Mti ulioanguka zamani wasimama ghafla

Mti ulioanguka zamani wasimama ghafla

Habari hii imetangazwa leo asubuhi na local radio inaitwa cg fm.kwa kuwa nipo tabora nafuatilia habari hii na kuleta hapa ukweli.ila ni kweli imetangazwa na redio yetu ya ndani

Cg fm iko kwa internet bana inaskika dunia nzima
 
Tz inamaajabu mengi sana hadi viongozi kutojua kwanini wananchi watz ni masikini.
 
Hahaha angalia taarifa ya habari tbc kesho saa 11 alfajiri

Kumi na moja alfajiri.........mimi huyu huyu.......tena TBC.......jamani jamani.......wewe sema umenimiss......mimi pia......
 
Kutangazwa Tbc au C.G fm sio kigezo cha mimi kuamini huu upuuzi, wewe niambie maeneo uliopo huo mti, na kwa kuwa nitakuwa likizo wiki ijayo nitakwenda kushuhudia mimi mwenyewe lakini nijuavyo mimi mti hauwezi kukaa miaka mitatu bila kugeuzwa kuni na wakazi wa Tabora,
 
Unaouita upuuzi umetangazwa na redio yako ya Taifa vipindi vyote vya habari, reporta na mkuu wa wilaya wameushuhudia huo mti. Sijui na we nikuite mpuuzi?

Haswaaa mi naona yeye ndio mpuuzi ktk hilo.
 
hilo si ajabu kutokea, ni kweli maana hata na mimi niko hapa mawinguni napaa bila mabawa kuelekea visiwa vya hawaii kwa mapumziko ya weekend.
 
Kutangazwa Tbc au C.G fm sio kigezo cha mimi kuamini huu upuuzi, wewe niambie maeneo uliopo huo mti, na kwa kuwa nitakuwa likizo wiki ijayo nitakwenda kushuhudia mimi mwenyewe lakini nijuavyo mimi mti hauwezi kukaa miaka mitatu bila kugeuzwa kuni na wakazi wa Tabora,

Kumbe kina Tomaso bado mna exist mpaka zama hizi? mi nilijua ni wakati wa Yesu tu! Usichosadiki nini sasa wewe hebu tuondolee upuuzi wako! ila kama hela inakuwasha weka mafuta au panda hiyo Nbs nenda
 
Habar ata mm nimeisikia kwenye taarifa ya habari Tbc fm ila imenishangaza sana

hawana tofauti na cloudsFM. habari za kijinga-jinga. wanaleta ushirikina kwenye habari!!!?? kitu (ushirikina) kisichotambuliwa na taifa na mihimili yake yote.
 
Tanzania the truly nation of possibilities. naipenda nchi yangu jamani mweee! ila naiomba serikali ianzishe idara maalum ya kutunza kumbukumbu za maajabu haya ili vizazi vijavyo vihabarike.
 
Maajabu hayaishi katika nchi hii maana kuna kikombe kilikuwepo ukitoa jero tu na kunywa maji ya dawa yaliyopo kwenye hiko kikombe unapona magonjwa yote.
 
Hizo porojo mnazotuaminisha nyinyi pamoja na hao CG fm TBC sio wote tunaoweza kuziamini hata kidogo, wewe sema huo msufi ulikuwa sehemu gani, hata kama ni ushirikina lazima uchanganye na zako kidogo, mti uanguke ukae miaka mitatu bila kugeuzwa kuni??? kwa Tabora ninayoifahamu mimi, hao watangazaji wenyewe akina Vituko Salala, Salumu Kabendera aliekuwa mpiga picha pale karibu na CCM, au Juma kapipi wa kilileni ndio niwaamini? Jamani hebu changanyeni na zenu kidogo, Kama huo msitu ulikuwa Jeshini then i can agree this story zaidi ya hapo huu ni Upuuzi kabisa
 
Hizo porojo mnazotuaminisha nyinyi pamoja na hao CG fm TBC sio wote tunaoweza kuziamini hata kidogo, wewe sema huo msufi ulikuwa sehemu gani, hata kama ni ushirikina lazima uchanganye na zako kidogo, mti uanguke ukae miaka mitatu bila kugeuzwa kuni??? kwa Tabora ninayoifahamu mimi, hao watangazaji wenyewe akina Vituko Salala, Salumu Kabendera aliekuwa mpiga picha pale karibu na CCM, au Juma kapipi wa kilileni ndio niwaamini? Jamani hebu changanyeni na zenu kidogo, Kama huo msitu ulikuwa Jeshini then i can agree this story zaidi ya hapo huu ni Upuuzi kabisa

Hata kama ni jeshini msufi miaka mitatu hauozi?
 
Hayo ndiyo maajabu ya dunia;

Wiki tatu zilizopita pale mbezi mwisho kwenye stend mpya kabla ya kukuta kale kasoko pana msitu;
kuna mtoto alikuwa analia humu mchana kweupe, walikuja polisi na mbwa wao kunusa ila hakuna kilichoonekana, lakini mtoto anaendelea kulia, mwisho kila mtu akaondoka kimya kimya;

Kisa kingine cha mti ulioota majani nikiwa nautazama huko mbeya nacho ni cha kushangaza.

Tuishie tu kusema duniani kuna vituko.
 
Kutangazwa Tbc au C.G fm sio kigezo cha mimi kuamini huu upuuzi, wewe niambie maeneo uliopo huo mti, na kwa kuwa nitakuwa likizo wiki ijayo nitakwenda kushuhudia mimi mwenyewe lakini nijuavyo mimi mti hauwezi kukaa miaka mitatu bila kugeuzwa kuni na wakazi wa Tabora,
Hivi kumbe msufi Nao unatoa kuni!!"""??????
 
wakazi wa uyui wamekuta mti ulioanguka miaka mitatu iliopita na uliungua na sasa umenyanyuka wamechua vipande vya miti na kuchukua mizizi kwa imani kuwa ni dawa sasa subiri watu watakavyofungwa kamba kwa imani hiyo
 
Eti Emmanuel Okwi karudi toka UGANDA nasikia FUFA walimzuia!?
 
Cha ajabu wanauharibu wa nini? Imani zingine bwana 1413547780777.jpg
 
Back
Top Bottom