Lema anapata kiburi cha kuropoka mitandaoni kwa sababu yeye ni kijana wa Mtei.
Mtei alikataa kushiriki kupigania uhuru, akakata kujitolea kuitumikia nchi katika kipindi kigumu na sasa anataka kuivuruga nchi kwa kupitia Chadema!!!
Ubinafsi mbaya sana...
Magamba bwana kwa kupotosha!
Unalijua lengo la kupigania uhuru wewe!?Ilikuwa ni kupigania nchi yetu ili tujiongoze wenyewe na kutoa haki sawa kwa watanzania wote bila ubaguzi wala manyanyaso.
Je,malengo hayo yamefikiwa?Wapigania uhuru wote wamemwaga damu zao bure,kwani yote waliyopigania mmeyatupa kapuni.Kama vile;
Mmeuza ardhi yetu bure kwa wageni na kuwafukuza watanzania wazalendo na kuwafanya manamba kwenye ardhi Yao wenyewe.
Mmegawa maliasili zetu bure kwa wageni kama gesi na kusaini mikataba ya siri yenye manufaa kwenu na kwa familia zenu.
Mmeharibu elimu kwa makusudi ili kizazi cha CCM ndicho kiendelee kuwa tabaka tawala milele.
Mmeua tembo wetu kwa tamaa tu ya utajiri na kuiba twiga kwa kuwasafirisha nje ya nchi kwa manufaa yenu binafsi na ya familia zenu.
Mmeua baadhi ya wale wote wanaowapinga kwa kuhofia kuhatarisha maslahi yenu na wengine kuwapa vilema vya kudumu.
Mmebaka watoto wetu na kuwaambukiza HIV kana kwamba hiyo ni agenda yenu mojawapo kwenye kampeni zenu huku mkitamba kuwa hakuna wa kuwagusa.
Mmefanya ufisadi wa kutisha kwenye makampuni ya serikali huku mkiwalazimisha wananchi walipe madeni na hasara mliyoyaingizia hayo makampuni kwa makusudi,kama ambavyo mmewapandishia bei ya umeme kwa 68% na kuwakejeli juu kwa kuwaambia kama hawawezi wawashe vibatari!
Mmeua miundo mbinu ya reli kwa makusudi ili muweze kufanya biashara kupitia mabasi na malori mnayoyamiliki wenyewe.
Mmetengeneza barabara zilizo chini ya kiwango ili muundelee kujitajirisha kupitia pesa za matengenezo za barabara hizo.NK..
Na kama hao wapigania uhuru wanaona hayo mnayoyafanya huko walipo wanajuta na pengine wanajiuliza walipoteza nguvu zao na maisha Yao kwa ajili ya nini?wakati hamuuenzi uhuru huo?