Mume wangu amempa mimba mdogo wangu

Mume wangu amempa mimba mdogo wangu

Kwakweli pole sana kwa hayo yaliyotokea inauma sana tena kwa plan zenu ambazo mmepanga kwa ajili ya maisha yenu alafu shetani anakuja na kuvuruga.kiukweli kwa wakristo uzinzi wa aina yoyote unavunja ndoa vinginevo muhusika uamue kusamehe na yeye muhusika Mme aonyeshe jitiada za pekee.kuanzia kwa wazazi viongozi wa kiroho na wapatanishi wengine wanaoweza kulimaliza.pole sana.
 
pole binti yangu. Kwa majaribu ya ulimwengu huu.

Mimi nina maneno machache ya kuchangia, juu ya jambo lako. Mosi katika maelezo yako ulieleza kwamba mlikubaliana na mwenza wako kwamba utabeba ujauzito baada ya kumalizia masomo yako.

Swali:
je! Mumeo Aliridhia kwa dhati kabisa kutoka moyoni mwake! Au ulilazimisha?

Pili:
katika jitihada zako za kutumikia mabwana wawili yaani mume na masomo. Niyupi ulikuwa unampa muda zaidi? Mume au masomo?

Nakuuliza maswali haya mawili kutokana na kwamba kwa mujibu wa maelezo yako katika mambo hayo mawili ndipo palipo zalisha tatizo binti yangu.

Nitarudi baada ya kunijibu
Asante.
MKUU, MASWALI YAKO YOTE HAYAHALALISHI MUME KUZAA NA SHEMEJIYE NA WALA HAYATAKATISHI KITENDO OVU ALICHOTENDA HUYO JAMAA HATA KIKANG'AA KAMA THELUJI. NI SAWA NA KUHANGAIKA KUIFUA KANIKI KWA JIK UKIDHANI ITANG'AA KAMA PAMBA. NEVER!
 
Kuna watu wanaachana then wanaanza kujutia maamuzi yao ikiwa too late. Ndoa sio uboyfriend/girlfriend kuwa mnaachana tu na tusione watu wanasherekea aniversaries tunahisi mambo ni mteremko humo ndani kuna mtu amesacrifice na kufight hard to keep the marriage(in most cases wamama.)Leah2 msamehe mume wako onesha ukomavu. Ndoa ni kusamehe over and over bila kuhesabu na kulipiza
funny enough, kuna watu humu ndani wanaona siye tunaosema samehe hatujaona ukubwa wa kosa alofanyiwa.
haiko hivyo ila tunaangalia hatma ya uamuzi atakao chukua.

nakupa mfano mdogo sana a sister of mine alikuwaga na mchumba, siku moja akamkuta mdogo wake tuko na huyo mchumba wake chumban kwa huyo mchumba wake wanapiga story. sister akakasirika sana akaona mdogo wake kamchukulia mchumba alicall off ule uchumba akasema nitapata mwingine wewe sio mwaminifu.

mama yangu mzazi alimwambia dada samehe usiachane na mchumba wako kwasabb kama hiyo, tena huyu dada alipakaza ukoo mzima mdogo wake kamchukulia bwana. huyu dada hakusikia ushauri wa mtu na alijua ukiachana na huyu utapata yule. miaka ikaenda yule bwana akatafuta mwanamke mwingine akaoa, mdogo mtu akaolewa na yeye yaani sister hadi leo hajaolewa. vilipomshinda akaamua kuzaa na mwanaume kwa ahadi ya kufunga ndoa baadae. miaka imepita mtoto sasa ni ten years hakuna ndoa mtu miaka ishafika 45. sasa mie huwaga najiuli pengine yule alomtolea mahari ndo alikuwa mume halisi wa sister. leo hii kamaliza makanisa dar yote akaiomba aoane na baba wa huyu mtoto na bado Mungu hajaruhusu. kuna mengi sana nyuma ya hili la leah2.

nataka kumwambia akiona Mungu kampa jaribu kama hili ajue anataka kumpromote kwenye daraja la juu kabisa inabidi yeye akae aangalie kusudi la Mungu katika hili na sio makusudi ya kibinaadamu. sisi sote tutakuwa wafariji wataabishaji kwake ila amtazame Mungu neema yake bado ipo na inamwita. naamini kipo Mungu alichomuandalia huyu dada ila ibilisi hataki lile kusudi litimie ndani yake.
 
