Mtu ukiwa na pesa, somesha mwanao international schools, achana na hizi exam based schools or education

Ndio nimsomeshe shule za maana akimaliza akahonge K ndio apate kazi?
Au km wa kiume bado aendelee kua tegemezi?
Kila mtu anapenda mwanae asome vizuri shida ipo hakuna uhakika wa ajira umemaliza akiba yako kasoma mwishowe aambiwe ajiajiri wakati kula yenyewe tabu, ni aibu mwanao kasoma ana digrii yake alafu akawe mmachinga, au auze genge au akalipwe mshahara wa laki 3 au 5 si bora aanze harakati zake mapemaaa.

Nimeishia msingi lakini kipato changu kwa mwezi hata mwenye madigrii yake hanifikii hapo nimefanya maujinga mengi tu.
 
Mpaka mtoto anamaliza shule, mfugale inanyanyuka na chenchi inabaki. View attachment 1609854
aisee!!!!


Hivi jamani lazima tujiulize kwanza tunataka elimu yakupambana na matatizo tulionayo au tunataka elimu yakujiweka katika level za dunia na kupata miashara ya world class .

Kwa Mimi ninavyoelewa elimu ya msingi niele inayokupa mwanga juu ya mazingira unayoyaishi na elimu ya juu niile inayokuandaa wewe kufanya Jambo flani. Sasa hii elimu ya juu huwa inazingatia Sana uchumi,maligafi jiografia,Sanasana katika Mambo ya sayansi na technology. So mm sioni Kama Kuna haja ya mtu kusoma elimu ya nchi za watu wenye uchumi wa mbali. Nakati wewe huna uchumi wa kukimbizana na hayo maarifa. Hafu by BTW maarifa hayatafutwi kwa kusoma tu tukiwa watu wakusoma tu hatutaweza kubuni Mambo yetu wenyewe. Tutaishia kusoma vya watu na kulipa liseni zisizokuwa na tija.

Jamani tuache kutafuta sababu elimu ya tz inatosha kabisa kuanzisha mapambano. Hafu tusi ilaumu Sana serikali nakati wanafunzi nao nichanzo kikubwa cha kuzolota kwa elimu maana ukiwa secondary utaskia watu wanataka kuwa T.O cjui na ukiwa chuo watu wataka kazi. Na mtaani kazi hamna
 
International schools are not for everybody, hata ulaya na marekani kuna private na public schools. Jambo la muhimu ni kuwa na mitaala inayoendana na wakati na mazingira. Mfano, kuna haja gani ya mwanafunzi wa sekondari kusoma masomo 8 hadi 10?
 
Mitahala ya kawaida ili kiwafanya watu kuwa na uwezo Mdogo wa kuhoji. Tanzania zaidi uijuavyo
You have a point.

Tangu enzi ya chama kimoja, wanasiasa wa Afrika wanaogopa sana wanafunzi wa vyuo.

Sifurahii kuona kila chuo muhimu Tanzania kina Rais mtaafu au waziri mstaafu kama mkuu wa chuo. Hii inaleta picha mbaya kuwa vyuo haviko huru kusomesha.
Mkuu wako kama ni Rais mtaafu, unaweza kweli kuandika thesis ya kukosoa uongozi wake bila ya kufukuzwa au kupewa adhabu?

Pia, kuwalazimisha wanafunzi kwenda jeshini (miaka ya nyuma) kabla ya kuanza chuo kimesababisha wazazi wengi kukataa kuwapeleka watoto wao vyuoni. Kuna vizazi viwili Tanzania wamebaki na Form 4 au Form 6 kwa sababu wazazi hawana uwezo wa kuwapeleka nje na wanaogopa kuwapeleka watoto wao jeshini kwa sababu tofauti.

Je, tumekosa wahitimu wangapi wangesaidia kubeba uchumi wa nchi kwa sababu hii?

Najua kuna nchi nyingi wana sheria hii kama Korea Kusini, mimi naongelea wazazi wa Tanzania na matatizo ya kiuchumi ya Tanzania ya miaka 1974-1984.
 
aisee!!!!


Hivi jamani lazima tujiulize kwanza tunataka elimu yakupambana na matatizo tulionayo au tunataka elimu yakujiweka katika level za dunia na kupata miashara ya world class .

Kwa Mimi ninavyoelewa elimu ya msingi niele inayokupa mwanga juu ya mazingira unayoyaishi na elimu ya juu niile inayokuandaa wewe kufanya Jambo flani. Sasa hii elimu ya juu huwa inazingatia Sana uchumi,maligafi jiografia,Sanasana katika Mambo ya sayansi na technology. So mm sioni Kama Kuna haja ya mtu kusoma elimu ya nchi za watu wenye uchumi wa mbali. Nakati wewe huna uchumi wa kukimbizana na hayo maarifa. Hafu by BTW maarifa hayatafutwi kwa kusoma tu tukiwa watu wakusoma tu hatutaweza kubuni Mambo yetu wenyewe. Tutaishia kusoma vya watu na kulipa liseni zisizokuwa na tija.

Jamani tuache kutafuta sababu elimu ya tz inatosha kabisa kuanzisha mapambano. Hafu tusi ilaumu Sana serikali nakati wanafunzi nao nichanzo kikubwa cha kuzolota kwa elimu maana ukiwa secondary utaskia watu wanataka kuwa T.O cjui na ukiwa chuo watu wataka kazi. Na mtaani kazi hamna
Nchi zote zinategemeana kielimu Mkuu.

Wanafunzi wa Archeology na lugha wanakuja kusoma Tanzania, Egypt au Ethiopia. Sociologists wanakuja kusoma jinsi tunavyoishi. Wanafunzi wa siasa na biashara wanakuja kufanya research tofauti Afrika.

Na sisi tunakwenda kwao kusoma zaidi kuhusu mbinu mpya za kutibu magonjwa na kupata ujuzi mwingine kama wa kufanya repair ndege za abiria au za kijeshi.

Hata Marekani, yenye vyuo zaidi ya 5000, inakaribisha wasomi wa dunia kila mwaka kuendeleza elimu. Inajua kila msomi ana ujuzi utakaosaidia kuitajirisha nchi yao.

Dunia ya sasa ni multiculrural na inategemeana sana kuliko unavyofikiri.
Hatujafika bado kiuchumi kujitemegea wenyewe kielimu. Ingekuwa hivyo, tusingeagiza magari au vifaa vya hospitali, tungetengeneza wenyewe.
 
Nchi zote zinategemeana kielimu Mkuu.

Wanafunzi wa Archeology na lugha wanakuja kusoma Tanzania, Egypt au Ethiopia. Sociologists wanakuja kusoma jinsi tunavyoishi. Wanafunzi wa siasa na biashara wanakuja kufanya research tofauti Afrika.

Na sisi tunakwenda kwao kusoma zaidi kuhusu mbinu mpya za kutibu magonjwa na kupata ujuzi mwingine kama wa kufanya repair ndege za abiria au za kijeshi.

Hata Marekani, yenye vyuo zaidi ya 5000, inakaribisha wasomi wa dunia kila mwaka kuendeleza elimu. Inajua kila msomi ana ujuzi utakaosaidia kuitajirisha nchi yao.

Dunia ya sasa ni multiculrural na inategemeana sana kuliko unavyofikiri.
Hatujafika bado kiuchumi kujitemegea wenyewe kielimu. Ingekuwa hivyo, tusingeagiza magari au vifaa vya hospitali, tungetengeneza wenyewe.
mkuu kujitegemea kielimu sio tu kuwa na uchumi wakuendana na maarifa ya watu flani. Ila pia nikuwatengeneza watu kuwa tayari kuweza kuendeleza maarifa kutoka kwenye maarifa A,B,C za misingi ya dunia. Hafu umesema kuwa nchi zitagemeana kielimu hiyo ni kidogo tu ila Sehemu kubwa watu ambao hawawekizi kati uvumbuzi ndio tegemezi kielimu kama sisi Africa. Ila mmarekani ndio anategemewa Sehemu kubwa na nchi mbalimbali na yeye hategemia Sana maarifa kutoka kwao ila return ya utegemezi wa nchi hizo unarudi Kama pesa. Mfano ndio hiyo ulioeleza hapo juu kuwa mmarekani inapokea wanafunzi toka nje. Pia vitu Kama license. Kununua product zao nk

Mkuu kujitegemea kielimu ni maswala ya kuumiza kichwa sio uchumi.
 
mkuu kujitegemea kielimu sio tu kuwa na uchumi wakuendana na maarifa ya watu flani. Ila pia nikuwatengeneza watu kuwa tayari kuweza kuendeleza maarifa kutoka kwenye maarifa A,B,C za misingi ya dunia. Hafu umesema kuwa nchi zitagemeana kielimu hiyo ni kidogo tu ila Sehemu kubwa watu ambao hawawekizi kati uvumbuzi ndio tegemezi kielimu kama sisi Africa. Ila mmarekani ndio anategemewa Sehemu kubwa na nchi mbalimbali na yeye hategemia Sana maarifa kutoka kwao ila return ya utegemezi wa nchi hizo unarudi Kama pesa. Mfano ndio hiyo ulioeleza hapo juu kuwa mmarekani inapokea wanafunzi toka nje. Pia vitu Kama license. Kununua product zao nk

Mkuu kujitegemea kielimu ni maswala ya kuumiza kichwa sio uchumi.
Mkuu, kila nchi inaenda katika stage sawasawa. Na wananchi wa nchi masikini wana bahati ya kuruka stage.
Mfano wa matumizi ya simu. Nchi tajiri ilianza na lisimu likubwa nyumbani mpaka kufika tochi nokia na apple. Nchi za kumasikini sasa zinatumia simu latest ya mkono na kuruka kutumia simu size ya walkie talkie au mchi wa mbuni. Pia M-pesa imeweza kuanzisha matumizi mengine ya simu kwa manufaa ya nchi masikini isiyo na watumizi wa benki wengi. Actually, M-pesa wako mbele kuliko Japan kwa kuwa Japan ni cash-based nation.

China ina viwanda vya kila aina. Lakini imefika tayari stage ya nchi tajiri. Wananchi wake wanataka mshahara mkubwa na maisha yanakuwa ghali. Kwa hivyo, viwanda vinahama na kwenda Vietnam, Indonesia na Malaysia. Nchi hizi zimeshajitayarisha kielimu , kisiasa na kibiashara kukaribisha wawekezaji. Nao watavuka stage hii na kuwa tajiri zaidi kama Singapore au Japan.

Tanzania ipo stage ya kwanza ya maendeleo. Ina raw materials lakini bado haina viwanda vingi vyenye kuipa mauzo mengi duniani. Inahitaji elimu ya nchi tajiri kujenga viwanda na kununua mashine za viwanda. Na pia inahitaji elimu ya kutengeneza vitu vyenye thamani kubwa ili ipate faida kubwa. Kahawa Arabica top quality ni $3 kwa kilo. Kuuza simu moja top quality ni $1000. Kilimo kinalisha nchi lakini hakitajirishi nchi. Na tunategemea elimu ya wenzetu kutuvuta stage ya nchi za ASEAN na baadae Dunia ya Kwanza.

Tanzania inazalisha $60 billion or so. Ina watu 56m. Itahitaji GDP $500B kufika stage ya ASEAN peke yake.

Hatuwezi kufika huko bila ya kubadili mfumo wa elimu yetu na fikra zetu . Siasa zetu zinazeta "political instability" ambayo inaleta "economic instability".

Mfano mdogo ni wa Ex-RC Makonda kwenda Clouds kuwaadhibu na wanausalama wa Ikulu au kumweka ndani mfanyabiashara yoyote kwa sababu katiba inamruhusu kufanya chochote kwa ubabe.

Angekuwa nchi zinazoheshimu sheria, asingepewa haki ya kufanya hivyo kwa sababu inaleta picha mbaya kwa wawekezaji na wafanyabiashara wa ndani wataogopa kuwekeza zaidi.

Tabia hii ndio sababu moja tu inayofanya tuzalishe $60B na sio $600B kwa mwaka.

We have a long way to go.
 
