Mtu akifa anaenda wapi?

Mtu akifa anaenda wapi?

Hata ulivyokuwa kiunoni mwa wazazi wako ulikuwa hujui kama utakaa kwenye uterus, ukakaa na hapo pia ulikuwa hujui kama utakuja duniani na ukaja

Sasa unapata wapi jeuri ya kuwa na confidence ya kujibu hivyo?
Wapo viumbe wengine ambao sio binadamu lakini mifumo yao ya uzazi, kuishi na kifo inafanana na binadamu,, kwanini Sasa kwa binadamu kifo chake kiwe tofauti?
 
Sayansi haijwahi kusema ukweli.
Ina Jaribu kusema ukweli.
Ngoma itarudi pale pale "Akili"
 
Binadamu tunapenda kujipa umuhimu sana mbele ya viumbe wengine.
Wewe na kuku mnashare vitu vingi sana in common. Tofauti ni za kimaumbile tu, ila wote tukifa, tuna-decompose kwa hatua zilezile.
Kiroho, binadamu na kuku wanatofautiana kabisa. Kuku hana roho inayoweza kuwasiliana na Mungu au kutafuta maana ya maisha ya milele; maisha yake huongozwa na silika na uhai wa kimaumbile pekee. Binadamu, tofauti na kuku, amepewa roho ya kipekee inayomfanya atafute uhusiano na Muumba, afikirie kuhusu maisha ya baadaye, na awe na hamu ya kuishi kwa maadili na imani.

Kinafsi, kuku ana nafsi ya kinyama tu nafsi inayojidhihirisha kwa hisia zake za hofu, njaa, tamaa ya kuzaliana, na tabia za kimaumbile. Hata hivyo, binadamu ana nafsi iliyo pana zaidi: ina akili, mawazo, hisia, na matamanio makubwa yanayohusiana si tu na maisha ya sasa, bali pia na ndoto, malengo, na maamuzi ya kimaadili. Kwa hiyo, tofauti kuu ni kwamba kuku ana nafsi ya kimsingi bila roho, lakini binadamu ana nafsi na pia roho, na hivyo kumpa upeo wa kipekee wa kiroho, kiakili, na kimaadili.
 
Kwani Lazaro alipokufa Yesu alipomfufua alitokea wapi?

Kitabu cha Wakristo kinasema alikuwa kaburini

YOHANA 11:38-44
38 Yesu akafika penye kaburi akiwa amefadhaika sana. Kaburi lenyewe lilikuwa katika pango ambalo mlango wake ulikuwa umezibwa kwa jiwe.

39 Akasema, “Ondoeni hilo jiwe.” Dada yake mare hemu, Martha, akasema, “Bwana, patakuwa na harufu kali kwani siku nne zimepita tangu azikwe.”

40 Yesu akamjibu, “Sikukuam bia kama ungeamini ungeuona utukufu wa Mungu?”

41 Kwa hiyo wakaliondoa lile jiwe. Yesu akaangalia mbinguni akasema, “Baba ninakushukuru kwa kunisikia.

42 Ninajua ya kuwa huwa unanisikia wakati wote, lakini nimesema hivi kwa faida ya hawa walio hapa, ili wapate kuamini ya kuwa umenituma.”

43 Baada ya kusema haya akapaaza sauti akaita, “Lazaro, toka nje!”

44 Yule aliyekuwa amekufa akatoka, mikono yake na miguu yake ikiwa imeviringishiwa vitambaa. Yesu akawaambia, “Mfungueni awe huru!”


Kwa hiyo binadamu akifa anaenda kaburini
 
Mfano mwepesi unaoweza kukuelewesha juu ya uwepo wa nafsi na roho ni pale unapolala, mwili wako unakuwa umechoka na unatulia kupumzika. Huu ndio unaouona kwa macho sehemu inayohitaji usingizi, chakula, na pumziko.

Wakati mwili unalala, nafsi yako bado inafanya kazi. Ndipo mtu anaweza kuota anatembea, anaongea, au yuko sehemu fulani, ilhali mwili wake bado uko kitandani.
Huo ni ubongo.
 
Huo ni ubongo.
Najiuliza kwani mtu akiwa amekufa ndio ikawa nitolee bila hiyo mbinguni na jehanam kuna hasara gani, kwanini watu wanatamini zaidi kuendelea kuishi baada ya kufa ? Kwani ukifa ukawa tu kama hukuzaliwa kuna tatizo gani?
 