MKUU, MASWALI YAKO YOTE HAYAHALALISHI MUME KUZAA NA SHEMEJIYE NA WALA HAYATAKATISHI KITENDO OVU ALICHOTENDA HUYO JAMAA HATA KIKANG'AA KAMA THELUJI. NI SAWA NA KUHANGAIKA KUIFUA KANIKI KWA JIK UKIDHANI ITANG'JJ KAMA PAMBA. NEVER!
muda mwingine yatupasa kujiuliza hivi tunaposhauri tunashauri ili kuponya mtu, ama tunashauri kishabiki ili kuumiza watu. tukiamua kuwa mahakimu basi je siye tu wasafi zaid na sana kuliko huyu mume wa leah2 ama nikutaka tu tuonekane kwa miandiko yetu kwamba tuko sawa ilihali mioyoni mwetu hatuko hivi.

Biblia inasema hivi ajionavyo mtu nafsini mwake ndivyo alivyo, na tuna kitabu cha yoshua bin sira kikasema usitie chumvi kwa jambo lolote iwe kwa heri ama shari na wala usipate kuitwa adui badala ya mpatanish.

Mwimba zaburi alisema heri wapatanish maana wao watamwona Bwana.

nimesema hayo yote nikiwa na lengo moja tu simaanish mimi ni mpatanish ila naangalia je ni jamii gani ambayo sisi tunataka kuijenga. Hivi tunataka kuwa na jamii yenye visasi na vinyongo ama jamii yenye kuheshimiana na kuchukuliana mizigo? ikiwa Kristo alisamehe na kutuchukulia mizigo kila leo iweje sisi tusimame kifua mbele tuone huu mzigo wa mume wa leah2 ni mkubwa sana hauchukuliki?

Je umewaza hatma ya mpasuko wa kifamilia ambao utatokea kwa akina leah2? je umejiuliza vipi familia ya mume wa leah2 itamchukuliaje mtoto atakayezaliwa? unaonaje kama leah2 akiweza kuyatatua kwa namna ambayo hata yeye mwenyewe haitampa mzigo nafsini na siku moja atajikuta kuwa na amani maisha yake yote kwa uamuzi huo?
 
Suala hili ni gumu, lina social psychology impacts kwa dada and mdogo mtu, jamii iwazungukayo na familia zote mbili ya mume na mke. Kwa kuwa huyo dada hajazaa mtoto katika hii familia, ni bora akafunga ukurasa wa hii ndoa akaondoka. Maana akizaa na huyo mume na watoto itakuwa shida ya kudumu baadae. Bora wigo wa tatizo uishie hapo ulipofikia. rahisi kusahau haya baada ya muda. chukulia tu as a broken relationship tu na songa Mbele.
Husisahau kuangalia na mapungufu yako binafsi yaliyopelelea haya kutokea ili utakapopata familia yasije kukupata haya tena.
 
muda mwingine yatupasa kujiuliza hivi tunaposhauri tunashauri ili kuponya mtu, ama tunashauri kishabiki ili kuumiza watu. tukiamua kuwa mahakimu basi je siye tu wasafi zaid na sana kuliko huyu mume wa leah2 ama nikutaka tu tuonekane kwa miandiko yetu kwamba tuko sawa ilihali mioyoni mwetu hatuko hivi.

Biblia inasema hivi ajionavyo mtu nafsini mwake ndivyo alivyo, na tuna kitabu cha yoshua bin sira kikasema usitie chumvi kwa jambo lolote iwe kwa heri ama shari na wala usipate kuitwa adui badala ya mpatanish.