Mimi naona mitaala ya kufundishia maana walimu waliotoka vyuo vyetu nao hufundisha hzo shule wakutoka nje ni wachache Sana,
Sipendi ku reply ila kwa uwongo wako nooo..nimesoma Forest hill,walimu wengi wageni,
Mimi naona mitaala ya kufundishia maana walimu waliotoka vyuo vyetu nao hufundisha hzo shule wakutoka nje ni wachache Sana,

Mimi naona mitaala ya kufundishia maana walimu waliotoka vyuo vyetu nao hufundisha hzo shule wakutoka nje ni wachache Sana,
 
Mkuu, kila nchi inaenda katika stage sawasawa. Na wananchi wa nchi masikini wana bahati ya kuruka stage.
Mfano wa matumizi ya simu. Nchi tajiri ilianza na lisimu likubwa nyumbani mpaka kufika tochi nokia na apple. Nchi za kumasikini sasa zinatumia simu latest ya mkono na kuruka kutumia simu size ya walkie talkie au mchi wa mbuni. Pia M-pesa imeweza kuanzisha matumizi mengine ya simu kwa manufaa ya nchi masikini isiyo na watumizi wa benki wengi. Actually, M-pesa wako mbele kuliko Japan kwa kuwa Japan ni cash-based nation.

China ina viwanda vya kila aina. Lakini imefika tayari stage ya nchi tajiri. Wananchi wake wanataka mshahara mkubwa na maisha yanakuwa ghali. Kwa hivyo, viwanda vinahama na kwenda Vietnam, Indonesia na Malaysia. Nchi hizi zimeshajitayarisha kielimu , kisiasa na kibiashara kukaribisha wawekezaji. Nao watavuka stage hii na kuwa tajiri zaidi kama Singapore au Japan.

Tanzania ipo stage ya kwanza ya maendeleo. Ina raw materials lakini bado haina viwanda vingi vyenye kuipa mauzo mengi duniani. Inahitaji elimu ya nchi tajiri kujenga viwanda na kununua mashine za viwanda. Na pia inahitaji elimu ya kutengeneza vitu vyenye thamani kubwa ili ipate faida kubwa. Kahawa Arabica top quality ni $3 kwa kilo. Kuuza simu moja top quality ni $1000. Kilimo kinalisha nchi lakini hakitajirishi nchi. Na tunategemea elimu ya wenzetu kutuvuta stage ya nchi za ASEAN na baadae Dunia ya Kwanza.

Tanzania inazalisha $60 billion or so. Ina watu 56m. Itahitaji GDP $500B kufika stage ya ASEAN peke yake.

Hatuwezi kufika huko bila ya kubadili mfumo wa elimu yetu na fikra zetu . Siasa zetu zinazeta "political instability" ambayo inaleta "economic instability".

Mfano mdogo ni wa Ex-RC Makonda kwenda Clouds kuwaadhibu na wanausalama wa Ikulu au kumweka ndani mfanyabiashara yoyote kwa sababu katiba inamruhusu kufanya chochote kwa ubabe.

Angekuwa nchi zinazoheshimu sheria, asingepewa haki ya kufanya hivyo kwa sababu inaleta picha mbaya kwa wawekezaji na wafanyabiashara wa ndani wataogopa kuwekeza zaidi.

Tabia hii ndio sababu moja tu inayofanya tuzalishe $60B na sio $600B kwa mwaka.

We have a long way to go.
nimekuelewa Sana unachokieleza ni kutafuta maendeleo kwa kuvutia wawekezaji si ndio . Sasa kwenye hili swala serikali ndio zinawajibu wakufanya haya China imeendelea kwa serikali za Mao zhedong naimetumia hii kusomesha wanafunzi huku ikiandaa mazingira mazuri ya uwekezaji. Sasa mpendwa serikali za Africa zimeshindwa kufanya hilii kabisa kwakua zinakumbwa na Mambo mengi a figisu za hao wanaojiita mabeberu kwa kuwa resources zinawindwa vibaya mno. Rushwa nyingi zinaanzishwa na hao mabeberu kwa mfano kina tshombe na Mobutu wa congo wote hao ni mipango ya mabeberu. Hata hapa bongo in 1980's kulikua na mfumo bomba waelimu lakini yule waziri "x" waelimu inasemekana alipewa rushwa akanza kuleta Mambo ya physics with chemistry sijui kutoa michezo mashuleni. Ndio maana Magufuli amemuweka mmama kwa kuona anamsimamo flani.


