Muhimu kuchagua marafiki sahihii

Pdidy

JF-Expert Member
Nov 22, 2007
50,720
21,779
I kor 15:23
msidanganyike mazungumzo mabaya uharibu tabia njema
ukiwa kama mcha mungu unaitaji kutembea na mtu sahihi
mtu anaeongea anaeishi kwa kumuheshimu mungu,marafiki wabaya uamua hatima yako ya maisha,yawezekana uko na wavuta bangi wauza maadawa uwezekano mkubwa wa kuuza madawa upo na hivyo kumaliza hatima yako ya maisha,yawezekana marafiki zako wote ni wazinzi,huusika kwenda kuchukua wanawake pale afrika sana na kwingineko,mwisho wake na wewe utaamua kwenda kubeba ile mizoga na kuishi kama yeye anavyoishi,sikuzuii uachane na rafiki zako;ila ufahamu wako ndio utakaao amua,

matendo 1:3
kiwete mmoja alikuwa anaomba pesa kwa yohana kila mara na wanamsaidia;siku alipowaona akaomba pesa akawambia leo atuna pesa tunachokupa niuponyaji wa jina la yesu amka uende
yule kiwete akaamka na kuondoka,
ukitaka kupenya katika biashara unaitaji kukaa na watu wanaojua biashara;kuna kipindi unaitaji kujitenga na watu ili uweze kufanikiwa katika maisha yako ya kimungu;ukisoma mwanzo ibrahimu ilibidi aondoke amwache babake tera ndipo alipoanza kubarikiwa,
kuna watu ambao ukishikamana nao unapenya katik jina la yesu,petro alikaa na yesu akaachiliwa nguvu za yesu,dhambi ina nguvu ya kuambukiza,ukikaa na watu dhaifu unakuwa mdhaifu,ukika na wenye midomo michafu unakuwa na mdomo mchafu
 
Show ur character i ll show ur destiny
kaa na mtu aneomba anaesoma biblia.nawe utakuwa mtu wa maombi na neno la mungu,kaa na watu sio wanasema nini bali wanaosema neno la mungu linasema nini,
amos 3:3
watu wawili awawezi kwenda njia moja pasipokupatana si wote wanaoita bwana bwana watakaouona ufalme wa mungu

1 sam 18:20
ukitembea na watu waliopenya wenye kumjua mungu wenye kuenenda sawa na neno la mungu nawe utapenya katika maisha yako sema amen kama waamini
yawezekana unaitaji gari,nyumba nenda kwa mtu anaeishi kwenye nyumba yake mwambie mungu kama niingiapo hapa nami mwaka huu naitaji kuwa na nyumba yangu,usiende kwenye nyumba ya kupanga ukatolea unabii utabakia kupangisha ameni??tunaitaji kubadilishwa katika maisha yetu,tunaitaji ku risk maisha ,ili tuenende katika bwana,usiogope kuachana na rafiki yako ama amekutafutia mchumba ,alikuonyesha kiwanja,mungu ndie mweza yote

kuna watu wana roho za kupoteza;unaweza kushika pesa million na mamillion sababu uko na watu wa kupoteza utashangaa wiki zote pesa zimeisha ujui umefanyia nini,
yohana 8:31,32
""ukiijua kweli nayo kweli itakuweka huru""

yeremia 1 : 12
"naliangalia neno nipate kulitimiza" neno la mungu ni kweli

yoh 63:6
neno la mungu ni roho,ukilishika neno umelinda roho yako
hesabu 14:28 ""kadri mwombavyo ndivyo nitakavyotenda,mungu anaitaji kusikia mdomo wako uki shout ukiomba.usiogope kuomba marafiki wema wenye tabia njema wanaomtukuza mungu;usikubali kupotea sababu ya pombe;achana na marafiki walevi;mungu anaitaji kuokoa roho yako siku ya leo,mungu akakubadilishe akupe marafiki wapya wazuri wenye kumpendeza mungu ;watu wasio na nia mbaya juu ya roho yako
 
Mkuu huoni kwamba hao marafiki unaowaita wabaya pia wanakuhitaji ili waige mfano wa kutenda mema kutoka kwako? Sasa tuki-watenga/wakwepa watajifunzaje kuwa watu wema?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom