Mtwara: Madaktari wafanikiwa kuondoa damu kwenye ubongo wa mtoto

Suley2019

JF-Expert Member
Oct 7, 2019
1,820
4,573
1683809662700.png

JOPO la Madaktari katika Hospitali ya Rufaa ya Kanda Kusini, Mtwara wamefanya upasuaji wa kuondoa damu kwenye ubongo wa mtoto wa miaka tisa kwa mafanikio makubwa baada ya kutumia vifaa vya kisasa kufanya uchunguzi na kubaini tatizo hilo.

Akizungumza Kwa njia ya simu na chombo kimoja cha habari kuhusu upasuaji uliofanyika jana, Dk Hashimu Titto wa hospitali hiyo amesema kuwa wamefanya upasuaji wa kwanza kwa mafanikio makubwa kwa mtoto wa miaka tisa aliyegongwa na pikipiki.

“Zoezi la kutoa damu iliyovilia kwenye ubongo wa mtoto mdogo baada ya kupata ajali limefanyika kwa utaalam mkubwa na kwakweli limefanikiwa, awali tulifanya vipimo na uchunguzi na ikagundulika kuwa na damu kwenye ubongo iliyovilia baada ya kupata ajali ya kugongwa na pikipiki,”amesema.

Credit: Nipashe
 
Damu kwenye ubongo? Kweli?
Kwamba unataka kubisha au hujawahi sikia ama
Common kesi za kugongwa na gari au pkpk ajari
Shida huwa damu kuvilia kwenye UBONGO
muhimbili walikuwa hawajiangaishi Madocta
nduguyo anakufa huku unamuona na wakifanya watarudia hata mara 2 kurekebisha Hovyo sana

Kama mtwala wamefanikiw hilo HONGERA sana kwao MADOCTOR
hii inawezekana sasa MCHAWI ni VIFAA VYA KISASA au MADOCTA WAZOEFU
 
Keep monitoring tuone atapona, wengi end up with permanent neurological damage or death several days after surgery. Operation za kichwa zina very poor prognosis in tanzania and in Africa, I want results after 2weeks sio sasa
Upo sahihi
 
Keep monitoring tuone atapona, wengi end up with permanent neurological damage or death several days after surgery. Operation za kichwa zina very poor prognosis in tanzania and in Africa, I want results after 2weeks sio sasa

Penye mazuri pongeza. Hiyo hatua ni nzuri
 
Ohhh wow! Hongera kwao wataalamu wetu.
Watu kama hawa wanahitaji motisha yakutosha kabisa.
 
Back
Top Bottom