Mwimba zaburi alisema heri wapatanish maana wao watamwona Bwana.

nimesema hayo yote nikiwa na lengo moja tu simaanish mimi ni mpatanish ila naangalia je ni jamii gani ambayo sisi tunataka kuijenga. Hivi tunataka kuwa na jamii yenye visasi na vinyongo ama jamii yenye kuheshimiana na kuchukuliana mizigo? ikiwa Kristo alisamehe na kutuchukulia mizigo kila leo iweje sisi tusimame kifua mbele tuone huu mzigo wa mume wa leah2 ni mkubwa sana hauchukuliki?

Je umewaza hatma ya mpasuko wa kifamilia ambao utatokea kwa akina leah2? je umejiuliza vipi familia ya mume wa leah2 itamchukuliaje mtoto atakayezaliwa? unaonaje kama leah2 akiweza kuyatatua kwa namna ambayo hata yeye mwenyewe haitampa mzigo nafsini na siku moja atajikuta kuwa na amani maisha yake yote kwa uamuzi huo?
Nafikiri mpaka sasa Leah atakua kaamua kuendelea Na ndoa ama la!Ila naona kama zigo hili unataka kumtwisha Leah kana kwamba yeye ndo mharibifu.
Kwamba mtoto atakayezaliwa familia zitamwonaje? Hao wanzinzi ndo wanapaswa kujiuliza hayo maswali baada ya uzinifu wao,Na uasherati wao kwamba hivi huyu mtoto itakuwaje?pia wao ndo wameleta mpasuko kwenye hizi familia Na si Leah!
Huyu Dada si wakulaumiwa yaani watu wafanye yao then lawama ije kwake? ambaye ameamua kuchukua uamuzi wake!!
Umetolea mfano Wa dadako aliyemwacha mchumba ake kisa maongezi tu Na shemejie huo mf aise haufanani Na huu hata kidogo,mdogo wako kupewa mimba Na mmeo si Jambo jepesi hata kidogo ni zito linahitaji hekima Na Upendo kama Wa Yesu maumivu yake ni makubwa mno.
 
Nafikiri mpaka sasa Leah atakua kaamua kuendelea Na ndoa ama la!Ila naona kama zigo hili unataka kumtwisha Leah kana kwamba yeye ndo mharibifu.
Kwamba mtoto atakayezaliwa familia zitamwonaje? Hao wanzinzi ndo wanapaswa kujiuliza hayo maswali baada ya uzinifu wao,Na uasherati wao kwamba hivi huyu mtoto itakuwaje?pia wao ndo wameleta mpasuko kwenye hizi familia Na si Leah!
Huyu Dada si wakulaumiwa yaani watu wafanye yao then lawama ije kwake? ambaye ameamua kuchukua uamuzi wake!!
Umetolea mfano Wa dadako aliyemwacha mchumba ake kisa maongezi tu Na shemejie huo mf aise haufanani Na huu hata kidogo,mdogo wako kupewa mimba Na mmeo si Jambo jepesi hata kidogo ni zito linahitaji hekima Na Upendo kama Wa Yesu maumivu yake ni makubwa mno.
sina maana ya kumtwisha leah mzigo la hasha.
ila unajua kwenye ndoa tunaoana wawili ili kukamilishana only that. ikiwa mimi ni udhaifu sehem fulan basi mwenzangu ananikamilisha kwa namna fulan.
mume wake kakosea tena sana lakin je yeye kama mke hawez kurekebisha makosa yao? ni wazi kwamba utaona kwann yeye arekebishe makosa ya mtu baki na si wakosaji kujirekebisha. mie ninatofautiana hapo.
makosa ya mwenzi wangu mimi nitayarekebisha na pia yakwangu yeye atayarekebisha na katika kurekebishana tutaonyana na kusaidiana kuchukuliana manake mwisho wa siku tunataka tuone maisha kwetu yanasonga mbele na si kurudi nyuma.
sikatai uamuzi atakao chukua manake hiyo ni yeye mwenyewe lakin pia sishadadii sisi kutumika kujenga jamii iliyo ya vinyongo na visasi. ilimchukua mtu mmoja kuponya taifa zima Daudi aliponya Israel yote tena mahali ambapo hata Sauli hakutegemea sembuse huyu kuponya familia yake??
kwan kusamehe anatwishwa mzigo gani hasa mkubwa? hivi umewah kujiuliza athari za kutokusamehe? nijuavyo mimi kutokusamehe ni mzigo kuliko kusamehe. na kusamehe kunafungua mlango usoutegemea katika maisha yako.
 
