Bonnie1974
JF-Expert Member
- Mar 19, 2008
- 407
- 17
Mkulu hiyo hapo imenifanya nipate picha kama vile unamCROSS EXAMINE mshtakiwa.Kama ni mimi ungeweza kuniambia .... Isingekuwa ni big deal.
I am different charater on this palnet.
Ungekuwa na maswali machache tu ya kunijibu ili kutegeneza hii issue.
Ni uwuzi, tena uwazi kabisa kabisa..ungekuokoa...But dont do this to ua husband...maana mimi naye inawezekana tunatofautiana sana.
Lakini kwanza ..tell me all this very HONESTLY...hata kama ukisikia kufa...Just tell it as it was....Jibu kama mimi ni mume wako!
Was you forced into the act?
What really drove you to that ..Chap?
Ulikuwa fully aware when you went with him?
Unafikiri mimi ningetakiwa nifanye nini ... ili usiende naye ..hapa nina maana there was ..weakness in my part ndio maana..ukapata hiyo nafasi.
Na
Kabala sijaendelea..?
Ilikuwaje Baba wa mtoto akajua kuwa una mtoto naye?
Did you tell him?
Why?
Ulivyomuabia ..didi you fill Highhh..yaani ulikuwa unajisikai vizuri..yaani kama umemkomesha mumeo .....kitu kama hicho..just be very frankly...
Let me get all this answers before you get my advice...!
I am sure all will be very fine..if this is true..story..!
"You have no right to call me father and I got no right to call you son" aliwahi kuimba Lucky Dube akielezea tukio kama la Da'Maindainda!
Japo nimechelewa pls let me share a live example related to this one:
Nina rafiki yangu wa karibu mno ambaye alililewa katika mazingara kama haya, yeye ni mzaliwa wa kwanza kwa wazazi wake, akifuatiwa na wadogo zake watatu wawili wa kike na mmoja wa kiume kwenye familia yao ya watoto wanne! Kimaisha wazazi wake hawa hawakuwa na maisha mazuri sana na huyu rafiki yangu alijitahidi mno kujaribu kuweka mambo sawa ikiwa ni pamoja kuwahudumia wadogo zake pamoja na wazazi wake.
Huyu rafiki yangu pia alijitahidi kufungua biashara ndogo ndogo kijijini kwao pamoja na kununua mashamba na BABA zake wadogo walikuwa ndio wasimamizi. Maisha yalisonga mbele kwa staili hii hadi mwaka 2005 alipougua baba yake mzazi, Rafiki yangu alifanya juhudi zote za kumpatia matibabu baba yake kwa muda mrefu bila mafaniakio na bahati mbaya baba yake alifariki mwaka huo huo. Alifanya taratibu zote za mazishi na baada ya kumaliza mambo yaliendelea kama kawaida!
KASHESHE! iliibuka mwaka 2007, ikiwa ni miaka miwili baada ya kumzika baba yake! Aliibuka baba mwingine na kudai kuwa ni mwanae! (HUYU rafiki yangu keshaoa tangu mwaka 1998 na ana watoto wawili!) Huyu baba kila kitu anafanana naye! Hiii ilimuweka huyu rafiki yangu katika hali ya kuchanganyikiwa na kutoamini na hadi leo hii hataki hata kumuona huyo baba yake mzazi (japokuwa ni mtu anayejiweza kiuchumi na rafiki yangu mambo yake sio mazuri) huyu baba kamuahidi mambo kibao lakini jamaa kagoma kabisa
KIBAYA ZAIDI baada ya huyu baba kujitokeza jamaa ilibidi amvae mama yake ambaye yuko kijijini na kumuuliza, mama alishindwa kumjibu akamuelekeza kwa wajomba zake ambao walimwambia kuwa ni kweli na hata BABA aliyemzika alikuwa anafahamu kuwa hakuwa mwanae! Baba zake wadogo nao pia walikuwa wanalifahamu hilo na walipoona kuwa ameshafahamu wakaanza kumuwekea mipaka, biashara na mashamba wamechukia na imekuwa kama wamemtenga! Jamaa amekuwa mpweke sasa kwani ndugu wa upande wa baba aliyemlea hawamtaki na wa upande wa bilogical father hawafahamu na wala hataki kuwasikia!
