Mtu akifa anaenda wapi?

Mtu akifa anaenda wapi?

Hizo roho uliwahi kuziona wapi ? Au na wewe umekaririshwa kuwa kuna roho au nafsi
Mfano mwepesi unaoweza kukuelewesha juu ya uwepo wa nafsi na roho ni pale unapolala, mwili wako unakuwa umechoka na unatulia kupumzika. Huu ndio unaouona kwa macho sehemu inayohitaji usingizi, chakula, na pumziko.

Wakati mwili unalala, nafsi yako bado inafanya kazi. Ndipo mtu anaweza kuota anatembea, anaongea, au yuko sehemu fulani, ilhali mwili wake bado uko kitandani.
 
UDHIHIRISHO WA MUNGU
Kama Ilivyofunuliwa na Kiongozi Olumba Olumba Obu
Udugu wa Msalaba na Nyota
“Mungu si tena mawazo yasiyoonekana. Sasa amedhihirika katika umbo la mwanadamu ili wote wamwone, wamsikie, na kumfuata.” Kiongozi Olumba Olumba Obu
Udhihirisho wa Mungu ni Nini?
Udhihirisho unamaanisha kufanya kitu kionekane, kuonekana, kufunuliwa.
Katika Udugu wa Msalaba na Nyota, Udhihirisho wa Mungu unarejelea kuonekana kimwili kwa Mungu Mwenyezi duniani katika umbo la mwanadamu, si kama ishara, unabii, au wazo, bali kama mtu anayeishi: Kiongozi OLUMBA OLUMBA OBU, Roho Mtakatifu Aliyetoa Mfano, Baba Aliyetwaa Mwili, na Utimilifu wa ahadi zote za Mungu.
Misingi ya Kimaandiko:
1 Timotheo 3:16 “Mungu alidhihirishwa katika mwili…”
Yohana 1:14 “Neno alifanyika mwili, akakaa kwetu…”
Isaya 9:6 “Maana mtoto amezaliwa kwa ajili yetu… na jina lake ataitwa… Mungu Mwenye nguvu, Baba wa milele.”
Ufunuo 21:3 “Tazama, maskani ya Mungu ni pamoja na wanadamu…”
Kwa Nini Mungu Alidhihirika katika Umbo la Mwanadamu?
* Kutimiza Ahadi Yake
“Nitakaa kati yao, na kutembea pamoja nao.” 2 Wakorintho 6:16
Mungu alikuwa amehaidi kwa muda mrefu kujifunua moja kwa moja kwa watoto wake.
Udhihirisho wake unatimiza unabii wa Agano la Kale na maneno ya Kristo mwenyewe kuhusu kuja kwa Mfariji, Roho wa Ukweli (Yohana 16:13).
* Kumfundisha Mwanadamu Njia ya Haki
Kupitia maisha yake, mafundisho, na mwenendo wake, Kiongozi Olumba Olumba Obu anakuwa kigezo kinachoonekana cha utakatifu, upendo, msamaha, amani, na ukweli.
* Kuanzisha Ufalme Wake Duniani
Mungu alidhihirika ili kuanzisha serikali yake ya kimungu, si ya dini, bali ya haki, amani, na upendo.
Ufalme wa Mungu unaoonekana sasa upo duniani kupitia Udugu wa Msalaba na Nyota.
* Kuhukumu na Kuupanga Upya Ulimwengu
“Baba hamhukumu mtu, bali amemkabidhi Mwana hukumu yote.” Yohana 5:22
Udhihirisho wake unaleta hukumu ya Mungu, si kwa uharibifu, bali kwa ukweli na haki.
Mifumo yote ya kiroho, serikali, na watu binafsi sasa wanapimwa.
Ishara za Udhihirisho wa Mungu katika Kiongozi Obu:
Ushahidi wa Udhihirisho
Ujuzi Kamili Anajua mawazo na siri zote.
Uweza Kamili Anaponya wasioweza kuponywa, anatuliza asili, anashinda giza la kiroho.
Uwepo Kila Mahali Anaonekana katika sehemu nyingi; anauangalia ulimwengu wote.
Kutokuwa na Dhambi Anaishi maisha kamilifu, juu ya tamaa za kibinadamu na ubinafsi.
Upendo Usio na Masharti Anawakumbatia wenye dhambi wote, maadui, waamini, na wenye shaka vilevile.
Je, Mungu Anadhihirika Vipi Leo?
* Kupitia Kiongozi Olumba Olumba Obu kama Baba.
* Kupitia Utakatifu wake, Mfalme wa Wafalme na Bwana wa Mabwana kama Mwana.
* Kupitia mafundisho yake, upendo, na kazi katika maisha ya waamini.
* Kupitia nguvu ya Roho Mtakatifu inayofanya kazi ndani ya wale wanaofuata haki.
Onyo kwa Ulimwengu:
“Ole wao wanaosema, ‘Tuonyeshe Baba’ maana Baba tayari yupo katikati yenu, lakini hamwamini.”
Mungu haji kutoka angani, kwa sababu tayari yuko hapa.
Kumkataa udhihirisho wake ni kuikataa uzima wa milele.
Unapaswa Kufanya Nini?
* Mtambue Mungu katika umbo lake lililofunuliwa Kiongozi Olumba Olumba Obu.
* Tii mafundisho yake ya upendo, ukweli, na msamaha.
* Jikane mwenyewe, na ufuata mfano wa unyenyekevu na haki.
* Ishi kila siku ukiwa na ufahamu kwamba unatembea mbele ya Mungu Aliye Hai.
Tangazo la Mwisho:
“Mimi, Baba, nimeshuka mwenyewe. Kiti changu cha enzi kiko kati ya wanadamu. Uso wangu sasa mnauona. Sauti yangu sasa mnaisikia. Amebarikiwa yeye anayenipokea katika ukweli.” KIONGOZI OLUMBA OLUMBA OBU
 