...japo inawezekana sana, Leah alitumia nguvu bila maridhiano kwa kutaka kusoma kwanza ndipo abebe ujauzito, and that didn't go down very well with he hubby. Haya mambo yanahitaji maridhiano na makubaliano ya kweli, uwazi na kuwa na busara. Kwa sisi tulio ndani ya ndoa, mkishaoana tu, mara nyingi na wengi wetu tunahitaji kuanza kuwa na familia(watoto), hivyo kama Leah alifanya yote bila maridhiano na maelewano, part of the fault should be hers.

Hata hivyo, mbona wengi wanabeba ujauzito na bado wanachukua masters degree, PhD etc? Najua degree ya kwanza ndio kidogo ina shida, lakini hizi zingine mtu unaweza kusoma na kubeba mimba/kulea. Alikubali kuolewa, akubali kuwa mama, hamna namna.
 
Dah... pole sana ila chanzo cha haya yote ni wewe

ubize uliokuw nao plus mdgo wako ni msichana mdogo ambae hana kazi yupo tu nyumbani hata kama ingekuwa mimi!

Tulia muombe sana Mungu ila mi nakushaur huna chako hapo mapenzi ni sumu hao wataendelea kugegedana hata ukiwasamehe.... ila watabadilisha mfumo utakaokufanya usijue kabisa.... tafuta njia nyingine ya maisha yako using'anie siti yenye msumari kwa kisingizio cha kuwa dirishani... Asante
 
sina maana ya kumtwisha leah mzigo la hasha.
ila unajua kwenye ndoa tunaoana wawili ili kukamilishana only that. ikiwa mimi ni udhaifu sehem fulan basi mwenzangu ananikamilisha kwa namna fulan.
mume wake kakosea tena sana lakin je yeye kama mke hawez kurekebisha makosa yao? ni wazi kwamba utaona kwann yeye arekebishe makosa ya mtu baki na si wakosaji kujirekebisha. mie ninatofautiana hapo.
makosa ya mwenzi wangu mimi nitayarekebisha na pia yakwangu yeye atayarekebisha na katika kurekebishana tutaonyana na kusaidiana kuchukuliana manake mwisho wa siku tunataka tuone maisha kwetu yanasonga mbele na si kurudi nyuma.
sikatai uamuzi atakao chukua manake hiyo ni yeye mwenyewe lakin pia sishadadii sisi kutumika kujenga jamii iliyo ya vinyongo na visasi. ilimchukua mtu mmoja kuponya taifa zima Daudi aliponya Israel yote tena mahali ambapo hata Sauli hakutegemea sembuse huyu kuponya familia yake??
kwan kusamehe anatwishwa mzigo gani hasa mkubwa? hivi umewah kujiuliza athari za kutokusamehe? nijuavyo mimi kutokusamehe ni mzigo kuliko kusamehe. na kusamehe kunafungua mlango usoutegemea katika maisha yako.
Kumwucha huyo bwana haina maana kua asisamehe, awasamehe mme Na mdogo mtu then asonge mbele.
Laiti Leah angekua Na watoto kwa huyu mme hata mie ningemshauri ajikaze aendelee kuishi kwa ajili ya watoto sasa hakuna bora amwachie mdogo wake
Wao waendele kulea mtoto Na kujenga familia yao.
Gfsonwin pia bora mmewe hii Hali angekua anaijutia pia nakuona kua kafanya Jambo sio Lakini bwana huyu kakauka kauuu hata neno samahani/ nisamehe Mke wangu hakuna
Sasa unajiuliza hata ukimsamehe mtu kama huyu Na kuendelea nae si majanga??
Hata Yesu huwasamehe watu watubuo kwa kumanisha Na kunyenyekea kwake sio mtu hana time yupo yupo tu anasamehewa.
Huyu bwana hajaonyesha jitihada zozote kwa maelezo ya Leah ili kuokoa ndoa yake yeye anaona poa tu hapo ndo nauona ugumu wakuendelea Na mtu wanamna hii.
 
