Mtoto wa nje ya ndoa

Mtoto wa nje ya ndoa

DADA PLZ DO NOT TELL HIM U WILL REGRET ALL UA LIFE........LET NATURE TAKE IT'S CAUSE.....ATAKAPO JUA EITHER HUYO MUMEO AU MTOTO NDO HAPO UTAJUA JINSI YA KUJIELEZEA.......PLLZ USIMWAMBIE PLZ.....UTAJUTA DADANGU....PLZ PLZ MUME SAWA ANAKUPENDA LAKINI HATOKUSAMEHE NAKWAMBIA SIMSEMEI....LAKINI NDO HIVYO....nyamaza endelea tu kuishi till further NOTICE.:fencing::mad2::rant:

Jamani eeeeeeeeh huu ni ushauri wa kumuua kabisa do you bear in mind the situation she is in now? Kwamba jamaa wa nje anytime anaibuka and he is determined! ndio nature mnayozungumzia hapa? Keeping the secret now is more than a time bomb for her! Mnasema hivyo kwa kuwa hayajawafika; wakati mwingine extra marital affair zinawacost watu kazi na hii inaweza kuwa mojawapo ya vitisho vilivyombele yake! Acheni bwana; sio rahisi kubaki na siri namna hiyo karne hii!

Maindainda; kuna watoto mmeza na mumeo baada ya huyo wa nje?
 
Basi huyo ni Sadist; anaona au ameamua kukufanya weye ni sababu; yaelekea ulimpa ile kitu tamu kuzidi ya home kwake! Do pole sana!
Basi option B applies; hakuna dawa kama toba; ukitubu unasamehewa!

Tububi nyote kwani wote ni wakosaji na muongozwe sala ya toba na kasisi mnayemuamini mkisindikizwa na wazee wenye hekima wa kike na wa kiume!



Mkitubu mtapona na ndoa yenu itapata amani!
Na mkishasameheana hakuna kukumbushiana wala kujudge using makosa yenu ya zamani!



Sadist? Nakubali. Jamani nachoka mwenzenu, haya mambo ya kusubiri tukio linatokea lini mpaka wakati mwingine naumwa sijui naumwa nini
 
Kweli hapa kama mwanaume niliyeoa, mke wangu akija na taarifa kama hizi sijui, sijui nitafanya nini?? nitatamani dunia ipasuke inimeze nisionekane na wala kuishi na upuuzi wako. Sitakupenda tena sababu tunda langu ambalo linanifanya niwe unique, tunda ambalo linanifanya nitembee kifua mbele, yaani uwanja wangu wa nyumbani wewe umegawa kwa wengine. Hamu ya tendo la ndoa na wewe litakwisha, maana uwanja tayari utakuwa umevamiwa na magugu maji, nitahisi hamkufanya mara moja tuuu, mliendelea tena na tena kwani mlamba ASALI halambi mara moja. Bado ntahisi una wanaume dizaini hiyo wengi tuu, ntahisi hunijali wala kutambua mchango na uwepo wangu kwako. Nitajiuliza kwa nini uliamua kufunga ndoa na mimi ilhali bado una matamanio ya nje! HASIRA zitazidi kunipanda sitataka kukuona tena mbele ya upeo wa macho yangu wala karibu yangu, nitajiuliza siku zote hizi ulikaa kimya iweje leo unakuja KUNIUA na taarifa hii. Sitaweza kukupiga wala kukutukana ila nitahitaji unujibu maswali yangu kwa ufasaha. 1/ kwa nini ulilala na huyo mwanaume ilhali ukijua wewe ni mwana NDOA? 2/Ulikosa nini kwangu mpaka utoke nje ya NDOA 3/Kama ulishikwa na hamu ya GHAFLA kwa nini hukunipigia simu mie hata km umesafiri ningeweza ongea na wewe nikakupa ushauri wa kufanya na ukaepuka matamanio. baada ya hayo sasa itabaki kichwani mwangu maswali yasiyo na majibu kibao tu. kama aliweza vua nguo akapanda kitandani jamaa akammega kwa ridhaa yake, hatashindwa tena kunisaliti huyu. alilifurahia hilo tendo ndo maana miaka yote hii alikaa kimyaa!! Huyu hana tofauti na muuaji, fikiria (if) jamaa angekuwa na NGOMA, leo hii si ningekuwa na GRIDI ya taifa. Nikiendelea kuishi naye ikitokea kutoelewana tu na mimi ntahisi ataenda kwa yule jamaa yake akampe pumziko, au ntajua jamaa anampa kiburi. Kwa kweli MAISHA yangu yote utakuwa umeyaharibu!! hakutakuwa na raha tena ya MAISHA, NDOA itakuwa NDOANO, na mwisho wetu utakuwa hapo. NI KHERI LAWAMA KULIKO FEDHEHA

