GODZILLA
JF-Expert Member
- Dec 26, 2014
- 5,902
- 10,503
Tafuta wanasheria wakusaidie Bwana mdogo. Sheria hazisomwi namna hii ya kupesti maandishi na kukariri.SURA YA KUMI NA NNE
MAKOSA YANAYOHUSIANA NA DINI NA MAZISHI
125. Mtu yeyote ambaye atavunja, kuharibu na kuchafua mahali popote pa kuabudia au kitu chochote kinachoitwa kitakatifu na watu wa aina yeyote kwa madhumuni ya kufedhehesha dini ya kundi lolote la watu au kwa kufahamu kuwa kundi lolote la watu linataka kufanya uharibifu, hasara au uchafuzi kama fedheha kwa dini atakuwa ametenda kosa.
126. Mtu yeyote ambaye kwa hiari yake ataleta fujo kwenye mkusanyiko wowote ambao umekusanyika kihalali kufanya ibada au sherehe za dini ametenda kosa.
127. Mtu yeyote ambaye, kwa madhumuni ya kuumiza imani za mtu yeyote au kufedhesha dini ya mtu yeyote, au kwa kufahamu kuwa imani ya mtu yeyote inaweza kuumizwa, au dini ya mtu mwingine iko hatarini kufedheheshwa, ametenda kosa la kuingia kwenye eneo la kuabudia bila ruhusa eneo la makaburi matakatifu au kwenye eneo lolote ambalo limetengwa kwa ajili ya mazishi au kama bohari ya mabaki ya maiti, au atafanya dhuluma yeyote kwa maiti ya binadamu au atafanya fujo kwa watu wowote waliokusanyika kwa ajili ya mazishi, atakuwa ametenda kosa.
128. Mtu yeyote ambaye bila halali anazuia mazishi ya mwili wa mtu yeyote aliyekufa au mtu ambaye, bila mamlaka halali kwa niaba hiyo au vinginevyo kulingana na kanuni iliyowekwa na Waziri anayehusika na afya (ambayo unamuongoza Waziri aliyepewa mamlaka kufanya) anafukua kaburi, anapasua, au anafanya uharibifu wowote kwenye mwili wa mtu yeyote aliyekufa au ambaye, anawajibika kufanya maiti ya mtu yeyote izikwe, kwa hiari yake na bila kupewa idhini na mamlaka halali anapuuza kutimiza wajibu wake kwa makusudi , atakuwa ametenda kosa.
129. Mtu yeyote ambaye kwa dhamira ya kuudhi imani ya mtu yeyote ya dini yake akatamka maneno yeyote au akafanya sauti yeyote itakayosikiwa na mtu huyo au akafanya ishara mbele ya macho ya mtu huyo atakuwa ametenda kosa.
ᴸᵉᵍᵉⁿᵈᵃʳʸ
Sent using Jamii Forums mobile app