Habari za asubuhi wanajamvi,

Nimekuwa kwenye wakati mgumu kwa muda sasa.

Nimeolewa na Nina miaka miwili kwenye ndoa lakn sikuwa tayari kuzaa kwakuwa tulikubaliana mpaka nimalizie masomo yangu ya masters ambayo natarajia kumaliza mwaka huu.

Tumekuwa tunaishi vizuri tu na mume wangu nikimtii na kuwajibika kwa majukumu yangu yote kama mke kwa mumewe pamoja kuwa Ninafanya kazi na kusoma pia.

Mimi ni muajiriwa lkn mume wangu wangu ni mfanyabiashara kariakoo.

Nina mdogo wangu ambaye aligraduate mwaka jana akaomba akae kwangu wakati anatafuta kazi, sikuona shida nikamkubalia.

Tangu aje tumekuwa tukiishi vizuri tena kwa amani.

Kama Dada nilijitahidi kumtengea mdogo wangu bajeti yake toka kwenye mshahara wangu kwa kila mwenzi iliaweze kumudu kufuatilia mambo yake kirahisi.

Baada yakuwa nae kwa miaezi mitano nikaanza kuona mabadiriko kadhaa.
Akawa karibu na mume wangu sana, sikujali nikajua ni ushemeji tu.

Siku moja nilirudi nyumbani mapema sikukuta mtu.

Nikaendelea na maandalizi ya chakula cha jioni, nikiwa jikoni nikasikia sauti ya mume wangu na mdogo wangu wanabishana.

Niliposogea dirishani nisikilize vizuri huku nikichungulia nje nikaona dogo analia na mume wangu anambembeleza huku akimfuta machozi.

Nikatulia nione nini kinaendelea, nikasikia mume wangu anamwambia itabidi tuitoe maana Dada yako akijua wote tutakuwa nawakati mgumu..

Nikachukua simu yangu nikawa nawarekodi, baada ya muda wakaingia ndani nami nikajifanya sijui chchte.

Sikuwauliza chchte nikijipa muda wa kufanya utafiti zaidi.

Baada ya wiki, mdogo wangu akaniambia kuwa ana shida na Mimi.

Nikamsikiliza akaniambia kuwa ana mimba..

Sikuhamaki wala kuonyesha kama najua chchte, nilimuulize nani muhusika akajibu hajui.

Nikamwambia kama hujui sina namna ya kukusaidia siku ukijua utaniambia nijue jinsi ya kukusaidia.

Akaanza kulia na kunipigia magoti huku akisema nisamehe Dada, nikamwambia wala hujanikosea.

Nikamwambia wewe ni mtu mzima umeamua kuzaa kunashida gani?

Baba wa mtoto naamini yupo kwahiyo sikuhukumu.

Akasema, kuna jambo nataka nikwambie..
Niikamwambie aniambie..
Akasema lakini naomba unisamehe, shemeji ndo amenipa mimba.

Kwakweli niliumia sana, nikamuuliza wana muda gani tangu waanze mahusiano akajibu ni miezi minne sikujibu neno, nikaendelea na shughuli zangu.

Mume wangu alikuwa matembezi, aliporudi nikawaita wote wawili, nikamwambie Dogo aseme alichoniambia mbele ya shemeji yake.

Akasema tena ana mimba ya shemeji yake..mume wangu kusikia vile akataka kuwa mkali..

Nikamwambia hana haja ya kufoka, nikanyamaza sikusema wala kulaumu chchte.

Nikaamua kuwaita wazazi wangu na wake pia bila wao kujua,

Walipo kuja nikawambie Mimi ndiye niliyewaita lkn mume wangu na mdogo wangu ndiyo wanachakuwaambia.