Sasa mapendekezo yangu ni kutafuta maendeleo kwa kuanzia na vijana. Unajua hata U.S.A ilikua haijaendelea kuliko ulaya lakini ilipo anzisha high school iliwafanya vijana kuweza kuwa creative mno bila ya hata kuwa na vyuo vingi watu Kama kina Edison, Ford, wright brothers waliweza kufanya Mambo ambayo hata dunia ya leo haijayabadilisha. So kwa tz mm naona vijana tuanze kwa mfumo waelimu uliopo maana uko poa Sana sema hatujalenga katika objectives Bali ni kufaulu tu. Tz ni kati ya nchi chache zenye A level system ambao mm ninauona kuwa ni mzuri kwa sababu mtu unasoma misingi ya dunia.


Vijana tukiendelea kusema kila siku serikali hatutatoboa
 
nimekuelewa Sana unachokieleza ni kutafuta maendeleo kwa kuvutia wawekezaji si ndio . Sasa kwenye hili swala serikali ndio zinawajibu wakufanya haya China imeendelea kwa serikali za Mao zhedong naimetumia hii kusomesha wanafunzi huku ikiandaa mazingira mazuri ya uwekezaji. Sasa mpendwa serikali za Africa zimeshindwa kufanya hilii kabisa kwakua zinakumbwa na Mambo mengi a figisu za hao wanaojiita mabeberu kwa kuwa resources zinawindwa vibaya mno. Rushwa nyingi zinaanzishwa na hao mabeberu kwa mfano kina tshombe na Mobutu wa congo wote hao ni mipango ya mabeberu. Hata hapa bongo in 1980's kulikua na mfumo bomba waelimu lakini yule waziri "x" waelimu inasemekana alipewa rushwa akanza kuleta Mambo ya physics with chemistry sijui kutoa michezo mashuleni. Ndio maana Magufuli amemuweka mmama kwa kuona anamsimamo flani.


Sasa mapendekezo yangu ni kutafuta maendeleo kwa kuanzia na vijana. Unajua hata U.S.A ilikua haijaendelea kuliko ulaya lakini ilipo anzisha high school iliwafanya vijana kuweza kuwa creative mno bila ya hata kuwa na vyuo vingi watu Kama kina Edison, Ford, wright brothers waliweza kufanya Mambo ambayo hata dunia ya leo haijayabadilisha. So kwa tz mm naona vijana tuanze kwa mfumo waelimu uliopo maana uko poa Sana sema hatujalenga katika objectives Bali ni kufaulu tu. Tz ni kati ya nchi chache zenye A level system ambao mm ninauona kuwa ni mzuri kwa sababu mtu unasoma misingi ya dunia.


Vijana tukiendelea kusema kila siku serikali hatutatoboa
Mkuu Bruno, nimekuelewa sana ila napingana na mawazo yako kidogo.

Kwanza, "architect of development" wa China ni Deng Xiaoping na sio Mao Zedung. Mao alichukia matajiri na mfumo wa kibepari.

Pili, hamna nchi ambayo haijawahi kuibiwa na "mabeberu". China iligawanywa na wazungu lakini sasa imeweza kuikomboa HK na Macau. Taiwan itakuwa vigumu bila ya kuiharibu uchumi wa China. Marekani anatafuta njia ya kumrudisha nyuma kimaendeleo kama alivyofanya Iran, Iraq na nchi nyingine. China haitaingia kwenye mtego wa kuikomboa Tauwan kwa sababu itakuwa vita vya dunia vya tatu.

Anyway, sikubaliani kuwa vijana wana nafasi ya kutoboa bila elimu ya juu. Sababu ndogo ni kuwa hamna nchi inayojitoboa kirahisi hivyo. Njia kuu ya kujitajirisha ni kuuza bidhaa kwa wingi nje. Na huwezi kufanya hivi bila ya kutumia elimu ya juu yenye mfumo unaokwenda na wakati (MBA imeanza juzi tu UDSM) na kuwa na serikali inayoheshimu demokrasia na yenye sera nzuri za biashara.

Mabeberu wako na wataendelea kuwepo. Ukiwa na serikali bora, italinda maslahi ya nchi na pia itafanya biashara inayoheshimu sheria za biashara za kimataifa.
Nchi nyingi zina asilimalu lakini rasilimali ni mali iwapo umeshazalisha na kuuza. Vijana hawana uwezo wa kufanya biashara hizi bila ya mkopo na elimu.

