Kaka hii maada imekuwa ndefu na labda nikiri kuwa pia najifunza vitu vingi sana humu ndani,
kabla sijaenda mbali ningependa nikujibu hapo juu kwenye nyekundu,
kwa mtazamo wangu Matukio ndio yanatupa muda wa kusema PAst, Present na Future, na kama nilivyosema hapo hawali hiyo past, present na future actually sio time bali ni refference ya tukio na Kama hakuna tukio unalorefer basi huwezi kuwa na Past, present na future
Kama nilivyosema hapo hawali Mimi naamini muda ni Cycle, na labda nisema ni cycle na ndio maana inakuwa ni rahisi kupredict kuwa siku fulani na mwaka fulani Jua litapatwa na mwezi, ni kwa sababu ni mzunguko unaojirudiarudia
Lakini pia nakubali Muda ni linear kutokana na tafsiri ya matukio, nikiwa na maana muda unaoneka kuwa uko linear kwa sababu ya jinsi tunavyoyatafrisi matukio, labda nitoe mfano hapa
tuseme mwaka 2010 SAA SITA MCHANA, eruption imetokea kwenye Mlima Kilimanjaro, na mwaka 2014 SAA SITA MCHANA eruption imetokea Mlima Meru, sasa hapa ukiangalia utaona time inajirudia rudia tu kote ni saa sita mchana lakini sio mwaka mmoja, kuna tofauti ya miaka minne kutoka tukio moja kwenda lingine
maana yake nini?
kwa kuangalia mfuatano wa matukio utaona time ni linear, yaani tukio la pili limetokea miaka minne mbele ya la kwanza, lakini ukiangalia kiundani mwaka 2014 ni mjumuisho wa sekunde, dakika, saa, siku, wiki na miezi iliyokuwa inajirudiarudia (Cycle). siku, wiki na miezi iliyopo kwenye 2014 ndio hiyo hiyo iliyopo kwenye 2010 lakini 2014 ni jumla ya siku wiki na miezi ya 2010,2011,2012 na 2013
so time ni cycle ila tafsiri yetu ya matukio ndio inatuonyea kuwa time ni linear