Walipoulizwa wanasemaje dogo akaeleza kuwa anamimba ya shemeji yake..

Mume wangu alipoulizwa kwa unyonge sana alikubali. Wazazi wakaniuliza Nina maamuzi gani?
Nikawajibu nimeamua kumuachia mume mdogo wangu.

Wazazi wakanisihi nimsamehe na tuendelea na maisha ya ndoa..na dogo arudi kwa wazazi.

Niliwakatalia nakuwambia kuwa nisingeweza kuvumilia ndoa ya aina Ile..nikamwambia wasijipotezee muda wao kuniambia cha kufanya niliwaita waje wasikie uchafu niliofanyiwa then baada ya hapo mimi ndo nitoe maamuzi
Nilisisitiza maamuzi yangu nikutoendelea na ndoa tena.

Waliniambia nisichukue uamuzi bila kutafakari wakanipa wiki tatu za kufikiria Leo hii ni siku ya nane tangu nipewe muda wa kutafakari..

Niliwaomba niwe mbali na watuhumiwa wangu kipindi cha kutafakari.

Nikawasihisi watuhumiwa wao ndo wanipishe nyumbani kwangu, maana tunapoishi ni kwangu.

Wameondoka na sijui walipo kwenda.

Binafsi sijisikii kuendelea kuishi na huyu mwanaume ingawa kweli tumeshafunga ndoa lkn siwezi kuwa na raha ya ndoa ktk mazingira kama haya.

Najiuliza heshima yangu iko wapi?

Jamii inanionaje?

Na mtoto atayezaliwa ntamuonaje?

Naona dhambi hii ni kubwa sana siwezi kuibeba.

Wadau naomba msaada maamuzi niliyochukua naweza kuwa sahihi? Nisaidie plz.

Naomba plz sihitaji matusi wala mizaha nahitaji ushauri na faraja.

Naamini ktk wingi wamashauri hapakosi hekima.
Kama solution nikuacha utaacha wanaume wengi Wenzio wanakomaa
 
Pagumu hapo. Pole. Kuna maswali ya kujiuliza..Je, wakiishi pamoja uko tayari kumuita huyo mumeo shemeji? Mumeo alijuta na kuomba msamaha kwa dhati? Hapo kuna tatizo kubwa sana kwenye mahusiano wewe na mdogo wako. Chuki yako haitakwisha kwake akiendelea kuishi na Mumeo na ndo aibu itaendelea milele.
Ushauri mumeo akijirudi itakua nafuu na mdogo wako angeondoka angeolewa baadae na mtu mwingine ungepata nafuu kidogo ya chuki. Kwa sasa hata ukija pata mtu mwingine baadae wa kukuoa akisikia hii story anaweza kubadili mawazo.
Ukiweza kapatane na mumeo.
If it is True, pole nyingi sana dada Leah 2. Mkuu ametoa ushauri uliokwenda shule maana nimeguswa nao. Lakini!? haya mambo ni magumu, mwanaume hawezi akaishi na shemeji yake karibu hivyo hilo jambo lisitokee, haijalishi ni mlokole au vinginevyo, dawa yake kubwa ni kusamehe. Utaishi maisha mrua na hutajuta. Ukimwacha na ukiolewa na mwingine, mambo yatajirudia. Hivyo vitu ni kama kikombe cha chai kikinywewa chai, huoshwa na mwingine kukitumia tena.
 