Wakati wa kutoa sababu nyingi kwa nini Tanzania bado haina uwezo wa kuwapa maji safi na umeme wananchi wake wote hamna zaidi ya mfumo mbaya wa elimu na siasa. Tuna miaka karibu 60 ya uhuru. Nchi nyingine pia zilikuwa vitani na mabeberu lakini zimetoboa haraka sana (Singapore, Malaysia, Vietnam, Indonesia, Brazil)

This excuse hold no water. Hasa ukitegemea kuwa tukiwa na shida tunawatumia mabeberu hawa hawa kuomba msaada kwa zaidi ya miaka 50 mfululizo.

Mwalimu Nyerere mwenyewe, pamoja na kufuata siasa ya kijamaa za akina Mao na Karl Marx, alikwenda Scotland sio Beijing kusoma na aliamua kupata matibabu na kufariki nchi ya mabeberu ya Uiingereza sio China wala Urusi.

Whatever happened to live by example?

Elimu inayokwenda na wakati na yenye mfumo bora kutoka nursery mpaka chuo kikuu ndio njia pekee ya kupata maendeleo haraka. Singapore ni kisiwa chenye watu milioni 5, nusu wakiwa wageni. Rasilimali yake si dhahabu wala mbuga za wanyama bali elimu bora tu. Sasa ni matajiri kuliko beberu wa Uiingereza, mkoloni wake.
 
Uwezo wa kuajiri wengine unaweza kuwa ni kigezo kimoja wapo maana hata huko nje tunakokusifia si kwamba kila mtu kajiajiri. Lakini pia na wewe unaweza kuleta vigezo vingine na kuvijengea hoja badala ya kusema tu nilichoandika mimi hakitoshelezi.
Kuhusu IST kuwa msaada kwao binafsi na familia zao, hayta wa Kayumba pia ni msaada kwao na familia zao kwa uwezo wao. Je tuishie kuwa kila mtu asome kwaajili ya maendeleo yake binafsi na siyo ya jamii? ndio purpose ya elimu?

Hoja yangu ilikuwa ni vigezo gani wanavyotumia kusema elimu hiyo ni bora zaidi (ukiacha uwezo wa kujieleza kwa kingereza). Nimewafikirisha tu kwamba angalau tutumie kigezo cha uwezo wa elimu kutatua matatizo yaliyopo kwenye jamii ya Tanzania whether imepatikana international au Kayumba. Kama elimu ya intenational haiwezi kutatua changamoto za jamii kama hii ya Kayumba maana yake ni kwamba Tanzania kama nchi tutazidi kuwa masikini. Elimu yoyote ile ingekuwa bora zaidi kama ingeweza ku deal na matatizo yaliyopo kwenye context yetu sisi waTanzania. Ni mtazamo wangu tu.
Elimu sehmu nyingi Afrika ni kama mlango wa kurudisha maendeleo nyuma. Wenye elimu wengi wanaishia kupenda kupewa nafasi za juu za uongozi na kuabudiwa. Matokeo yake wageni kutoka nchi zilizoendelea ndiyo wenye uchungu na uelewa wa nini kifanyike ili Afrika iendelee. Shule nyingi za Kayumba zinatoa aina ya elimu aliyoipata rais Magufuli. Mwafunzi anapomaliza anakuwa hana uelewa wowote na alichosoma bali anageuka kuwa mungu mtu wa kupenda kuabudiwa.
 
Wewe ulikuwa na chuki tu na magu ukaamue umtaje hapa,kwani kuna msomi mwingine mwenye uzalendo na uchungu wa kuleta maendeleo Tanzania zaidi ya Magufuli?Hebu mtaje kama yupo,Tatizo mnapenda kiongozi anayeshobokea wazungu
Elimu sehmu nyingi Afrika ni kama mlango wa kurudisha maendeleo nyuma. Wenye elimu wengi wanaishia kupenda kupewa nafasi za juu za uongozi na kuabudiwa. Matokeo yake wageni kutoka nchi zilizoendelea ndiyo wenye uchungu na uelewa wa nini kifanyike ili Afrika iendelee. Shule nyingi za Kayumba zinatoa aina ya elimu aliyoipata rais Magufuli. Mwafunzi anapomaliza anakuwa hana uelewa wowote na alichosoma bali anageuka kuwa mungu mtu wa kupenda kuabudiwa.
 
