Prof. Makubi: Majeruhi wengi tunaowapokea MOI ni bodaboda ambao wanakuwa wameumia mifupa na ubongo

Nyakijooga

Senior Member
Dec 9, 2018
123
202
Mkurugenzi wa Taasisi ya Tiba ya Mifupa Muhimbili (MOI) Prof Abel Makubi amesema asilimia kubwa majeruhi wa ajali wanaowapokea ni 'bodaboda' na kuwa wengi wao wanakuwa waneumia mifupa na ubongo.

Ameyasema hayo leo jijini Dar es Salaam Machi 25, 2024 katika Mkutano wa Kimataifa wa wataalamu wa ubongo,mishipa ya fahamu na uti wa mgongo ulioandaliwa na MOI kwa kushirikiana na Chuo na Hospitali ya Well Cornel iliyopo nchini Marekani
WhatsApp Image 2024-03-25 at 18.35.56_1bca79a9.jpg

WhatsApp Image 2024-03-25 at 18.35.58_833a3852.jpg
“Kwa wastani kwenye idara ya magonjwa ya dharura tunapokea wagonjwa 15 hadi 20 ambao wanatokana na dharura mbalimbali na 60% zinatokana na ajali na wengi ni bodaboda, tatizo ni kubwa wengi wanakuwa wameumia mifupa na ubongo,”ameeleza.

Aidha akieleza kuhusu mkutano huo unaofanyika kwa siku nne, amesema unatoa mafunzo ya tiba inayotokana na ajali zinazoumiza ubongo na kuwa yatawasaidia wataalamu kuwatibu watu walioumia kwa ajali zilizoathiri ubongo na mgongo.

“Wataalamu wanajengewa uwezo kuwatibu kwa umahiri na kupunguza matatizo yanayotokana na ajali tumekuwa tukishirikiana kwa muda wa miaka 12,” amesema.
WhatsApp Image 2024-03-25 at 18.35.56_f8cd1396.jpg

WhatsApp Image 2024-03-25 at 18.35.57_60e85a75.jpg

WhatsApp Image 2024-03-25 at 18.35.58_3c76f278.jpg
Ameongeza kuwa kupitia ushirikiano huo, wataalamu kutoka ndani na nje ya nchi wamekuwa wakifanya kazi kwa kushirikiana, kufanya tafiti katika maeneno ya tiba ya ubongo na wamekuwa na vifaa vya zaidi ya bilioni moja ambavyo vimewasaidia katika upasuaji wa ubongo.

“Pia tunapata wataalamu kutoka Marekani ni ushirikiano wa faida kwa pande zote mbili kila mwaka tunakutana,” amesema.

Licha ya hivyo Prof. Makubi amesema idadi ya wataalamu hao bado ni ndogo, ambapo ameweka wazi kuwa MOI kuna madaktari bingwa 12 na nchi nzima wako 23 ikilinganishwa na idadi ya Watanzania.

Kwa upande wa Daktari Bingwa wa Upasuaji wa Ubongo, Uti wa Mgongo na Mishipa ya Fahamu, Dk Hamisi Shabani amesema kabla upasuaji wa uti wa mgongo wagonjwa walikuwa wanapelekwa nje lakini sasa wote wanatibiwa ndani.

“Sasa imepatikana hamasa ya madaktari kujifunza, mimi nilikuwa daktari wa tatu walipokuja sasa wako 23, ila sio somo gumu ambalo watu wanatakiwa kukimbia imekuwa rahisi kwetu kuongeza ujuzi tofauti na awali,” amesema.

Amesema wana wanafunzi sita kutoka nje ya nchi na wanne wa ndani ya nchi na kwamba watatumia teknolojia mpya baada ya vifaa kuletwa vya endoscopy, ambapo mgonjwa atakaa saa chache hospitali.

Ameongeza kuwa bado kuna uhaba wa madaktari bingwa, ambapo kwa viwango vya Shirika la Afya Duniani (WHO) kwa nchi zinazoendelea daktari mmoja anatakiwa kuhudumia wagonjwa 100,000 kwa mwaka, huku kwa sasa nchini daktari mmoja akihudumia wagonjwa milioni 1.2 kulingana na idadi ya Watanzania .

Pia Prof Roger Hartl kutoka Chuo cha Well Cornel amesema amejifunza mbambo mengi baada ya kuja Tanzania ambayo yamemsaidia kuhudumiwa wagonjwa wake huko Marekani.

“Tumetengeneza mfumo wa kufundisha wataalamu kwa kubadilishana ujuzi wanakuja kwetu na sisi tunakuja kwao ili kuhakikisha tunahudumia wagonjwa kwa namna ya kufanikiwa ,”ameeleza.
 
