Mume na mtoto wa Kike.

Poleni wanajamvi,leo nimekuja na mjadala hapa wa mzazi wa kiume kutopenda uzao wake wa kwanza uwe wa Kike na hii kasumba ipo kwa wanaume weng sana ukubali ukatae jibu ni ndio,hata pindi mke anapokua mjamzito mwanaume ataanza utabiri wa mtoto wa kiume tena na kumpa jina kabisa na si wa kike.
Sasa mimi najiulizaga kwanini mtoto wa kiume anapewa nafasi kubwa sana kuliko wa Kike?
Kama wewe ungependa mtoto wako wa kike awe ndo first born?
Hebu tujadili tubadilishe hii kasumba.

Kwangu mimi majibu yote A,B,C ni sawa tu

Apate mtoto sawa
Apate wa kike sawa
Wa kiume sawa
Asipoza sawa

Hivi kwani umeoa ili iweje?
 
weye hutaki kuwazalia wanaume wenzie wajao wake kama wewe walivyokuzalia mke? usiwe na ubaguzi huo mkuu, halafu mungu watu kama wewe wabaguzi ndio anawaleteaga wale wale usiowataka

Eee! Unaniombea mabaya DEMBA eee?
...
Jaman! Mi thio mbagudhi! Nimesema tu itakua bonge la dissaptment! Thi unajua tena ukitegemea kitu afu ukikose!
...
Thina maana ya kuwakataa or kuwachukia Mtoto wa kike and/or mama watoto!
...
but nikiambiwa nichague.......!
 
Mtoto ni mtoto tu, awe wa kike au wa kiume. Unapoanza kuchagua na ikatokea usivyotaka hutakaa umlee huyo mtoto kwa mapenzi ya ukweli na mwishowe lazima toto liwe Nunda au atafute upendo pembeni (na kama ni binti amemiss upendo wa baba, kidume kikimwambia kinampenda lazima azamie huko bila kufikiri mara mbili).
 
Sio wanaume wote wenye iyo akili. Wengi siku hizi wameshaelewa kuwa wao ndio wana uwezo Wa kufanya Mtoto awe Wa kike au kiume. Tena wengi ninaowafahamu wanawafurahia sana watoto wa kike

hujanipata mkuu, nauliza kama kina mama pia huwa wanapenda mtoto wa kwanza awe wa jinsia fulani?
 
Eee! Unaniombea mabaya DEMBA eee?
...
Jaman! Mi thio mbagudhi! Nimesema tu itakua bonge la dissaptment! Thi unajua tena ukitegemea kitu afu ukikose!
...
Thina maana ya kuwakataa or kuwachukia Mtoto wa kike and/or mama watoto!
...
but nikiambiwa nichague.......!
haya bana mungu akupe sawasawa na hitaji lako.
 
Kuna hospital 1 hv ya wachina kubwa tu kwa hapa dar,hy ki2 wanafanya,unaulizwa unataka me au ke?jiau utalo wapa nikwe inakuwa kama ulivyo chagua.siambiwi nimeshuhudia mwenyewe zaid ya x3
 
Poleni wanajamvi,leo nimekuja na mjadala hapa wa mzazi wa kiume kutopenda uzao wake wa kwanza uwe wa Kike na hii kasumba ipo kwa wanaume weng sana ukubali ukatae jibu ni ndio,hata pindi mke anapokua mjamzito mwanaume ataanza utabiri wa mtoto wa kiume tena na kumpa jina kabisa na si wa kike.
Sasa mimi najiulizaga kwanini mtoto wa kiume anapewa nafasi kubwa sana kuliko wa Kike?
Kama wewe ungependa mtoto wako wa kike awe ndo first born?
Hebu tujadili tubadilishe hii kasumba.
Hakuna ukweli wowote ila wazazi tunapenda kuwa na watoto wa jinsia mchanganyiko
 
Kwangu mimi majibu yote A,B,C ni sawa tu

Apate mtoto sawa
Apate wa kike sawa
Wa kiume sawa
Asipoza sawa

Hivi kwani umeoa ili iweje?

ndoa ya kweli / pete ya heshima ni mtoto;
mtoto wa kiume ni wa hapo hapo daima lakini wa kike ni wa kwenda kwa mume wake tu.
 
mtoto wa kwanza akiwa wa kiume ana percent ya kuokoa jahazi,then wakifuata wa kike poa tu!!

Wengine pia wanakuwa machizi tu hawaokoi jahazi wala mtumbwi cha msingi ni kuomba mungu akupatie mtoto wa kherii... Kwan wavuta bangi na wabwia unga ,wezi na majambazi c hao hao wanaumee
 
mtoto ni mtoto. Utachagua wa kiume anakuja kuwa garasa na yule wakike akawa mkombozi. Kuchagua kunaweza leta laana ndani ya nyumba kwani ukipewa ambacho hukukitaka manung'uniko hayatakuisha na baraka alizokuwa nazo ukazikosa.
 
Mie napenda sana mtoto wa jinsia aliyopendezwa nayo muumba mwenyewe. Na wote nitawapa haki sawa kuanzia elimu na upendo kama baba.... hayo ya me au ke ni yupi bora ni kutokuonyesha heshima kwa mungu muumba na laweza leta laana.
 
Mie napenda sana mtoto wa jinsia aliyopendezwa nayo muumba mwenyewe. Na wote nitawapa haki sawa kuanzia elimu na upendo kama baba.... hayo ya me au ke ni yupi bora ni kutokuonyesha heshima kwa mungu muumba na laweza leta laana.


Nimeipenda. Nilitaka nikugongee like ila sikukiona kitufe cha like. Ila pokea like like like.
 
kweli elimu kwa hawa wanaume inahitajika,hawajui tu kwamba wao ndio chanzo cha mtoto kuzaliwa ke au me!!!!!
 
mi naona mtoto ni mtoto tu kwani kuna wengine wanahangaika kila kukicha kutafuta hata wa kike wasiotakiwa na hawawapati....ni kumshukuru M
 
...mtoto wa kike ni tunu kutoka kwa Mungu......namtafuta kwa nguvu zote,,,dumes wanatosha......so hata hawa dumes wakinichenjia, dada yao hawezi kamwe..... c mwajua vidume huwa tunatekwa na wakina ''KE''...
 
kweli elimu kwa hawa wanaume inahitajika,hawajui tu kwamba wao ndio chanzo cha mtoto kuzaliwa ke au me!!!!!

Kwahiyo kuzaliwa ke au me ni mpango wa mwanaume ila kutozaliwa kabisa nao ni mpango wa mwanaume? I stand for correction ninaamini mambo mengi ya kitabibu ila sio yote, linapokuja swala la uzazi(uumbaji for this matter) huwa naamini ni mipango ya Mungu. Nina watoto wanne nilitamani sana first born awe wa kiume nikashindwa nilijaribu timing zote wa pili wa kike, wa tatu wa kike nikakata tamaa I didnt struggle for the forth surprising akaja wa kiume
 
Back
Top Bottom