MY TAKE
SIKUSHAURI CHOCHOTE- ila kwa mwanaume MKE ni KIDONDA, kwa hiyo jitayarishe kwa lolote hata kulimwa RISASI(SIKUTISHI)



Chimunguru umejibu vizuri, ila umejibu kama mwanaume wa kiafrika - wanawake ndiyo wana makosa. Mimi nimesema story yangu, wapo wasiosema. Kina mama wengi wametendewa haya. Sisemi hivi kuhalalisha la kwangu, la hasha, nalionea aibu sana. If only this man could leave me alone.........basi sitaki lingine lolote, hata yeye simtaki kamwe
 
Jamani eeeeeeeeh huu ni ushauri wa kumuua kabisa do you bear in mind the situation she is in now? Kwamba jamaa wa nje anytime anaibuka and he is determined! ndio nature mnayozungumzia hapa? Keeping the secret now is more than a time bomb for her! Mnasema hivyo kwa kuwa hayajawafika; wakati mwingine extra marital affair zinawacost watu kazi na hii inaweza kuwa mojawapo ya vitisho vilivyombele yake! Acheni bwana; sio rahisi kubaki na siri namna hiyo karne hii!

Maindainda; kuna watoto mmeza na mumeo baada ya huyo wa nje?

Ndiyo yupo
 
wapendwa wana JF; Wahenga w "Uungwana ni vitendo"

Nilichangia hii post kwa "uzoefu" niliponzwa na jambo moja; kuna post inafanana na hii amabapo wahusika mume na mke walijeruhiana; yaani mume alianza kwa kuzaa na mtu mwingine nje na bibie roho ilimuuma akalipiza kisasi. Na kwa kuwa ni muda na ilifana kiasi mazingira nilikuja hapa na kuanza kuchangia moja kwa moja nikizichanganya topic mbili tofauti.

Nimekuja kugutushwa na muhusika kuwa ni yeye ndio mkosaji; na katu sio mumewe na hana hisia kuwa mumewe kamkosea na wanapendana sana.

Nimefunzwa kwetu kuwa ukikosa unaomba msamaha; ili upate amani!

Sina amani kwa sasa kwani nimewapinga wengi wenu nikiwa na hiyo dhana kichwani;

Niwieni radhi ndugu zangu, turudi kuikoa hii ndoa!
 
Chimunguru umejibu vizuri, ila umejibu kama mwanaume wa kiafrika - wanawake ndiyo wana makosa. Mimi nimesema story yangu, wapo wasiosema. Kina mama wengi wametendewa haya. Sisemi hivi kuhalalisha la kwangu, la hasha, nalionea aibu sana. If only this man could leave me alone.........basi sitaki lingine lolote, hata yeye simtaki kamwe

Kumbe humtaki hata huyo mume, mwambie basi dear unaogopa nini?
 
wapendwa wana JF; Wahenga w "Uungwana ni vitendo"

Nilichangia hii post kwa "uzoefu" niliponzwa na jambo moja; kuna post inafanana na hii amabapo wahusika mume na mke walijeruhiana; yaani mume alianza kwa kuzaa na mtu mwingine nje na bibie roho ilimuuma akalipiza kisasi. Na kwa kuwa ni muda na ilifana kiasi mazingira nilikuja hapa na kuanza kuchangia moja kwa moja nikizichanganya topic mbili tofauti.

Nimekuja kugutushwa na muhusika kuwa ni yeye ndio mkosaji; na katu sio mumewe na hana hisia kuwa mumewe kamkosea na wanapendana sana.

Nimefunzwa kwetu kuwa ukikosa unaomba msamaha; ili upate amani!

Sina amani kwa sasa kwani nimewapinga wengi wenu nikiwa na hiyo dhana kichwani;

Niwieni radhi ndugu zangu, turudi kuikoa hii ndoa!

