Mtikila kumshitaki Lowassa kwa kukwepa kodi

Mtikila kumshitaki Lowassa kwa kukwepa kodi

Kukwepa kodi,hiyo no kazi ya TRA. Mtikila aishtaki TRA kwa kushindwa kumkamata Lowassa. Mtikila Ana matatizo ya akili nasikia. Siyo tu nasikia,nimeshuhudia katika mikutano yake. Faulty reasoning. Anaongea normally,halafu kila baada ya PRECISELY ten minutes anaongea nonsense.
Andrew Nyerere ukipata nafasi naomba umwambie Manyerere Jackton namtafuta!
 
Last edited by a moderator:
Kama lowasa amekwepa kodi je huyo mgombea Mwenza anahusikaje au naye alikuwa ccm
 
Nakushukuru Sana Mkuu Kwa Kuliweka Hili Sawa Na Kumwambia Ukweli Wake Huyo Andrew Nyerere Kwani Kwa Tunaomjua Tumeshamsamehe Ila Ana Matatizo Makubwa Mno Na Mengi Yake Yameanzia Katika Kizazi Cha Koo. Nimesikitika Mno Kwa Comment Yake Ile. Nawaombeni Jamani Tumsamehe Tu Andrew Nyerere!

Wewe nawe kwa kujifanya mjuwaji hadi unakera!
 
Wewe nawe kwa kujifanya mjuwaji hadi unakera!

Usiyempenda Kaja Na Ukiona Nayajua Mengi Basi Ujue Kuwa Pia Nina Uwezo Mkubwa Wa AKILI Na Wa Kufahamu MAMBO Kuliko Wewe Na Mnavyozidi Kunichukia Ndiyo Mnaniweka Tu Juu Kama Lowassa Na Diamond Platinumz.
 
OKW BOBAN SUNZU

Mkuu huyo mtikila unaye mlisha hayo maneno mida hii yupo kwenye mipango ya kuiondosha ccm madarakani,yule ni mpinzani wa kweli siyo makanjanja
 
Last edited by a moderator:
Kwani wale wnzake walilipa kodi? kwani kutia nia kugombea ni biashara ulipie kodi TRA? anatumiwa vibaya huyu.

Naamini huyo mleta uzi ameamua kumlisha maneno mtikila
 
Pia awashtaki Viongozi wa CHADEMA ambao wamekuwa wakihubiri kwa miaka mingi kuwa Lowasa nk kuwa ni mafisadi kwa kuwataja majina bungeni na mikutano ya hadhara.Wananchi wakawaamini walichokuwa wakisema na hivyo wakawapigia kura na kuwawezesha kuingia bungeni ambako wamekula mamilioni ya kodi za wapiga kura waliowaamini kuwa akina lowasa mafisadi.

Lakini mnamo mwezi huu kwa mshangao wa wapiga kura wengi CHADEMA wale wale waligeuka na kusema Lowasa si fisadi wakati kipindi kile waomba kule waltumia kete ya ufisadi hewa kujinadi ili wapate kura kwa kulaghai wananchi kuwa lowasa fisadi wakati si fisadi

Kesi ambayo Mheshimiwa Mtikila anayotakiwa awafungulie CHADEMA na viongozi wa CHADEMA ni kujipatia nafasi za kisiasa bungeni kwa njia ya kutapeli wapiga kura kwa hoja hewa ya ufisadi usiokuwepo na hivyo aiombe mahakama iwapige marufuku Viongozi na wabunge wa CHADEMA na wapiga filimbi wa hamelini wao Akina Lipumba,Makaidi NA james mbatia kutogombea nafasi yeyote ya kisiasa na warudishe pesa zote walizopata bungeni kwa hoja ya utapeli hewa ya ufisadi ili kukomesha utapeli wa vyama na wanasiasa nchini Tanzania.
 
Je ccm pesa iliyopata kwa kuuza form kwa wagon beta urais ililipa kodi ya mapato?

Ccm ni wezi wakubwa kwani kwa makusudi walikuwa wanauza form hata kwa watu ambao walijua kabisa kuwa hawana vigezo kama yule jamaa wa std seven
 
Wakati mwingine unatakiwa utumie akili zako bila kuambiwa na mtu mwingine. Mliwakamata wangapi wakitoa au kupokea rushwa kutoka kwa EL au washirika wao? Mchungaji ameshachoka anatafuta kick katika siasa

Hilo ni swali la msingi sana na tunasubiri majibu
 
Back
Top Bottom