Hata ulivyokuwa kiunoni mwa wazazi wako ulikuwa hujui kama utakaa kwenye uterus, ukakaa na hapo pia ulikuwa hujui kama utakuja duniani na ukaja

Sasa unapata wapi jeuri ya kuwa na confidence ya kujibu hivyo?
kama reasoning yako iko severly restricted/compromised, u must believe in anything about religion and any religion (invented by your fellow human beings)
 
😡 hakuna moto/jehanam, hizo verse zimetengenezwa ili kuleta utulivu duniani, na kudhibiti tabia za watu, Mungu hana vitisho na kama alituumba hawezi tutupa motoni tuunge for endless time, akiwa anatuona na kufurahia maumivu tunayopata
I believe if there is any kind of god, he cannot be a sadist, If he really is all-powerful and all-knowing, why does he let his own creation go through so much shit?

View: https://youtu.be/TpawdjeH-8w?t=31

haya maswali yapo makini sana
 
Hakuna uhai kabla ya kuzaliwa, Vivyo hivyo hakuna uhai baada ya kufa.

Hukuwa na uhai kabla hujazaliwa, Vivyo hivyo hutakuwa uhai baada ya kufa.

Hakuna roho.

Mtu akifa haendi popote.

Ukifa unaoza na kuwa udongo.
 
Kuna wahindu huwa dini yao imejificha sana ila wanazo logic kidogo kuliko hawa wana mbinguni
ukiweka logic unaonekana huna spiritual mkuu, mimi wangekua wanasema "hilo sjui" nisingekua na shida sana ila kitu kikiwa hakileti mantiki anakimbilia spiritual huu ni utapeli wa wazi
 
at the cross

Msingi wa sadaka ya Yesu Kristo upo hapa:

1. Sadaka za Dini za Asili
Katika tamaduni nyingi za Kiafrika, imani ya mizimu na roho za mababu ilikuwa na nafasi kubwa katika maisha ya kila siku. Watu waliamini kwamba mababu waliokufa bado wanashirikiana na walio hai, na walihitaji kupewa heshima ili wasije wakaleta mikosi au matatizo. Sadaka za damu ya wanyama kama vile kuku, mbuzi au ng’ombe zilitolewa ili “kupooza” mizimu na kuhakikisha familia au jamii nzima inabaki salama. Damu ilichukuliwa kama kitu cha thamani kwa sababu ndani yake kuna uhai wa mnyama, na kumwaga damu ilikuwa kama kutoa kitu muhimu sana kwa ulimwengu wa roho.

Lengo la kutoa sadaka hizo lilihusiana na masuala ya maisha ya kila siku. Mfano, kama kijiji kimekumbwa na ukame, au mtu anaumwa kwa muda mrefu bila tiba, familia ingeenda kutafuta mganga wa jadi ambaye angependekeza kafara ya damu. Damu hiyo ingepelekwa chini ya mti mtakatifu, kando ya kaburi la babu, au mahali ambapo mizimu waliaminiwa kukaa. Watu waliona kafara hii kama njia ya kuondoa mikosi na kupata baraka mpya. Kwa namna hiyo, sadaka ilitambulika zaidi kama mkataba wa kiroho kati ya walio hai na waliokufa.

Mfano wa kawaida ni jamii za Wazaramo na Wanyamwezi, ambapo kuku au mbuzi huchinjwa kwenye sherehe fulani, damu yake ikimwagwa ardhini kama “kifungu” cha maombi. Wazee husema maneno ya kutuliza mizimu, wakiamini kwamba baada ya sadaka hiyo, mambo yatanyooka. Ingawa sadaka hizo zilituliza mioyo ya watu, hazikuwa na nguvu ya kudumu katika kuondoa uovu wa ndani wa mwanadamu au dhambi mbele ya Mungu.

Hivyo basi, sadaka kwa mizimu zililenga zaidi kutuliza nafsi na jamii, kuliko kutoa suluhisho la kiroho la kudumu. Ziliwapa watu hisia ya usalama, lakini kimsingi hazikubadilisha hali ya dhambi. Sadaka hizi ni mfano wa kiu cha mwanadamu kutafuta upatanisho na ulimwengu wa roho, kiu ambacho kilihitaji kujibiwa kwa njia ya kina zaidi na ya kweli.

2. Sadaka za damu katika Agano la Kale

Katika historia ya Israeli, Mungu aliweka utaratibu wa sadaka kupitia Sheria ya Musa. Lengo lilikuwa kuwafundisha Waisraeli kwamba dhambi si jambo dogo bali inaleta mauti. “Kwa kuwa uhai wa mwili u katika hiyo damu” (Mambo ya Walawi 17:11), Mungu aliamua damu iwe alama ya upatanisho. Wanyama wasio na dosari walichinjwa, damu yao ikimwagwa juu ya madhabahu, kama ishara kwamba dhambi imesamehewa kwa muda kwa gharama ya maisha ya mwingine.

