Mume na mtoto wa Kike.

Faru dume

JF-Expert Member
Dec 7, 2012
471
116
Poleni wanajamvi,leo nimekuja na mjadala hapa wa mzazi wa kiume kutopenda uzao wake wa kwanza uwe wa Kike na hii kasumba ipo kwa wanaume weng sana ukubali ukatae jibu ni ndio,hata pindi mke anapokua mjamzito mwanaume ataanza utabiri wa mtoto wa kiume tena na kumpa jina kabisa na si wa kike.
Sasa mimi najiulizaga kwanini mtoto wa kiume anapewa nafasi kubwa sana kuliko wa Kike?
Kama wewe ungependa mtoto wako wa kike awe ndo first born?
Hebu tujadili tubadilishe hii kasumba.
 
Ayayayayayayaaaa!
Haki ya mama! Nitafraize mtoto wangu wa mwanzo akiwa Jembe!
Hata wote wakiwa me poa tu!
But mutoto ya mwanzo tu ke! Ooppss! Bonge la dissapoitment kwa keli!
 
Awe wa kiume au wa kike cha muhimu awe na adabu nzuri kwa familia na jamii iliyotuzunguka. Hayo ya propaganda watajua wenyewe waliopitwa na wkt wenye akili zilizodidimia.
 
Ayayayayayayaaaa!
Haki ya mama! Nitafraize mtoto wangu wa mwanzo akiwa Jembe!
Hata wote wakiwa me poa tu!
But mutoto ya mwanzo tu ke! Ooppss! Bonge la dissapoitment kwa keli!

Kwanini jembe na si Mpini?
 
Ayayayayayayaaaa!
Haki ya mama! Nitafraize mtoto wangu wa mwanzo akiwa Jembe!
Hata wote wakiwa me poa tu!
But mutoto ya mwanzo tu ke! Ooppss! Bonge la dissapoitment kwa keli!
weye hutaki kuwazalia wanaume wenzie wajao wake kama wewe walivyokuzalia mke? usiwe na ubaguzi huo mkuu, halafu mungu watu kama wewe wabaguzi ndio anawaleteaga wale wale usiowataka
 
Awe wa kiume au wa kike cha muhimu awe na adabu nzuri kwa familia na jamii iliyotuzunguka. Hayo ya propaganda watajua wenyewe waliopitwa na wkt wenye akili zilizodidimia.
na adabu njema inapaswa kujengwa na wewe mzazi,
 
tunabadilisha nini? maana hakuna binadamu anayepanga jinsi ya motto anayezaliwa

Ziko familia mtoto wa kwanza akiwa wa kike mume hua hana raha anajihisi aibu na mke kumkosesha raha matokeo mtt kulelewa kiunyonge ila ni elimu ndogo sana walionao wanatakiwa kuelimishwa hasa sehemu za vijijini wengine hufikia ht kuacha wake zao au kutafuta mwengne apate mtt wa kiume. Maskini hawajui walifanyalo kwan mtt awe wa kike au kiume ni ww mume na sperms zko....
 
mfumo unamafanya mwanamme kupenda uzao wake wa kwanza uwe wa kiume kwa kuwa hamna utamaduni wa mtoto wa kike kuridhi
 
Poleni wanajamvi,leo nimekuja na mjadala hapa wa mzazi wa kiume kutopenda uzao wake wa kwanza uwe wa Kike na hii kasumba ipo kwa wanaume weng sana ukubali ukatae jibu ni ndio,hata pindi mke anapokua mjamzito mwanaume ataanza utabiri wa mtoto wa kiume tena na kumpa jina kabisa na si wa kike.
Sasa mimi najiulizaga kwanini mtoto wa kiume anapewa nafasi kubwa sana kuliko wa Kike?
Kama wewe ungependa mtoto wako wa kike awe ndo first born?
Hebu tujadili tubadilishe hii kasumba.

We mleta mada ni ke /me? umeolewa /umeoa? kama majibu yako yanafika kwa swali la pili nini maoni yako..
 
mfumo unamafanya mwanamme kupenda uzao wake wa kwanza uwe wa kiume kwa kuwa hamna utamaduni wa mtoto wa kike kuridhi

Naamini ulimaanisha kurithi....Mkuu unaweza nipa utamaduni wa makabila ya kusini mwa Tanzania? Je yanaendana na mchango wako?
 
Poleni wanajamvi,leo nimekuja na mjadala hapa wa mzazi wa kiume kutopenda uzao wake wa kwanza uwe wa Kike na hii kasumba ipo kwa wanaume weng sana ukubali ukatae jibu ni ndio,hata pindi mke anapokua mjamzito mwanaume ataanza utabiri wa mtoto wa kiume tena na kumpa jina kabisa na si wa kike.
Sasa mimi najiulizaga kwanini mtoto wa kiume anapewa nafasi kubwa sana kuliko wa Kike?
Kama wewe ungependa mtoto wako wa kike awe ndo first born?
Hebu tujadili tubadilishe hii kasumba.

je kina mama pia huwa wanapenda mtoto wa kwanza awe wa jinsia fulani?
 
Sioni cha kujadili hapa zaidi kuna watu humu jamvi muda ndani ya ndoa ni mia minne na zaidi bila mtoto leo mnaongelea jinsia ?

Ni kama mnakufuru hakika,mtoto ni zawadi toka kwa Mungu .
 
je kina mama pia huwa wanapenda mtoto wa kwanza awe wa jinsia fulani?

Sio wanaume wote wenye iyo akili. Wengi siku hizi wameshaelewa kuwa wao ndio wana uwezo Wa kufanya Mtoto awe Wa kike au kiume. Tena wengi ninaowafahamu wanawafurahia sana watoto wa kike
 
Back
Top Bottom