Mti ulioanguka zamani wasimama ghafla

Mti ulioanguka zamani wasimama ghafla

nabiidaniel

JF-Expert Member
Joined
Feb 25, 2014
Posts
2,087
Reaction score
2,853
Mti aina ya msufi ulioanguka miaka mitatu iliyopita, na baadae kuungua na moto wilayani Uyui mkoani Tabora, leo mchana katika hali ya maajabu umesimama wenyewe huku baadhi ya wananchi wakishuhudia.
Baadhi ya wananchi wameurukia ili kupata angalau gamba lake kwa imani za kishirikina.


attachment.php

 
Mti aina ya msufi ulioanguka miaka mitatu iliyopita, na baadae kuungua na moto wilayani Uyui mkoani Tabora, leo mchana katika hali ya maajabu umesimama wenyewe huku baadhi ya wananchi wakishuhudia.
Baadhi ya wananchi wameurukia ili kupata angalau gamba lake kwa imani za kishirikina.

Unatuhadithia au unatuambia?
 
kama mwewe aliweza kunyukua ng'ombe ni lipi lisilowezekana??

na je vipi yule ng'ombe aliyekutwa kwenye paa la nyumba juu?

mambo mengine ni kwikwi bandugu!
 
Uyui Kubwa sana hebu tuambie sehemu husika kisha tuwaulize wenyeji, pili ulikuwa unanyenyuka taratibu au fasta? kwa jinsi niwajuavyo wakazi wa Tabora mti hauwezi kuanguka na usigeuzwe kuni kwa kipindi cha miaka mitatu unless uniambie uliangukia karibu na jeshi la Anga njia ya kwenda kakola,
nitakuwa wa mwisho kuamini huu upuuzi
 
Habari hii imetangazwa leo asubuhi na local radio inaitwa cg fm.kwa kuwa nipo tabora nafuatilia habari hii na kuleta hapa ukweli.ila ni kweli imetangazwa na redio yetu ya ndani
 
Habar ata mm nimeisikia kwenye taarifa ya habari Tbc fm ila imenishangaza sana
 
hii habar nmeiona tbccm leo saa 2 mpaka mwenyekiti wa mtaa amethibitisha hlo..mpaka nimeshtuka dahh
 
Watu wameshuhudia kwa macho mti ukisimama wenyewe kwa mlio mkubwa sana. Ingekuwa nchi za wenzetu tukio lingeingia kwenye guines record, lakini kwa sisi tunaoishi dunia iliyosahaulika, ngoja tusimuliane wenyewe kwa wenyewe. Ila linasisimua
 
Uyui Kubwa sana hebu tuambie sehemu husika kisha tuwaulize wenyeji, pili ulikuwa unanyenyuka taratibu au fasta? kwa jinsi niwajuavyo wakazi wa Tabora mti hauwezi kuanguka na usigeuzwe kuni kwa kipindi cha miaka mitatu unless uniambie uliangukia karibu na jeshi la Anga njia ya kwenda kakola,
nitakuwa wa mwisho kuamini huu upuuzi
Unaouita upuuzi umetangazwa na redio yako ya Taifa vipindi vyote vya habari, reporta na mkuu wa wilaya wameushuhudia huo mti. Sijui na we nikuite mpuuzi?
 
Khaaaaaa!!!!........hebu nisimulieni vizuri..........ilikuwaje na sababu ni nini.......?........na kama mnaweza kutupiamo hata tupicha tuwili tutatu hivi.............
 
Khaaaaaa!!!!........hebu nisimulieni vizuri..........ilikuwaje na sababu ni nini.......?........na kama mnaweza kutupiamo hata tupicha tuwili tutatu hivi.............

Hahaha angalia taarifa ya habari tbc kesho saa 11 alfajiri
 
kama ni TBC inapotezea mchakato wa katiba kwani wamekosa majibu ni vipi marehemu Shida alipiga kura, halafu ni kivipi Zakhia Meghji amepiga kura Zanzibar, sasa wanapotezea kwa ushirikina wao. Elimu ni muhimu sana kwa watanzania wasiendelee kudanganywa na hawa majangili.
 
Khaaaaaa!!!!........hebu nisimulieni vizuri..........ilikuwaje na sababu ni nini.......?........na kama mnaweza kutupiamo hata tupicha tuwili tutatu hivi.............
nakutumia whatsapp
 
kama ni TBC inapotezea mchakato wa katiba kwani wamekosa majibu ni vipi marehemu Shida alipiga kura, halafu ni kivipi Zakhia Meghji amepiga kura Zanzibar, sasa wanapotezea kwa ushirikina wao. Elimu ni muhimu sana kwa watanzania wasiendelee kudanganywa na hawa majangili.

Kama theluthi mbili ilipatikana hata miti iliyokufa inaweza kuinuka na kumea tena.

ONLY IN TANZANIA
 
Back
Top Bottom