Kumwucha huyo bwana haina maana kua asisamehe, awasamehe mme Na mdogo mtu then asonge mbele.
Laiti Leah angekua Na watoto kwa huyu mme hata mie ningemshauri ajikaze aendelee kuishi kwa ajili ya watoto sasa hakuna bora amwachie mdogo wake
Wao waendele kulea mtoto Na kujenga familia yao.
Gfsonwin pia bora mmewe hii Hali angekua anaijutia pia nakuona kua kafanya Jambo sio Lakini bwana huyu kakauka kauuu hata neno samahani/ nisamehe Mke wangu hakuna
Sasa unajiuliza hata ukimsamehe mtu kama huyu Na kuendelea nae si majanga??
Hata Yesu huwasamehe watu watubuo kwa kumanisha Na kunyenyekea kwake sio mtu hana time yupo yupo tu anasamehewa.
Huyu bwana hajaonyesha jitihada zozote kwa maelezo ya Leah ili kuokoa ndoa yake yeye anaona poa tu hapo ndo nauona ugumu wakuendelea Na mtu wanamna hii.
hivi lakin tumepata nafasi ya kumsikiliza huyu bwana kwa upande wake?
mie toka mwanzo nimesema ni kosa sana huyu bwana katenda na kiukweli inapaswa ajutie kosa lake lakin ninachopingana nachom ni leah kuamua kuvunja ndoa tu kisa mtoto kazaliwa. ndio uzinzi kikristo unavunja ndoa lakin je atakutana na mwanaume yupi ambaye hatakuwa mzinzi?
 
Kumwucha huyo bwana haina maana kua asisamehe, awasamehe mme Na mdogo mtu then asonge mbele.
Laiti Leah angekua Na watoto kwa huyu mme hata mie ningemshauri ajikaze aendelee kuishi kwa ajili ya watoto sasa hakuna bora amwachie mdogo wake
Wao waendele kulea mtoto Na kujenga familia yao.
Gfsonwin pia bora mmewe hii Hali angekua anaijutia pia nakuona kua kafanya Jambo sio Lakini bwana huyu kakauka kauuu hata neno samahani/ nisamehe Mke wangu hakuna
Sasa unajiuliza hata ukimsamehe mtu kama huyu Na kuendelea nae si majanga??

Hata Yesu huwasamehe watu watubuo kwa kumanisha Na kunyenyekea kwake sio mtu hana time yupo yupo tu anasamehewa.
Huyu bwana hajaonyesha jitihada zozote kwa maelezo ya Leah ili kuokoa ndoa yake yeye anaona poa tu hapo ndo nauona ugumu wakuendelea Na mtu wanamna hii.
Inaweza kuwa yapo mengi sisi hatiyajui, kwa mume mwenye mapenzi kwa mkewe, nakuhakikishia akikosea atapiga goti kuomba msamaha. Kuna kitu kinaniambia Leah anaweza kuwa unbearable kwa mumewe, mambo mengi ya chumbani hatuyajui hivyo one sided story won't give us the real picture behind this scenario.

Hatujui kama kweli walikaa na kuridhia as a family, kama mumewe alimkubalia kusoma kwanza ndipo wazae au alitumia ubabe( kumbuka kuna wanawake ni wababe sana kwa waume zao).

Japo yote haya hayafuti makosa ya jamaa kulala na shemeji yake, ana makosa makubwa, kaidhalilisha jamii yake na kamuumiza mkewe. Lakini I'm certain partly she's at fault.
 
aise pole sana
1. uko sahihi na maamuzi yako, kwani mipango ya kuzaa baada ulimshirikisha na alikubali.
2. Huyo mdogo wako azae tu wasijaribu kuitoa.
3. usikilize moyo wako, je huyo mumeo unampenda kweli na unahisi ni mwanaume ambaye ungependa kudumu nae for the rest of life, mitazamo yenu na upeo wenu wa kufanya mambo uko on the same page? Je hataweza kulirudia kosa tena in future? Majibu ya maswali ndio yakupe mweelekeo wa kurudiana nae au kutorudiana nae.
All the best.
 
hivi lakin tumepata nafasi ya kumsikiliza huyu bwana kwa upande wake?
mie toka mwanzo nimesema ni kosa sana huyu bwana katenda na kiukweli inapaswa ajutie kosa lake lakin ninachopingana nachom ni leah kuamua kuvunja ndoa tu kisa mtoto kazaliwa. ndio uzinzi kikristo unavunja ndoa lakin je atakutana na mwanaume yupi ambaye hatakuwa mzinzi?
Hahahahaaa
 
