Mtu anaanzaje kumchukia ndugu yake?

Mtu anaanzaje kumchukia ndugu yake?

mediaman

JF-Expert Member
Joined
Mar 20, 2011
Posts
451
Reaction score
688
Nilikuwa naendesha gari langu kwa kasi, macho mbele bila kutazama tazama kushoto au kulia kwa barabara. Ndugu yangu aliniona akanisimamisha nimpe lifti lakini bahati mbaya mimi sikumuona nikampita. Tulipoonana uso kwa uso alikuwa amejaa hasira, akaniuliza kwanini siku ile alinisimamisha sikusimama. "Kwakuwa siku hizi umenunua Hummer, unatuona sisi ndugu zako hatufai, eeh? Hutaki hata kutusalimia njiani. Haya, we endelea tu." Ndugu yangu alinifokea kisha akaondoka. Japo sikuona kosa langu nilimfuata nikaenda kumuomba msamaha yaishe.

Siku nyingine ndugu yangu huyo alinipigia simu kuniomba nimkopeshe milioni mbili. Nikamjibu kuwa hapa nilipo hata laki mbili sina. Pesa nilizokuwa nazo zimetumika kukarabati nyumba yangu. Kabla sijamaliza kujieleza alikata simu kwa hasira, baadaye akanifuata nyumbani na kuanza kunigombeza: "Sema leo tujue moja, undugu umevunjika? Kwanini siku hizi hutaki kuwasaidia ndugu zako?"

Dawa ya moto sio moto, nikamjibu kwa upole kuwa ni kweli sina pesa. Nikipata nitampa hata bila kudai anirudishie. Aliondoka kwa hasira huku akiongea mwenyewe njia nzima mpaka mtaa wetu wakajua tumekosana. Huo ni mfano tu wa maisha ya ndugu na ndugu wanaokosana na kuchukiana hata kwa mambo madogo madogo.

Najiuliza mtu anaanzaje kumchukia ndugu yake? Anaanzaje kupanga kulipa kisasi au kumfanyia fitina ndugu yake kwa sababu ya mambo kama hayo huku anakiri kwamba yeye ni mcha Mungu? Katika 1Yoh 3: 14-15 tunaambiwa kwamba mtu asiyempenda ndugu yake anakaa mautini. Na kwamba yeyote amchukiaye ndugu yake anafananishwa na muuaji, na kwamba muuaji hana uzima wa milele ndani yake. Katika 1 Yohana 4:20 tunaambiwa pia kwamba Mtu akisema, anampenda Mungu, huku anamchukia ndugu yake, ni mwongo; kwa maana asiyempenda ndugu yake ambaye anamwona, hawezi kumpenda Mungu ambaye hamwoni.

Ulishawahi kuchukiwa na ndugu yako au jirani yako? Ulichukua hatua gani?
 
Pesa, Madaraka/Vyeo, Mali, nazo zinasababisha Ndugu kuchukiana, ukipata mafanikio kidogo tu tayari..

Wanaamini kupitia mafanikio hayo utaweza kuwasaidia chochote muda wowote..

Ndio tunarudi kwenye ule msemo "Huwezi kuridhisha watu wote kwa wakati wote" Na pia binadamu hawaridhiki, unaweza ukamsaidia mara moja ya pili ukakwama kidogo kumsaidia ila cha ajabu atasahau hata lile la kwanza

Vitu hivi vinatokea cha msingi wavumilie, tenda wema/hisani kadiri uwezavyo ila isizidi kipimo ukajisahau na wewe.. Chuki humtafuna anayeihifadhi... Wasamehe na Songa mbele... Maisha hayajawahi kuwa na usawa hata siku moja
 
Pesa, Madaraka/Vyeo, Mali, nazo zinasababisha Ndugu kuchukiana, ukipata mafanikio kidogo tu tayari..

Wanaamini kupitia mafanikio hayo utaweza kuwasaidia chochote muda wowote..


Ndio tunarudi kwenye ule msemo "Huwezi kuridhisha watu wote kwa wakati wote" Na pia binadamu hawaridhiki, unaweza ukamsaidia mara moja ya pili ukakwama kidogo kumsaidia ila cha ajabu atasahau hata lile la kwanza

Vitu hivi vinatokea cha msingi wavumilie, tenda wema/hisani kadiri uwezavyo ila isizidi kipimo ukajisahau na wewe.. Chuki humtafuna anayeihifadhi... Wasamehe na Songa mbele... Maisha hayajawahi kuwa na usawa hata siku moja
Naona umerudi kukamata namba moja yako mkuu 😀
 
Nilikuwa naendesha gari langu kwa kasi, macho mbele bila kutazama tazama kushoto au kulia kwa barabara. Ndugu yangu aliniona akanisimamisha nimpe lifti lakini bahati mbaya mimi sikumuona nikampita. Tulipoonana uso kwa uso alikuwa amejaa hasira, akaniuliza kwanini siku ile alinisimamisha sikusimama. "Kwakuwa siku hizi umenunua Hammer, unatuona sisi ndugu zako hatufai, eeh? Hutaki hata kutusalimia njiani. Haya, we endelea tu." Ndugu yangu alinifokea kisha akaondoka. Japo sikuona kosa langu nilimfuata nikaenda kumuomba msamaha yaishe.

