Mume: Hakuna kutengeneza nywele

Mume: Hakuna kutengeneza nywele

kataip

Senior Member
Joined
Aug 21, 2013
Posts
150
Reaction score
93
Habari wanaume mje mtujuze.

Mume anapomzuia mkewe kwenda kusuka au kutengeneza nywele kwa mafundi au saloon au kuja fundi au mtu wasaloon anamaasha nini?

Wakati anamuoa kamkuta na nywele safi za asili gharama ya kusuka kwa wiki anaweza tumia 1000 au 2000some time mwanamke anajigharamia.

Best yangu ana wakati mgumu wajuzi wa mambo wasomi wa mambo ya ndoa vitabu vya mungu vinasemaje?

Na huyu mwanaume anatatizo gani?

Karibuni nisiwachoshe
 
waume wa hivyo nuksi, utakuta anakibustan huko kimechachamalisha nywele kichwani kama nungunungu na analipia garama kila wiki...huyo mume mpuuzi tu,anabana bajet kwa mke ili akalipie upande mwingine
 
Kusuka ya elfu tu shida.......huyo unaweza mwambia ishu za lace wig au hata kubond tu weave akakuelewa......?......pole mwanamke mwenzetu kwa kumeza kimeo.........
 
Tatizo kwenda kusuka au tatizo kupewa pesa ya kusuka????
 
Kama hataki hivo na anamnunulie vifaa ajitengeneze mwenyewe nyumbani........akiwa ana vifaa vyake saloon watamsahau kabisa akikataa hili basi huyo baba ana lake jambo.....
 
Namshauri aweke dawa...anunue mafuta na steaming yake, shampoo...atafute hand drier zipo hadi za elfu 25 kariakoo....awe anajitengeneza mwenyewe home simple tu.
 
Kusuka ya elfu tu shida.......huyo unaweza mwambia ishu za lace wig au hata kubond tu weave akakuelewa......?......pole mwanamke mwenzetu kwa kumeza kimeo.........

siku atakayosema anataka kubond ndio siku atakayopewa nauli ya kwenda kwao kwa hali inavyoonyesha.
Nawashangaa sana wanaume wa hivyo, usipompendezesha mkeo wataka apendezeshwe na nani? Khaaaa
 
Kama hataki hivo na anamnunulie vifaa ajitengeneze mwenyewe nyumbani........akiwa ana vifaa vyake saloon watamsahau kabisa akikataa hili basi huyo baba ana lake jambo.....

anashindwa elfu moja ya kusukia ataweza kumnunulia hivyo vifaa my dia?
Huyo mume mfujaji tu anataka kumfuja mkewe kusudi ili apate nafasi ya kuchepuka
 
Hilo janaume jinga, ila nywele za buku ni zipi hizo twende kilioni?
 
Hilo janaume jinga, ila nywele za buku ni zipi hizo twende kilioni?

No, siyo jinga sema approaching yake inaweza haikuwa nzuri!!

Nina miaka zaidi ya kumi kwenye ndoa, mke wangu hajawahi kanyaga saloon!! Ukimuona yupo smart na anabadilisha mitindo ya nywele kila siku na ni yoyote unayofahamu.

Aliacha kwenda saloon baada ya kugundua kuwa kuna wanaume wanawatumia wahudumu wa saloon kama makuwadi!!

So, kila akienda saloon anakuwadiwa kwa nguvu zote!! Na wanampa na mbinu zote, bahati nilishtuka mapema nikambana akanipa full story.

Tangu hapo mke wangu saloon ni big no!! Lengo ni kujaribu kupunguza ile risk ya kuchange tabia kwa ajili ya familia yangu na mimi mwenyewe.

Kama una swali uliza utajibiwa
 
Naona watu wamekomalia kwenye kigezo cha pesa(kubana matumizi au ubahili), sometimes kuna vitu vingi nje ya pesa vnavyoweza mzuia, kuna watu wengine wanavutiwa sana na mwanamke akiwa hajasuka kuna dini zingine zinakataza mwanamke kusuka, nikilemba tu.
 
Habari wanaume mje mtujuze
Mume anapomzuia mkewe kwendakusuka au kutengeneza nywele kwa mafundi au saloon au kuja fundi au mtu wasaloon anamaasha nini ? Wakati anamuoa kamkuta na nywele safi za asili ghalama ya kusuka kwa wiki anaweza tumia 1000 au 2000some time mwanamke anajigharamia. Best yangu ana wakati mgumu wajuzi wa mambo wasomi wa mambo ya ndoa vitabu vya mungu vinasemaje?
Na huyu mwanaume anatatizo gani?
Karibuni nisiwachoshe

nivizuri ukaenda kwenu ili upate muda mzuri wa kufanya hayo uyatakayo,umeolewa na ujue fika utakutana na changamoto mpya,sasa kuendelea kukari lifestyle ile ile utakuwa unajipa jaka moyo.
 
Acha nipite tu

Kwa hiyo saluni mke haendi, je mume anaenda au haendi????
 
waume wa hivyo nuksi, utakuta anakibustan huko kimechachamalisha nywele kichwani kama nungunungu na analipia garama kila wiki...huyo mume mpuuzi tu,anabana bajet kwa mke ili akalipie upande mwingine

Hatimaye umeonekana
 
Mkuu jaribu kumuuliza mambo hayo yalianza anzaje manake kama alimkuta anasuka alipaswa kumwambia from the first day alipo implement hiyo amri ya kutosuka/sukwa kwani alimkuta anasuka na ndio maana moyo wake ulimdondokea ote sasa itakuaje akiacha. Lkn pia huenda kuna tatizo lingine ni vizuri rafiki yako akatatua mgogoro huu kwa hekima bila ugomvi. Wakae wazungumze aulize kwa ustaarabu sababu za kukatazwa na mwisho nae atoe mtazamo wake utakaomshawishi bwana mkubwa kubadili msimamo wake. Kama ujuavyo maisha hayana kanuni moja.
 
nivizuri ukaenda kwenu ili upate muda mzuri wa kufanya hayo uyatakayo,umeolewa na ujue fika utakutana na changamoto mpya,sasa kuendelea kukari lifestyle ile ile utakuwa unajipa jaka moyo.


mnapenda sana kutishia mwanamke aende kwao. komesha Lady j dee habashi kwaoo
 
Back
Top Bottom