Honestly hii hali imemuathiri sana kisaikolojia na hata kiutendaji ameshuka sana pamoja na ushauri anaoupata mara kwa mara!
Tofauti kwa huyu rafiki yangu ni kuwa watu wengi katika familia walikuwa wanalifahamu hili baada ya mama kuamua kumueleza ukweli baba'ke kuwa wakati anaolewa alikuwa na mimba ya mtu mwingine, na huyu bwana (mwenye mimba) hakuwahi hata mara moja kujitokeza kwa mtoto.
Da'Mainda hili jambo ni gumu na lahitaji busara za ziada, ila kama ulivyoamua mueleze mumeo na pia mtoto kuepusha mabalaa ya uzeeni!
Huwezi kuwaelewa kamwe......Bibi Kizee,
Asante sana. Kuna wakati huwa siwaelewi wanaume kabisa, kwa jinsi wanavyokuwa na double standards.
Aisee hii issue inaonekana ngumu sana lakini mwisho wa siku ni ukweli tu unaotakiwa kwa mmeo na mtoto. Maana ukiacha harafu jamaa yule akaja kudai mtoto itakuwa tatizo kubwa.
Kwa wale wajuao sheria - Kisheria, huyu mtoto ni wa nani?
Kama ni wa Biological father, naweza kufanyaje awe wa kwangu?
Kama alivyoshauri Pundit, hata kama hayupo katika birth certificate, anaweza kushinda kwa kuangalia Vinasaba-DNA, kama ni mtu anaependa fujo au kuna watu hawajali ndoa zao au zimewashinda na wanaweza kutumia chochote ili mke/mume apate EXIT way. Najaribu kuwa mwangalifu hapa.
Nimewaambia jamaa zangu wa4 wakapime DNA j3 yawezekana huyu mahindamahinda akawa mke wa mmoja wao....
acha kabisa kauli hizo ndio zimenifanya nizidi kusogeza goal....Usiwapandishe presha wenzio, kwanza usikute na wao wana watoto nje kwa kujijua/kutojijua!..
Ukimchunguza sana bata hautamla nakwambia!..Wakina maindainda wapo wengi kwenye jamii sema ujasiri wa kusema ukweli hawana vile wamekosea na wataaibika pia kuogopa talaka na vitu kama hivyo!
acha kabisa kauli hizo ndio zimenifanya nizidi kusogeza goal....
yaani waendelee kuhudumia watoto wasio wao? mambo ya Saleh wa clouds Fm noma.....ushaolewa kwanini uzini nje?
acha kabisa kauli hizo ndio zimenifanya nizidi kusogeza goal....
yaani waendelee kuhudumia watoto wasio wao? mambo ya Saleh wa clouds Fm noma.....ushaolewa kwanini uzini nje?
Msanii kaka ukimwi unatafuta mwenyewe...
Hii ni kesi ngumu kiasi ...
Ifuatayo inaweza kuwa majibu ya kesi yako...
Habari insikitisha na inahuzunisha.
Ningependa kusema yafuatayo kwa dada yetu. Nami ninasema haya kama muislamu, lakini kama mhusika si muislamu, basi ningemshauri aende kwa viongozi wa dini yake, au katika taasisi za kijamii zinazohusika na maswala ya kusaidia kina mama wenye matatizo ya ndoa, akapatiwe ushauri nasaha.
Anyway, katika mafundisho ya mtume Muhammad (SAW) mtoto ni wa baba mwenye ndoa (MTOTO NI WA KITANDA) na mzinzi hana lake (MZINZI AKALE MAWE), kapoteza nguvu zake na muda wake na siku ya kiama atakuja kuadhibiwa na mola wake. Usijihisi unyonge, kata mawasiliano na huyo mtu kabisa, na akiendelea kukufuata fuata, tumia njia zote za halali kumzuia kwani anataka kukuvurugia maisha yako.