Lawama ziende Kwa Rais wetu mpendwa Samia Suluhu Hassan.

Yeye badala ya kuwaongezea adhabu kali bodaboda watii sheria Kwa lazima, yeye kawafutia adhabu kutoka 30K Hadi 10K.

Madhara yake ndio haya
 
Anakosea kuwaita bodaboda hao ni Maafisa usafirihaji kwa mujibu wa ccm..
Na asilimia kubwa siku hizi kwenye vijiwe vyao kuna picha mama, pia vizibao(reflector) zao zina picha.
Boda mbona hutumila na vyama vyote? Au hujaona wakishiriki maandamano na misafara ya wapinzani?.
 
Maelezo mazuri yenye matumaini yasiyo na SIASA wala UCHAWA ndani yake. Siku zote mimi naamini Madaktari bingwa ni watu wenye mioyo ya kipekee sana hasa umkute na uzoefu wa si chini ya miaka 10 mara nyingi anapokuona mgonjwa anachowaza ni kuokoa maisha yako tu.

Hongera sana kwao
 
Lawama ziende Kwa Rais wetu mpendwa Samia Suluhu Hassan.
Yeye badala ya kuwaongezea adhabu kali bodaboda watii sheria Kwa lazima, yeye kawafutia adhabu kutoka 30K Hadi 10K.

Madhara yake ndio haya
Duuh nilidhani utazungumza kuwe na mpango wa ajira kwa vijana ili wapungue huko kwenye ajali wewe unazungumzia fine daah Mzee wa Mbalizi hii sio sawa..
 
Duuh nilidhani utazungumza kuwe na mpango wa ajira kwa vijana ili wapungue huko kwenye ajali wewe unazungumzia fine daah Mzee wa Mbalizi hii sio sawa..
Bodaboda ni ajira za muda mfupi, siyo mwarobaini wa tatizo la ukosefu wa ajira.

Je nchi zote duniani Zina biashara ya bodaboda?

Great thinkers wakune vichwa kutatua tatizo la ajira, waache kujificha nyuma ya kivuli Cha bodaboda
 
Bodaboda ni ajira za muda mfupi, siyo mwarobaini wa tatizo la ukosefu wa ajira.
Je nchi zote duniani Zina biashara ya bodaboda?

Great thinkers wakune vichwa kutatua tatizo la ajira, waache kujificha nyuma ya kivuli Cha bodaboda
Yap ndio maana nasema wangeweza ingawaje ni ngumu wangefuta hizi mambo za boda boda zinadumaza sana akili wasifikiri kuwa na ajira za ukweli kwa vijana ardhi ipo na vijana kama nguvu kazi ipo ila tupo busy na siasa za uchaguzi kila kukicha.
 
Bodaboda ni ajira za muda mfupi, siyo mwarobaini wa tatizo la ukosefu wa ajira.
Je nchi zote duniani Zina biashara ya bodaboda?

Great thinkers wakune vichwa kutatua tatizo la ajira, waache kujificha nyuma ya kivuli Cha bodaboda
Kimsingi, tatizo la Ajira kwa Vijana ni Janga la Kidunia, lakini ktk nchi zetu hizi za ki-Afrika tatizo hili ni kubwa zaidi, hii ni kutokana na Serikali zilizopo kwenye hizi nchi ziko very weak for each and everything. Almost ni kama hakuna Serikali kwenye hizi nchi.
 
NINACHO WAPENDEA JAMAA
1.KUKIMBIA HOVYO BILA SBB
2.KUPIGA HONI HOVYO, KUPIGA MUZIKI KWA SAUTI YA JUU
3. KU-OVERTAKE MAGARI HOVYO HOVYO
4.KUWASHA TAA FULL LIGHT
5.WANAJIONA WENYE HARAKA KUPITA WENGINE
6.NDIO WATU PEKEE WANAOZIJUA SHERIA ZOTE ZA BARABARANI.
7.ASIMILIA KUBWA HAWANA LESENI

VYEMA, AJALI ZIKAENDELA KUTOKEA.
ILI WATU WAACHE KUZITUMIA
 
Aliposema Bilioni moja ,ni fedha shilingi bilioni moja? Kwamba vifaa vyenye thamani hiyo?
 
Mkurugenzi wa Taasisi ya Tiba ya Mifupa Muhimbili (MOI) Prof Abel Makubi amesema asilimia kubwa majeruhi wa ajali wanaowapokea ni 'bodaboda' na kuwa wengi wao wanakuwa waneumia mifupa na ubongo...
Lema alishatoa angalizo.
 
Back
Top Bottom