Muhimbili waanza kulipisha tozo ya kuegesha magari, utaratibu utakuwa kwenye majaribio kwa wiki mbili

Replica

JF-Expert Member
Aug 28, 2017
1,446
7,822
Majaribio ya utaratibu mpya wa maegesho ya kulipia katika Hospitali ya Taifa Muhimbili yameanza wiki hii, ikiwa ni jitihada za kupunguza msongamano wa magari.

Akizungumzia utaratibu huo, Mkurugenzi Mtendaji wa hospitali hiyo, Profesa Mohammed Janabi alisema majaribio yatadumu kwa wiki mbili.

“Tutakapoanza rasmi, wanaoingia na magari watakuwa wakilipia Sh500 kwa saa na kwa wanaoingia na wagonjwa tutawapa dakika 30 za bure kwa ajili ya kushusha wagonjwa, ikizidi hapo ndipo watalipia,” alisema.

Profesa Janabi alisema mgonjwa atakayefika hospitalini akiendesha gari na ikatokea akalazwa, hatatakiwa kulipia gharama za maegesho. Kundi lingine ambalo halitahusika na malipo ya maegesho ni la wafanyakazi wa hospitali hiyo.

Alisema malipo ya maegesho siyo suala jipya katika hospitali hiyo, kwa kuwa miaka ya 1990 kulikuwa na utaratibu huo.

Muhimbili.jpg

“Utaratibu huu wa maegesho ya kulipia unakuja na faida mbili. Moja ni kuiingizia hospitali kipato na mbili, ni kudhibiti msongamano wa magari,” alisema Profesa Janabi.
Pia, alisema utafiti uliofanyika kwa mwezi mzima ulibaini kila siku yanaingia magari kati ya 3,000 na 3,500.

Akizungumzia malipo ya maegesho, Bahati Masanika, aliyefika Muhimbili kumpeleka mgonjwa alisema ni changamoto kwao.

“Kwa mfano, mimi natokea mkoani niko hapa tangu asubuhi na sasa ni saa tisa, maana yake natakiwa kulipia muda wote ambao nimekaa hapa, kwa hiyo nitakuwa nalipia hela nyingi.”

Kwa upande wake, Daudi Mbwambo ambaye ni dereva wa teksi katika eneo hilo alisema suala hilo ni sahihi kwa kuwa watu walikuwa wanaweka magari bila mpangilio. Pia, alikiri wapo wanaoegesha magari hospitalini na kuyachukua wanapotoka kazini jioni.

Chanzo: Mwananchi

Pia soma: Wanaopaki magari Hospitali ya Muhimbili kuanza kulipia
 
Kuna watu wana attend clinic tofauti kila siku. Mfano dialysis. Hapo ni kuwaongezea mzigo wagonjwa na wauguzaji.

Yapo maeneo ambapo serikali inaweza kukusanya pesa ila kwa hospital ni maamuzi ya kipuuzi na kutojali utu.

Kama suala la watu kuja kufanya parking maeneo hayo mbona ni rahisi kuwagundua na kuwabaini. Lakini adhabu hii kuwaunganishia na watu wenye wagonjwa au wagonjwa wenyewe ni uonevu.
 
Kama nitakuwa nakumbukumbu, tozo za kuegesha magari maeneo ya Hospitali ya Taifa Muhimbili na Posta Kuu katikati ya Jiji Dar es salaam zilifutwa na Bunge, iweje Muhimbili wazirudishe bila kupitia Bungeni??
 
Sasa bwana dokitari atatakiwa kutibu bwana mugonjwa upesi upesi hahahaha
 
Hizo tozo wanunulie dawa,maana watakusanya milioni 50 kwa mwezi, dawa za magonjwa madogo madogo na vifaa ya uzazi iwe bure,
Hizo pesa zisiende mifukoni
 
Majaribio ya utaratibu mpya wa maegesho ya kulipia katika Hospitali ya Taifa Muhimbili yameanza wiki hii, ikiwa ni jitihada za kupunguza msongamano wa magari.

Akizungumzia utaratibu huo, Mkurugenzi Mtendaji wa hospitali hiyo, Profesa Mohammed Janabi alisema majaribio yatadumu kwa wiki mbili.

“Tutakapoanza rasmi, wanaoingia na magari watakuwa wakilipia Sh500 kwa saa na kwa wanaoingia na wagonjwa tutawapa dakika 30 za bure kwa ajili ya kushusha wagonjwa, ikizidi hapo ndipo watalipia,” alisema.

Profesa Janabi alisema mgonjwa atakayefika hospitalini akiendesha gari na ikatokea akalazwa, hatatakiwa kulipia gharama za maegesho. Kundi lingine ambalo halitahusika na malipo ya maegesho ni la wafanyakazi wa hospitali hiyo.

Alisema malipo ya maegesho siyo suala jipya katika hospitali hiyo, kwa kuwa miaka ya 1990 kulikuwa na utaratibu huo.


“Utaratibu huu wa maegesho ya kulipia unakuja na faida mbili. Moja ni kuiingizia hospitali kipato na mbili, ni kudhibiti msongamano wa magari,” alisema Profesa Janabi.
Pia, alisema utafiti uliofanyika kwa mwezi mzima ulibaini kila siku yanaingia magari kati ya 3,000 na 3,500.

Akizungumzia malipo ya maegesho, Bahati Masanika, aliyefika Muhimbili kumpeleka mgonjwa alisema ni changamoto kwao.

“Kwa mfano, mimi natokea mkoani niko hapa tangu asubuhi na sasa ni saa tisa, maana yake natakiwa kulipia muda wote ambao nimekaa hapa, kwa hiyo nitakuwa nalipia hela nyingi.”