Sipendi ku reply ila kwa uwongo wako nooo..nimesoma Forest hill,walimu wengi wageni,
Mimi hyo forest hill ndio naiskia leo hyo shule Mimi naongelea conditions za sasa za serikali kuhusu kuajiri watu wa nje wenye same qualifications na wabongo maana Organization nyingi ni few experts tu ndio wanaruhusiwa so uongo wangu uko wapi hapo? Au ujapitia masharti ya Sasa ya international expert maana hyo forest ya uchochoroni na ukute Ina waalimu wakenya wasio hata na kibali
 
Wewe ulikuwa na chuki tu na magu ukaamue umtaje hapa,kwani kuna msomi mwingine mwenye uzalendo na uchungu wa kuleta maendeleo Tanzania zaidi ya Magufuli?Hebu mtaje kama yupo,Tatizo mnapenda kiongozi anayeshobokea wazungu
Kuwa na uzalendo na uchungu tu hakutoshi kumfanya kuwa rais mzuri! Na nakubaliana na wewe kabisa kuwa Magufuli ana uchungu na umaskini wetu. Tatizo lipo wapi? Tatizo ni kuwa Magufuli hana karama za uongozi. Magufuli anajua matatizo yetu, Magufuli ana uchungu na matatizo yetu lakini kwa bahati mbaya sana ni kuwa Magufuli hana karama na vision za uongozi. Hapo ndipo tatizo linapoanzia. 1. Magufuli hapendi challenges na criticism. 2. Magufuli japo anajua matatizo yetu na ana uchungu nayo lakini hana vision afanye nini kutukwamua.
3. Magufuli hana convincing power bali anatumia nguvu kufanya hata sehemu ambazo hakutakiwa. 4. Magufuli analigawa Taifa badala ya kuliunganisha. Kwa kifupi ana mangufu mengi sana yanayosababishwa kukosa karama za kuongoza. Matokeo yake ni kuwa anajikuta amezungukwa na wasahabiki ambao muda wote wanamshangilia badala ya kumsaidia.
 
Tatizo lao ni moja..

Ukija kumwingiza kwenye haya maisha ya mtanzania ya kupambania kombe hawezi

Yaani ni wazubaifu mno.
 
Nitajie mtu mmoja mwenye karama ya uongozi na ambaye ametusaidia au kuisaidia nchi kimaendeleo baada ya Nyerere?
Kuwa na uzalendo na uchungu tu hakutoshi kumfanya kuwa rais mzuri! Na nakubaliana na wewe kabisa kuwa Magufuli ana uchungu na umaskini wetu. Tatizo lipo wapi? Tatizo ni kuwa Magufuli hana karama za uongozi. Magufuli anajua matatizo yetu, Magufuli ana uchungu na matatizo yetu lakini kwa bahati mbaya sana ni kuwa Magufuli hana karama na vision za uongozi. Hapo ndipo tatizo linapoanzia. 1. Magufuli hapendi challenges na criticism. 2. Magufuli japo anajua matatizo yetu na ana uchungu nayo lakini hana vision afanye nini kutukwamua.
3. Magufuli hana convincing power bali anatumia nguvu kufanya hata sehemu ambazo hakutakiwa. 4. Magufuli analigawa Taifa badala ya kuliunganisha. Kwa kifupi ana mangufu mengi sana yanayosababishwa kukosa karama za kuongoza. Matokeo yake ni kuwa anajikuta amezungukwa na wasahabiki ambao muda wote wanamshangilia badala ya kumsaidia.
 
Ni kweli wewe umeona,wale wamezoea spoon feeding kwenye kila kitu.
Kama hana mzazi au mjomba kwenye maofisi au serikalini ndio basi tena
Tatizo lao ni moja..

Ukija kumwingiza kwenye haya maisha ya mtanzania ya kupambania kombe hawezi

Yaani ni wazubaifu mno.
 
Ni kweli wewe umeona,wale wamezoea spoon feeding kwenye kila kitu.
Kama hana mzazi au mjomba kwenye maofisi au serikalini ndio basi tena
Tunakutana nao mtaani

Hata hawa wa english medium za kawaida ni wazito

Ant social
Yaani ni changamoto
 
Back
Top Bottom