Pamoja na kuwa nimesema hayo kuna maswala mawili matatu:
Swala la kwanza ni la uzinzi na kutunza hesima ya ndoa. Kesi ya dada yetu huyu ni Case Study nzuri za athari ya mambo kama haya na inaweza ikampelekea mtu katika Dilemma na Stress ambazo hazina ufumbuzi sahihi. Ushauri wangu katika hili ni kuwa TUBU kwa mola wako, jiwekee ahadi ya kweli ya kutorudia tena, huku ukiendelea kujuta kwa yale uliyoyafanya.
Kuhusu mumeo, jitahidi kumfanyia mema mengi sana, ili kujenga mazingira ya kuwa hata kama atajua kwa namna yoyote basi atakuwa tayari kukusamehe. Pia jitahidi kuwafanyia mema familia ya mumeo kwani katika jamii zetu za kiafrika (familia) nao pia wana mchango wao katika usalama na ufanisi wa maisha ya ndoa.
La mwisho ni kuwa usimwambie mumeo, isipokuwa kama hakuna namna nyingine ya kuficha maovu ambayo yamepita. Nasema hivi kwa sababu mbili: Kwanza ni kuwa Mungu hapendi kutangaza / kueneza habari za maovu, isipokuwa kama unafanya hivyo ili kudai haki yako (Rejea 4:148). Sababu ya pili ni kuwa hatujui nini reaction ya huyo jamaa kama utamweleza habari kama hizo. Anaweza kuamua kukuuwa, hivyo utakuwa umejisababishia kifo au maangamizi, Jambo ambalo; again, ni haramu.
Binafsi kama jambo kama hili litanitokea, my WORST possible reaction will be to divorce the woman, and let her free.
hio nimeona kaka mmoja mwenye maarifa ya DINI ya Kiislam akijaribu kutoa ushauri wake, ukiona Haukutoshi, basi tafuta wengine...
Siku hizi unalea mimba mtoto akishazaliwa tu basi unahakikisha unafanya DNA kuhakikisha mtoto aliyezaliwa ni wako hasa kama anafanana na bibi au babu wa Babu wa Mke wako ambao si ajabu wewe hujui hata wanafananaje. Akili mkichwa!!!!
Siku hizi unalea mimba mtoto akishazaliwa tu basi unahakikisha unafanya DNA kuhakikisha mtoto aliyezaliwa ni wako hasa kama anafanana na bibi au babu wa Babu wa Mke wako ambao si ajabu wewe hujui hata wanafananaje. Akili mkichwa!!!!
Mchongoma,
Nimekuelewa, thanks. Nadhani tatizo kubwa lako ni hiyo jinsia tofauti maana watoto unao. If,I may ask, would you have felt differently if that child was of same sex like those at home?
Lakini, kama mtoto anapata malezi mazuri, anakua, kwanini unataka akutambue kuwa wewe ni baba yake siku moja? Umpe jina lako au?Hivi akikuita kikao wewe na mama yake kuwahoji mlivyofanya hutaona aibu? Kwanini unamtaka at some point kama anaendelea vizuri, mi nashauri kula jiwe unless yule mama ataachika kwa sababu yoyote ile au yule baba atagundua na kumkataa. Dont pressurize that woman to say or do anything pls.
Mwanamke wa kawaida hawezi kumuita mtoto wake pembeni na kumwambia baba yako ni mwingine wakati analelewa na baba mwingine. Protect her/him from this please. Mtamchanganya mtoto atahisi ha-fit hapo nyumbani wala huko kwako kwenye wengine, mwishowe ataamua kula unga, au ulevi na kukimbilia ktk mahusiano ya ma-boyfriend au ma-girlfriend kadhaa akitafuta mtu wake atakaemjali, who may take advantage na kum-break zaidi na zaidi. Utampoteza mtoto baba, shauri yako.
INaona na mimi nimetoa ushauri leo. Mengi nimejifunza humu na nakaribia kuhitimu na kuhitimisha.