Kwa upande wake, Daudi Mbwambo ambaye ni dereva wa teksi katika eneo hilo alisema suala hilo ni sahihi kwa kuwa watu walikuwa wanaweka magari bila mpangilio. Pia, alikiri wapo wanaoegesha magari hospitalini na kuyachukua wanapotoka kazini jioni.

Chanzo: Mwananchi

Pia soma: Wanaopaki magari Hospitali ya Muhimbili kuanza kulipia
Yaani hii nchi, integrity ni ndogo sana. Hapo Janabi anaona kafanya ubunifu mkubwa kumbe ni kuongeza mzigo kwa wagonjwa na ndugu zao. Vitu vya hovyo na aibu sana, sijui huko Mecca wanaendaga kufanya nini, shame on them.
 
Nilisikiliza msemaji kipindi cha asubuhi kupitia Radio One. Alieleza vizuri zana maboresho ya Hospitali na baadae akaelezea suala la packing. Alisema lengo la msingi sio kukusanya mapato, bali kupunguza msongamano wa magari kwani kumekuwa na watu wanaoacha magari yashinde pale kutwa nzima baadhi wakiwa ni wafanyabiashara wa maeneo ya karibu au majirani wa hospitali.

Pamoja na nia yao njema Nina ushauri ufuatao:

1. Sioni kama ni sawa kuchaji mtu packing ambaye amekuja kuletea chakula mgonjwa ambacho hospitali haitoi (labda pengine yale masaa ya chakula yawe bure)

2. Mgonjwa wa nje anayekuja kupata matibabu anatarajia ndani ya masaa mawili hivi awe amepata huduma na kuondoka. Sasa, kama atakaa pale kwa masaa sita kwa sababu fulani za matibabu au za kiutendaji wa hospitali naona kama sio sawa kuchajiwa

3. Najiuliza pia kuwa, huduma wanayotoa ni ya kulipia (sio bure), lakini pia wanatoa huduma ambayo kimsingi hakuna mbadala wake Nchini (ni hospitali ya ngazi ya juu kabisa) hivyo inakuwa kama wanataka kunufaika na monopoly kwani kama zingekuwepo Hospitali nyingi za ngazi hiyo, mtu angejichagulia aende pengine na wao wangepata ushindani na hivyo kufanya wateja wawe wachache

4. Kwenye hospitality Industry (mahotel nk); hutoa huduma ya packing bure kwasababu mteja analipia huduma atakayopewa lakini pia, hawategemei wateja waje kwa miguu hivyo packing ni sehemu ya huduma wanayotoa kwani bila hiyo packing ya kueleweka hata biashara hawapati. Naamini Hospitali zinafuata utaratibu huo huo wa hospitality industry

5. Nilimsikia msemaji akisema wata toa muda wa nusu saa ya kwanza bure; nikasikitika kwani hiyo ni "copy paste" bila kuangalia huduma yao. Maduka makubwa (moles) huweka muda huo (30mins to 1hr) bure kwani wanajua wateja wengi wa kawaida hutumia muda huo kufanya manunuzi; hivyo huwapa fursa ya kununua na kuondoka kwa haraka bila malipo ya packing ni ili kupisha wengine. Sioni kama hii inafaa kwa mazingira ya Muhimbili kwani mteja hajipimii muda wa huduma bali anapimiwa na taratibu za hospitali na kiuhalisia, Muhimbili hakuna huduma inapatikana kwa muda wa nusu saa

6. Nafikiri wangeweka utaratibu mwingine wa kutambua magari yanayo kaa Hospitali mara kwa mara na kwa masaa/siku nyingi ili yachukuliwe hatua. Kimsingi Muhimbili ni Hospitali ya TAIFA YA SERIKALI ambapo lengo la msingi kabisa ni kutoa huduma na sio kufanya biashara lakini pia ni kioo cha hizi hospitali nyingine za mikoani ambazo zinaweza kuiga huo utaratibu na kuleta mtafaruku!

Sio kwamba napingana nao ila, naona kama wakifuata uhalisia itakuwa vigumu kutekelezeka
 
Dalili za mwisho wa Dunia,Daktari badala ya kuwafikiria wanaokuja kuuguza wanatumia gharama kubwa kiasi gani? Kuna wengine wanauguza mgonjwa Hadi wanafilisika na bado mgonjwa anakufa,na wanabaki na Deni hospitali lakini bado mnaona hao watu walipe na hela ya maegesho ya magari,wajue kabisa kwenda hospitali sio Jambo la kifurahisha watu wanapitia kipindi kigumu mno.
 
Kuna watu wana attend clinic tofauti kila siku. Mfano dialysis. Hapo ni kuwaongezea mzigo wagonjwa na wauguzaji.

Yapo maeneo ambapo serikali inaweza kukusanya pesa ila kwa hospital ni maamuzi ya kipuuzi na kutojali utu.

Kama suala la watu kuja kufanya parking maeneo hayo mbona ni rahisi kuwagundua na kuwabaini. Lakini adhabu hii kuwaunganishia na watu wenye wagonjwa au wagonjwa wenyewe ni uonevu.
Umenena sahihi, kwamba wanataka wagonjwa waende Kwa miguu. Nchi hii shida sana, sijui mwokozi atatoka wapi. Kila kitu wanataka kiwe Kodi tu.
 
Times 500= 1.5-1.75m per day. You can see how people are easily playing with numbers
Mind you, charges are per hour not per day. One can be subjected to pay more than 500 depending on hours stayed. This country bwana.
 
Back
Top Bottom