Nimesoma huu uzi zaidi ya mara tatu, kusema ukweli leah2 una nguvu, namuomba Mungu anipe ujasiri wa kupokea na kubeba mazito kwa style yako. Ninavyofikiri, maamuzi yoyote utakayochukua bado hayatakuwa in your favor. Wathungu wanasema you lose either way. Cha muhimu ni kuwa strong mwisho wa siku machungu yatapungua na maisha yataendelea.
 
funny enough, kuna watu humu ndani wanaona siye tunaosema samehe hatujaona ukubwa wa kosa alofanyiwa.
haiko hivyo ila tunaangalia hatma ya uamuzi atakao chukua.

nakupa mfano mdogo sana a sister of mine alikuwaga na mchumba, siku moja akamkuta mdogo wake tuko na huyo mchumba wake chumban kwa huyo mchumba wake wanapiga story. sister akakasirika sana akaona mdogo wake kamchukulia mchumba alicall off ule uchumba akasema nitapata mwingine wewe sio mwaminifu.

mama yangu mzazi alimwambia dada samehe usiachane na mchumba wako kwasabb kama hiyo, tena huyu dada alipakaza ukoo mzima mdogo wake kamchukulia bwana. huyu dada hakusikia ushauri wa mtu na alijua ukiachana na huyu utapata yule. miaka ikaenda yule bwana akatafuta mwanamke mwingine akaoa, mdogo mtu akaolewa na yeye yaani sister hadi leo hajaolewa. vilipomshinda akaamua kuzaa na mwanaume kwa ahadi ya kufunga ndoa baadae. miaka imepita mtoto sasa ni ten years hakuna ndoa mtu miaka ishafika 45. sasa mie huwaga najiuli pengine yule alomtolea mahari ndo alikuwa mume halisi wa sister. leo hii kamaliza makanisa dar yote akaiomba aoane na baba wa huyu mtoto na bado Mungu hajaruhusu. kuna mengi sana nyuma ya hili la leah2.

nataka kumwambia akiona Mungu kampa jaribu kama hili ajue anataka kumpromote kwenye daraja la juu kabisa inabidi yeye akae aangalie kusudi la Mungu katika hili na sio makusudi ya kibinaadamu. sisi sote tutakuwa wafariji wataabishaji kwake ila amtazame Mungu neema yake bado ipo na inamwita. naamini kipo Mungu alichomuandalia huyu dada ila ibilisi hataki lile kusudi litimie ndani yake.
Sawa kabisa niliwahi kupata somo la mume kuwa jaribu kwa mke. Kuna waliovumilia wakapata baraka na heshima kubwa kwa familia na jamii zao. Na mimi nimeishi hiyo experience kwa wazazi wangu na kwangu pia. Inataka moyo sana situation kama hizi ila mbele huko atakuwa level nyingine sana. Huko nje hakuko sawa sana kama tunavyoona tukiwa ndani na hakuna mtu mkamilifu jamani
 
Sawa kabisa niliwahi kupata somo la mume kuwa jaribu kwa mke. Kuna waliovumilia wakapata baraka na heshima kubwa kwa familia na jamii zao. Na mimi nimeishi hiyo experience kwa wazazi wangu na kwangu pia. Inataka moyo sana situation kama hizi ila mbele huko atakuwa level nyingine sana. Huko nje hakuko sawa sana kama tunavyoona tukiwa ndani na hakuna mtu mkamilifu jamani
inataka mtu kuwa na jicho la tatu kuona mambo kwa upeo unaoyaona wewe.
mume anapokuwa jaribu kwa mke nakuambia kunakuwa kuna daraja zuri sana kwa huyu mke Mungu anataka kumpandisha sasa utulivu, subira, uvumilivu na furaha ndivyo vitakavyokufanya uvuke ulipo.

na najaribu hili liko ili kumpandisha mama na sio baba, cha muhimu usiangalie ukubwa wa kosa ila tazama wewe katika misingi ya Mungu unatakiwa kufanya nini?
 
Back
Top Bottom