Tuikokoe ndoa hii ya kazi gani jamani mwenzenu hata hamtaki huyo mume. Sasa si amwache tu mwenzie atafute ustaarabu mwingine, mbona wanawake tuliotulia tupo tu jamani hatuolewi, walioolewa hawatulii kuna nini? Halafu anasema huyo mumewe yupo hapa JF, ina maana kisa hiki hajakiona siku zote hizi, basi lazima kalishwa limbwata si haba!
 
wapendwa wana JF; Wahenga w "Uungwana ni vitendo"

Nilichangia hii post kwa "uzoefu" niliponzwa na jambo moja; kuna post inafanana na hii amabapo wahusika mume na mke walijeruhiana; yaani mume alianza kwa kuzaa na mtu mwingine nje na bibie roho ilimuuma akalipiza kisasi. Na kwa kuwa ni muda na ilifana kiasi mazingira nilikuja hapa na kuanza kuchangia moja kwa moja nikizichanganya topic mbili tofauti.

Nimekuja kugutushwa na muhusika kuwa ni yeye ndio mkosaji; na katu sio mumewe na hana hisia kuwa mumewe kamkosea na wanapendana sana.

Nimefunzwa kwetu kuwa ukikosa unaomba msamaha; ili upate amani!

Sina amani kwa sasa kwani nimewapinga wengi wenu nikiwa na hiyo dhana kichwani;

Niwieni radhi ndugu zangu, turudi kuikoa hii ndoa!

Tuikokoe ndoa hii ya kazi gani jamani mwenzenu hata hamtaki huyo mume. Sasa si amwache tu mwenzie atafute ustaarabu mwingine, mbona wanawake tuliotulia tupo tu jamani hatuolewi, walioolewa hawatulii kuna nini? Halafu anasema huyo mumewe yupo hapa JF, ina maana kisa hiki hajakiona siku zote hizi, basi lazima kalishwa limbwata si haba!
 
Da sophy; ukiona mwenzio ananyolewa wewe unajiandaa; usirudie kosa nililofanya mimi; niliunganisha mambo ; hapa mwanamume asiyetakiwa ni huyo jmaa wa ne aliyekutana naye briefly; sio mumewe!

Na usimlaumu Maindainda; a coin has two sides remember; pamoja na makosa yyake she still is wife material na good mother vinginevyo ; shem angekuwa kashtukia game siku nyiiiiiingi kama sio kupashwa live kabisaa mbona ndo ndio huko uswahilini wanavyofanya!
 
Tuikokoe ndoa hii ya kazi gani jamani mwenzenu hata hamtaki huyo mume. Sasa si amwache tu mwenzie atafute ustaarabu mwingine, mbona wanawake tuliotulia tupo tu jamani hatuolewi, walioolewa hawatulii kuna nini? Halafu anasema huyo mumewe yupo hapa JF, ina maana kisa hiki hajakiona siku zote hizi, basi lazima kalishwa limbwata si haba!


Da Sophy, soma vizuri mada kabla hujachangia. sijasema simtaki mume, bali huyo mwingine, na nina maana yangu ninaposema hivyo, najua ninachokiongea
 
@ Maindainda

Narudia wito wangu; ikiwa wewe ni mkristo; Tengeneza kwanza na Mungu wako! Tubu na uombe msamahama tena liwe ni zoezi la kila wakati; Mlilie Mungu kuomba msamaha na kuomba aiponye roho yako! Mkabidhi Mungu yote yanayokusibu na mwache yeye atende; wala usijaribu kulitatua hili kwa akili ya kibinadamu. Soma kitabu kitakatifu cha Biblia ; Isaya sura yote ya 55; Sikumbuki ni kifungu cha ngapi lakini nanukuu "Mawazo yenu si mawazo yangu na njia zenu si njia zangu, asema Bwana" Mungu atatenda kwa nama anavyojua yeye wee endelea kuomba ukiamni kuwa yupo Bwana atatenda.

Pili nakuasa uvunje kabisa mawasiliano na huyo jamaa; yaani hakuna kumpa hata dk 1 ya kuusikiliza huo utumbo na ikiwezekana badilisha "namna unavyowasiliana na watu" na ukishabadili yeye asijue.

