Amiliki
JF-Expert Member
- May 6, 2011
- 2,085
- 1,005
Hivi mtu ukienda CCM ni lazima kwanza ujitoe akili ndio ukubalike huko! Sasa hii Agenda ya Baba wa Dr. Slaa kwamba Mwampamba anamjua huku akishindwa kumtaja inatija gani kwa Mtanzania ambae ananunua Unga wa Ugali kwa Shilingi 1500 kwa Kilo huku kilo ya nyama ya Ng'ombe ikifikia 6000? Je Inatija gani kwa Mzazi ambaye mwanaye amepata Division 0? Inatija gani kwa taifa ambalo 62% ya wanafunzi waliomaliza form four wamepata Division 0? Inatija gani katika kutokomeza wimbi hili la Ugaidi linalozidi kushamiri sasa hivi nchini? Inaweza vipi kuzuia kuuawa kwa Mapadri na Wachungaji kuchinjwa? Inaweza vipi kuzuia Makanisa kuchomwa kila uchwao? CCM mkiendelea na walemavu wa akili kama hawa na kuwafanya ndio misukule ya kupeleka sera zenu kwa wananchi hakika kihama chenu kitakuwa kabla 2015.