BINADAMU ana vitu vitatu vikuu 3
1)MWILI HUU WA NYAMA
asili yake ni mavumbi ya udongo,kuharibika,mauti ,akifa mwili huu huharibika.
2)Nafsi ..utashi..akili..memory kumbukumbu data..hizi hazifutiki,maarifa,ufahamu
3)ROHO..hii ni pumzi ya Mungu ya uhai aliyotupulizia wanadamu wote,na hii Roho pumzi ya uhai..haifi,isipokuwa Mungu pekee anaweza kuua Roho na mwili,mara nyingi Roho haifi...milele.
BAADA YA MTU KUFA/KUFARIKI
ROHO huacha mwili dakika hiyohiyo na kuvaa mwili mpya ambao hauharibiki na KUSHUKA KUZIMU
KUZIMU ni njiapanda ya kwenda either NJIA YA KUZIMU YA MATESO au kwenda njia ya MBINGUNI
Kuna tofauti kati ya Kuzimu ya mateso na JEHANAMU .
Utakatifu wako ukiwa duniani/matendo yako ukiwa hai duniani ndio yatakayo amua roho yako itakapokwenda baada ya kufa.
UTAVUNA ULICHOPANDA.
YESU alieleze hatima baada ya kufa kwa kutumia mfano wa TAJIRI NA MASIKINI LAZARO..baada ya hawa watu wawilli kufa TAJIRI ALIKWENDA KUZIMU YA MOTO kutokana na matendo yake mabaya ya uchoyo n.k akiwa duniani,na masikini Lazaro alikwenda mbinguni.
TAJIRI NA LAZARO
Luka 16:19-31 “Akasema, Palikuwa na mtu mmoja, tajiri, aliyevaa nguo za rangi ya zambarau na kitani safi, na kula sikuzote kwa anasa. Na maskini mmoja, jina lake Lazaro, huwekwa mlangoni pake, ana vidonda vingi, naye alikuwa akitamani kushibishwa kwa makombo yaliyoanguka katika meza ya yule tajiri; hata mbwa wakaja wakamramba vidonda vyake. Ikawa yule maskini alikufa, akachukuliwa na malaika mpaka kifuani kwa Ibrahimu. Yule tajiri naye akafa, akazikwa. Basi, kule kuzimu aliyainua macho yake, alipokuwa katika mateso, akamwona Ibrahimu kwa mbali, na Lazaro kifuani mwake. Akalia, akasema, Ee baba Ibrahimu, nihurumie, umtume Lazaro achovye ncha ya kidole chake majini, auburudishe ulimi wangu; kwa sababu ninateswa katika moto huu. Ibrahimu akasema, Mwanangu, kumbuka ya kwamba wewe uliyapokea mambo mema yako katika maisha yako, na Lazaro vivyo alipata mabaya; na sasa yeye yupo hapa anafarijiwa, na wewe unaumizwa. Na zaidi ya hayo, kati yetu sisi na ninyi kumewekwa shimo kubwa, ili wale watakao kutoka huku kwenda kwenu wasiweze; wala watu wa kwenu wasivuke kuja kwetu. Akasema, Basi, baba, nakuomba, umtume nyumbani kwa baba yangu, kwa kuwa ninao ndugu watano, ili awashuhudie, wasije wao pia wakafika mahali hapa pa mateso. Ibrahimu akasema, Wanao Musa na manabii; na wawasikilize wao. Akasema, La, baba Ibrahimu, lakini kama akiwaendea mtu atokaye kwa wafu, watatubu. Akamwambia, Wasipowasikia Musa na manabii, hawatashawishwa hata mtu akifufuka katika wafu.”
YESU NI KWELI MFANO HUU SIO MFANO WA KUFIKIRIKA KINADHARIA TU BALI NI HALI HALISI.
KUZIMU NI HALISI UNAWEZA KWENDA NA UKARUDI ,HATA SASA WAPO WATU WANAENDA KUZIMU NA KURUDI ,HASA WASHIRIKINA ,WACHAWI WAGANGA WA KIENYEJI,WATU MAARUFU,IKIWEMO FREEMANSORY,MITUME NA MANABII WA UONGO,WASANII,WANASIASA N.K
NB Kuzimu umegawanyika vipengele zaidi ya vitatu ,ile sehemu ya mateso wanaenda kuzimu wengi hawafiki hapo ,wanafikia mapokezi na kusaini mikataba na kupewa mahitaji nguvu,mafanikio mvuto n.k
illa kuna enzi za kuzimu au maeneo zaidi ya moja.
View: https://youtu.be/35jly4iZ5ns?si=baGYbXbXkpiJgF08
View: https://www.youtube.com/live/_tI94qsZM_g?si=ZzBrgJTSj1C9BJ15
View: https://youtube.com/playlist?list=PLXTmPgeqbJ0kKsxAotPQkrszE6Qt_Y0qk&si=F-wiPlDs89ptqmyv