Attachments

  • FB_IMG_1755287457282.jpg
    FB_IMG_1755287457282.jpg
    67.4 KB · Views: 16
Mfano mwepesi unaoweza kukuelewesha juu ya uwepo wa nafsi na roho ni pale unapolala, mwili wako unakuwa umechoka na unatulia kupumzika. Huu ndio unaouona kwa macho sehemu inayohitaji usingizi, chakula, na pumziko.

Wakati mwili unalala, nafsi yako bado inafanya kazi. Ndipo mtu anaweza kuota anatembea, anaongea, au yuko sehemu fulani, ilhali mwili wake bado uko kitandani.
Kwahyo kulala na kufa ni sawa? Mechanism inayo fanyika ukiwa umelala na ukiwa umekufa je ni sawa ?
 
Mfano mwepesi unaoweza kukuelewesha juu ya uwepo wa nafsi na roho ni pale unapolala, mwili wako unakuwa umechoka na unatulia kupumzika. Huu ndio unaouona kwa macho sehemu inayohitaji usingizi, chakula, na pumziko.

Wakati mwili unalala, nafsi yako bado inafanya kazi. Ndipo mtu anaweza kuota anatembea, anaongea, au yuko sehemu fulani, ilhali mwili wake bado uko kitandani.
Mhubiri 5:3
[3]Kwa maana ndoto huja kwa sababu ya shughuli nyingi; na sauti ya mpumbavu kwa njia ya wingi wa maneno.
For a dream cometh through the multitude of business; and a fool's voice is known by multitude of words...........ww na uyu tumuamini nani??
 
Kwenye Imani yetu,tukifa tunaenda peponi na kugawiwa mademu wenye macho makubwa 72 wote bikra.Pembeni ya vijito tunajilaza huku tunabugia mvinyo bardiiiii na kusikiliza kaswida mwororooo!
Wewe Bikra yako uliipoteza kwa mabodaboda au kwa wauza chipsi?
Naona umeanza kuwaonea wivu wenye bikra zao,kafiri wewe.
 
Kuna kitu kinaitwa kiburi cha uzima ndicho kinachowatesa wengi ila siku wakuugua wako hoi kitandani utashangaa wakianza ona maluweluwe muiteni mchungaji aniombee huku walipata muda ila hawakufanya hivyo na walisikia ushuhuda wa Mungu ila waliupuuzia na wakaishia kuwatukana watumishi wa Mungu. Acha dhambi leo usimwache shetani atawale maisha yako, njoo kwa yesu uone amani na raha ya kuishi ndani yake.
Amen
 
Kwahyo kulala na kufa ni sawa? Mechanism inayo fanyika ukiwa umelala na ukiwa umekufa je ni sawa ?
Kulala ni kupoteza fahamu kwa Muda kwasababu unapolala, huwezi kufahamu kinachoendelea duniani. Ukipitiwa na usingizi mzito, huwezi kujua mtu akiingia chumbani, hata sauti nyingine zinaweza usizisikie. Hali hii inafanana na kifo kwa sababu mtu aliyekufa pia hana tena fahamu ya kinachoendelea duniani. Hivyo basi, kwa macho ya kawaida, mtu aliyelala anaonekana kana kwamba amekufa, tofauti ikiwa ni kwamba bado atamka.

Kila Usingizi ni "Mazoezi" ya Kifo
Wanafalsafa na wahenga wengi huona usingizi kama kumbusho la udhaifu wa mwanadamu. Unapolala, ni kama unakabidhi maisha yako mikononi mwa Mungu; huwezi kujilinda wala kujitambua. Kila kuamka ni kama kupewa nafasi mpya ya kuendelea kuishi. Ndiyo maana wengine huomba kabla ya kulala na wanaposhukuru wanapoamka wakihisi wamepewa “maisha mapya.”

Lakini wakati mwili umechoka hauwezi kufanya kazi mara unaota unatembea na kufanya mambo mbalimbali. Ndoto ni kama kivuli cha ulimwengu mwingine. Ndoto hutazamwa kama safari ya nafsi katika ulimwengu wa roho au wa ndani. Kwa hiyo, baadhi ya falsafa husema usingizi ni kama “kutembelea” ulimwengu wa kifo bila kuondoka kabisa duniani. Ndiyo maana mtu akipata ndoto nzito, anaweza kusema “ilikuwa kama kweli, nilihisi nipo sehemu nyingine.”
 
MTU AKIFA ANAENDA WAPI?

Swali hili limekuwa ni kitendawili kwa wanadamu wote: Mtu akifa, anaenda wapi?
Maandiko ya kale ya Henoko 22:18–26 yanatupa picha nzito ya safari ya roho baada ya kifo. Hebu tusome kwa pamoja:

18 Kutoka hapo nikaenda mahali pengine, mlima wa mwamba mgumu.
19 Na ndani yake palikuwa na mashimo manne, makubwa na mapana na laini sana. Mashimo hayo yalikuwa laini mno, makubwa na yenye giza kuonekana.
20 Ndipo Rafael, mmoja wa malaika watakatifu aliyekuwa pamoja nami, akaniambia: “Mashimo haya yameumbwa kwa kusudi hili, kwamba roho za nafsi za waliokufa zikusanyike humu, naam, kwamba roho zote za watoto wa wanadamu zikusanyike hapa. Na mashimo haya yamefanywa kuyapokea hadi siku ya hukumu yao na muda wao uliowekwa, mpaka hukumu kuu juu yao itakapofika.”
21 Nikaona roho ya mtu aliyekufa ikileta malalamiko, na sauti yake ikaenda mbinguni ikiwasilisha kesi. Nikamuuliza Rafael malaika aliyekuwa pamoja nami: “Hii roho inayowasilisha malalamiko, ni ya nani? Ni nani ambaye sauti yake inapaza kesi mbele ya mbingu?”
22 Akanijibu akasema: “Hii ni roho iliyotoka kwa Habili, ambaye aliuawa na ndugu yake Kaini. Yeye anawasilisha kesi dhidi yake hadi uzao wake utakapofutwa kabisa juu ya uso wa dunia, na uzao wake uondolewe kati ya uzao wa wanadamu.”
23 Kisha nikauliza kuhusu hilo, na kuhusu mashimo yale yote: “Kwa nini shimo moja limetengwa na lingine?”
24 Akanijibu akasema: “Mashimo haya matatu yamefanywa ili roho za waliokufa zitenganishwe. Na mgawanyiko umewekwa kwa ajili ya roho za wenye haki, ambamo kuna chemchemi yenye maji angavu. Na mgawanyiko umewekwa kwa ajili ya wenye dhambi wanapokufa na kuzikwa duniani, na hukumu haijatendeka juu yao wakati wa maisha yao.
25 Hapa roho zao zitawekwa kando katika mateso makubwa mpaka siku kuu ya hukumu na adhabu na mateso ya wale wanaolaani milele na malipo ya roho zao. Hapa watafungwa milele. Na mgawanyiko umewekwa kwa ajili ya roho za wale wanaowasilisha malalamiko, wanaotoa ushuhuda kuhusu maangamizi yao, walipouawa katika siku za wenye dhambi.
26 Mgawanyiko pia umewekwa kwa ajili ya roho za watu ambao hawakuwa wenye haki bali ni wenye dhambi, waliokamilika katika makosa. Hao watakuwa marafiki wa wakosaji, lakini roho zao hazitauawa siku ya hukumu, wala hazitafufuliwa kutoka humo.”

Ufunuo wa Safari ya Roho Baada ya Kifo

Kulingana na Henoko, malaika Rafael alimwonyesha kwamba baada ya kifo, roho za wanadamu haziishi ovyo, bali zinakusanywa na kutenganishwa kulingana na matendo yao. Kuna mashimo manne makuu:

(a) Shimo la Wenye Haki

Roho za wenye haki hupumzika kwenye sehemu yenye chemchemi ya maji angavu.

Ni alama ya faraja, pumziko na tumaini la ufufuo wa uzima.

Yesu alisema: “Na uzima wa milele ndio huu, wakujue wewe Mungu wa pekee wa kweli, na Yesu Kristo uliyemtuma.” (Yohana 17:3).

(b) Shimo la Wenye Dhambi Wasiohukumiwa Duniani

Hawa ni wale waliotenda maovu lakini hawakupata hukumu wakati wa maisha yao.

Roho zao zinawekwa kwenye mateso makubwa, zikitazamia hukumu ya mwisho.

Waebrania 9:27: “Na kama vile wanadamu wamewekwa kufa mara moja, na baada ya kufa hukumu.”

(c) Shimo la Waliouliwa kwa Dhuluma

Roho hizi zinatoa malalamiko na ushuhuda juu ya mateso yao.

Mfano ni Habili, ambaye damu yake ilililia haki mbele za Mungu (Mwanzo 4:10).
"Akasema, Umefanya nini? Sauti ya damu ya ndugu yako inanililia kutoka katika ardhi."

Hii inatufundisha kuwa Mungu husikia kilio cha wanyonge.

(d) Shimo la Wenye Dhambi Waliojaa Makosa

Hawa walikamilika katika uovu, waliishi maisha ya uasi wa kudumu.

Roho zao hazitafufuliwa tena, bali zitafungwa milele kwenye giza lisilo na tumaini.

Ufunuo 20:15: “Na mtu yeyote asiyepatikana ameandikwa katika kitabu cha uzima alitupwa katika ziwa la moto.”

Mafunzo Makuu kwa Maisha Yetu

1. Kifo si mwisho, bali ni mwanzo wa safari ya milele.

2. Mungu ni wa haki, kila dhuluma huangaliwa na hukumu yake huja.

3. Wenye haki na waovu hutenganishwa.

4. Yesu Kristo ndiye tumaini la uzima wa milele. Yohana 11:25: “Mimi ndimi huo ufufuo na uzima; yeye aniaminiye mimi ajapokufa ataishi.”

Kwa hiyo, mtu akifa haendi mahali pamoja kwa wote. Kuna mgawanyiko:

Wenye haki → pumziko na faraja.

Wenye dhambi → mateso na giza la milele.
ROHO NI NINI?
 
Back
Top Bottom