Suley2019
JF-Expert Member
- Oct 7, 2019
- 1,815
- 4,565
Waziri wa Maji Jumaa Aweso (Mb) ameiagiza Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) kuhakikisha inafanya maboresho kwenye mitambo ya uzalishaji maji ya Ruvu Chini na Ruvu Juu hususani pampu za kusukuma maji ili kuwezesha huduma ya maji iweze kupatikana kwa ufasaha na kwa wananchi wote.
Mhe. Waziri ametoa maagizo hayo wakati alipotembelea na kukagua hali ya uzalishaji wa maji na upatikanaji wa maji Dar es Salaam na Pwani na kujiridhisha juu ya upatikanaji wa maji ya kutosha kwenye chanzo cha maji ya Mto Ruvu.
Ameongeza kwa kusema ameridhishwa na hali ya upatikanaji wa maji kutoka Mto Ruvu kwa kuwa vyanzo vyote vya Ruvu Juu na Ruvu Chini maji yapo ya kutosha, hivyo kazi kubwa inayohitaji kufanyika ni maboresho ya pampu za kusukuma maji kwenye Mitambo ili huduma iweze kupatikana kama kawaida.
Mhe. Waziri ametoa maagizo hayo wakati alipotembelea na kukagua hali ya uzalishaji wa maji na upatikanaji wa maji Dar es Salaam na Pwani na kujiridhisha juu ya upatikanaji wa maji ya kutosha kwenye chanzo cha maji ya Mto Ruvu.
Ameongeza kwa kusema ameridhishwa na hali ya upatikanaji wa maji kutoka Mto Ruvu kwa kuwa vyanzo vyote vya Ruvu Juu na Ruvu Chini maji yapo ya kutosha, hivyo kazi kubwa inayohitaji kufanyika ni maboresho ya pampu za kusukuma maji kwenye Mitambo ili huduma iweze kupatikana kama kawaida.