Siku nyingine ndugu yangu huyo alinipigia simu kuniomba nimkopeshe milioni mbili. Nikamjibu kuwa hapa nilipo hata laki mbili sina. Pesa nilizokuwa nazo zimetumika kukarabati nyumba yangu. Kabla sijamaliza kujieleza alikata simu kwa hasira, baadaye akanifuata nyumbani na kuanza kunigombeza: "Sema leo tujue moja, undugu umevunjika? Kwanini siku hizi hutaki kuwasaidia ndugu zako?"

Dawa ya moto sio moto, nikamjibu kwa upole kuwa ni kweli sina pesa. Nikipata nitampa hata bila kudai anirudishie. Aliondoka kwa hasira huku akiongea mwenyewe njia nzima mpaka mtaa wetu wakajua tumekosana. Huo ni mfano tu wa maisha ya ndugu na ndugu wanaokosana na kuchukiana hata kwa mambo madogo madogo.

Najiuliza mtu anaanzaje kumchukia ndugu yake? Anaanzaje kupanga kulipa kisasi au kumfanyia fitina ndugu yake kwa sababu ya mambo kama hayo huku anakiri kwamba yeye ni mcha Mungu? Katika 1Yoh 3: 14-15 tunaambiwa kwamba mtu asiyempenda ndugu yake anakaa mautini. Na kwamba yeyote amchukiaye ndugu yake anafananishwa na muuaji, na kwamba muuaji hana uzima wa milele ndani yake. Katika 1 Yohana 4:20 tunaambiwa pia kwamba Mtu akisema, anampenda Mungu, huku anamchukia ndugu yake, ni mwongo; kwa maana asiyempenda ndugu yake ambaye anamwona, hawezi kumpenda Mungu ambaye hamwoni.

Ulishawahi kuchukiwa na ndugu yako au jirani yako? Ulichukua hatua gani?

Wanaionea wivu HAMMER yako....
1620055006271.png
 
Pesa, Madaraka/Vyeo, Mali, nazo zinasababisha Ndugu kuchukiana, ukipata mafanikio kidogo tu tayari..

Wanaamini kupitia mafanikio hayo utaweza kuwasaidia chochote muda wowote..


Ndio tunarudi kwenye ule msemo "Huwezi kuridhisha watu wote kwa wakati wote" Na pia binadamu hawaridhiki, unaweza ukamsaidia mara moja ya pili ukakwama kidogo kumsaidia ila cha ajabu atasahau hata lile la kwanza

Vitu hivi vinatokea cha msingi wavumilie, tenda wema/hisani kadiri uwezavyo ila isizidi kipimo ukajisahau na wewe.. Chuki humtafuna anayeihifadhi... Wasamehe na Songa mbele... Maisha hayajawahi kuwa na usawa hata siku moja
Hakika: "chuki humtafuna anayeihifadhi".
 
Sasa si bora wewe kakutolea povu hajakulaani?

Mie niliambiwa najidai, mtu akasema naombea apate ajali na gari lake na hiyo kazi afukuzwe tuone kama ataendelea kujidai

Hao watu wanasema hivyo ni wale ndugu zako umekua nao bega kwa bega katika hali zote na kuna wakati umejinyima ili uwawekee sawa mambo yao. Kumbe vyovyote unavyofanya hauwaridhishi.

Nilichokuja kugundua, binadamu wote kama sio wengi wetu tuna roho ya ubinafsi ( kwanini isiwe mimi) tofauti inakuja pale unapojitahidi kuishinda hiyo roho mbaya na inakupa furaha ya kuishi na watu.

Hivyo basi, ukiwa kwenye jamii, ukiwa kazini, ukiwa na ndugu, jua kabisa watu hawafurahii mafanikio yako, kuanzia wanaosema hadi wale walionyamaza, enenda kwa tahadhari.

Si kazi ndogo kuifunza nafsi iushinde ubaya kwa wema. Ufurahie kwa dhati mafanikio ya mwingine, sio rahisi, lakini ukiweza kufikia hapo, utajiepusha na maradhi mengi sana.

Mwisho, nauchukia umasikini sana!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom