Hospitali ya Taifa Muhimbili na urasimu wa kutoa Medical Report

X men

Member
Dec 26, 2021
11
23
MUHIMBILI NA URASIMU WA MEDICAL REPORT.

Nimekuwa nikiuguza mgonjwa wodini pale Jengo la Watoto Hospitali ya Muhimbili kwa vipindi tofauti tofauti, ilikuwa kuomba Medical Report ni bure, lakini kuanzia Prof. Janabi alipoingia kupata Medical report ya mgonjwa ni lazima ulipie Laki moja (Tsh. 100,000/=)

Hilo sio tatizo sana, tatizo linakuja kwamba hata baada ya kulipia hizo gharama inakupasa tena kuanza kuzunguka kuwatafuta madaktari kuwaomba waandike hiyo report, usumbufu zaidi ni kwetu sisi ambao tunatoka mkoani ukiwasiliana na watu wa masjala/PS wanakwambia mtafute daktari wake ama mpigie simu mwambie akuandikie sisi tumeshapeleka file kwake!!

Nina zaidi ya wiki 2 sasa, niko mkoani report inahitajika ofisini ila kila nikiwasiliana na wanaopaswa kuifuatilia report wananizungusha tu, sasa wameweka vipi gharama ya huduma kama hawawezi kuitoa hiyo huduma vizuri?

Hili jambo linatakiwa kushughulikiwa haraka, ni usumbufu sana!!

Majibu ya Muhimbili, soma hapa: Hospitali ya Muhimbili yatoa ufafanuzi kuhusu keri ya ucheleweshwaji wa utoaji wa Medical Report
 
MUHIMBILI NA URASIMU WA MEDICAL REPORT.

Nimekuwa nikiuguza mgonjwa wodini pale Jengo la watoto Muhimbili kwa vipindi tofauti tofauti, ilikuwa kuomba Medical Report ni bure, lakini kuanzia Prof Janabi alipoingia kupata Medical report ya mgonjwa ni lazima ulipie Laki moja (100,000/=)

Hilo sio tatizo sana, tatizo linakuja kwamba hata baada ya kulipia hizo gharama inakupasa tena kuanza kuzunguka kuwatafuta madaktari kuwaomba waandike hiyo report, usumbufu zaidi ni kwetu sisi ambao tunatoka mkoani ukiwasiliana na watu wa masjala/PS wanakwambia mtafute daktari wake ama mpigie simu mwambie akuandikie sisi tumeshapeleka file kwake!!

Nina zaidi ya wiki 2 sasa, niko mkoani report inahitajika ofisini ila kila nikiwasiliana na wanaopaswa kuifuatilia report wananizungusha tu, sasa wameweka vipi gharama ya huduma kama hawawezi kuitoa hiyo huduma vizuri?

Hili jambo linatakiwa kushughulikiwa haraka, ni usumbufu sana!!
Medical report mara nyingi inahitajika ukitaka kumpeleka mgonjwa nje ya Tanzania unaandaliwa na mkuu wa kitengo hospitali, hili la kulipia ndio nalisikia leo hupaswi kulipia.

By the way medical report kazini kwako wao ya nini?
 
KIZIMKAZI taifa limemshinda watanganyika tuamke kila sehemu ni kilio. Natena wafanyakazi hawana woga wwte. Cjui baada y kugundua kua mbona YY kauza Bandari. Hali ni Tete
 
Medical report mara nyingi inahitajika ukitaka kumpeleka mgonjwa nje ya Tanzania unaandaliwa na mkuu wa kitengo hospitali, hili la kulipia ndio nalisikia leo hupaswi kulipia.

By the way medical report kazini kwako wao ya nini?
Maybe anataka kuhama mkoa
 
Huyu Janabi ni mtu mjinga sana....hivi kwa aina na hali za kiuchumi za wagonjwa wa MNH unawatoza laki moja just for medical report?....
Huyu jamaa serikali inamlea sana simply because alikuwa na JK...
Ila ni mtu wa hovyo sana...
 
Huyu Janabi ni mtu mjinga sana....hivi kwa aina na hali za kiuchumi za wagonjwa wa MNH unawatozalaki moja just fo medical report?....
Huyu jamaa serikali inamlea sana simply because alikuwa na JK...
Ila ni mtu wa hovyo sana...
Ni mtu wa hovyo kweli kweli maana hili swala la medical report hata mimi limenikuta.Maana kuna kipindi nlikuwa mgonjwa nyumbani nikawa natibiwa na Bima wakuu wangu walitaka Medical report so ili nilazimu nilipie laki kama ilivyo.Unaenda kuandikiwa report na Dokta ukiingia ndani anakujibu subiri amalize kuwa tibu wagonjwa wote Report ataandika mwisho.Ukisubiria mpaka mwisho baada ya kukuandikia report ukienda kwa wale makarani wakuchapie una wakuta wamefunga wanakwambia njoo kesho.

Kesho ukienda ana kuchapia tena vizuri ukienda kwa Dokta wako kwa ajili ya kusaini ana kujibu subiri amalizie wagonjwa wake kuwatibu.Ukienda mwisho baada ya kuwatibu wagonjwa wake anasoma hiyo riport anagundua tena karani kakosea Grammaly na utaratibu ya uwandishi.Unarudi tena karani unaambiwa kaenda kula una kaa unamsubiri akitoka kula ana kujibu muda umeenda sana hiyo kazi ataifanya kesho....

Any way acha niishie hapo tuu maana sitotaka kukumbuka zile taabu.
 
Rafiki yangu Janabi amekua mtu wa hovyo hivi?
Medical report ni haki ya mgonjwa.
Hospitali binafsi kubwa nilizowahi kutibiwa nilikua napewa bila shida yoyote na kwa wakati.
Kwa kweli Tanzania ni nchi ya kuajabia.
 
Kilichoongezeka ni ripoti kulipiwa. Ugumu wa kuipata upo siku nyingi sana.

Kwenye miaka ya 2000 huko nishafuata ripoti ya mzee wangu zaidi ya wiki mbili.
 
Habari za Mchana!
Utaratibu wa kulipia Medical Report umekuwepo takribani miaka mitano iliyopita. Haukuanzishwa na Prof. Janabi.

Kuhusu kuchelewa kupatikana Report hiyo, tumelichukua jambo hili ili kuliboresha zaidi.

Asanteni

Aminiel Aligaesha
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano
Hospitali ya Taifa Muhimbili
0784 648646
 
Habari za Mchana!
Utaratibu wa kulipia Medical Report umekuwepo takribani miaka mitano iliyopita. Haukuanzishwa na Prof. Janabi.

Kuhusu kuchelewa kupatikana Report hiyo, tumelichukua jambo hili ili kuliboresha zaidi.

Asanteni

Aminiel Aligaesha
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano
Hospitali ya Taifa Muhimbili
0784 648646
Ufafanuzi wako haujagusa bei...hebu gusa hilo...
Asante
 
Medical report mara nyingi inahitajika ukitaka kumpeleka mgonjwa nje ya Tanzania unaandaliwa na mkuu wa kitengo hospitali, hili la kulipia ndio nalisikia leo hupaswi kulipia.

By the way medical report kazini kwako wao ya nini?
Wewe ni daktari wa wanyama ,au mengineyo

Toka lini ,mkuu wa kitengo akaandika medico ripoti ,,anayeandika ni daktari aliyemuatendi mgonjwa ,muhuri pekee ndo kesi ya department husika....
 
Habari za Mchana!
Utaratibu wa kulipia Medical Report umekuwepo takribani miaka mitano iliyopita. Haukuanzishwa na Prof. Janabi.

Kuhusu kuchelewa kupatikana Report hiyo, tumelichukua jambo hili ili kuliboresha zaidi.

Asanteni

Aminiel Aligaesha
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano
Hospitali ya Taifa Muhimbili
0784 648646
Kiongozi, huo utaratibu wa kulipia sidhani kama upo official kwasababu hata ukilipia control number unayopewa sio ya medical report unapewa ya kulipia gharama za tiba, sababu nini?? Nafikiri ni jambo jema kama mtu akishalipia basi apewe huduma kwa wakati isiwe tena kero
 
MUHIMBILI NA URASIMU WA MEDICAL REPORT.

Nimekuwa nikiuguza mgonjwa wodini pale Jengo la Watoto Hospitali ya Muhimbili kwa vipindi tofauti tofauti, ilikuwa kuomba Medical Report ni bure, lakini kuanzia Prof. Janabi alipoingia kupata Medical report ya mgonjwa ni lazima ulipie Laki moja (Tsh. 100,000/=)

Hilo sio tatizo sana, tatizo linakuja kwamba hata baada ya kulipia hizo gharama inakupasa tena kuanza kuzunguka kuwatafuta madaktari kuwaomba waandike hiyo report, usumbufu zaidi ni kwetu sisi ambao tunatoka mkoani ukiwasiliana na watu wa masjala/PS wanakwambia mtafute daktari wake ama mpigie simu mwambie akuandikie sisi tumeshapeleka file kwake!!

Nina zaidi ya wiki 2 sasa, niko mkoani report inahitajika ofisini ila kila nikiwasiliana na wanaopaswa kuifuatilia report wananizungusha tu, sasa wameweka vipi gharama ya huduma kama hawawezi kuitoa hiyo huduma vizuri?

Hili jambo linatakiwa kushughulikiwa haraka, ni usumbufu sana!!

Majibu ya Muhimbili, soma hapa: Hospitali ya Muhimbili yatoa ufafanuzi kuhusu keri ya ucheleweshwaji wa utoaji wa Medical Report
Hao si ndo walikuwa wanajinadi siku za karibuni kwamba sasa wanaweza kupandikiza uboho kwenye mifupa? Sasa Kama kuandaa medical report ni shida kwao, kupandikiza uboho wanaweza kweli hao?
 
Habari za Mchana!
Utaratibu wa kulipia Medical Report umekuwepo takribani miaka mitano iliyopita. Haukuanzishwa na Prof. Janabi.

Kuhusu kuchelewa kupatikana Report hiyo, tumelichukua jambo hili ili kuliboresha zaidi.

Asanteni

Aminiel Aligaesha
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano
Hospitali ya Taifa Muhimbili
0784 648646
Urasimu wa upataji ya hii medical report umetengeneza mazingira ya rushwa mdogo aliangaika Sana week mbili ikabidi arudi kituo Cha kazi anatakiwq kuja muhimbili Kila mwezi kwa ajili ya matibabu sasa bosi hamwelewi ndio maana ilihitajika hiyo medical report.
 
Back
Top Bottom