Mto Ruvu umekaushwa - hatari kuu ya maisha ya wana Dar es Salaam

Mhifadhi mwandamizi

New Member
Oct 26, 2022
1
1
Wakuu,

Nimesoma katika magazeti kadhaa Kwa kipindi Cha hivi karibuni habari kuhusiana na ukame unaotokana na mabadiliko Tabia ya nchi ambayo pamoja na mambo mengine yanasababishwa Kwa kiasi kikubwa sana na shughuli za Binaadamu.

Leo gazeti la JAMVILAHABARI wameandika kuhusu MTO RUVU kukaushwa na wakieleza namna mambo kama ufugaji, kilimo, ukataji miti na uchimbaji Madini unavyo athiri mto huo muhimu.

Sote tunafahamu umuhimu wa mto RUVU kwa maisha ya mwana Dar, uchumi wa Taifa na maendeleo ya nchi kwa ujumla.

Nawaomba wanajukwaa tushauriane Kwa pamoja na tufuate suluhu ya mambo haya ya Utunzaji wa mazingira.

Hivi ni Hadi lini patakuwepo na ukame huu wa kujitakia wenyewe?

Hivi Hadi lini tutaendelea kupata shida ya maji na umeme kipindi cha kiangazi?

Hivi wataalamu wetu wa Mifugo na Kilimo, wameshindwa kabisa kutengeneza mifumo kwa wadau wao Ili wafuge na walime bila kuathiri mwelekeo na mtiririko wa waji?

Hivi ni sahihi kabisa Kwa mtu kwenda kuchimba na kuchenjua Madini kwenye chanzo Cha maji?

Je hivi ni sawa kabisa Kwa mtu kichepusha mtiririko wa maji kupeleka shambani kwake Ili amwagilie maji apate hela halafu watu wanalalamika mgao?

Tutafakari pamoja

=====================

WALIVYOANDIKA JAMVI LA HABARI.

MTO RUVU UMEKAUSHWA MTO RUVU UMEKAUSHWA - Jamvi La Habari

Wakati mgao wa ,maji ukiendelea jijini Dar es salaam, hali imezidi kuwa mbaya sana katika kina cha maji kwa mto ruvu unaotegemewa kwa kiasi kikubwa kuzalisha maji jijini humo kutokana na kuharibiwa vibaya sana kwa mto huo na mito mingine midogo midogo kama mto mvuha, mgeta, Dutumi na mingine Zaidi ya 40

Uchunguzi uliofanywa na JAMVI LA HABARI umejionea namna ambavyo vyanzo hivyo muhimu vya maji vilivyoathirika huku shughuli za kibinaadamu zikiwa ni chanzo kikubwa cha uharibifu huo.

IMG-20221031-WA0054(2).jpg
====
 
Ulimwengu ulipofikia sio tena wakati wa kuwaza kupata maji kutoka mto ruvu pekee. Kuna njia nyingi za kuweza kupata maji serikali na mamlaka husika wajipapambue. Huku mtaani kwangu raia tu kachimba kisima anasupply kwa watu bei ya unit ni 2000 na mpaka leo hatujawahi kupata mgao.

Kuna mabadiliko ya tabia nchi yanayosababisha ukame, kwa nini wanaenda kujenga mradi wa kuzalisha umeme huku Rufiji kwa kutegemea tena maji? Wakati kuna njia ya mbadala za kuzalisha umeme wa uhakika?
 
Wakuu,

Nimesoma katika magazeti kadhaa Kwa kipindi Cha hivi karibuni habari kuhusiana na ukame unaotokana na mabadiliko Tabia ya nchi ambayo pamoja na mambo mengine yanasababishwa Kwa kiasi kikubwa sana na shughuli za Binaadamu.
Hili suala la maji kukauka mto Ruvu ni upumbavu na ufisadi wa Watanzania uliopita kifani. Wkati wa kuweka mambomba ya gesi ya Songo Songo, Tanzania ilipewa ofa ya kutandaziwa mabomba ya maji bure ili mradi tu serikali inunue mambomba. Tulikataa kwa sababu tulitaka hilo suala lipitie kwenye tenda ili ulaji uwepo.

Na hata tuliambiwa siku mtakapoamua kuweka mambomba yenu basi msitumie njia yetu ya gesi itabidi mtengeneze yenu, hatukujali. Leo hii maji ya Dar yangekuwa yanatoka Rufiji na Ruvu ingekuwa ina supply mkoa wa Pwani peke yake
 
Mbuzi wa tanzania wana akili kuliko viongozi wa kitanzania.
 
Watanzania hawajaamua tu akili zipo nyingi tu,Kama mbuzi wa mjini ni Kama wamefundishwa kuvuka Barbara kwa usalama,haushangai kuona wanavuka kwenye zebra crossing.
Angalau wao hutunza kesho kwa kumumunya chakula usiku kucha sio akina makamba.
 
Naionea huruma kodi yetu iliyojenga bwawa la nyerere maana halitakuja fikia uzalishaji hata asilimia 40
 
Wakuu,

Nimesoma katika magazeti kadhaa Kwa kipindi Cha hivi karibuni habari kuhusiana na ukame unaotokana na mabadiliko Tabia ya nchi ambayo pamoja na mambo mengine yanasababishwa Kwa kiasi kikubwa sana na shughuli za Binaadamu.