Tatu; usifanye haraka ya kumwambia Mumeo; ndio sababu ya kuomba; ikiwa itahitajika yeye kujua utafika wakati muafaka na naamini huyo jamaa wa nje hana ubavu wa kuja kudai mtoto as if aliwaazimeni kitenge! ikiwa atachukua hatua ya kisheria hapo ndio utakapomweleza mwenzi wako na kwa kuwa utakuwa ukimwomba Mungu; basi hili pia will be taken care. Ukionyesha kutojali kwa vitisho vyake lazima atajiuliza mara mbili huyu jamaa na hakuna mwanaume mwenye ujasiri huo kirahisi hivyo believe me! labda ikiwa amesha sign death warranty yake yeye mwenyewe!

kwa kuwa huko kwake hakuko shwari nahisi he wants to blackmail you usimwonyeshe hofu hata chembe. Wako waliosamehewa makosa mabaya kuliko yako ndo Raha ya neno upendo! kwa Mungu wetu yote ni mepesi.

Nimeanza kuomba kwa ajili yenu; Mungu akutie nguvu na pole sana!
 
Hili tatizo ni timing bombing kama baba wa huyo mtt ni mkorofi, any time can happen jamaa anaweza akaja anytime kwa husband wako, usiposema kwa ss anaweza kutumia advantage kukutumia kwa lolote coz akitaka kale kamchezo huwezi kukataa kwasababu atakuambia nakuja nyumbani kwako kumfuata mtoto then ww utaogopa c unajua wanaume tunapenda kuumia weakness fulan

Pia ukisema, kuna advantage ya ww kuwa umezungumza ukwel unaokusumbua kwa mda mrf ila disadvantage ni nyingi sana kwan reaction ya huyo husband wako itakuwa kubwa sn

Pia inaonekana huyo mtt kafanana na mama ndio maana huyo jamaa hajashituka mpaka sasa, kosa ulilolifanya ww ni pale ulivyomumbia huyo jamaa kuwa unamimba yake hilo ni kosa kubwa sn ww ungeuchuna kwan angejulia wap na hata akijua unamkatalia?.
Kuna tafiti ilifanyika dar kupima DNA za watoto na wazazi wa kiume 40% ya wanaume waligundulika wale watoto si wao lakin wanaishi nao hiyo tafit haikuwekwa hadharani kwa sababu ya kuofia ndoa nying kuvunjika
Kama kosa limetendeka na unaona litahatarisha ustaw wa maisha yako ni bora ukae kimya siri ya mtoto aijuae ni mama

Kwa hali iliyofikia kwa hapo its better umuambie jamaa ila -ve impact ni kubwa sn hasa kama uyo baba wa mtt akiwa ni mkorofi atakusumbua sn utakosa peace of mind kama co mkorofi pls umfuate muongee kiutu uzima umwambie kosa lilishatendeka umuombe akuache utulie na ndoa yako mtoto akue at least afikishe 25 years hata yakitoea kwa huko co mbaya kwa ss mtamuathiri sn mtt kisaikolojia

NAOMBA UFANYE MAAMUZI SAHIHI KWA FAIDA YA MAISHA YAKO
 
Maindainda hope bado hujamwambia mzee kuhusu hili swala, my advise kama kweli unampenda mme basi endelea kutunza siri yako. Think of the outcome than the burden you have in your head, Wengi wanishi kwa furaha na upendo katikat ndoa zao si kwa sababu hawacheat ila kwa sababu tu hawajui kama wenza wao wanacheat. I am trying to imagine after you vomit your words kwa mme kama hakuwa mlevi sasa atalala bar, hatakuwa na amani even if takupa taraka tayari umesha mharibia maisha yake na watoto wenu. It is too late to tell him the story!!
What you need to is just to good to your husband and keep on praying Mungu aweza yote provide umedhamilia kuacha hiyo dhambi basi Mungu atakusamehe na kukulinda lakini kama bado unaendelea na hako kamchezo even if somewhere else really God will punish you na utaaibika kwa matendo yako.
my last word: FOR PEACE AND HARMONY OF YOUR MARRIGAE KEEP QUIET!!! hiyo ndiyo siri yako ya maisha usimwambie mtoto wala baba huyo jamaa anayetaka kuleta funjo ameona some weakness on you be strong and tell him you don't care whatever he will do. yeye anataka tu umtulize tena kwa kufanya naye uasharati which is very..very ...very bad!!! take care. Wazungu wanasema always say the truth but not all the truth you have to say!!
Kabla hujasema ebu angali mtoto anavyompenda baba yake mlezi na baba anavyo mpenda mtoto why do you want break that bond. it seems you are too selfish unajali zaidi amani ya moyo wako than the fate of your family!!... hiki kitendo kimeniuma sana.
anyway Nakutakia maisha mema katika ndoa yako..
 
USUTHUBUTU KUSEMA. Just sacrifice your feelings for the sake of your children and your husband. Kwa Jinsi Inavyokupain wewe, itampain mume wako mara 10 zaidi kwa maisha yake yote. Itawacost na kuwapain watoto wenu kwa maisha yao yote endapo mkiachana na mumeo. Umefanikiwa kumpunguzia mumeo miaka kumi ya machungu (kwa kumficha) na sasa kama unampenda endelea kumpunguzia, ukimwambia haitasaidia.
 
Usishangae siku unamwambia mumeo naye akakujulisha rasmi kuwa naye miaka yote alikuwa na Da Sophy kisiri! Jipu la makalioni ukilificha kuna siku litakutumbukia mchana kweupe ukiwa ngomani uadhirike maradufu. Bora ulitafutie wasaa ulitumbue kistaarabu kwa nusukaputi.
 
1. Hana uhalali wa mtoto mwanamme yeyote nje ya ndoa yake ya halali

2. Na anapobambikwa au kujibambika mtoto mwanamme pasipo na ndoa ya halai hata kama atakubaliana
na mzinifu mwenzake( mfano kama katika maisha ya unyumba bila ya kuwepo ndoa halali) basi ndio pale
jina la "mtoto wa haramu (bastard)" ndipo humuangukia yule mtoto. Maana yake ni mtoto wa baba wa
kubandikiwa.

3.Katu mtoto hawi haramu kwa mama yake. Atakuwa wa zinaa pale yule mwanamke hayupo kwenye ndoa,
lakini akiwa katika ndoa halali, basi baba wa mtoto ni mume tu, si vinginevyo kama suala lile limebakia
absolutely ndani ya moyo wa yule mwanamke.

4. Litabakiaje tu ndani wa moyo wako???. Hii itawezekana tu ikiwa zinaa ilipita kiajali/accident kwa mfano
rape ambapo akijitokeza mwanamme(rapist) au akitambuliwa na victim baada ya vyombo kufanya kazi zao
ipasavyo na rapist ku-confess, basi adhadu inayostahili hupewa yule rapist tu sio victim, kifo!!!

5. Katu hawezekani mwanamme kujua uingiaje wa mimba, potelea mbali kujua mimba ile ni kutokana na
yeye kama ilikuwa ni ajali tu, hapa kuna namna!!! Haya ni mawasiliano na maridhiano ambalo ni kosa jipya
mbali na kitendo cha zinaa chenyewe, na ndio mtego mkubwa uliyojinasisha wewe.

6. Upumbavu wa mawasiliano na makubaliano ya namna hii pengine sijui kama hukuwahi hata kumsimulia
shoga yako mama nanihii. Kama umefanya hivyo basi ni mtego mwengine huo na kosa jipya la tatu.

7. Ni haramu kujifaharisha kwa maovu yake mtu, kwa maana safari ya kujikwamua huwa complicated. Kama
hapa wewe ulikuwa na kosa mbele ya Mwenyezi Mungu tu kwa kitendo cha zinaa, na kingekuwa kitendo
cha nobility (heshima kubwa) kwako kama ungekuwa humo ndani ya ndoa, yaani hujaolewa kukataa na
katu kutomtaja yoyote kuwa ndio uliyezini nae, hata huyo jamaa. Na hata kama adhabu ingekufika kwa
maana usingekuwa na njia isipokuwa kukubali kitendo cha zinaa tu peke yake kwa maana mimba ingekuwa
wazi. Lakini hapa Mwenyezi Mungu alishakuhifadhi kwa kukujaalia kuwemo ndani ya ndoa, nini
kilichokupelekea wewe kuutawanya na kuudhihirisha uchafu wako??? Ametakasika Mwenyezi Mungu, ni
wewe mwenyewe.

