Viongozi wa sasa wana mengi ya kujifunza kutoka kwa Mtei. Mtei hakukubaliana na sera za Mwalimu kuhusiana na Uchumi. Ishu ilikuwa kushusha thamani ya shilingi ili TZ ikopeshwe na IMF. Mwalimu hakupenda hili, kwa kujua hulka ya Mwalimu na kwa utashi wake akaandika barua ya kujiuzulu akaenda kumpa Mwalimu nyumbani kwake Msasani. Alipofika aliulizwa kama hajakutana na mtu wakati anakwenda kwa Mwalimu. Mtei akajibu hajakutana na mtu. Mwalimu nae alikuwa ameshamwandikia barua akimtaka ajiuzulu, Mtei alipishana na mtu aliyekuwa ampe barua kutoka kwa Mwalimu. Mtei alikubaliwa kujiuzulu na baada ya muda alipewa nafasi nyingine serikalini. Kitu cha kujifunza hapa ni kusimamia unachoamini, maana sera za Mtei zilikuja kutekelezwa muda si mrefu baada ya yeye kujiuzulu. Nchi gan maskini leo haitekelezi masharti ya IMF? Serikali haikopi fedha IMF?
Viongozi wetu siku hizi hawawezi kusimamia wanachoamini, tena wapo wengi. Kuna Celina Kombani, Werema na wengine wengi. Enzi za Mwalimu hawa wote wangejiuzulu. Fikiria Rais Kikwete anashauri mtihani wa darasa la nne na kumi (form two) usiwe kikwazo cha mtu kuendelea na masomo, hakuna hata mtaalamu mmoja wa elimu pale wizarani aliyempinga (kuna maprofesa wengi tu pale) kwamba hatuna namna nyingine ya kupima uelewa wa wanafunzi na kuwasaidia. Kurudia darasa si adhabu, ni kumpa mwanafunzi nafasi ya kujifunza tena ambacho hakuelewa. Wanabaki wanasema chini chini kwamba hapa ushauri wa mkuu sio mzuri.
Chadema inafadhiliwa na mataifa ya nje. Je bajeti ya serikali yetu nani anachangia? Mataifa ya nje ni mabaya kwa chadema ila mazuri kwa Serikali? CCM inafadhiliwa na nani kama sio kodi zetu kupitia EPA, Kagoda, Richmond na Meremeta? Mikataba mibovu ya madini wamesaini chadema? Nani kawapa mabepari migodi na mashirika yetu kwa bei karibu na bure? Mangungo wa Msovero ni nani leo hii?