Kila aina ya sadaka ilikuwa na maana maalum. Sadaka ya dhambi ilitolewa mtu akifanya kosa la kisheria, sadaka ya amani iliashiria shukrani, na sadaka ya kuteketezwa ilionyesha kujitolea kwa Mungu. Lakini zote zilihusisha damu, zikionyesha kuwa hakuna msamaha bila kumwaga damu. Kwa mfano, kila mwaka kulikuwa na Siku ya Upatanisho (Yom Kippur), ambapo Kuhani Mkuu pekee aliingia Patakatifu pa Patakatifu nyuma ya pazia, na kunyunyiza damu juu ya kiti cha rehema kwa ajili ya taifa zima (Mambo ya Walawi 16:14-15).

Mfano hai ni katika Kutoka 12, ambapo damu ya mwana-kondoo ilipakwa milangoni mwa Waisraeli usiku wa Pasaka. Malaika wa mauti alipowaona, aliwapita bila kuua wazaliwa wao wa kwanza. Hii ilikuwa picha ya nguvu ya damu kuokoa kutoka hukumu. Hata hivyo, damu hii haikuondoa kabisa dhambi zao, bali iliwakumbusha kila mara hitaji la sadaka kubwa zaidi.

Kwa hivyo, sadaka za Agano la Kale zilikuwa kivuli cha kile kilichokuwa kimepangwa na Mungu. Ziliwafundisha watu maana ya toba na ukaribu na Mungu, lakini hazikuwa suluhisho la milele. Zilikuwa maandalizi ya kuja kwa Sadaka ya Kristo, ambaye ndiye Kondoo wa Mungu wa kweli.

3. Sadaka ya Yesu Kristo na pazia kupasuka

Yesu Kristo alikuja kama utimilifu wa sadaka zote. Yeye hakuwa tu mwanadamu mkamilifu bali pia Mwana wa Mungu. Alijitoa mwenyewe msalabani, akimwaga damu yake kwa ajili ya dhambi za ulimwengu mzima. Tofauti na wanyama wa Agano la Kale, Yesu hakuwa na dhambi na sadaka yake haikuhitaji kurudiwa mara kwa mara. Alitoa dhabihu ya mara moja, ambayo inatosha kwa vizazi vyote (Waebrania 10:12-14).

Kifo cha Yesu kilionyesha kuwa gharama ya dhambi imelipwa kikamilifu. Badala ya damu kufunika dhambi kwa muda mfupi, damu yake ilifuta kabisa deni la dhambi kwa yeyote anayemwamini. Hii ndiyo maana Injili zinaita Yesu “Kondoo wa Mungu aichukuaye dhambi ya ulimwengu” (Yohana 1:29). Kwa damu yake, mwanadamu anaweza kupata msamaha wa kweli na uzima wa milele.

Mfano wa nguvu wa ushindi wa Yesu ulionekana pale pazia la hekalu lilipopasuka kutoka juu hadi chini wakati alipokufa (Mathayo 27:51). Pazia hilo lilikuwa kizuizi kati ya mwanadamu na uwepo wa Mungu. Kwa kupasuka kwake, Mungu alionyesha kwamba njia ya kuingia Patakatifu pa Patakatifu imefunguliwa si kwa damu ya wanyama tena, bali kwa damu ya Kristo. Sasa kila mtu anaweza kumkaribia Mungu moja kwa moja kwa jina la Yesu.

Hii ndiyo maana kuu ya sadaka ya Yesu. Tofauti na sadaka za mizimu Afrika ambazo ziliwapa watu tumaini la muda, na tofauti na sadaka za Agano la Kale ambazo zilikuwa kivuli tu, Yesu alileta suluhisho la kweli na la milele. Kwa damu yake, pazia limepasuka, na mwanadamu ana uhuru wa kuingia katika uwepo wa Mungu bila kizuizi.
 
  • Thanks
Reactions: _ly
Hakuna uhai kabla ya kuzaliwa, Vivyo hivyo hakuna uhai baada ya kufa.

Hukuwa na uhai kabla hujazaliwa, Vivyo hivyo hutakuwa uhai baada ya kufa.

Hakuna roho.
Kabisa uhai unaanza siku mimba imetungwa na uhai una koma siku unakufa, kinachobaki kuendelea nimchakato wa mwili wako ndani ya udongo kuzalisha nishati nyingine kuendeleza mzunguko wa uhai kwa viumbe wengine.
 
Back
Top Bottom