BWANKU M BWANKU
JF-Expert Member
- Jan 12, 2019
- 328
- 414
Mbunge wa Jimbo la Muhambwe Mkoani Kigoma Mhe. Dkt. Florence George Samizi ameendelea na ziara yake ya kuelezea Utekelezaji wa Ilani ya CCM Jimboni pamoja na kusikiliza na kutatua kero za Wananchi ambapo Jana alikuwa na Mkutano wa hadhara Kata ya Kibondo.
Akiwa Kata ya Kibondo Wananchi wameishukuru sana Serikali ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa mbolea ya ruzuku ya kupandia ikifika kwa wakati mazao yametoka vizuri.
Hata hivyo, mbolea ya kukuzia imechelewa kufika katika Jimbo la Muhambwe na Mhe. Mbunge Dkt. Samizi aliwasiliana kwa simu na Waziri wa Kilimo Mhe. Hussein Bashe na kuahidi kuwa atahakikisha mbolea ya kukuzia inafika Muhambwe ifikapo alhamisi wiki hii.
Serikali ya Rais Samia imeendelea kufanya makubwa kwenye kilimo ikiwemo kuongeza Bajeti ya Kilimo kutoka Bilioni 294 hadi 954 na Ruzuku ya Mbolea kufikia Bilioni 150.
#KaziInaendeleaMuhambwe
Akiwa Kata ya Kibondo Wananchi wameishukuru sana Serikali ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa mbolea ya ruzuku ya kupandia ikifika kwa wakati mazao yametoka vizuri.
Hata hivyo, mbolea ya kukuzia imechelewa kufika katika Jimbo la Muhambwe na Mhe. Mbunge Dkt. Samizi aliwasiliana kwa simu na Waziri wa Kilimo Mhe. Hussein Bashe na kuahidi kuwa atahakikisha mbolea ya kukuzia inafika Muhambwe ifikapo alhamisi wiki hii.
Serikali ya Rais Samia imeendelea kufanya makubwa kwenye kilimo ikiwemo kuongeza Bajeti ya Kilimo kutoka Bilioni 294 hadi 954 na Ruzuku ya Mbolea kufikia Bilioni 150.
#KaziInaendeleaMuhambwe