8. Hata hivyo, bado una nafasi ya (1) kuzuia kusababisha fitina hapa ulimwenguni na (2) kutubia kwa
Mwenyezi Mungu, sambamba na (3) kumuomba msamaha mumeo ili upone na adhabu ya huko akhera.
Haya yote yako mikononi mwako. Lakini lazima uwe very sincere, very sincere kama unavyoanza kuonyesha
hapa. Na wala usijidanganye hata siku moja kwamba haya yataishia hapa duniani tu, kwa maana huo ni
mtego mwengine wa kishetani ambao ukiuingia ndio basi tena, moto huooooo, unakusubiri. Hili ni lazima
kesho akhera lifike. Ila ninaloelekea kukushauri mwisho wake utakuwa ni kwamba kama utafanya vizuri
katika kipengele na. 3 basi mumeo atasafisha moyo wake hapa hapa duniani na atatengeneza huruma
juu ya mkewe hapa hapa duniani ili ziwe ndio nguvu zake za kusimama na kumtetea mkewe juu ya jambo
hilo dhidi yake huko kesho mbele ya haki. Ama kipengele no. 1 na 2 ni rahisi kuvitekeleza. No. 1 kinahitaji
majuto, ujasiri, utulivu na No. 2 kinahitaji sincererity

1. Kuzuia kusababisha fitina hapa duniani:
- Never ever speak, hata salamu, hata kumtizama njiani huyo jamaa, ikitokea jicho halina pazia na
kumuona basi geuza macho chini na upite na zako, maisha na milele mpaka uzoee hivvo. Never
kujibu salamu yake sembuse kuzungumza nae.
- Kumbuka ni makosa haramu kumuambia mtoto jambo hili, na wala SIO HAKI YAKE kama
wanavyodai baadhi ya wengi eti mtoto kulijua. Nani ana haki ya kudhalilishwa???

2. Kutubia kwa Mwenyezi Mungu:
- Hili ni rahisi kidogo. Linajumuisha (a) kusitisha mara moja kosa, (b) kujutia kosa lako lile
(c) kutia nia katu kutofanya tena (d) kuomba msamaha (hapa ni M.Mungu na mumeo) na
(e) kulipa fidia kwa waathirika na kosa kama ipo (hapa haipo zaidi ya kumtaka radhi mumeo,
kumbuka yule jamaa hatambuliki kisheria na familia na ndoa yake viko safe). Ni familia yako
wewe, integrity yako na ndoa yako ndio viko maweni hapa. Hivi vipengele a, b, c, d, e ni lazima
vipambwe na SINCERERITY, SINCERERITY, SINCERERITY.
Kumbuka, japokuwa usisafirie hili, kwamba weeeengi watakaokwenda kesho akhera na mazigo
mazito zaidi ya hayo ya kwako.
3. Kumuomba msamaha mumeo:
- Ni lazima umtayarishe kwa muda mrefu, hata ikiwezekana matayarisho ya muda sawa na
maisha mliyoishi kama mke na mume au kiasi cha kuwa mzoefu mahiri wa vipengele No. 1 & 2 hapo
juu ili apokee vizuri maombi yako. Kwa kifupi badilika kitabia to his appreciation.
- Msamaha wako uwe sambamaba na SINCERERITY yako hapo juu ya kwamba unamuomba huruma
yake kama mumeo kwanza kwa kumdhalilisha yeye na pili kujidhalilisha wewe mwenyewe na
kwamba katika yote hayo wewe ndio msababishaji. Hivyo akuhurumie kwa mateso yanayokusibu
moyoni mwako kwa maisha yote haya, na vile vile akusaidie katika kukamilisha kuutafuta msamaha
wa Mwenyezi Mungu ili uokoke na adhabu ya moto.
- Ni vizuri ukawa unahadithia baadhi ya sifa za matukio matukio yaliyojiri katika muda wote wa
maisha yenu ambayo mmeishi pamoja yanaashiria heshima, mapenzi na matukuzo juu yake kama
mumeo ukiondosha kosa hilo, na kama kuna practical tranformation umepitia kuelekea hapo.
- Ikiwezekana iwe usiku mwingi kidogo watu wote wamelala

Kila la kheri, anza sasa
 
Back
Top Bottom