Leo gazeti la JAMVILAHABARI wameandika kuhusu MTO RUVU kukaushwa na wakieleza namna mambo kama ufugaji, kilimo, ukataji miti na uchimbaji Madini unavyo athiri mto huo muhimu.

Sote tunafahamu umuhimu wa mto RUVU kwa maisha ya mwana Dar, uchumi wa Taifa na maendeleo ya nchi kwa ujumla.

Nawaomba wanajukwaa tushauriane Kwa pamoja na tufuate suluhu ya mambo haya ya Utunzaji wa mazingira.

Hivi ni Hadi lini patakuwepo na ukame huu wa kujitakia wenyewe?

Hivi Hadi lini tutaendelea kupata shida ya maji na umeme kipindi cha kiangazi?

Hivi wataalamu wetu wa Mifugo na Kilimo, wameshindwa kabisa kutengeneza mifumo kwa wadau wao Ili wafuge na walime bila kuathiri mwelekeo na mtiririko wa waji?

Hivi ni sahihi kabisa Kwa mtu kwenda kuchimba na kuchenjua Madini kwenye chanzo Cha maji?

Je hivi ni sawa kabisa Kwa mtu kichepusha mtiririko wa maji kupeleka shambani kwake Ili amwagilie maji apate hela halafu watu wanalalamika mgao?

Tutafakari pamoja

=====================

WALIVYOANDIKA JAMVI LA HABARI.

MTO RUVU UMEKAUSHWA MTO RUVU UMEKAUSHWA - Jamvi La Habari

Wakati mgao wa ,maji ukiendelea jijini Dar es salaam, hali imezidi kuwa mbaya sana katika kina cha maji kwa mto ruvu unaotegemewa kwa kiasi kikubwa kuzalisha maji jijini humo kutokana na kuharibiwa vibaya sana kwa mto huo na mito mingine midogo midogo kama mto mvuha, mgeta, Dutumi na mingine Zaidi ya 40

Uchunguzi uliofanywa na JAMVI LA HABARI umejionea namna ambavyo vyanzo hivyo muhimu vya maji vilivyoathirika huku shughuli za kibinaadamu zikiwa ni chanzo kikubwa cha uharibifu huo.

View attachment 2402715====
Tusipofikiri kama watu wanaotaka ukombozi na tukabaki kuwekeza kwenye zile zile akili za '47 tutabaki tukilia milele wakati wenzetu wakicheka.
Yaani kweli zamani hizi ni za nchi kama nchi kubaki kwenye kutegemea maji ya mvua za Mungu? Kwani Mungu alipokuumba alikuwekea akili ya nini?
Kwa nini serikali isiwaze juu ya maji taka kuya recycle kama baadhi ya miji inavyofanya?
Halafu kibaya zaidi bwana la umeme linalojengwa la Nyerere ni la kutegemea maji kama ya mto ruvu.
Maana yake ni kwamba mvua zisiponyesha lile bwana ni sifuri hakuna umeme. Tena ukizingatia limejengwa katika namna ya kuharibu mazingira kwa kukata miti ya ujazo mkubwa hatari.
Kamwe huwezi kupata hali nzuri ya maisha kwa kutegemea life style ile ile iliyokupa hali mbaya uliyo nayo. Ndiyo sisi Tanzania!
 
Huyo mwandishi, wakati akiripoti tarifa zake, alikuwa eneo la tukio lakini?

Huo mto wenyewe anaujua?
 
Tunaelekea kwenye Mass extinction huku tukichekacheka.
Ukistaabu ya Musa utaona ya Farao.
Huko Kenya,Somalia na Ethiopia kuna ukame unaenda mwaka wa tatu.
Huko Kajiado Kenya kwa sababu ya ukame mbuzi kwa sasa anauzwa sh 100 ya Kenya,na ngombe sh 500 ya Kenya badala 20,000 hadi 50,000 Kenyan shillings.
Kukauka kwa mto Ruvu hakujakuja kwa kuvizia,dalili za upungufu wa maji mto huo sio jambo geni.
Lakini hata Arusha na Manyara hali sio shwali mifugo imeadhilika kwa kiasi kikubwa,
Tumieni wataalamu wetu kikamilifu sio tu kuwaachia wanasiasa katika mambo ya ujuzi katika malengo na muendelezo wa kudhibiti ukame.
Tulipotaka kujenga bwawa la Nyerere kwa kukata miti milioni 6 ili tupishe ujenzi wa mradi huo.Mzungu namba mmoja Germany alipiga kelele kuwa bora atusaidie tutumie nishati yetu bwelele ya gesi asilia,akidai tutaongeza majanga,Kuna waliosema wanatuonea wivu! Hatukumuelewa,sasa ndio watu wengi wanaanza kumuelewa.
Ili tunusuru Bwawa la Nyerere lisigeuke white elephant,ianzishwe vita ya kupanda miti nchi nzima kwa miaka mitano mfululizo,kudhibiti ukulima kingo ya mito,kuhamasisha matumizi ya gesi yetu ianze kutumika majumbani,kudhibiti kwa kupunguza ufugaji wa kuhamahama tujikite na zero grazing, Kilimo kizingatia uboreshaji wa udogo ili uwe na afya.
 
Back
Top Bottom