaniambia nijue jinsi ya kukusaidia.

Akaanza kulia na kunipigia magoti huku akisema nisamehe Dada, nikamwambia wala hujanikosea.

Nikamwambia wewe ni mtu mzima umeamua kuzaa kunashida gani?

Baba wa mtoto naamini yupo kwahiyo sikuhukumu.

Akasema, kuna jambo nataka nikwambie..
Niikamwambie aniambie..
Akasema lakini naomba unisamehe, shemeji ndo amenipa mimba.

Kwakweli niliumia sana, nikamuuliza wana muda gani tangu waanze mahusiano akajibu ni miezi minne sikujibu neno, nikaendelea na shughuli zangu.

Mume wangu alikuwa matembezi, aliporudi nikawaita wote wawili, nikamwambie Dogo aseme alichoniambia mbele ya shemeji yake.

Akasema tena ana mimba ya shemeji yake..mume wangu kusikia vile akataka kuwa mkali..

Nikamwambia hana haja ya kufoka, nikanyamaza sikusema wala kulaumu chchte.

Nikaamua kuwaita wazazi wangu na wake pia bila wao kujua,

Walipo kuja nikawambie Mimi ndiye niliyewaita lkn mume wangu na mdogo wangu ndiyo wanachakuwaambia.

Walipoulizwa wanasemaje dogo akaeleza kuwa anamimba ya shemeji yake..

Mume wangu alipoulizwa kwa unyonge sana alikubali. Wazazi wakaniuliza Nina maamuzi gani?
Nikawajibu nimeamua kumuachia mume mdogo wangu.

Wazazi wakanisihi nimsamehe na tuendelea na maisha ya ndoa..na dogo arudi kwa wazazi.

Niliwakatalia nakuwambia kuwa nisingeweza kuvumilia ndoa ya aina Ile..nikamwambia wasijipotezee muda wao kuniambia cha kufanya niliwaita waje wasikie uchafu niliofanyiwa then baada ya hapo mimi ndo nitoe maamuzi
Nilisisitiza maamuzi yangu nikutoendelea na ndoa tena.

Waliniambia nisichukue uamuzi bila kutafakari wakanipa wiki tatu za kufikiria Leo hii ni siku ya nane tangu nipewe muda wa kutafakari..

Niliwaomba niwe mbali na watuhumiwa wangu kipindi cha kutafakari.

Nikawasihisi watuhumiwa wao ndo wanipishe nyumbani kwangu, maana tunapoishi ni kwangu.

Wameondoka na sijui walipo kwenda.

Binafsi sijisikii kuendelea kuishi na huyu mwanaume ingawa kweli tumeshafunga ndoa lkn siwezi kuwa na raha ya ndoa ktk mazingira kama haya.

Najiuliza heshima yangu iko wapi?

Jamii inanionaje?

Na mtoto atayezaliwa ntamuonaje?

Naona dhambi hii ni kubwa sana siwezi kuibeba.

Wadau naomba msaada maamuzi niliyochukua naweza kuwa sahihi? Nisaidie plz.

Naomba plz sihitaji matusi wala mizaha nahitaji ushauri na faraja.

Naamini ktk wingi wamashauri hapakosi hekima.
Pole.Kazi ipo.
 
Pamoja na kwamba hii imeshatokea, napenda kutoa ushauri kwa wanawake mlioamua kuolewa timizeni wajibu wenu kwa waume zenu!
Biblia inasema Mungu ameumba jambo jipya duniani, mwanamke atakuwa mlinzi wa mumewe.
Nitoe maana chache za mwanamke kumlinda mwanamume,
1) Ni lazima mwanamke adhibiti dalili yoyote inayoashiria mumewe kutoka nje ya ndoa. "Mdharau mwiba mguu humwota tende"
2) Mpatie mumeo kila apendacho kwa ufanisi wa hali ya juu, kama ni chakula mwulize anapendelea nini halafu kiandae mwenyewe kwa ubora wa hali ya juu kwa uwezo wako wote maana huyo ndiye mumeo,
Kama ni penzi mpatie kila anapohitaji hadi aridhike mwenyewe. Ukimnyima au ukimbania ujue kuna siku atatafuta mbadala na atapatiwa anachohitaji kwa ubora anaotaka. Ndiyo maana Mungu amesema" MSINYIMANE isipokuwa MMEPATANA kwa muda ili mpate faragha kwa kusali"
Mwanamke usiamue mambo peke yako bila kuridhiana/kukubaliana na mumeo.

USHAURI WANGU:

1) Msamehe mumeo, huyo ni mume tu sio rahisi kihivyo kumuacha mumeo. Ukumbuke kuwa kuna wanaume wengine wanatembea hadi na mama wakwe zao! Sembuse kutembea na shemeji yake! Lkn hawajagundulika tu. Na baadhi wamegundulika. (Siombei itokee tena kwa yeyote) Leo mumeo katembea na mdogo wako, umeita wazazi, je angetembea na mama mkwe wake ungemwita nani?
Au unauhakika gani endapo utaachana na huyu, yule atakayekuoa hatakuwa zaidi ya huyu?
Narudia nakushauri msamehe mumeo, umpende zaidi na use naye karibu zaidi,maisha yataendelea.
2) Mdogo wako mshauri asitoe mimba(asiue) kumbuka hiyo ni kazi ya mikono ya Mungu, isiharibiwe na mtu yeyote. Mtoto akizaliwe mpende kama watoto wako utakaozaa.
3) Jitahidi kumpendeza mumeo kwa uwezo wako wote, usiseme moyoni mwako "hata nisipomtimizia matakwa yake atavumilia" kumbuka wanaume ni wepesi wa kutafuta alternative ways when they encounter an obstacle! Ndiyo maana ukifuatilia sababu kubwa ya wanaume wengi kuwa na nyumba ndogo ni "KUNYIMWA TENDO LA NDOA NA WAKE ZAO WA NDOA" . Wanawake wengi hudhani wanawakomoa/wanawaadhibu waume zao kuwanyima tendo la ndoa lkn kumbe wanatengeneza mwanya wa mambo mabaya zaidi.




Sent using Jamii Forums mobile app
 
Duh,pole sana mamii.imba mungu akupe hekima,busara na mpya as nisamehe.ili uweze kuwa na amani na hao watu.wasamehe ktk roho na kweli hata km hutarudiana na mumeo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom