VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,140
- 18,006
Tutawajua.Tutawajua kama walikuwa wanafiki au wakweli.Tutawajua kama walifurahia kilichofanywa kwao au walichukia. Tutawajua kama kuchoma kwao majengo kulikuwa ni mikwara mbuzi tu na hawakuwa serious. Tutawajua wana-Mtwara na Lindi Jumapili. Siku ya uchaguzi wa Serikali za Mitaa.
Najua wanakumbuka kilichotukia.Wanakumbuka songombingo la gesi asilia na utawala wa kijeshi huko. Wanakumbuka kiapo chao cha kuishikisha adabu CCM huko Mtwara na Lindi. Sasa muda umewadia. Muda wa utekelezaji wa kiapo chenu ni sasa. Muda wa kuonesha ukweli wa kauli zenu ni huu.
CCM tukishinda kwa ushindi wa kimbunga Mtwara na Lindi,wana-Mtwara na Lindi mjiandae kutulipa nyumba na majengo mengineyo mliyoachoma huku mkiapa kutuchapa bakora za kiuchaguzi. Ni muda wenu wa kufanya uamuzi mgumu.
Mambo yote ni Jumapili tarehe 14/12/2014! Wana-Mtwara na Lindi kazi ni kwenu!
Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam
Aione: THE BIG SHOW
Najua wanakumbuka kilichotukia.Wanakumbuka songombingo la gesi asilia na utawala wa kijeshi huko. Wanakumbuka kiapo chao cha kuishikisha adabu CCM huko Mtwara na Lindi. Sasa muda umewadia. Muda wa utekelezaji wa kiapo chenu ni sasa. Muda wa kuonesha ukweli wa kauli zenu ni huu.
CCM tukishinda kwa ushindi wa kimbunga Mtwara na Lindi,wana-Mtwara na Lindi mjiandae kutulipa nyumba na majengo mengineyo mliyoachoma huku mkiapa kutuchapa bakora za kiuchaguzi. Ni muda wenu wa kufanya uamuzi mgumu.
Mambo yote ni Jumapili tarehe 14/12/2014! Wana-Mtwara na Lindi kazi ni kwenu!
Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam
Aione: THE BIG SHOW
Last edited by a moderator: